RC aagiza wahujumu korosho wapigwe risasi!

Keil

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2007
Posts
2,214
Reaction score
804
Nimeshindwa kuelewa kama hii ni spinning ama ni makosa ya mwandishi wa habari? Kichwa habari kama hicho ukisoma haraka haraka unaweza kudhani kwamba Mkuu wa Mkoa ameagiza watu wajichukulie sheria mkononi kwa kuwatwanga risasi wahujumu wa korosho. Lakini kumbe ni usanii wa wana siasa wa Bongo. Huyo Mhagama mwenyewe sina hakika kama ana maanisha hayo aliyoyasema, si ajabu alikuwa akiwakejeri wakulima wa zao la korosho ambao ndiyo watakao umia, maana inawezekana korosho zikanunuliwa na bado wakulima wasilipwe haki yao kwa wakati muafaka! Hii ndiyo Bongo bwana, longolongo kuanzia juu mpaka chini.

 
Nadhani ametumia msemo tu kama vile yule kiongozi aliyesema viongoze wakishindwa kutimiza ahadi zao "wanyongwe 2010"
 
Kama yeye ni kiongozi inatakiwa awe makini na maneno anayoyatumia. Kuagiza watu wapigwe risasi mimi naona ni maneno mazito sana na hakupaswa ayatumie. Je ikatokea mtu akapigwa kweli risasi na walinzi atasemaje?
 
If at all the reporting is accurate,

Nataka kuungana na Choveki kulaani viongozi wasiowajibika kwa kutoa matamko yenye uzito unaoweza kusababisha utovu wa amani.Huyu bwana ameonyesha ni jinsi gani asivyothamini sio tu maisha ya watu, bali pia mchakato mzima wa utawala wa sheria.

Ndiyo viongozi wetu hao, wanatafuta majibu ya haraka kwa matatizo magumu. Hii inaonyesha kukosekana kwa sifa za uongozi, uwezo wa kuwasiliana, uelewa wa mambo kwa upana na uvivu wa kufikiri.

Naamini kuna sheria zinazoweza kuwabana viongozi wazembe kama hao wawajibishwe kwa matamshi hatari kama haya.
 
Tanzania kuna "Utawala" wa "sheria".
Hakuna mahakama yoyote itakayomhukumu mhujumu kifo hapa Tanzania, naona mkuu alipitiwa tu, akajikuta anaropoka.
Tumsamehe tu, akikua ataacha!
 
Tanzania kuna "Utawala" wa "sheria".
Hakuna mahakama yoyote itakayomhukumu mhujumu kifo hapa Tanzania, naona mkuu alipitiwa tu, akajikuta anaropoka.
Tumsamehe tu, akikua ataacha!

See,

attitude nonchalant kama hizi ndiyo zinachangia tatizo.

1.Utamsamehe vipi mtu hata hajaomba msamaha.

2.Hata kama ameomba msamaha, kama tamko kama hilo ni kosa kisheria huna nguvu ya "kumsamehe".Unaweza kumsamehe in the court of public opinion lakini mahakamani msamaha wako ni ziro.

subiri wajinga wajinga wanaochukua amri kama mbwa wampige ndugu yako risasi kweli utajua uzuri wa "kumsamehe"

Sasa hivi mwendo unaotakiwa ni zero tolerance kwa wajinga wajinga kama hawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…