Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila amesema nchi 25 kutoka Afrika zinatarajia kuhudhuria katika mkutano wa kahawa utakao fanyika nchini Tanzania kuanzia kesho Februari 21 Hadi 22 wenye lengo la kujadili namna ya kulikuza zao hilo.
Mkutano huo kwa siku ya kesho uta hudhuriwa na mawaziri wa kilimo wa nchi hizo na kesho kutwa utahudhuriwa na wakuu wa nchi wa mataifa ya Afrika huku zaidi ya washiriki 1,000 kutoka ndani na nje ya nchi wakitarajia kuhudhuria.
Chalamila amesema Mkutano huo ni wa tatu kufanyika hapa nchini hivyo una tija kwa Taifa katika nyanja mbalimbali ikiwemo kukuza uchumi kwa wafanyabiashara wa zao hilo na Taifa kwa ujumla.