n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,015
- 2,680
* Ni kwa kuongea na simu wakati wa mkutano
Na Fadhili Abdallah, Kigoma
MKUU wa mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia, amemtimua kwenye kikao cha Bodi ya Barabara mbunge,Sijapata Nkayamba (Viti Maalum CCM) kwa kuongea na simu wakati kikao kikiendelea.
Kabla ya hatua hiyo, Simbakalia na wajumbe wengine wa kikao hicho, walilazimika kumvumilia mbunge huyo kutokana na simu zake kuathiri mwenendo wa kikao kwa kutoa milio yenye kelele kila mara.
Kama haitoshi, moja ya simu ya mbunge huyo iliita ambapo aliamua kuipokea na kuanza kuongea hali iliyoonekana kuingilia utulivu na usikivu wa wajumbe.
Hali hiyo ilimfanya, Simbakalia kumuagiza mbunge huyo kutoka kwenye kikao na kwenda kuongea na simu zake na kwamba angeruhusiwa kurudi baada ya kumaliza maongezi na simu hizo kuzizima.
Baada ya kuongea kwa muda, mbunge huyo alimweleza mkuu wa mkoa kwamba amemaliza na kuomba kikao kiendelee, lakini Simbakalia alishikilia msimamo wake wa kumtaka mbunge huyo kutoka ukumbini kwanza.
Kufuatia hali hiyo, kikao kilisimama kwa dakika kadhaa wakati wajumbe wakisubiri kutekelezwa kwa amri hiyo ya mkuu wa mkoa Kigoma ambaye alikuwa mwenyekiti.
Hatimaye mbunge huyo alilazimika kutoka nje ya ukumbi wa mikutano uliopo ofisi za mkuu huyo wa mkoa eneo la Mnarani mjini Kigoma.
Serikali imeshatoa maelekezo ambayo yamekuwa yakibandikwa kwenye kumbi mbalimbali za mikutano na wakati mwingine kutolewa kwa tangazo la kuwataka wajumbe wa vikao na hata watu binafsi kuzima simu zao au kutoa milio ili kuepuka usumbufu.
Na Fadhili Abdallah, Kigoma
MKUU wa mkoa wa Kigoma, Joseph Simbakalia, amemtimua kwenye kikao cha Bodi ya Barabara mbunge,Sijapata Nkayamba (Viti Maalum CCM) kwa kuongea na simu wakati kikao kikiendelea.
Kabla ya hatua hiyo, Simbakalia na wajumbe wengine wa kikao hicho, walilazimika kumvumilia mbunge huyo kutokana na simu zake kuathiri mwenendo wa kikao kwa kutoa milio yenye kelele kila mara.
Kama haitoshi, moja ya simu ya mbunge huyo iliita ambapo aliamua kuipokea na kuanza kuongea hali iliyoonekana kuingilia utulivu na usikivu wa wajumbe.
Hali hiyo ilimfanya, Simbakalia kumuagiza mbunge huyo kutoka kwenye kikao na kwenda kuongea na simu zake na kwamba angeruhusiwa kurudi baada ya kumaliza maongezi na simu hizo kuzizima.
Baada ya kuongea kwa muda, mbunge huyo alimweleza mkuu wa mkoa kwamba amemaliza na kuomba kikao kiendelee, lakini Simbakalia alishikilia msimamo wake wa kumtaka mbunge huyo kutoka ukumbini kwanza.
Kufuatia hali hiyo, kikao kilisimama kwa dakika kadhaa wakati wajumbe wakisubiri kutekelezwa kwa amri hiyo ya mkuu wa mkoa Kigoma ambaye alikuwa mwenyekiti.
Hatimaye mbunge huyo alilazimika kutoka nje ya ukumbi wa mikutano uliopo ofisi za mkuu huyo wa mkoa eneo la Mnarani mjini Kigoma.
Serikali imeshatoa maelekezo ambayo yamekuwa yakibandikwa kwenye kumbi mbalimbali za mikutano na wakati mwingine kutolewa kwa tangazo la kuwataka wajumbe wa vikao na hata watu binafsi kuzima simu zao au kutoa milio ili kuepuka usumbufu.