Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha amewataka Viongozi wa Chama cha Msingi Kisuke katika Halmashauri ya Ushetu wilayani Kahama kusitisha utunzaji wa nyaraka za ofisi katika Jaba lililokuwa katika Ghala la kuhifadhia Zao la Pamba.
RC Macha ametoa agizo hilo leo wakati akiendelea na ziara ya kutembelea Wakulima na kukagua maendeleo ya zao pamba katika Halmashauri hiyo na kubaini uwepo wa uzembe katika utunzaji wa nyaraka za Amcos hiyo yenye jumla ya Wakulima 100.
Soma: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani amewashauri viongozi wa AMCOS kuwa na desturi ya kutatua changamoto katika maeneo yao bila kusubiri viongozi wa ngazi za juu ikiwa ni pamoja na kutunza vyema nyaraka na pembejeo.
RC Macha ametoa agizo hilo leo wakati akiendelea na ziara ya kutembelea Wakulima na kukagua maendeleo ya zao pamba katika Halmashauri hiyo na kubaini uwepo wa uzembe katika utunzaji wa nyaraka za Amcos hiyo yenye jumla ya Wakulima 100.
Soma: Uzi Maalum wa Vibweka na Hekaheka za wanasiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Ushetu Mhe. Emmanuel Cherehani amewashauri viongozi wa AMCOS kuwa na desturi ya kutatua changamoto katika maeneo yao bila kusubiri viongozi wa ngazi za juu ikiwa ni pamoja na kutunza vyema nyaraka na pembejeo.