#COVID19 RC Kunenge aonesha wasiwasi dozi 15,000 za Uviko-19 ambazo hazijatumika zinaweza ku expire kama hazitatumika. Aweka mikakati ya kuhakikisha zinatumika

#COVID19 RC Kunenge aonesha wasiwasi dozi 15,000 za Uviko-19 ambazo hazijatumika zinaweza ku expire kama hazitatumika. Aweka mikakati ya kuhakikisha zinatumika

Tripo9

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2009
Posts
4,357
Reaction score
3,550
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema kuna chanjo 15,000 za Uviko-19 hazijatumika mkoani humo huku kukiwa na changamoto kwa kuwa baada ya mwezi mmoja kuanzia leo Jumamosi Septemba 25, 2021 zitafikia mwisho wa matumizi yake.

Ameeleza kuwa mkoa umepata dozi 15,000 za chanjo ya Uviko-19 ambazo bado hazijatumika kati ya 30,000 zilizopokelewa, zitumike katika kipindi kifupi kijacho.

Kunenge amesema kwa kuanza wameamua kukutana na kamati ya afya ya msingi ngazi ya mkoa na wilaya, wataalamu kutoka Wizara ya Afya na Tamisemi ili kwa pamoja kufanya tathimini na kujipanga upya kwa kuongeza wigo mpana wa utoaji chanjo hiyo ili iishe yote kabla ya muda wake wa kuharibika haujafika.

"Chanjo hizi zina muda wake maalumu na tumeangalia mpaka sasa katika mkoa wetu katika chanjo 30,000 tulizopokea sasa hivi tumefikia asilimia 50 ya dozi hizi kwa maana zimetumia kama 15,000 tu , nusu ya chanjo hizo bado hazijatumika na ni mwezi mmoja tu umebaki lazima tutumie mbinu shiriki na hizi zitumike kwa hiyo kikao hiki ni kikao cha kutafuta majibu," amesema Kunenge akibainisha kuwa idadi ya waliochanja ni ndogo ikilinganishwa na wakazi wa mkoa huo huku akitaka wakuu wa wilaya kusimamia utoaji wa chanjo.

Chanzo: Mwananchi
 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema kuna chanjo 15,000 za Uviko-19 hazijatumika mkoani humo huku kukiwa na changamoto kwa kuwa baada ya mwezi mmoja kuanzia leo Jumamosi Septemba 25, 2021 zitafikia mwisho wa matumizi yake.

Ameeleza kuwa mkoa umepata dozi 15,000 za chanjo ya Uviko-19 ambazo bado hazijatumika kati ya 30,000 zilizopokelewa, zitumike katika kipindi kifupi kijacho.

Kunenge amesema kwa kuanza wameamua kukutana na kamati ya afya ya msingi ngazi ya mkoa na wilaya, wataalamu kutoka Wizara ya Afya na Tamisemi ili kwa pamoja kufanya tathimini na kujipanga upya kwa kuongeza wigo mpana wa utoaji chanjo hiyo ili iishe yote kabla ya muda wake wa kuharibika haujafika.

"Chanjo hizi zina muda wake maalumu na tumeangalia mpaka sasa katika mkoa wetu katika chanjo 30,000 tulizopokea sasa hivi tumefikia asilimia 50 ya dozi hizi kwa maana zimetumia kama 15,000 tu , nusu ya chanjo hizo bado hazijatumika na ni mwezi mmoja tu umebaki lazima tutumie mbinu shiriki na hizi zitumike kwa hiyo kikao hiki ni kikao cha kutafuta majibu," amesema Kunenge akibainisha kuwa idadi ya waliochanja ni ndogo ikilinganishwa na wakazi wa mkoa huo huku akitaka wakuu wa wilaya kusimamia utoaji wa chanjo.

Chanzo: Mwananchi
Yaani kujipendekeza ili kubaki vyeoni ni kazi sana. Hivi nani anasumbuka na uviko 19 sasa??????????? Hivi vile vifo vya maelfu kwa mamilioni Tanzania vipo wapi???????????? Je hizo chanjo wanaenda kumuambia nani ajikinge na kitu ambacho kila siku mikusanyiko ni kila sehemu na hakuna anayeugua ugua???????
 
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge amesema kuna chanjo 15,000 za Uviko-19 hazijatumika mkoani humo huku kukiwa na changamoto kwa kuwa baada ya mwezi mmoja kuanzia leo Jumamosi Septemba 25, 2021 zitafikia mwisho wa matumizi yake.

Ameeleza kuwa mkoa umepata dozi 15,000 za chanjo ya Uviko-19 ambazo bado hazijatumika kati ya 30,000 zilizopokelewa, zitumike katika kipindi kifupi kijacho.

Kunenge amesema kwa kuanza wameamua kukutana na kamati ya afya ya msingi ngazi ya mkoa na wilaya, wataalamu kutoka Wizara ya Afya na Tamisemi ili kwa pamoja kufanya tathimini na kujipanga upya kwa kuongeza wigo mpana wa utoaji chanjo hiyo ili iishe yote kabla ya muda wake wa kuharibika haujafika.

"Chanjo hizi zina muda wake maalumu na tumeangalia mpaka sasa katika mkoa wetu katika chanjo 30,000 tulizopokea sasa hivi tumefikia asilimia 50 ya dozi hizi kwa maana zimetumia kama 15,000 tu , nusu ya chanjo hizo bado hazijatumika na ni mwezi mmoja tu umebaki lazima tutumie mbinu shiriki na hizi zitumike kwa hiyo kikao hiki ni kikao cha kutafuta majibu," amesema Kunenge akibainisha kuwa idadi ya waliochanja ni ndogo ikilinganishwa na wakazi wa mkoa huo huku akitaka wakuu wa wilaya kusimamia utoaji wa chanjo.

Chanzo: Mwananchi
Siwazi mwage tu na kusainisha makaratasi ya uongo ,chanjo chanjo ni kupoteza muda wa kuwa tumikia wananchi katika mambo ya maendeleo
 
Mh. Makalla kwanini hizo chanjo usijidunge zote ili uishi milele? Hiyo Corona mnaiyoipigia kelele iko wapi? watu wakiona kuna tatizo watazichangamkia wenyewe bila kuhamasishwa, ukiona chanjo zimedoda basi jua hiyo Corona mnayoihubiri kila siku, huku mitaani watu wanaishi nayo kawaida tu. BTW Mh. Karibu Juliana Pub tuitokomeze Corona. 🙂🙂
 
Juzi tumezika kijana wa miaka kama 45 Covid kakaa Hosp wiki na jana tumezika mzee wake wote walikuwa wanaumwa ni siku moja tu inasikitisha sana haya mambo baadhi ya family wanayopitia. so sad
 
Juzi tumezika kijana wa miaka kama 45 Covid kakaa Hosp wiki na jana tumezika mzee wake wote walikuwa wanaumwa ni siku moja tu inasikitisha sana haya mambo baadhi ya family wanayopitia. so sad
Hawakua wamechanja mkuu?
 
Hawakua wamechanja mkuu?
Hapana mkuu jamaa kaumwa kama siku kumi tu ila mzee wake siku 3 tu yule bwana tumezika saa kumi Alkhamis mzee tumezika Ijumaa mchana. Tough. Kuna mtu kaniambia huu ugonjwa una survive ila ukiona mtu anafariki katika family basi chance kubwa wanaondoka na wengine ni kama genetic fulani hivi sasa sijui lina ukweli hili.
 
Hapana mkuu jamaa kaumwa kama siku kumi tu ila mzee wake siku 3 tu yule bwana tumezika saa kumi Alkhamis mzee tumezika Ijumaa mchana. Tough. Kuna mtu kaniambia huu ugonjwa una survive ila ukiona mtu anafariki katika family basi chance kubwa wanaondoka na wengine ni kama genetic fulani hivi sasa sijui lina ukweli hili.
Siyo genetic, ni kwamba mtu wa familia akiumwa, wanafamilia wanaona haya kuchukua tahadhari zote ikiwemo kumtenga na kuvaa barakoa ili asijisikie kama wanamnyanyapaa. Wanakuja kuanza kuchukua tahadhari baadae sana wakishachelewa. Hili nimeliona sana.
 
Siyo genetic, ni kwamba mtu wa familia akiumwa, wanafamilia wanaona haya kuchukua tahadhari zote ikiwemo kumtenga na kuvaa barakoa ili asijisikie kama wanamnyanyapaa. Wanakuja kuanza kuchukua tahadhari baadae sana wakishachelewa. Hili nimeliona sana.
Nacho ongelea hapa sikupata corona ziko family nyingi tu family nzima wanapata corona na wamepona family ya mdogo wangu walipata wote tu lakini wamepona ila kuna mtu kasema akiondoka mmoja katika family basi chance kubwa mwingine ataenda same family, kwa maoni yake ziko family zinawachukuwa vibaya nadhani tumesikia juzi kwa Hans pope na yule waziri wa ulinzi yeye na Mama yake mifano mingi sana, ziko family nyingi zimepitia na wote kupona.
 
Yaani kujipendekeza ili kubaki vyeoni ni kazi sana. Hivi nani anasumbuka na uviko 19 sasa??????????? Hivi vile vifo vya maelfu kwa mamilioni Tanzania vipo wapi???????????? Je hizo chanjo wanaenda kumuambia nani ajikinge na kitu ambacho kila siku mikusanyiko ni kila sehemu na hakuna anayeugua ugua???????
Kuna comments huwa nazisoma halafu najiuliza hivi Mungu aliyetupa ubongo/brain sawa na races nyingine kama wazungu, wachina, Wahindi etc ni wa kulaumiwa kweli? Profesa wa genetics aitwaye Witson aliwahi kuandika kwenye moja ya machapisho yake kwamba of all races in the world Waafrika ndiyo the most inferior, mwanzoni nilimchukia sana huyu bwana but kila ninapoona watu kama mleta comments na wengine wengi tuu, naanza kuona kwamba huyu profesa anaweza kuwa sahihi.
 
Back
Top Bottom