Kuna jamaa hapo kushoto kaviiimba tumbo ka mpira wa criketMkuu wa mkoa wa Dar es salaam mh Makalla amesema zoezi la kulirejesha jiji pamoja na mkoa mzima katika hadhi yake litaanza ambapo Wamachinga wanaofanya biashara zao barabarani na katika hifadhi za barabara wataondolewa.
Makalla amesema wamachinga wote wanapaswa kufanya biashara katika maeneo rasmi yaliyotengwa na siyo vinginevyo.
Chanzo: Clouds tv
cc: Mmawia
======
RC MAKALLA: MARUFUKU MACHINGA KUFANYA BIASHARA KWENYE NJIA ZA WATEMBEA KWA MIGUU.
- Asema agizo hilo ni kwa Wafanyabiashara Mkoa mzima.
- Amtaka DC Ilala na Uongozi wa Machinga kuweka utaratibu mzuri kuwapanga Machinga Kariakoo.
- Awapo mbinu ya kufunga baadhi ya Mitaa Kariakoo kwaajili ya kufanya Biashara.
- Wamachinga wakiri kuingilia maeneo ya watembea kwa miguu na kuahidi kuhama.
- Aeleza dhamira yake ya kuboresha mandhari ya Dar es salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amepiga marufuku ufanyaji wa Biashara Kwenye maeneo hifadhi ya barabara zote za Mkoa huo baada ya utaratibu huo kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani na ongezeko la ajali.
RC Makalla ametoa maelekezo hayo alipotembelea Soko la Kariakoo na kujionea Kero ya Ufanyaji biashara holela Kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.
Kutokana na hilo RC Makalla amewaelekeza Mkuu wa Wilaya ya Ilala kufanya kikao na Wafanyabiashara hao Jumatatu ya *September 13 na kuainisha maeneo ya kuwapeleka wote waliovamia hifadhi ya Barabara.
Aidha RC Makalla amewaelekeza Kuangalia utaratibu mzuri wa kufunga na kufungua baadhi ya Mitaa Kariakoo kwaajili ya kufanya biashara Kutokana na ufinyu wa maeneo ili Waweze kupata riziki.
Hata hivyo RC Makalla amesema kwa tathimini aliyofanya amebaini Hali ya Ufanyaji biashara holela Dar es salaam ipo kwa kiwango kikubwa na kuwanyima watembea miguu haki zao za msingi.
Pamoja na hayo RC Makalla ameelekeza Manispaa zote za Mkoa huo kuweka Vibao vya kuzuia biashara Kwenye maeneo ya watembea kwa miguu.
View attachment 1930496View attachment 1930497View attachment 1930498
View attachment 1930499
Dah hongera mkuu tumeshajua una JeepNapenda sana kupita hii njia ya kaliakoo nikiwa na gari yangu Jeep ,! wale wamachinga huwa wananikera sana bora waondolewe tu
Narudia tena wewe unalipwa hapo hujui maana ya machinga.... machinga hawawezi kaa mbali ya wateja... wanatakiwa kuwa mjini... hayo maeneo unayo yataja ni yapi? machinga complex? Tusubiri afanikiwe nikuletee zawadi...... uwezi kuwatoa machinga mjini
Mkuu suala hapa sio kuwafukuza wamachinga bali nikuwapanga vizuri katika maeneo yao ya kazi. Aidha wengi wa wamachinga unaowaona leo wanafanya umachinga kwa niaba ya wafanyabiashara wakubwa ambao wanakwepa kulipa kodi na malipo ya leseni mbalimbali za kibiashara za kuamua kuwapatia hao wachinga.Hakuna nchi hapa East Africa ni maskini kuliko sisi kwa hali zote yaani kifedha na kirasilimali ambazo hazina wamachinga kabisa kwny miji yao?
Ndani ya Kariakoo unawapanga wapi?Mkuu suala hapa sio kuwafukuza wamachinga bali nikuwapanga vizuri katika maeneo yao ya kazi. Aidha wengi wa wamachinga unaowaona leo wanafanya umachinga kwa niaba ya wafanyabiashara wakubwa ambao wanakwepa kulipa kodi na malipo ya leseni mbalimbali za kibiashara za kuamua kuwapatia hao wachinga.
Mkuu Tough lady hawa watu tunao wazungumza wamachinga sio wa Kariakoko tu ni Dar yote kama sio Tanzania mzima. Wanatakiwa wapangwe kwa mujibu na taratibu za kisheria, na ionekane kweli ni mmachinga kweli na si mmachinga kwa mbinu za kukwepa KODINdani ya kariakoo unawapanga wapi?
Walitembea kwa miguu yao au unadhani walishushwa toka mbinguni?
Hata Mh Paul Makonda aliwapiga marufuku hao wafanyabiashara na tamko la Mwanza likapindua meza na yeye kushindwa katika zoezi hilo! Sasa huyu nae amesema hivyo kama Mh Hagaya hana taarifa, basi hili nalo ni katika kutengeneza tatizo na wao wenyewe kulirekebisha na sie kushangilia tu!!Nampongeza kwa hili
Jeshi kubwA kwa mtaji wa kura haliwezi guswaItapigwa simu moja tu toka juu kusitisha zoezi zima unapunguza kula za mheshimiwa. Badala yake yeye atatoka na atatuacha sisi wamachinga.