Pre GE2025 RC Mtanda azungumzia suala la Katibu wa BAVICHA- Mwanza kupotea, asema serikali haina lengo la kumteka yeyote yule

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Amesema kuwa ameona taarifa ya jeshi la polisi kuhusu kutekwa kwa Katibu huyo,

Soma: Pre GE2025 - Amani Manengelo, Katibu wa BAVICHA Mkoa wa Mwanza, ameripotiwa kutekwa na kupotea tangu tarehe 14.02.2025 huko Misungwi

"Nitaliita jeshi la polisi ambalo lina dhamana ya kuilinda amani, usalama na kupitia mkutano huu nimuagize kamanda wa jeshi la polisi. Nimeiona taarifa ambayo jeshi la polisi wameitoa leo, kwanza kabisa niwahakikishieni serikali ya awamu ya sita ya Rais Samia na mimi nikiwa mkuu wa mkoa wa Mwanza hatuna lengo la kumteka mtu yeyote yule awe CHADEMA, awe mfanyabiashara kwa sababu hatuna ugomvi na mtu yeyote."

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Your browser is not able to display this video.

Soma: Polisi Mwanza: Tunachunguza tukio la kutekwa kwa Katibu wa Bavicha Mwanza
 
Angalau ameongea vizuri sana kwa hekima , utulivu, na kwa kutambua nafasi yake kama, mlezi, mlinzi, kiongozi, mfariji Mkuu wa mkoa wa Mwanza, hongera sana bwana Said Mtanda βœ…βœ…βœ…
 
Sema hiyo tarehe alliyotekwa inaibua maswali mengi. Ilikuwa siku ya Valentine. Hisia zangu zinaniambia huyo yupo sehemu kajifungia anafaidi penzi.
 
Msako Maalum wa kumtafuta Amani Katibu wa bavicha aliyepotea mkoani Mwanza utaanza Wakati wowote ukiwashirikisha Chadema, Polisi na family ya Amani

Jambo TV

Ahsanteni sana 🐼
 
Msako Maalum wa kumtafuta Amani Katibu wa bavicha aliyepotea mkoani Mwanza utaanza Wakati wowote ukiwashirikisha Chadema, Polisi na family ya Amani

Jambo TV

Ahsanteni sana 🐼
Baada ya kuambiwa kesho kuna maandamano ndo wametoka na kuongea?

Walikuwa wapi siku zote?
 
Mtanda kumbe anaelewa kuwa cheo ni dhamana apo nimekukubali lakini kama huyo kijana itakuwa ni ishu ya siasa atutakubali uhuni tutachomoa betri..
 
Angalau ameongea vizuri sana kwa hekima , utulivu, na kwa kutambua nafasi yake kama, mlezi, mlinzi, kiongozi, mfariji Mkuu wa mkoa wa Mwanza, hongera sana bwana Said Mtanda βœ…βœ…βœ…
Kwakweli ameongea kiume, amesema vizuri, ndivyo kiongozi anapaswa kuzungumza
 
Hawezi kukubali
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…