RC Tanga alia na mrundikano wa wahamiaji haramu mkoani kwake

RC Tanga alia na mrundikano wa wahamiaji haramu mkoani kwake

Binti 1

Member
Joined
Dec 1, 2018
Posts
30
Reaction score
65
Mkuu wa mkoa wa Tanga, Omari Mgumba ametoa kilio cha mlundikano wa wahamiaji haramu katika magereza yaliyopo katika mkoa huo mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan hii leo.

Akizungumza mbele ya Rais Samia ambaye yupo mkoani humo kwa ziara ya siku mbili, mkuu huyo wa mkoa amesema kwamba mkoa huo una mahabusu na wafungwa takribani 2,053 ambapo kati yao, 946 wanatoka katika mataifa mengine.

Mkuu huyo wa mkoa ameongeza kuwa, kati ya hao 946, zaidi ya 830 ni wahamiaji haramu au "wasafirishwaji" ambao wameshamaliza kutumikia adhabu zao na kinachosubiriwa ni kukamilika kwa utaratibu wa kuwarudisha makwao.

Aidha, RC huyo amemuomba Rais Samia kuwahimiza viongozi wa mataifa husika kukamilisha mchakato wa kuwarudisha watu hao katika mataifa yao.

RC Tanga.jpg
 
Kwa sababu mwenye dhamana yupo na yeye anaomba kusaidiwa na mheshimiwa
 
Nchi nyingi zinarudisha wageni makwao wao wanataka kuwafunga wakishajua kiswahili huko jela baadae wanarudi kama Watanzania.
 
Weee RC mpuuzi sana sio kila kitu kinamwitaji Rais akifanyie kazi, my RC kwani huna idara ya immigrations hapo mkoani kwako?hawa ndio kazi yao ,na pili jiulize hao illegal immigrants waliingiaje hapo mkoani kwako kama vyombo vya ulinzi vinafanya kazi yake ?,walitakiwa wasimudu hata to cross that border
 
Wahamiaji haramu ni dili linalotajirisha watu, na lina mkono wa wakubwa. Inapotokea wakakamatwa ni kwamba wahusika wamedhulumiana.

Kwa hiyo wachache wanatolewa kafara, ndio unakuta inatangazwa kwa mbwembwe kwamba wahamiaji kadhaa wamekamatwa lakini hutasikia kama kuna aliyehukumiwa kwa kusafirisha wahamiaji haramu kama walikuwa wanasafiri wenyewe.
 
Back
Top Bottom