Real Madrid v Liverpool: UEFA Champions League Final - May 26, 2018. Madrid wins for the 3rd time in a row!

Kama hujacheza mpira huwezi jua nachokisema.. Mimi sio kushabikia tu, naujua na ninaucheza
Uko sahihi sana na hasa kama unaucheza/umewahi kuucheza. Hao wanaodhani ama kuwa na umri mkubwa au kuangalia mpira tangu Dunia iumbwe ndo kujua mpira hawana nafasi ya kusema neno, ndani yake kachanganya na mapenzi.

Ramos alikusudia kufanya UHUNI ule, si yeye wala beki mwingine yeyote aliyeweza kupanda juu kwa dakika zote 30 Mo Salah alizocheza, na yeye alionekana kutota vilivyo, hiyo ilikiwa ni sababu ya kufanya vile, alitupia mkono kumvutia chini, akishajua amefanikiwa anajitoa, amemfanyia hivyo Mane pia.

Carvajal ana tatizo la ankle, alipopiga mpira kwa kisigino na kwa bahati mbaya akaguswa kidogo mguuni, ikawa ankle imetoneshwa, si jeraha jipya.
 
Wewe hujacheza mpira mahaba ya kuapia kuwa Liver lazima ashinde ndo yamekufikisha hapo, kwani Sarah ndo mchezaji wa kwanza kuumia katika fainali? Na katika hilo tukio unaona kabisa wote walikuwa wanagombania mpira Ramos akaucheza
Ronaldo mwenyewe aliumia fainali ya mataifa ulaya kwa rafu ya mtu na akatoka akilia ila maisha yaliendelea, hawa liver sijui vipi.
 
Ramos ni muhuni kama wahuni wengine wa Yombo,Manzese,TandAle au Keko.
 
Huyo Salah sio Malaika ni Mchezaji kama wengine, Rejea kuumia kwa Ronaldo Katika fainali ya Euro mwaka Jana.

Ukiwa uwanjani kuna kuumia sasa kama ulitaka wacheze kama wajawazito bila purukushani umefeli.
 
Huyo Salah sio Malaika ni Mchezaji kama wengine, Rejea kuumia kwa Ronaldo Katika fainali ya Euro mwaka Jana.

Ukiwa uwanjani kuna kuumia sasa kama ulitaka wacheze kama wajawazito bila purukushani umefeli.

Watu wameumizwa na Salah kuumia huenda sababu ya tabia zake za upole na uungwana ila wanasahau kuumia ni sehemu ya mpira wapo wachezaji kibao wanaokosa WC sababu ya kuumia uwanjani ila inashangaza hili na Ustadhi kupigiwa kelele kama ni kitu kigeni vile na wanasahau hata Carvajal nae aliumia ila hakuna anayepiga kelele.
 

Utakuwa na makengeza wewe

Hiyo hiyo tazama vizuri Ramos alivojigeuza hewa alipokuwa kwenye landing process

1 aliuvuta mkono wa sala

2. Akajibinuwa kuuvunja 100% akiwa na nusu nyingine ya mkono upande mwingine

Ukitaka kuelewa alifanya makisudi tazama alivojigeuza kuhama ambapo angedondokea akajirushia kufanya haribifu kwa sala
 
Madrid bingwa mkuu, mara ya 13 akimpiga Liver 3-1.
Hizi zingine ni visingizio tu, mpira wengine bado tunacheza ndondo mpaka leo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…