HOSEA 4:6 Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa.
Wewe hujui kuwa Tanzania inaongoza kwa mapenzi na ufisadi, ndo maana wazungu wakijaribu tu wanaingia mazima kabisa na kutangaza ndoa kwa dada zetu!! Uchumi uwe duni, elimu mbovu, umasikini uliokithiri alafu hadi kwenye idara ya mapenzi tuwe chini jaman...., ni ajabu lakini ni kweli! tumewekeza zaidi kwenye ufisadi na mapenzi pata picha aina ya taifa tulilonalo watanzania
nimeanza na east africa nikaja clouds nikahamia radio one nikaenda kiss fm, majic fm, passion, 100.5, capital... Zote hizi mida hii mapenzi tu. Hivi hakuna zaidi ya hili?
Hiyo inaitwa copy and paste. Wanafanya kuwa usiku ni ngono tu! Anyway sikiliza station za dini utapata burudiko la moyo wako. Bwana Yesu apewe sifa.
WAACHENI WAMWAGE SHULE...Wtz kutokana na uelewa mdogo kuhusu mapenzi tumekuwa tukiangukia kwenye soln. ya kale "kutoka nje" pindi itokeapo tofauti...hivyo kuligharimu taifa na janga la ukimwi...
nimeanza na east africa nikaja clouds nikahamia radio one nikaenda kiss fm, majic fm, passion, 100.5, capital... Zote hizi mida hii mapenzi tu. Hivi hakuna zaidi ya hili?
kuna tofauti ya mapenzi na ngono. Sema tunaongoza kwa ngono. Kwa ishu ya ufisadi inatia shaka maana tumechaguliwa kuwa wenyeji wa masuala ya kupambana na rushwa katika Afrika. 'Tuna nafuu' katika hilo
usiku wa saa ngapi..
Vipindi vya dini je? Hakuna redio zake?
Halafu rekebisha heading ya uzi... Sema karibu zoooote za FM!
Hata watoe masomo kama hayo wanafunzi wenyewe mida hiyo wanakuwa night club,kuhusu masomo wataingia na madesa tuu!!Afadhali waanzishe mihadhara ya masomo ya secondary schools k.m lkutoko EA radio leo usiku tutakuwa na somo la Biology kuanzia saa 6-8, historia kuanzia saa 8-9. Binadamu haishii kwa mapenzi na ngono tu. Redio nying sana lakini hazina kipya. Ukija TBR ndio bora liende VOT na CG FM zinaboa sana
Unafikiri ni wote wanaochaguliwa ni wasafi???unajua alowachangua aliangalia vigezo gani na how objective was she/he??