KERO Redio na TV Matangazo ya Kamari sasa hii hali imepitiliza

KERO Redio na TV Matangazo ya Kamari sasa hii hali imepitiliza

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Lethergo

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2023
Posts
6,534
Reaction score
11,421
Salamu Wakuu.

Niende moja kwa moja bila kuwachosha wala kuwapotezea muda.

Hili suala la Redio na Tv na kamari sasa ishakua kero yaani unakuta kipindi cha Redio au kipindi cha Televisheni Mtangazaji mwanzo mpaka mwisho hakuna anachotangaza chochote kipindi kimepewa Jina jingine ila kinachofanyika kwenye kipindi ni kingine, kwanini kipindi kisiitwe tu kamari ili watu waelewe kwamba hapa nimefungulia Redio nasikiliza kipindi cha kamari au nimefungulia Televisheni naangalia kamari? Kwanini isiwe hivyo?

Zamani kulikua na 'Jackpot Bingo' ilikua haimisiwi hivi ilikua na muda maalum na mtu ukiangalia unajua kabisa muda huu naangalia kamari.

Mamlaka zinazohusika basi angalieni namna ya kuweka hili jambo sawa, sasa tumechoka na hizi kamari yaani kipindi unasikiliza mwanzo mpaka mwisho ni kamari kamari kamari ooh huyu ameshinda laki 2 weka 1000 ushinde laki 2 ooh huyu ameshinda laki 5 weka 1000 ushinde laki 5 ooh huyu ameshinda million weka 1000 ushinde million, jamani tumechoka sio wote wacheza kamari.

Mamlaka zinazohusika Bodi ya Michezo ya kubahatisha na TCRA na wengineo ziwaambie wenye kuhusika na redio TV na wamiliki pamoja waendesha vipindi, vipindi vya kamari ni bora vibadirishwe majina na viwekewe muda wake maalum ili mtu ajue kabisa hapa ninasikiliza hiki kipindi nasikiliza kamari tu sio kipindi kinapewa jina jingine ila mwanzo mwisho mtu unasikiliza kamari tupu.
 
Unazungumzia Papaso na TBC hiki kinachoanza saa 4 usiku au kile kipindi cha asubuhi cha redio fulani fulani hapo mjini Dusalamu?
 
Hoja nzuri nakuunga mkono. Tatizo TCRA haijishuhulishi na maudhui yenye manufaa kwa wasikilizaji bali kujiingiza kwenye siasa ya kulinda CCM.. Taasisi zote za kiserikali na umma ni mikono ya chama fulani.
 
Hoja nzuri nakuunga mkono. Tatizo TCRA haijishuhulishi na maudhui yenye manufaa kwa wasikilizaji bali kujiingiza kwenye siasa ya kulinda CCM.. Taasisi zote za kiserikali na umma ni mikono ya chama fulani.
Kwa hio kamari ni mbinu za watawala changamsha bwege?
 
Kubeti kumegeuka ajira, Tuone wagombea watakao kemea hili piga kura yako vizuri.
Sio kwamba kubet kumekua ajira, kamari zimekuepo tangu na tangu ila sasa hivi kamari imepitiliza kiasi kwamba mtu unajua unaangalia televisheni kipindi cha maana kumbe unaangalia kamari au unasikiliza redio unajua ni kipindi cha maana kumbe unasikiliza kamari basi km ni hivyo vipindi vya namna hio viwepo sawa ila vipewe majina yao yanayohusu kamari tu sio kutuchanganyia humo kipindi kinaeleza jambo fulani humo humo mtangazaji anachanganya na mikamari hio hapana

Mamlaka zinazohusika waliangalie hili suala sio linaachwa tu km kipindi ni cha kamari basi kiwe ni cha kamari tupu watu wanaopenda kamari wataendelea nacho na kipewe jina la kikamari kamari na maudhui yake yawe ni ya kikamari kamari sio kipindi kinazungumzia masuala ya kijamii mambo ya afya na mengineyo
hujakaa sawa inapigishwa kamari humo humo aiseee tumechoka sasa
 
Kuna wadau uzi wanaupita huu uzi km wanaaga maiti uzi wa moto unachoma
 
Salamu Wakuu.

Niende moja kwa moja bila kuwachosha wala kuwapotezea muda.

Hili suala la Redio na Tv na kamari sasa ishakua kero yaani unakuta kipindi cha Redio au kipindi cha Televisheni Mtangazaji mwanzo mpaka mwisho hakuna anachotangaza chochote kipindi kimepewa Jina jingine ila kinachofanyika kwenye kipindi ni kingine, kwanini kipindi kisiitwe tu kamari ili watu waelewe kwamba hapa nimefungulia Redio nasikiliza kipindi cha kamari au nimefungulia Televisheni naangalia kamari? Kwanini isiwe hivyo?

Zamani kulikua na 'Jackpot Bingo' ilikua haimisiwi hivi ilikua na muda maalum na mtu ukiangalia unajua kabisa muda huu naangalia kamari.

Mamlaka zinazohusika basi angalieni namna ya kuweka hili jambo sawa, sasa tumechoka na hizi kamari yaani kipindi unasikiliza mwanzo mpaka mwisho ni kamari kamari kamari ooh huyu ameshinda laki 2 weka 1000 ushinde laki 2 ooh huyu ameshinda laki 5 weka 1000 ushinde laki 5 ooh huyu ameshinda million weka 1000 ushinde million, jamani tumechoka sio wote wacheza kamari.

Mamlaka zinazohusika Bodi ya Michezo ya kubahatisha na TCRA na wengineo ziwaambie wenye kuhusika na redio TV na wamiliki pamoja waendesha vipindi, vipindi vya kamari ni bora vibadirishwe majina na viwekewe muda wake maalum ili mtu ajue kabisa hapa ninasikiliza hiki kipindi nasikiliza kamari tu sio kipindi kinapewa jina jingine ila mwanzo mwisho mtu unasikiliza kamari tupu.
Kaka hao ndio wadhamin wa kipindi unachopenda kusikiliza na juwa hao pia wamwekeza katika kipindi ili kupata airtime pia juwa radio na tv bila wadhamin hakuna mahali wataweza kupata pesa ya kuendesha shuhuli zao na kulipa mishahara kwa wafanyakazi.
 
Kaka hao ndio wadhamin wa kipindi unachopenda kusikiliza na juwa hao pia wamwekeza katika kipindi ili kupata airtime pia juwa radio na tv bila wadhamin hakuna mahali wataweza kupata pesa ya kuendesha shuhuli zao na kulipa mishahara kwa wafanyakazi.
Vipindi vya redio na TV vipo kwa kipindi kirefu unaposema wadhamini sijakataa, nimeshauri kwamba vipindi visiwe vyote vinaingiziwa matangazo ya kamari kuwe na vipindi vinavyotambulishwa wazi kua hiki ni kipindi cha kamari, huwezi ukawa unazungumza masuala ya barabarani humo humo inapigishwa kamari kipindi kinaongelea masuala ya afya humo humo inapigishwa kamari, hapana hio sio sawa na haijakaa sawa vipindi vya kamari viwe na muda na vitambuliwe kua hiki kipindi kinahusu kamari tu na sio vinginevyo
 
Vipindi vya redio na TV vipo kwa kipindi kirefu unaposema wadhamini sijakataa, nimeshauri kwamba vipindi visiwe vyote vinaingiziwa matangazo ya kamari kuwe na vipindi vinavyotambulishwa wazi kua hiki ni kipindi cha kamari, huwezi ukawa unazungumza masuala ya barabarani humo humo inapigishwa kamari kipindi kinaongelea masuala ya afya humo humo inapigishwa kamari, hapana hio sio sawa na haijakaa sawa vipindi vya kamari viwe na muda na vitambuliwe kua hiki kipindi kinahusu kamari tu na sio vinn
Hao ni wadhamin ambao wamelipa kupromote aina ya biashara yao ambayo ni kamari ni sawa hata mdhamin mwingine nae akijitokeza. Au una shida na kamri kwa upande wako.
 
Hao ni wadhamin ambao wamelipa kupromote aina ya biashara yao ambayo ni kamari ni sawa hata mdhamin mwingine nae akijitokeza. Au una shida na kamri kwa upande wako.
Hivi unaelewa vizuri ninachozungumzia? Nazungumzia michezo ya kubahatisha yaan kamari hizi za tuma 1000 tuma 1000 acha hizo kamari za makampuni ya kubet kwa hio na hizi 1000 1000 pia ni wadhamini yaan kipindi kizima mtangazaji badala atangaze kipindi yeye kakomalia utume 1000 upate million, sijui unanielewa?
 
Hizi:
MCHONGO PESA
CHEZA PESA
PAKUA MKWANKA
PESA FASTA
N.K

YAAN UNASIKILIZA KIPINDI ILA WANATANGAZA HAYO MAMBO TU
 
Back
Top Bottom