Redio na TV zinaharibu Kiswahili: "Kumwambukiza" mtu upako au uwezo.

Redio na TV zinaharibu Kiswahili: "Kumwambukiza" mtu upako au uwezo.

Ambiente Guru

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2012
Posts
2,605
Reaction score
1,085
Nimesikia redio za hapa nchini (Mfano za Rev. Dk G. Rwakatare na Rev. Mtume Ephata) kutumia neno "Kumwambukiza" mtu uwezo au kipawa cha kufanya miujiza au upako. Je ni kiswahili sanifu?. Neno "kuambukiza" linatumika kwenye mambo chanya au hasi? TV na Redio watangazaji lafudhi zao zinapotosha kiswahili (ITV, Ch 10, ) mfano kusema; Malelia au marelia badala ya Malaria. Badala ya li wanaweka ri. Wanaweka msingi mbovu kwa watoto na wanaweza kuwafelisha mitihani.
 
Mijitu mingi ya bara ndiyo yenye tabia hiyo ya kuweka "R" badala ya "L", hii ni kutokana na kuathiliwa na lugha za makabila ya asili. Ni vema kabla ya kupew kaz ya utangazaj wapewe mafunzo ya kutamka maneno ya kiswahil kw ufasaha ili wasikichanganye
 
Wapuuzi sana, tena kama hawa radio presenters ndio zero kabisa, utaskia 'nyimbo hii ilipigwa kipindi hiko'
 
Mijitu mingi ya bara ndiyo yenye tabia hiyo ya kuweka "R" badala ya "L", hii ni kutokana na kuathiliwa na lugha za makabila ya asili. Ni vema kabla ya kupew kaz ya utangazaj wapewe mafunzo ya kutamka maneno ya kiswahil kw ufasaha ili wasikichanganye
Kwani weye mkuu ni JITU la wapi???
 
Mijitu mingi ya bara ndiyo yenye tabia hiyo ya kuweka "R" badala ya "L", hii ni kutokana na kuathiliwa na lugha za makabila ya asili. Ni vema kabla ya kupew kaz ya utangazaj wapewe mafunzo ya kutamka maneno ya kiswahil kw ufasaha ili wasikichanganye

Na wewe pia ni jitu la bara uliyeathirika na hizo 'L' na 'R'.
 
renyewe naro hiro rijamaa rijitu ra bala ila rinajifanya ra pwani kwa vile rinaishi tandare kwa bibi nyau!!
Mkuu hiri riajamaa ritakua rikazi ra MWANANYAMARA kwa bibi...Ira rikiwa nyuma ya keyboard rinajifanya la PWANI
 
Tunalipisha kundi zima la 2pac lituburudishe.
 
Back
Top Bottom