Relationship Between Parent and Child Vs Dod/Cat/Pet....!!!🙃

Relationship Between Parent and Child Vs Dod/Cat/Pet....!!!🙃

Kasie

Platinum Member
Joined
Dec 29, 2013
Posts
22,379
Reaction score
41,294
Hello Ladies and Gentlemen at MMU, it has been long time haven't had my pen and paper but today I have a piece to share and discuss if you won't bother neither mind....!!

Screenshot_2024-07-29-19-57-51-81_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg


The matter on the table is personal and it depends with culture and how one was raised...

NB allow me to mix language so as open wide discuss and receive different views 😊.

Kichwa cha mada ni mahusiano kati ya mzazi na watoto ukilinganisha mahusiano ya mzazi na wanyama kama mbwa paka na jamii ya wanyama wafugwao.

Dunia inaenda kasi sana, imefikia kipindi mtu anaona kuwa na mtoto wa kumzaa au wa kumlea ni kadhia na historia inatupa taswira.

Screenshot_2024-07-29-19-56-39-91_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg


Kuna wazazi walifanikiwa kupata watoto wa kuwazaa kuwalea watoto na mwisho wa siku watoto wakageuka kuwa mwiba kwa wazazi hao, kama ushawahi sikia jina la Mzee Kuzaa Si Kupata....

Kuna waliofikia umri wa kuwa na watoto ila sababu ya ugumu wa maisha wakaona bora wasizae ila bora wawe na mnyama wa kufugwa (paka/mbwa) walau awaondolee upweke.

Screenshot_2024-07-29-19-56-08-17_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg


Binafsi wakati nakua wazazi wangu walipenda mbwa, ila walikuwa wale mbwa wa kukaa banda la nje, marufuku kuingia ndani, ila tukiwa watoto tulicheza na mbwa na hata mtaani tulitoka nao na ilikuwa ubabe flani hivi hakuna wa kutuchokoza...

Taswira rejea hapo juu, baadhi ya matukio duniani wazazi kuuliwa na watoto wao ili warithi mali, wengine kutumia vibaya mali za wazazi na watoto wengine kutokuwa tuu na adabu, utii na heshima kwa wazazi wao kiasi mzazi anaona hivi ya nini nilizaa huyu kiumbe....!!

Majuto Mjukuu, wenzetu (ughaibuni) aidha kwa ugumu wa maisha, sharia zilizowekwa na nchi zao kuhusu matunzo ya mtoto wengine wao wanaona bora kutokuwa na mtoto na badala yake wanakuwa na mbwa wawili au watatu ambapo hao mbwa hawahitaji kupelekwa shule kufundishwa haki za mtoto na saa nyingine kumjibu mzazi atakavyo na kumuitia polisi ikiwezekana (mtoto anampandia mzazi kichwani) na mzazi akifanya fyokoo anapokonywa mtoto na serikali...!!! Balaa.....😌

Wengine wanaona mbwa/paka hatomjibu jeuri, hatokuwa na mawazo kuwa atabadili jinsia kutokana na demokrasia ya dunia n.k n.k.

Dunia inaenda kasi, mambo ni mengi, kuwa na watoto ni jambo nzuri, njema na la kumpendeza Mungu. Ila kulea hao watoto hata waweze kuwa binadamu si jambo jepesi, tumeshuhudia hayo kwa ndugu jamaa na marafiki.

Screenshot_2024-07-29-19-58-34-10_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg


Mbwa anawekewa bili ya msosi maalum, mbwa anatibiwa kila inapohitajika na ana Bima ya matibabu, mbwa analala ndani kwenye nyumba safi, anaogeshwa na kupanda gari la mzazi wake, mbwa anatoka outing na wengine wanapanda nao ndege kwenda safari zao au matembezi..

Screenshot_2024-07-29-19-59-09-70_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg


Kuna waliosema, heri kuzaliwa mbwa ulaya, kuliko.....

Si kuwa mtu wa hivyo amejidharau ama amekata tamaa....

Pengine ni ugumu wa maisha anaopitia wakati akipata taswira huduma anayopata mbwa/paka ulaya hizo hela hao wazazi si wanazichezea tuu... Ila kila mtu na maammuzi yake, ndo ule usemi, usimpangie mtu matumizi ya pesa zake.

Screenshot_2024-07-29-19-59-53-71_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12.jpg


Hili jambo limechukua nafasi kubwa sana mashariki ya mbali ukilinganisha na kwetu Afrika.
Wako wa Afrika wanaolea mbwa kama binadamu ila ni wa kuhesabu, huko kwa wenzetu unaweza sema kufuru.

Mbwa/paka ni mnyama rafiki sana kwa mwanadamu, hana baya, unafiki wala husuda au wivu.
Si watu wote wanapenda wanyama wa kufugwa ila dunia inakoelekea.... God knows.

Sina hadidu rejea yeyote kuthibitisha nilichoandika badala yake ni yale niliyoyaona na kushuhudia huku na kule nilikokuwa duniani...

Tembea Uone.....!!😉

Alamsiki.
 
Hello Ladies and Gentlemen at MMU, it has been long time haven't had my pen and paper but today I have a piece to share and discuss if you won't bother neither mind....!!

View attachment 3056524

The matter on the table is personal and it depends with culture and how one was raised...

NB allow me to mix language so as open wide discuss and receive different views [emoji4].

Kichwa cha mada ni mahusiano Katie ya mzazi na watoto ukilinganisha mahusiano ya mzazi na wanyama kama mbwa paka na kamili ya wanyama wafugwao.

Dunia inaenda kasi sana, imefikia kipindi mtu anaona kuwa na mtoto wa kumzaa au wa kumlea ni kadhia na historia inatupa taswira.

View attachment 3056519

Kuna wazazi walifanikiwa kupata watoto wa kuwazaa kuwalea watoto na mwisho wa siku watoto wakageuka kuwa mwiba kwa wazazi hao, kama ushawahi sikia jina la Mzee Kuzaa Si Kupata....

Kuna waliofikia umri wa kuwa na watoto ila sababu ya ugumu wa maisha wakaona bora wasizae ila bora waweza na mama wa kufugwa (paka/mbwa) wala u awaondoe upweke.

View attachment 3056516

Binafsi wakati nakuja wazazi wangu walioenda mbwa, ila walikuwa wale mbwa wa kukaa Banda la nje, marufuku kuingia ndani, ila tukiwa watoto tulicheza na mbwa na hata mtaani tulitoka nao na ilikuwa unable flani hivi hakuna wa kutuchokoza...

Taswira rejea hapo juu, baadhi ya matukio duniani wazazi kuuliwa na watoto wao ili warithi mali, wengine kutumia vibaya mali za wazazi na watoto wengine kutoka tuu na adabu, utii na heshima kwa wazazi wao kiasi mzazi anaona hivi ya nini nilizaa huyu kumbe....!!

Majuto Mjukuu, wenzetu (ughaibuni) aidha kwa ugumu wa maisha, sharia zilizowekwa na nchi zao kuhusu mafunzo ya mtoto wengine wao wanaona bora kutoka na mtoto na badala yake wanakula na mbwa wawili au watatu ambayo hao mbwa hawahitaji kupelekwa shule kufundishwa haki za mtoto na saa nyingine kumjibu mzazi atakavyo na kumuitia polisi ikiwezekana (mtoto anampandia mzazi kichwani) na mzazi akifanya fyokoo anapokonywa mtoto...!!!

Wengine wanaona mbwa/paka hatomjibu jeuri, hatokuwa na mawazo kuwa atabadili jinsia kutokana na demokrasia ya dunia n.k n.k.

Dunia inaenda kasi, mambo ni mengi, kuwa na watoto ni jambo nzuri, njema na la kumpendeza Mungu. Ila kumlea hao watoto hata waweza binadamu si jambo jepesi, tumeshuhudia hayo kwa ndugu jamaa na marafiki.

View attachment 3056528

Mbwa anawekewa nilikuwa ya mdosi maalum, mbwa anatibiwa kila inapohotajika na ana Bima ya matibabu, mbwa analala ndani kwenye nyumba safi, anaogeshwa na kupanda gari la mzazi wake, mbwa anatoka outing na wengine wanapanda nao ndege kwenda safari zao au matembezi..

View attachment 3056530

Kuna waliosema, heri kuzaliwa mbwa ulaya, kuliko.....

Si kuwa mtu wa hivyo amejidharau ama amekata tamaa....

Pengine ni ugumu wa maisha anaopitia wakati akipata taswira huduma anayopata mbwa/paka ulaya hizo hela hao wazazi si wanazichezea tuu... Ila kila mtu na maammuzi yake, ndo ile usemi, usimpangie mtu matumizi ya pesa zake.

View attachment 3056531

Hili jambo limechukua nafasi kubwa sana mashariki ya mbali ukilinganisha na kwetu Afrika.
Wako wa Afrika wanaolea mbwa kama binadamu ila ni wa kuhesabu, huko kwa wenzetu unaweza sema kufuru.

Mbwa/paka ni mnyama rafiki sana kwa mwanadamu, hana baya, unafiki wala husuda au wivu.
Si watu wote wanapanda wanyama wa kufugwa ila dunia inakoelekea.... God knows.

Sina hadidu rejea yeyote kuthibitisha nilichoandika badala yake ni yake niliyoyaona na kushihudia huku na kule nilikokuwa duniani...

Tembea Uone.....!![emoji6]

Alamsiki.
hii si ni asubuhi mbona unatupa alamsiki

Ama upo maandishi ma3 USA?
 
Yote ni ubinafsi wa mwanadamu, na pia mwanadamu kuwa mzito wa kupokea changamoto.
Akili ya mwanadamu kuna wakati inazidiwa na utashi wa hayawani!
Mwanadamu kadri anavyo pata upeo ndio anazidi kupoteza critical think akitaka kuacha asili yake na kupendelea maisha ya hayawani.

Hata hivyo uzazi utaendelea maadamu asili haitaacha asili yake.

Asante mleta mada , mada yako inatupa changamoto kujua tulipo tuendako baada kutazama tuliko toka.
 
Mkuu unazungumzia nini kuhusu wale watu wapweke au wajane ambao wanafanya ngono na wanyama kama mbwa, paka, mbuzi, farasi, punda, panya, n.k.
nilivyomuelewa anazungumzia sheria zilizowekwa kwa ajili ya kuwalinda watoto zinawafanya wawe na utovu wa nidhamu kwa wazazi wao

pia kuna kuzaa mtoto lakini kutokana na tabia zake ukajikuta unamuita litoto

Watu wanaona ya nini kuteseka bora nilee mbwa au lipaka ambao hawana dharau wala kiburi
 
nilivyomuelewa anazungumzia sheria zilizowekwa kwa ajili ya kuwalinda watoto zinawafanya wawe na utovu wa nidhamu kwa wazazi wao

pia kuna kuzaa mtoto lakini kutokana na tabia zake ukajikuta unamuita litoto

Watu wanaona ya nini kuteseka bora nilee mbwa au lipaka ambao hawana dharau wala kiburi
Ooooooh sawa hapo nimekusoma Sasa nimekuelewa lakini mtoto umleavyo ndivyo akuavyo

Inategemea mtoto wako amemlea kwa misingi gani
 
Yote ni ubinafsi wa mwanadamu, na pia mwanadamu kuwa mzito wa kupokea changamoto.
Akili ya mwanadamu kuna wakati inazidiwa na utashi wa hayawani!
Mwanadamu kadri anavyo pata upeo ndio anazidi kupoteza critical think akitaka kuacha asili yake na kupendelea maisha ya hayawani.

Hata hivyo uzazi utaendelea maadamu asili haitaacha asili yake.

Asante mleta mada , mada yako inatupa changamoto kujua tulipo tuendako baada kutazama tuliko toka.

Hii ndo ile wanasema, wanadamu wanaweka sheria za kuwahukumu/ kuwabana/ kuwakandamiza wanadamu wenyewe.

Zlamani au miaka kadhaa huko nyuma, kulea watoto ilikuwa jukumu la jamii, mtoto alionywa, aliadhibiwa na jamii na mzazi husika anapata taarifa ya kilichoendelea.

Ila siku/ miaka kadhaa baadae mtoto ni wa mzazi husika, hata afanye kosa gani jamii inamtizama tuu haishiriki tena kurekebisha tabia. Hii imeleta athari kubwa sababu si muda wote mzazi husika anakuwa na mtoto wake kumfunza inavyopaswa kuwa.

Mbaya zaidi, jamii yenyewe imekuwa chanzo cha kufundisha mabaya kwa watoto wasiokuwa na uangalifu yakinifu kutoka kwa wazazi wao.

Malezi yamekuwa tabu, kuepuka lawama wengine wameona isiwe tabu hazai mtoto kabisa. Zamani watu walikuwa wakizaa wanawaachia bibi na babu walee mjukuu, sikuhizi bibi na babu wanaenda vacations kula pension zao, na watoto wamekuwa wakaidi hawawatii babu na bibi basi tafrani tupu.

Kila mtu na lwake, ila asili ya familia inapigwa vita mbaya sana...
 
nilivyomuelewa anazungumzia sheria zilizowekwa kwa ajili ya kuwalinda watoto zinawafanya wawe na utovu wa nidhamu kwa wazazi wao

pia kuna kuzaa mtoto lakini kutokana na tabia zake ukajikuta unamuita litoto

Watu wanaona ya nini kuteseka bora nilee mbwa au lipaka ambao hawana dharau wala kiburi
Yeah imekuwa tafrani haswa...
 
Back
Top Bottom