Mkiambiwa haya mapambano yanatengenezwa watu wanasema sisi waswahiliKabla mashabiki hawaja poa wanatangaza rematch wacha wapige pesa
Kwani kibonge ikitokea kapigwa naye si atakuwa ataharibu rekodiHaina maana tayari kashaharibu rekodi yake tayari
Hyo rematch ikiwa haina siasa Joshua anaanguka kwa mara ya pili
Chibonge alitishaInabidi ajipange haswa bila hivyo atachezea tena kichapo kwa tumbo tumbo ataanza kutakiwa na mabondia wakawaida wa uzito wake ila wasio na mafanikio wakaoshe nyota.
Hata Mfaume mfaume anamtaka AJ
Kibonge yuko fiti sana! Aj tatizo ni mkata pumzi mapema.marudiano atapigwa tena.andy yupo vizuri ,sikuwahi kumjua kabla,baada ya kumbonda AJ ndio nikaingia chimbo kuangalia mapambano yake yaliyopita.yuko safi kiufundi aisee,sina shaka nae na nina hakika hajabahatisha.Andy Ruiz Jr aka Destroyer nyota inazidi kung'ara upande wake.
Pambano la juzi dhidi ya Anthony Joshua lilikuwa ni pambano lilimwingizia kipato mara 10 ya ambacho amewahi kukipata.
Ameingiza takribani USD 5 Mil kwenye hilo pambano, wakati kiasi kikubwa alichowahi kupata ni USD 500,000.
Rematch inapangwa kwamba atapata USD si chini ya 10 Mil. Ukiacha add ons.
Tipwa Tipwa anairudisha Boxing kwenye ramani, mimi binafsi nilipunguza kuangalia boxing kwa sababu imepoteza mvuto, watu wanajilinda na kukwepa zaidi ya punching, ila Tipwa Tipwa kanionyesha radha ambayo sikuiona wakati Mayweather anapigana na Manny Pacq, Joshua vs Klitchko, Wilder vs Fury, etc etc.
Na kitendo cha kumshinda Joshua, ukilinganisha na body buildups zao, records na odds walizopewa, Randy kafurahisha watu wengi sana.
Namwombea pambano lake la kurudiana ashinde.
Kuna watu tulikuwa tunasema kwamba Joshua hajawahi kukutana na real tests, na muda wote kambi yake walikuwa wanakwepesha kumpa mapambano yenye uzito, lakini katokea Randy katuthibitishia.
Ama kweli, kurukaruka siyo dawa ya ulimbo.
Kibonge yuko fiti sana! Aj tatizo ni mkata pumzi mapema.marudiano atapigwa tena.andy yupo vizuri ,sikuwahi kumjua kabla,baada ya kumbonda AJ ndio nikaingia chimbo kuangalia mapambano yake yaliyopita.yuko safi kiufundi aisee,sina shaka nae na nina hakika hajabahatisha.
Mi nilisema joshua hii mechi kauza ili apate rematch apige mpunga zaidi