BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Utafiti wa Taasisi ya Utafiti REPOA unaonesha Watanzania wana hofu ya kukosa huduma muhimu za kijamii endapo watamchagua kiongozi yeyote kutoka vyama vya upinzani.
Utafiti huo umeonesha kuwa asilimia 88 ya wananchi waliohojiwa walisema hawapo tayari kuandamana kuishinikiza Serikali kuwapatia huduma, huku asilimia 77 wakisema njia watakayoitumia ni kuwasilisha kero zao kwa viongozi wa Serikali za mitaa yao.
Hata hivyo, Mtafiti Mwandamizi wa Repoa, Dk Hubert Shija alisema walibaini kati ya watu wanne, watatu hupendelea kuwa karibu na mtu wa chama kingine cha upinzani lakini mtu mmoja kati ya wanne hajali lolote.
Asilimia 96 ya wananchi wanaamini utoaji wa huduma bora ni jukumu la Serikali na hawaoni muunganiko wa ulipaji wa kodi kubwa na kupata huduma.
Wananchi hao walisema kukiwa na ufanisi wa utoaji huduma na kuwashirikisha viongozi wa kisiasa utoaji wa huduma utakuwa mzuri.
Utafiti huo umeonesha kuwa asilimia 88 ya wananchi waliohojiwa walisema hawapo tayari kuandamana kuishinikiza Serikali kuwapatia huduma, huku asilimia 77 wakisema njia watakayoitumia ni kuwasilisha kero zao kwa viongozi wa Serikali za mitaa yao.
Hata hivyo, Mtafiti Mwandamizi wa Repoa, Dk Hubert Shija alisema walibaini kati ya watu wanne, watatu hupendelea kuwa karibu na mtu wa chama kingine cha upinzani lakini mtu mmoja kati ya wanne hajali lolote.
Asilimia 96 ya wananchi wanaamini utoaji wa huduma bora ni jukumu la Serikali na hawaoni muunganiko wa ulipaji wa kodi kubwa na kupata huduma.
Wananchi hao walisema kukiwa na ufanisi wa utoaji huduma na kuwashirikisha viongozi wa kisiasa utoaji wa huduma utakuwa mzuri.