RingaRinga
JF-Expert Member
- Jul 10, 2015
- 1,047
- 521
Lile kusanyiko Kubwa la aina yake lililowahi kutokea nchini mwanzoni mwa utawala wa B.W. Mkapa June 1996 (miaka 20 iliyopita) leo lipo mjini Mwanza ambapo mwinjilisti wa kimataifa R. Bonnke atalitikisa jiji la miamba al maarufu Rock City kwa mahubiri yake ambayo huwavuta wengi.
Kusanyiko hili huvutia watu wengi wengine kutoka mikoa ya jirani ambapo pamoja na wengi kuja kushuhudia mahubiri wengine huvutiwa kushuhudia maandalizi makubwa ambayo hufanywa kufanikisha kutaniko hilo.
Matumizi ya teknolojia za kisasa na ghali ambazo huchukua muda wa kutosha kufungwa katika viwanja vya Furahisha, promo za kutosha kupitia vyombo vya habari na mapokezi makubwa ambayo hupewa mhubiri huyu naamini vitasababisha viwanja vya furahisha kutapika.
Mliokuwepo na kushuhudia mkutano wa 1996 mnakumbuka nini?
Mkutano huu utaacha gumzo kama la 1996 lililochukua muda kusahaulika?
Tuendelee kupeana updates za yale yanayoendelea hapo jijini na eneo la mkutano, picha mbalimbali zitanogesha zaidi habari hii.
Nipo nje ya jiji.
SAHIHISHO:
CfaN ambao ndio wasimamizi wa mahubiri haya wamemleta Daniel Kolenda na si Reinhard Bonnke
Kusanyiko hili huvutia watu wengi wengine kutoka mikoa ya jirani ambapo pamoja na wengi kuja kushuhudia mahubiri wengine huvutiwa kushuhudia maandalizi makubwa ambayo hufanywa kufanikisha kutaniko hilo.
Matumizi ya teknolojia za kisasa na ghali ambazo huchukua muda wa kutosha kufungwa katika viwanja vya Furahisha, promo za kutosha kupitia vyombo vya habari na mapokezi makubwa ambayo hupewa mhubiri huyu naamini vitasababisha viwanja vya furahisha kutapika.
Mliokuwepo na kushuhudia mkutano wa 1996 mnakumbuka nini?
Mkutano huu utaacha gumzo kama la 1996 lililochukua muda kusahaulika?
Tuendelee kupeana updates za yale yanayoendelea hapo jijini na eneo la mkutano, picha mbalimbali zitanogesha zaidi habari hii.
Nipo nje ya jiji.
SAHIHISHO:
CfaN ambao ndio wasimamizi wa mahubiri haya wamemleta Daniel Kolenda na si Reinhard Bonnke