Nyie wana CHA DEMU mbona mnafikiri sana katika kuibiwa kwa kura na si kujiamini katika ushindi???? Unajua mfa maji haachi kutapatapa... Kama kweli CHA DEMU ina uhakika wa kushinda uchaguzi mkuu hiyo 31 October, basi na isubiri matokeo na si kushupalia kuibiwa kwa kura.
Swali langu ni kwamba... Hivi kigezo cha kujua mtu anakubalika ni nini? wingi wa mkusanyiko wa watu ktk mhadhara? Kusoma sana JF na kutuma hoja? au ni nini? Tusiwe wachochezi wa mambo yasiyo na msingi na kupata kisingizio cha kuhatarisha amani ya nchi yetu hapo baadae.
Sipendi nasema sipendi kuona visingizio vya kutaka kuleta fujo na uvunjifu wa amani.
Nawakilisha Oktoba 31