Revolution strategy: Kutoka kuchagua viongozi wa wanyonge hadi kumaliza unyonge wenyewe

Revolution strategy: Kutoka kuchagua viongozi wa wanyonge hadi kumaliza unyonge wenyewe

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,186
Reaction score
7,492
1594184335742.png
Ukosoaji wa watungaji na wasimamiaji wa sera ni jambo jema kwa kuwa huwasaidia wahusika kujitathmini na kujisahihisha. Kuwasifu na kuwapongeza ni jambo jema pia kwa kuwa huwatia moyo. Hata hivyo, jambo muhimu zaidi ambalo ndilo husaidia kutupeleka mbele zaidi kama taifa ni kufikiri ni namna gani bora zaidi ya kutatua matatizo sugu yanayotukabili.

Mara zote katika kipindi cha uchaguzi kama hiki, tumekuwa tukijadili nani ni ‘kiongozi wa wanyonge’. Ijapokuwa ni kweli kwamba jamii yetu ina ‘wanyonge’ wengi, lakini kwa kuwa unyonge sio sifa ya kujivunia; badala ya kujadili nani ni ‘kiongozi wa wanyonge’, ni vyema kujadili jamii yetu inatokaje kwenye unyonge.

Unyonge unasababishwa na matatizo sugu yanayoisumbua jamii yetu. Aidha, ni wazi kuwa tatizo sugu kupita yote kwa sasa ni ukosefu wa ajira kwa vijana na tatizo hilo linatarajiwa kukua siku hadi siku na hatimae kufikia kiwango kisichoelezeka. Kwa mantiki hiyo, tunaweza kusema wanyonge namba1, ni vijana wasio na kazi na hivyo kutoingiza kipato.Suala hili lisipoangaliwa kwa umakini wa ziada, huenda badae likazua janga kubwa la kiuchumi, kijamii na kiusalama pia.

Tatizo hili linasababishwa na mambo makuu mawili. Kwanza mfumo wa elimu unaoua vipaji na kumfundisha mtoto vitu ambavyo havifanyi kazi kwenye maisha ya kawaida hivyo elimu kutomsaidia kijana kuwa na uwezo wa kukabiliana na mazingira yake na pili ukosefu wa mitaji unaosababisha kijana kushindwa kujiajiri.

Wakati tuna durusu muelekeo wa kisera 2020-2025-2030; ni muhimu kufanya mapinduzi ya kisera na kimuelekeo kulenga kutatua changamoto tajwa hapo juu ili tutoke kwenye kile kiitwacho ‘Unyonge’.Tunaweza kuangalia uwezekano wa kufanya yafuatayo;-

  • Elimu ya msingi ibaki kama ilivyo ili kumuwezesha kila mtoto kujua mambo ya msingi kwa mhutasari,

  • Kuanzia ngazi ya sekondari, watoto wachague masomo kama matatu tu wanayopenda wenyewe (kwa ushauri wa waalimu wao) ili waweze kuyamudu vizuri. Ikumbukwe kwamba imethibitika kisayansi kwamba ili mtu afanikiwe kimaisha, hapaswi kufahamu kila kitu bali anatakiwa ku ‘master ‘ maeneo machache.

  • Kuanzia kidato cha kwanza (pamoja na masomo matatu aliyochagua hapo juu) kila mtoto aruhusiwe kuchagua fani 2 anazopenda na anahisi anazimudu na aanze kuzifanyia kazi kwa ubinifu wake binafsi. Kazi ya mwalimu itakuwa ni ‘coaching’ kwa mtoto na sio kumfundisha kwa sababu mtoto atakuwa ana uelewa na mapenzi zaidi kwenye fani hizo kuliko mwalimu, Hivyo akiwa 'coached' kwenye anachokipenda na kukimudu, anaweza kufanya maajabu.

  • Siku ya mtihani, (kwenye fani husika)mwanafunzi atapimwa kutokana na mwenendo wake kwa kipindi chote ambacho amekuwa ‘coached’. Aidha, mwanafunzi anaweza kujitungia mtihani wake mwenyewe kwenye fani ambazo amekuwa anazifanyia kazi, na jopo linatathmini uwezo wa mtoto kutatua matatizo aliyochagua kutatua.

  • Ikifika kwenye level ya kwenda kwenye vyuo vikuu, wakati wachache wakipewa mikopo waende vyuo vikuu, wengi watapewa mikopo wakatekeleze miradi yao ambayo tayari wameshajenga umahiri kwayo. Aidha, wataendelea kuwa ‘coached’ na wataalam kwa miaka kadhaa kabla ya kusimama wenyewe.
Tukifanya hivyo, tutatatua tatizo la ukosefu wa ajira, tutaibua na kukuza vipaji, tutahamashisha ubunifu, tutapunguza tatizo la mikopo isiyo na matokeo, elimu zisizo na manufaa na kuzalisha wanafunzi wanaoitwa wasomi ila hawawezi kutumia elimu yao kukabiliana na mazingira ispokuwa kuajiriwa ajira ambazo hazipo na tutapiga hatua ambayo itaishangaza dunia.

Kinyume chake tukiendelea na mfumo huu wa elimu za vijana wote wanapiga madesa, kukariri, kupata vyeti, kukariri wakoloni walivyotupiga na kutunyanyasa, tulivyofanywa watumwa na kisha vijana kusubiria ajira ambazo kimsingi hazipo; tutakuwa hatujitendei haki, hatutendei haki nchi yetu, na hatutendei haki vizazi vijavyo.

Aidha, Tukichagua kuendelea na mfumo kama ulivyo, pamoja na athari tajwa hapo juu, tutakuwa tumeamua kuendelea kuwapa ‘mabeberu wa ubeberuni’ nafasi za kutuonesha kazi. Nadhani ni vyema tukalitafakari suala hili na kuona namna ya kufanya mapinduzi makubwa yatakayofuta hili jina la ‘wanyonge’ na kuingia kwenye level nyingine.
 
Hiyo syllabus inafuatwa na nchi gani?

Pili watoto wengi watakwambia Mimi ninataka ķuwa Dr au pilot , hivyo utataarisha wengi kwenye hiyo fani?
Na nini itakuwa catalyst ya yeye kufanya vizuri? Utashi wake wa kutaka kuwa Dr au Pilot au Mwalimu au Fundi au ushindani na wanafunzi wenzie ndio utamfanya afanye vizuri.

Katika Maisha kuna vichocheo vingi.
 
Kwa maoni yangu, kujadili siasa za madaraka, yaani nani anagombea nini au nani awe nani ni sawa, lakini tunatakiwa kuwa makini kuepuka kujadili sura za watu badala ya mawazo. Hakuna namna tunaweza kupata suluhu ya matatizo sugu bila kuboresha aina ya mawazo tuliyonayo juu ya mazingira yetu na matatizo yanayoikabili jamii.

Kwa mantiki hiyo ni muhimu zaidi kuwekeza muda, akili na rasilimali nyingine kujadili na kuchambua ni wazo lipi linatatua tatizo lipi kwa namna bora zaidi. Vinginevyo bado tutakuwa tunachelewa sana kufikia Tanzania tuitakayo.

Albert Einstein aliwahi kututanabaisha kuwa, tatizo haliwezi kutatuliwa na mawazo yaliyolitengeneza. Kama tutakubaliana kwamba tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana kweli lipo, na mfumo wa elimu haujengi uwezo wa kutosha kwa wahitimu kutumia ujuzi waliopata shuleni kujiajiri, lakini pia vijana hao hawana mtaji wa kuanzisha miradi licha ya serikali kuwakopesha mamilioni ya pesa; ni muhimu sasa kuangalia ni maeneo gani tunatakiwa kufikiri kwa level inayofuata ili kubadilisha aina ya matokeo tunayopata.
 
Tuondokane na CCM sasa imekuwa aibu kuwa na chama madarakani kwa miaka 60.
 
Hiyo syllabus inafuatwa na nchi gani?

Pili watoto wengi watakwambia Mimi ninataka ķuwa Dr au pilot , hivyo utataarisha wengi kwenye hiyo fani ???
Na nini itakuwa catalyst ya yeye kufanya vizuri ?? Utashi wake wa kutaka kuwa Dr au Pilot au Mwalimu au Fundi au ushindani na wanafunzi wenzie ndio utamfanya afanye vizuri .

Ktk Maisha kuna vichocheo vingi
Mkuu umeibua hoja za msingi. Labda tukuulize wewe ushauri wako ni nini sasa? Je! unakubali kuna tatizo la ukosefu wa ajira na linaongeka? unakubali kuwa mfumo wa elimu hauwezeshi vijana kujiajiri na kuingiza elimu hiyo kwenye matendo labda waajiriwe na nafasi za kuajiriwa ni chache sana? unakubaliana kuwa wanaotakiwa wajiajiri hawana mtaji na hawawezi kupata mtaji mpaka pawe na 'external force'? tunafanyaje sasa? Unaamini maono ya kisiasa yanayotoa muelekeo wa kisera yanaweza kusaidia kitu?

Umetoa mfano wa udaktari na urubani. Kuna aina ya fani ni lazima kusoma darasani. kwa watakaochagua fani husuka watasoma darasani lakini kwa kuspecialize kutokea mapema kabisa kwa mfano udaktari. Lakini ushangae sasa, huo udaktari wenyewe mfano kwenye korona tumerudi kwenye tiba asili na zimesaidia kwa kiasi flani. Waliozibuni walisoma kwa utaratibu gani? Urubani kwa mfano uliousema, hivi unajua urubani ni kama udereva? unahitaji zaidi 'skills' na sio 'academics' yaani la saba anaweza kuwa dereva mzuri kuliko PhD holder?

Mwisho wa siku, ili tuweze kufanikiwa kama taifa, tunatakiwa kujifunza kufanya vitu vyetu sisi kama sisi na sio kuiga wengine. Hakuna namna tunaweza kufanikiwa kwa kufuata mkumbo, tujifunze kwa wengine lakini tufanye kivyetu na kwa ubunifu wetu wenyewe.
 
Tuondokane na ccm sasa imekuwa aibu kuwa na chama madarakani kwa miaka 60.
Mkuu hebu fafanua zaidi kidogo na wengine waelewe kwamba kuondoka kwa CCM kutasaidiaje kutatua tatizo la msingi linazungumziwa hapa?
 
Mkuu hebu fafanua zaidi kidogo na wengine waelewe kwamba kuondoka kwa CCM kutasaidiaje kutatua tatizo la msingi linazungumziwa hapa?
CCM ni mfumo wa zamani tangu ilipoundwa TANU mwaka 1954. Mfumo huu ulikuwa na lengo la kupata uhuru kutoka kwa wakoloni. Waliopo kwenye mfumo huu bado wana mawazo ya kizamani na sio creative. Mfano tu, tangu uhuru kilimo cha Tanzania kimebakia kile kile cha jembe la mkono. Hatuwezi kuendelea bila kuachana na mifumo ya zamani. Hakuna kosa kubwa kama analofanya jiwe kuua upinzani.
 
Ccm ni mfumo wa zamani tangu ilipoundwa TANU mwaka 1954. Mfumo huu ulikuwa na lengo la kupata uhuru kutoka kwa wakoloni. Waliopo kwenye mfumo huu bado wana mawazo ya kizamani na sio creative. Mfano tu, tangu uhuru kilimo cha Tanzania kimebakia kile kile cha jembe la mkono. Hatuwezi kuendelea bila kuachana na mifumo ya zamani. Hakuna kosa kubwa kama analofanya jiwe kuua upinzani.
Sasa mkuu, hebu tuje na hayo mawazo mapya halafu wayachukue na kuachana na mawazo ya kizamani kama unavyosema, au wayachukue chama chochote kile. Ni muhimu kuelewa kwamba ishu si nani anaendesha gari, ishu anayeendesha anaendeshaje na kuelekea wapi na alitakiwa aendesheje kama mbadala. Kufikiri kuwa sura ya mwendeshaji ndio huamua namna ya kuendesha na muelekeo ni matokeo ya athari ya mfumo wa elimu tunaouzungumizia miongoni mwa mambo mengine.

Kwa mfano umetoa mfano wa kilimo cha mkono na kilimo cha trekta, nijuavyo mimi kilimo ni suala la mtu binafsi na shamba lake, kwa hiyo ukiona mtu analima na mkono maana yake hana mtaji wa kutumia trekta, au sio? hapa wewe ungekuwa ndio CCM na unafanya maamuzi unafanya nini? ili kama wazo lako zuri wengine waliige na kulifanyia kazi kuboresha hali ya mambo!

Mathalan kuhusu hili la ukosefu wa ajira kwa vijana na changamoto ya mifumo ya elimu, unadhani nini cha kuboresha au kurekebisha bila kujali anayeboresha ni nani?

Kwa maoni yangu hili jibu la 'Tatizo CCM' ni jibu ya juu juu sana au tunaweza kusema ni jibu rahisi kwa maswali magumu linalolenga kujifariji na kujiepusha kufikiri ili kustarehesha nafsi. Matokeo yake wanaofikiri hili ndilo jibu la matatizo yote, wanajikuta hawachangii kutatua tatizo lolote kwenye jamii zaidi ya kulalamika.
 
Sasa mkuu, hebu tuje na hayo mawazo mapya halafu wayachukue na kuachana na mawazo ya kizamani kama unavyosema, au wayachukue chama chochote kile. Ni muhimu kuelewa kwamba ishu si nani anaendesha gari, ishu anayeendesha anaendeshaje na kuelekea wapi na alitakiwa aendesheje kama mbadala. Kufikiri kuwa sura ya mwendeshaji ndio huamua namna ya kuendesha na muelekeo ni matokeo ya athari ya mfumo wa elimu tunaouzungumizia miongoni mwa mambo mengine.

Kwa mfano umetoa mfano wa kilimo cha mkono na kilimo cha trekta, nijuavyo mimi kilimo ni suala la mtu binafsi na shamba lake, kwa hiyo ukiona mtu analima na mkono maana yake hana mtaji wa kutumia trekta, au sio? hapa wewe ungekuwa ndio CCM na unafanya maamuzi unafanya nini? ili kama wazo lako zuri wengine waliige na kulifanyia kazi kuboresha hali ya mambo!

Madhalan kuhusu hili la ukosefu wa ajira kwa vijana na changamoto ya mifumo ya elimu, unadhani nini cha kuboresha au kurekebisha bila kujali anayeboresha ni nani?
Ndio maana ccm itakaa madarakani miaka mingi ijayo kwani watanzania wengi akili zao ni kama zako. Mataifa yenye akili hubadilisha vyama kila miaka 4-8, rejea Uingereza, marekani,nk. Yale mataifa maskini ndio huweka chama kimoja miaka 50. Watanzania bado uelewa mdogo sana.
 
Ndio maana ccm itakaa madarakani miaka mingi ijayo kwani watanzania wengi akili zao ni kama zako. Mataifa yenye akili hubadilisha vyama kila miaka 4-8, rejea Uingereza, marekani,nk. Yale mataifa maskini ndio huweka chama kimoja miaka 50. Watanzania bado uelewa mdogo sana.
Mkuu, kwa mfano malawi imekuwa ikibadili vyama mara kadhaa, ina maendeleo zaidi ukilinganisha na nchi nyingine za afrika? zambia je? vipi Libya ya Gadafi?

Any way labda nikupe mfano ulionyooka, China kuna chama kimoja miaka yote lakini ni Nchi ya 2 au ya 1 kwa uchumi imara duniani, unaweza kusemaje kuhusu hili?

Kwa maoni yangu, kinacholeta mafanikio yoyote ni mawazo, mitizamo na nidhamu. Vitu hivyo vikiwa bora, kwa kubadilisha vyama au bila kubadilisha vyama mafanikio ya maana hutokea na vikikosekana, kwa kubadilisha au kutobadilisha vyama, hakuna cha kipekee sana kitakachotokea. Wewe unalionaje hili?
 
solution ni elimu ya ufundi stadi( VETA) ipewe kipaumbele, kuliko elimu ya kukariri inayotolewa vyuo vikuu
Mkuu umeongea point muhimu sana, lakini hata sasa VETA ipo lakini bado tatizo la msingi liko pale pale.

Nikupe mfano wa tofauti kidogo, hivi unajua mtu aliyeishia la saba kisha akajifunza kilimo kimtaa mtaa anaweza kuwa na matokeo bora kuliko mwenye shahada ya kilimo? kumbuka ili elimu iwe na maana inatakiwa isaidie kuboresha matokeo na kama haisaidii kuboresha matokeo ni tatizo kubwa.

Sasa unajua kwa mfano darasa la 7 na mwenye shahada wanaweza kupewa mwaka mmoja, kila mmoja akapambane shambani kwa mbinu ajuazo yeye aje na matokeo, hatimaye la 7 akaja na gunia 100, wa shahada akaja na gunia 0? hii maana yake nini, na kisera nini cha kufanya ili kuhakikisha tunatumia rasilimali zetu kwa faida na sio kwa mazoea?
 
Kwa mfano mkuu Laki Si Pesa, wote tunakubaliana kuwa kilimo ni sekta ya kipaumbele Tanzania. Lakini sasa mjadala unakuja kwamba je! ili kuendeleza hicho kilimo, tunahitaji wahitimu wengi wa elimu za juu, au tunahitaji zaidi elimu ya field, ubunifu na mitaji? Kwa maoni yangu ili kupunguza idadi ya wanyonge tunahitaji zaidi hiki cha pili na kama hivyo ndivyo, mapendekezo kwenye mada ya msingi yanabakia kuwa muhimu.

Vinginevyo, tunaweza kuwa na darasa la saba ambaye anazalisha gunia 100 za mazao kila mwaka kwa miaka 15 hivyo si mnyonge, na muhitimu wa shahada ambaye muda wotewa miaka 15 alikuwa darasani, hajaajiriwa maana nafasi chache, anadaiwa mkopo wa kusomea milioni 20, na hawezi kulipa maana hana kipato, mfukoni hana hata shilingi, na miaka 15 ametumia darasani. Hapo nani mnyonge kati ya hao wawili?

Kwa hiyo ni katika mazingira kama hayo tunashauri umuhimu wa kudurusu sera kwa utulivu zaidi hasa katika vipindi hivi vya uchaguzi.
 
Free Mdude 2020 Mwaga Pombe
Moja ya vitu vinavyoshangaza ni kwamba inapokuja mijadala ya kisera kama hii, wanaodai ni vyama mbadala wanakuwa hawana mawazo mbadala yoyote. Wao ni kuitaja taja CCM randomly tu. Ndio maana sisi wengine pamoja na kuwa tunaamini kuwa demokrasia na uwepo wa vyama vingi ni muhimu; tunaona pia kuwa aina ya vyama mbadala vilivyopo Tanzania kwa kiwango kikubwa havina tumaini lolote la maana na huo ni udhaifu mkubwa. Kwa bahati mbaya hawatambui kama wana tatizo , hivyo hawaoneshi kuwa na mpango wa kujirekebisha. Ni katika mazingira hayo watu huamua kuupuuza, sio kwa sababu dhana ya demokrasia ya vyama vingi ni mbaya, bali aina ya vyama mbadala tuliyo nayo.
 
Moja ya vitu vinavyoshangaza ni kwamba inapokuja mijadala ya kisera kama hii, wanaodai ni vyama mbadala wanakuwa hawana mawazo mbadala yoyote. Wao ni kuitaja taja CCM randomly tu. Ndio maana sisi wengine pamoja na kuwa tunaamini kuwa demokrasia na uwepo wa vyama vingi ni muhimu; tunaona pia kuwa aina ya vyama mbadala vilivyopo Tanzania kwa kiwango kikubwa havina tumaini lolote la maana na huo ni udhaifu mkubwa. Kwa bahati mbaya hawatambui kama wana tatizo , hivyo hawaoneshi kuwa na mpango wa kujirekebisha. Ni katika mazingira hayo watu huamua kuupuuza, sio kwa sababu dhana ya demokrasia ya vyama vingi ni mbaya, bali aina ya vyama mbadala tuliyo nayo.


Ueleweki
 
Tatizo la ajira halimalizwi simply kwa wengi kukimbilia kwenye kilimo, hasa baada ya kuwezeshwa vitu kama mbolea na mitaji. Lazima tujue baada ya kuvuna hayo mazao yatapelekwa wapi? je, yatakuwa na ubora wa kuuza nje? hapa niseme ndio kwasababu wengi watakuwa walishapata elimu hivyo watajua nini wafanye ili wapate mazao mengi, lakini pia sio rahisi kuuza mazao yote nje kutokana na ushindani toka kwa mataifa mengine.

Lakini ukumbuke, wengi wakiwekeza kwenye kilimo mwisho wa siku mazao yao yanaweza kuwa mengi hivyo waishie kuyauza kwa bei ya hasara na hicho kilimo kisiwasaidie hivyo dhana nzima ya kilimo kama chanzo cha ajira kupoteza maana.

Kwangu sekta ya kilimo inaendana moja kwa moja na sekta ya viwanda, huu ndio utakuwa muda muafaka wa kufufua viwanda kwaasababu moja, raw materials zitapatikana kwa wingi toka kwenye kilimo, na pili, viwanda navyo vina nafasi kubwa sana ya kuajiri watu wengi kwa wakati mmoja hivyo vitasaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza tatizo la ajira hapa nchini.

Ninachojaribu kusema hapa ni kwamba, hizi sekta mbili, ya kilimo na viwanda, zinafanya kazi kwa kutegemeana kwa kiasi kikubwa. Hivyo wakati tukiwekeza nguvu nyingi kwenye kilimo, basi tusiisahau na sekta ya viwanda kutokana na umuhimu wake kwenye suala la ajira kwa ujumla. Hivyo wakati unafikiria kufufua sekta ya kilimo, na sekta ya viwanda lazima ifufuliwe kwa wakati huo huo ili kuchukua kile kitakachotoka mashambani kwa wakati.
 
Mkuu, kwa mfano malawi imekuwa ikibadili vyama mara kadhaa, ina maendeleo zaidi ukilinganisha na nchi nyingine za afrika? zambia je? vipi Libya ya Gadafi?

Any way labda nikupe mfano ulionyooka, China kuna chama kimoja miaka yote lakini ni Nchi ya 2 au ya 1 kwa uchumi imara duniani, unaweza kusemaje kuhusu hili?

Kwa maoni yangu, kinacholeta mafanikio yoyote ni mawazo, mitizamo na nidhamu. Vitu hivyo vikiwa bora, kwa kubadilisha vyama au bila kubadilisha vyama mafanikio ya maana hutokea na vikikosekana, kwa kubadilisha au kutobadilisha vyama, hakuna cha kipekee sana kitakachotokea. Wewe unalionaje hili?
Malawi wamepiga hatua kubwa na kuna uhuru na demokrasia sana kuliko Tanzania, haya ni maendeleo. Malawi siku hizi wana production kubwa ya sukari kumbuka tumenunua sukari kutoka kwao pamoja na udogo wa nchi yao kulinganisha na ya kwetu. Kumbuka Malawi wana population density kubwa kuliko sisi. Zambia, nenda kaone wana mipango mizuri zaidi kuliko sisi iwe mipango miji, matumizi ya ardhi n.k.

China wanamaendeleo ndio lakini kumbuka China ni nchi ya dunia ya tatu sio first world. Pia jua kwamba China kwasababu ya utawala wa chama cha kikomunist kuna uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu. Mambo mengi yanayotendekea China hayatangazwi; watu wananyongwa bila vigezo vya kutosha, kuna ukandamizaji mkubwa sana wa wanyonge, watu wana uawa kama kuku, kumbuka wakati corona ilianza kama uliona ile video ungedodosha machozi jinsi watu waliambukizwa walivyokuwa wakikamatwa na kupelekwa kwenye chumba cha kuuwawa, kisa wana corona. Kuna uovu mwingi mno unaotokea China. Ndani ya china kuna mamia ya mamilioni maskini wa kutupa usione majengo makubwa na miji mizuri ukafikiri basi kila mtu anaishi hivyo China. Wachina wengi wamekimbia China na wanaishi kila mahali duniani, hii sio dadili nzuri, wengi ni wakimbizi wa umaskini na ubabe wa kikomunist huko China.

Russia ilikuwa vizuri miaka ya 80, na ilikuwa superpower wakati demokrasia ikitawala Russia, watu wengi walikwenda kusoma Russia lakini sana wamekuwa authoritarian, chama kimoja cha Putin na huwezia amini Russia imeangukia kwenye ukabila na tena vita ya koo, na imerudi kuwa dunia ya pili. Demokrasia ni muhimu sana na ndio tatizo la nchi za Afrika.
 
Mkuu denooJ umeongea jambo la msingi sana. Lakini pia wanaosema kilimo hawasemi watu wote wakalime. Hakuna sekta inayoweza kusimama peke yake, kwa hiyo uko sahihi kabisa. Suala ni kwa namna gani tunaweza kuwa na viwanda vingi zaidi? hapo ndio tunazungumzia ubunifu. Tunakuwaje na ubunifu? hapo ndio tunazungumzia mfumo wa elimu? tunaboreshaje mfumo wa elimu? hapo ndio tunazungumzia sera na mfumo wa elimu.

lakini vipi viwanda bila mtaji? hapo ndio tunajaribu kufikiri ni vipi vijana wanaweza kupata mikopo ambayo ni productive. Kwa hiyo unachosema ni kweli kwamba kuna vitu vingi vinategemeana.
 
Back
Top Bottom