Riadha zarejea kwa kishindo; Wakenya Helen, Faith na Cheruiyot wang'aa na kupeperusha bendera ya Kenya kwenye 2020 Diamond League Monaco, Ufaransa

Riadha zarejea kwa kishindo; Wakenya Helen, Faith na Cheruiyot wang'aa na kupeperusha bendera ya Kenya kwenye 2020 Diamond League Monaco, Ufaransa

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Faith-Kipyegon.jpg


Baada ya muda mrefu hatimaye calendar ya mashindano ya riadha duniani imeanza tena. 'First leg' ya 2020 Diamond League(DL) ilianza kule Monaco, Ufaransa ijumaa hii.

Protokali zote mpya za COVID-19 zilizingatiwa, huku mashabiki 5,000 tu wakikubaliwa kwenye ukumbi wenye capacity ya watu 16,000.

Wanariadha wote walioshiriki na wasimamizi pia walilazimika kupimwa kabla ya hafla yenyewe. Wakenya waliibuka kidedea kwenye mbio zao, baada ya siku nyingi za mazoezi bila 'action'.

Bingwa wa dunia kwenye 5000m kwa wanawake Helen Obiri alistahimili ushindani mkubwa wa wahabeshi na akashinda kwa muda wa 14:22.12.

Naye bingwa wa dunia kwenye 1500m kwa wanawake Faith Kipyegon akaibuka mshindi kwenye mbio za 1000m na Timothy Cheruiyot akaibuka wa kwanza kwenye mbio za 1500m.
Obiri, Cheruiyot and Kipyegon shine at DL meet in Monaco
 
Safi sana, athletics huwa zinanifanya nikeshe kwa kweli napenda sana haswa ukiangalia Ke vs Eth athletes wanavyoufanya mchezo uonekane rahisi, ila nadhani ni miongoni na michezo tough on the planet! Well done guys! Whats' the major one coming up next after this?
 
Nasubiri kwa hamu ushindani baina ya Bekele na Kipchoge, umekua ukiahirishwa ila utafanyika tu, japo huwa nampigia debe Kipchoge ila namkubali sana Bekele, yuko vizuri sana jamaa yaani hata form yake wakati anakimbia huwa very relaxed.
Utakua ushindani usio wa kawaida na haujawahi kutokea.

 
Safi sana, athletics huwa zinanifanya nikeshe kwa kweli napenda sana haswa ukiangalia Ke vs Eth athletes wanavyoufanya mchezo uonekane rahisi, ila nadhani ni miongoni na michezo tough on the planet! wel done guys. Whats' the major one coming up next after this?
2nd leg itakuwa Stockholm, Sweden wiki ijayo. Baadaye mapema mwezi ujao Luissanne, Switzerland alafu Brussels, Belgium n.k n.k, ya mwisho mwezi Oktoba kule Uchina. Ndio hii hapa calender ya 2020 Diamond League.
Calendar - Diamond League Wahabeshi tumekuwa tukiwacharaza charaza kwenye riadha hadi wamejichokea wenyewe. Kwa sasa kuna mganda anawatoa wakenya kijasho, anaitwa Cheptegei.

Yeye ndiye aliyeibuka kama 'man of the event' kule Monaco baada ya kushinda na kuvunja rekodi ya Kenenisa Bekele, ya miaka 16, kwenye mbio za 5000m.
r
 
Faith-Kipyegon.jpg
Baada ya muda mrefu hatimaye calendar ya mashindano ya riadha duniani imeanza tena. 'First leg' ya 2020 Diamond League(DL) ilianza kule Monaco, Ufaransa ijumaa hii.

Protokali zote mpya za COVID-19 zilizingatiwa, huku mashabiki 5,000 tu wakikubaliwa kwenye ukumbi wenye capacity ya watu 16,000.

Wanariadha wote walioshiriki na wasimamizi pia walilazimika kupimwa kabla ya hafla yenyewe. Wakenya waliibuka kidedea kwenye mbio zao, baada ya siku nyingi za mazoezi bila 'action'.

Bingwa wa dunia kwenye 5000m kwa wanawake Helen Obiri alistahimili ushindani mkubwa wa wahabeshi na akashinda kwa muda wa 14:22.12.

Naye bingwa wa dunia kwenye 1500m kwa wanawake Faith Kipyegon akaibuka mshindi kwenye mbio za 1000m na Timothy Cheruiyot akaibuka wa kwanza kwenye mbio za 1500m.
Obiri, Cheruiyot and Kipyegon shine at DL meet in Monaco
Hongera kwa Wakenya wenzetu walioshinda.
 
Nasubiri kwa hamu ushindani baina ya Bekele na Kipchoge, umekua ukiahirishwa ila utafanyika tu, japo huwa nampigia debe Kipchoge ila namkubali sana Bekele, yuko vizuri sana jamaa yaani hata form yake wakati anakimbia huwa very relaxed.
Utakua ushindani usio wa kawaida na haujawahi kutokea.


Huyo mjamaa wa Total running productions nimewatch video zake karibu zote. Yuko sawa kwa kuchambua wanariadha. Anatema facts after facts. Baada ya siku mtu anajifunza mambo mengi tu.
 
2nd leg itakuwa Stockholm, Sweden wiki ijayo. Baadaye mapema mwezi ujao Luissanne, Switzerland alafu Brussels, Belgium n.k n.k, ya mwisho mwezi Oktoba kule Uchina. Ndio hii hapa calender ya 2020 Diamond League.
Calendar - Diamond League Wahabeshi tumekuwa tukiwacharaza charaza kwenye riadha hadi wamejichokea wenyewe. Kwa sasa kuna mganda anawatoa wakenya kijasho, anaitwa Cheptegei.

Yeye ndiye aliyeibuka kama 'man of the event' kule Monaco baada ya kushinda na kuvunja rekodi ya Kenenisa Bekele, ya miaka 16, kwenye mbio za 5000m.
r
Wahabeshh kwisha habari yao. huyu Cheptegei atakua wa kule northern UG, kutokana na jina lake huyu!
 
Nchi ya barakoa!!!watakimbia wakiwa wameyavaaa?
Wanariadha wote na wasimamizi pia walipimwa na watakuwa wanapimwa kabla ya kukubaliwa kushiriki kwenye mashindano. Alafu nchi gani hiyo ndio ya barakoa? Maanake wanariadha wote walioshiriki wametoka kwenye nchi ambazo barakoa huwa zinavaliwa, sanasana wakati huu wa janga la Corona.
 
Hellen Obiri namkubali sana huyu dada yaani huwa natamani hata awe ndugu wa kufikia. Mungu akinijalia nitakutana naye siku moja afike Tanzania apandikize spirit yake ya kujituma
Kama kawa Obiri aliwaacha wenzake mataani na 'kick' yake, kwenye lap ya mwisho.
 
Safi sana ishara tosha dunia inarejea kazini baada ya Corona.
Sidhani hali itarejea kama ilivyokuwa hapo awali, maanake mashabiki wamebanwa kweli kweli kwasababu ya 'social distancing'. Ila kuna faida yake pia kwa upande wa media, ambazo zimewezeshwa zaidi kurusha mashindano yote live kwa watizamaji kote duniani.
 
Sidhani hali itarejea kama ilivyokuwa hapo awali, maanake mashabiki wamebanwa kweli kweli kwasababu ya 'social distancing'. Ila kuna faida yake pia kwa upande wa media, ambazo zimewezeshwa zaidi kurusha mashindano yote live kwa watizamaji kote duniani.
Cha muhimu wapo kazi.
 
Mojawapo ya michezo ya kudhalilisha utu wa mwafrika ni riadha. Unfortunately my personal view. Wewe kama sio mwanajeshi kwenye uanja wa vita, why should you run? in the first place?
 
Mojawapo ya michezo ya kudhalilisha utu wa mwafrika ni riadha. Unfortunately my personal view. Wewe kama sio mwanajeshi kwenye uanja wa vita, why should you run? in the first place?
Kwahivyo waafrika tu ndio huwa wanashirikishwa kwenye riadha?
 
Mojawapo ya michezo ya kudhalilisha utu wa mwafrika ni riadha. Unfortunately my personal view. Wewe kama sio mwanajeshi kwenye uanja wa vita, why should you run? in the first place?
Duuh kwani unawaza nini mkuu ebu funguka maana nahisi unamengi zaidi ya kutushirikisha tofauti na hiyo conclusion ulioiweka hapo
 
Back
Top Bottom