Riba za mabenki

Kwa lugha rahisi, mkopo wa muda mrefu, unakupa ahueni kwenye jumla ya pesa utakayoirejesha, lakini marejesho ya kila mwezi yanakua juu.

Ukiamua kulipa kwa muda mfupi, utafurahia kurejesha jumla ya kiwango kidogo lakini makato ya kila mwezi yatakua juu.
 

Haujui unaloongea kaka
Au hauna elimu ya mikopo so be patient acha wanaojua waongelee

Mkopo wa muda mrefu makato kwa mwezi ni makubwa ila pesa unayorudisha kama deni ni ndogo mfano umekopa 1M kwa kato la elfu 95 kila mwezi kwa mwaka mzima ina maana
95,000 * 12 ambapo ni 1,114,000
Ukichukua ulicho kopa - jumla ya deni= faida ya kampuni yaani
1,114,000- 1,000,000= 1140,000

Ukikopa 1M kwa miaka mitano kwa kato la 35,000 inamaana ni
35,000* 60= 2,100,000
Inamaana
2,100,000-1,000,000=1,100,000 faida ya kampuni

So makato madogo muda mrefu unalipa deni kubwa
Makato makubwa muda mdogo unalipa deni dogo


Muda ndio unatengeneza ukubwa wa deni kwasababu ya concept of Time value of Money
 

Kujua kitu na kukosea kutoa maelezo ni vitu viwili tofauti.

Ukisoma kwa makini post yangu ya awali, angalia maelezo ya mwanzo, nilichotaka kuandika kwenye kipengele cha pili ni kinyume chake, kuna kitu kikaingilia kati nikawa nimepost kabla ya kufanya marekebisho kwenye upande wa mkopo wa muda mfupi.

Naweza nikawa kwrli sijui kitu kama ulivodai, lakini nimefanya kazi bank kwazaidi ya nusu mlongo.

Nimekua mkopaji mzuri tu wa mabenki kadhaa.

Nimefanya kazi kwrnye mifumo ya benki kubwa tu na taasisi za kifedha.

Kuna wakati ni bora kujikita kwenye hoja.
 

Samahani pia kama ntakua nimekuattach nimefanya kazi microfinance zaidi ya tatu na benk takribani 2 mpka nlipo amua kuacha na kufanya issue zangu so niko na experience pia
So tujikite kwenye mada vizuri ili kwa pamoja tusaidie wengine
Samahani sana kama nlikukwaza pia
 

You are right Sir!
 
Hapa ndio watu huwa wanashindwa kuelewa.
 

Natumae mleta mada atakua umepata muongozo...


Cc: mahondaw
 
Na pia tatizo lingine watu wengi hawajui aina ya riba ya mkopo anaoomba kama ni REDUCING BALANCE ama ni FLATE RATE.

Picha hapa chini inaonesha watu wawili (A & B) ambao wote wamekopa 10,000,000/= kwa riba ya 17% na kwa muda sawa wa miezi 12 mmoja kwa REDUCING BALANCE na mwingine kwa FLATE RATE Lakini marejesho na riba tofauti.
 
Baadhi huwa wanachaji prosessing fee 1% ya mkopo, kama anayekopa 1m na anayekopa 20m wote proces zake ni vile vile iweje watofautiane kwenye gharama? Huu ni wizi wa wazi kwa watumishi wa serikali na BOT wanafumbia macho swala hili.
Kingine baadhi ya taasisi za serikali huwa na vitengo vya mikopo ambapo hatua za awali za maombi unaanzia hapo, hiyo processing fee inazisaidiaje hizi idara za mikopo katika kuwasaidia wateja wa mabenki ambao ni wakopaji?
 
Baadhi ya benki huwa ukitaka ku settle down deni lako kwa kulilipa cash huwa wanatoza kama laki hivi za usumbufu, hii nayo imekaaje?
 
Samahani kaka, bank km Nmb ukikopa 6 M urejeshe ndani ya miaka miwili makato yatakuwaje?

Hapo inategemea rate zao zipo kiasi gani.
Endapo hiyo pesa unafanyia biashara na una uhakika wa kuingiza pesa nzuri miaka miwili itakua sawa kwa sababu makato yatakua makubwa.

Ukiwa ni mwajiriwa na hii pesa unakamilisha jsmbo hauifanyii biashara izalishe, bora ufanye miaka mitatu au minne ili ubakiwe na kitu kwenye mshahara wako.
 
Tunathamini mchango wako.
 
Wengi tunapopewa mikopo hatunaga muda wa kupiga hesabu tunachofanya tu ni kuangalia ni sh ngapi basi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…