Matanga
JF-Expert Member
- Nov 13, 2019
- 2,281
- 3,976
.
Nadhani wengi mnamjua Ricardo Izecson dos Santos, ni huyo huyo anaejulikana kwa jina la Ricardo Kaka, namba 10 bora sana katika kizazi chake
.
Najua nikikuuliza unamkumbuka Kaka kwa lipi, 90% kama si 95 watanikumbusha stori za usiku wa UEFA na AC MILAN
.
Basi ngoja nikurudishe nusu fainali usiku wa nusu fainali UEFA pale Old Trafford 2006-7, Man Utd anaibuka mshindi 3-2 goli la ushindi likifungwa na Wazza dakika za mwisho kabisa, ila stori kubwa ilikuwa kiwango bora kabisa cha Kaka
.
AC Milan ya mastermind Carlo Anceloti, kila mpira aliougusa uligeuka dhahabu, alifunga magoli mawili usiku ule, yote upande uleule, moja anawagonganisha Evra na Gabriel Heinze kichwa na goti
.
Ila kuna kitu kilitokea si kawaida ya mshika dini huyu. Unaweza hisi ni kipi? Hold on, usiumize kichwa, nipo kwa ajili yako nakujuza
.
Katikati ya Mechi Giggs alimchezea rafu Kaka, kulikua hamna namna, mtu wa Mungu alikua hashikiki, ila paap ghafla Kaka amemind akampiga roba moja ya kimafia Giggs
.
Giggs aliwahi kukiri, alipopigwa ile roba, alijiuliza "hivi kweli mtu alieshika dini anaweza kufanya kitendo kama hiki?"
.
Baada ya mechi kuisha, United wakiwa dressing room kwenye spika bila shaka kwa mbali inapiga Don't Matter ya Akon, ghafla mlango unafunguka akaingia Kaka na Gennaro Gattuso mtukutu, watu kimyaa
.
Ila ujio ulikuwa wa kheri, Kaka alimuomba Gattuso akawe mkarimani sababu anajua kiingereza aliwahi cheza pale Scotland klabu ya Rangers
.
Kaka aliomba msamaha kwa Giggs ya kuwa hakufanya swala la uungwana kumkwida
.
Giggs alimwambia Gattuso "mwambie Kaka ni kawaida hasira uwanjani kwa mchezaji hasa mechi yenye uzito kama hii ya nusu Fainali Uefa" Gattuso akatafsiri na kumwambia Kaka
.
Kaka alimpatia Giggs "Catholic Orthodox Icon" hii ni picha ya Yesu ambayo imechorwa kwa ustadi nia ni kutukumbusha upendo, pia aliinama kwa heshima akiomba msamaha, chumba kizima kilipiga makofi
.
Giggs anasema mpaka leo hajawahi ona mtu mpole, mwenye adabu na mkarimu kama Kaka
.
Ni hasira za kibinadamu tu [emoji16]
Nadhani wengi mnamjua Ricardo Izecson dos Santos, ni huyo huyo anaejulikana kwa jina la Ricardo Kaka, namba 10 bora sana katika kizazi chake
.
Najua nikikuuliza unamkumbuka Kaka kwa lipi, 90% kama si 95 watanikumbusha stori za usiku wa UEFA na AC MILAN
.
Basi ngoja nikurudishe nusu fainali usiku wa nusu fainali UEFA pale Old Trafford 2006-7, Man Utd anaibuka mshindi 3-2 goli la ushindi likifungwa na Wazza dakika za mwisho kabisa, ila stori kubwa ilikuwa kiwango bora kabisa cha Kaka
.
AC Milan ya mastermind Carlo Anceloti, kila mpira aliougusa uligeuka dhahabu, alifunga magoli mawili usiku ule, yote upande uleule, moja anawagonganisha Evra na Gabriel Heinze kichwa na goti
.
Ila kuna kitu kilitokea si kawaida ya mshika dini huyu. Unaweza hisi ni kipi? Hold on, usiumize kichwa, nipo kwa ajili yako nakujuza
.
Katikati ya Mechi Giggs alimchezea rafu Kaka, kulikua hamna namna, mtu wa Mungu alikua hashikiki, ila paap ghafla Kaka amemind akampiga roba moja ya kimafia Giggs
.
Giggs aliwahi kukiri, alipopigwa ile roba, alijiuliza "hivi kweli mtu alieshika dini anaweza kufanya kitendo kama hiki?"
.
Baada ya mechi kuisha, United wakiwa dressing room kwenye spika bila shaka kwa mbali inapiga Don't Matter ya Akon, ghafla mlango unafunguka akaingia Kaka na Gennaro Gattuso mtukutu, watu kimyaa
.
Ila ujio ulikuwa wa kheri, Kaka alimuomba Gattuso akawe mkarimani sababu anajua kiingereza aliwahi cheza pale Scotland klabu ya Rangers
.
Kaka aliomba msamaha kwa Giggs ya kuwa hakufanya swala la uungwana kumkwida
.
Giggs alimwambia Gattuso "mwambie Kaka ni kawaida hasira uwanjani kwa mchezaji hasa mechi yenye uzito kama hii ya nusu Fainali Uefa" Gattuso akatafsiri na kumwambia Kaka
.
Kaka alimpatia Giggs "Catholic Orthodox Icon" hii ni picha ya Yesu ambayo imechorwa kwa ustadi nia ni kutukumbusha upendo, pia aliinama kwa heshima akiomba msamaha, chumba kizima kilipiga makofi
.
Giggs anasema mpaka leo hajawahi ona mtu mpole, mwenye adabu na mkarimu kama Kaka
.
Ni hasira za kibinadamu tu [emoji16]