Ripoti TCRA: Watumiaji wa Intaneti Tanzania wafikia Milioni 34.4

Ripoti TCRA: Watumiaji wa Intaneti Tanzania wafikia Milioni 34.4

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
1698247249580.png

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa taarifa ya mwenendo wa Sekta ya Mawasiliano katika kipindi cha July hadi September mwaka huu ambapo imesema kumekuwa na ongezeko la Watumiaji wa Intaneti kwa 1.24% kutoka Watumiaji 34,047,407, mwezi June 2023 hadi kufikia 34,469,022 mwezi September 2023.

Mkurugenzi Mkuu wa CRA ,Dkt Jabir Bakari ametoa taarifa hiyo leo October 25,2023 Jijini Arusha ambapo amesema baadhi ya sababu kuu zinazochangia ongezeko la matumizi ya intaneti zimeendelea kuwa ni uwepo wa maudhui ya Kiswahili kwenye mtandao ikijumuisha kuongezeka kwa programu-tumizi (applications) kwa lugha ya Kiswahili.
 

Attachments

Na ukute katika hao watumiaji wote unaeza kuta hata nusu ya hao watumiaji hawana taarifa zao rasmi😅
 
Takwimu hii ya watumiaji wa internet na takwimu ya watumiaji JamiiForums uongo mtupu😂😂
 
Kwenye watumiaji wa internet huwa wanajuaje maana kuna wenye simu wanaoweka bando sawa hawa unaweza kuwajua ila kuna wengine wanajoin wifi za maofisi na sehemu mbalimbali ambao kwa sasa nao ni wengi yaani mtu hajawah kuweka bado ila yupo online ..
 
Watoa na orodha ya site au apps zenye watumiaje wengi zaidi bongo.
 
Back
Top Bottom