Ripoti ya CAG 2021/22: Huduma za Hospitali ya Mloganzila haziridhishi

Ripoti ya CAG 2021/22: Huduma za Hospitali ya Mloganzila haziridhishi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Mloganzila1.jpg
Tathmini iliyofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) umeonesha Hospitali hiyo ina Utendaji Duni uliosababisha kuzorota kwa huduma za Afya, hivyo kushusha mapato.

CAG alibaini gharama matumizi zinazidi mapato kwa 7% hadi 19 kuanzia mwaka 2018/19 na 2021/22 kiasi cha kuongeza nakisi kutoka Tsh. Bilioni 1.92 mwaka 2018/19 hadi Tsh. Bilioni 5.81 mwaka 2021/22.

Sababu nyingine zilizochangia kushuka mapato ni Misamaha isiyo na udhibiti, kuongezeka madai yanayokataliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya pamoja na huduma duni za Kibingwa za Kulaza Wagonjwa binafsi na wa Umma.

Kwa mujibu wa Ripoti ya CAG amesema, Utendaji duni unaweza kusababisha kuzorota kwa huduma za afya hospitalini kutokana na mapato duni ambayo hayawezi kukidhi gharama za uendeshaji na ugumu wa kufikia malengo ya kimkakati kutokana na kupungua kwa mapato kulingana na gharama zinazotumika.

Ninapendekeza kuwa Hospitali ya Mloganzila (a) ihakikishe huduma za kibingwa zinaimarishwa hospitalini hapo ili kuongeza wagonjwa binafsi na wa umma, (b) ihakikishe inaendana na mwongozo wa Mfuko wa Bima ya Afya ili kupunguza idadi ya madai yanayokataliwa, na (c) kuweka misamaha kielektroniki ili kuimarisha udhibiti wa misamaha inayotolewa.
 
Kaangalia mlogazila tu ukweli huduma ya afiya kwa masini bado shida
 
humu hawakujui we watukane tu! yaan MLOGANZILA kizuri pale ni MOCHWARI tu! ndio maana wanauwa sana
Mortuary penyewe huduma very slow, miezi miwili iliyopita nilienda kuchukua mwili wa mpendwa mmoja pale, almost four hours tunangojea na hapo sie ni number 2 kwa kuwahi
 
Ile hosptali anaeiuwa ni yule mkurugenzi wake, mkurugenzi anasababisha mambo mengi muhimu kuwa na urasimu.....akiondolewa huyu mkurugenzi pale mambo mengi yatakwenda vizuri.
 
Back
Top Bottom