Ripoti ya Uchunguzi wa Maabara: Mashine moja ilikuwa na hitilafu. Upimaji wa COVID19 umehamishiwa katika Maabara mpya iliyopo Mabibo

Waanze sasa na kutupa Updates za huo ugonjwa ili tuendelee kwa nguvu zote kujikinga badala tu ya kutuambia tupige kelele kwa kisingizio eti hiyo Corona imekwiisha.

Update alitoa Rais hukusikia? Wagonjwa wote wanaoumwa Covid-19 watapona. Vile vile alisisitiza kuwa ugonjwa upo tuendelee kuchukua tahadhari. Hapa Kazi Tu!
 
Nimepata taarifa kuwa jiji la Dar limeshambuliwa sana na Corona baada ya watu kupuuzia hatua za kujikinga. Mambo yamevurugika kabisa.
Acha hizo bhana... mamlaka imeshasema maambukizi yamepungua Sasa hizi taarifa zako umezipata wapi?
 
Baada ya kamati iliyoundwa kubaini chanzo cha samples za vipimo vya matunda na wanyama kukutwa na corona imebaini kulikuwa na hitilafu katika mashine ya maabara kuu ya serkali ripoti ya kamati imeabaini

Akisoma matokeoa ya kamati hiyo waziri Ummy Mwalimu amesema mashine hiyo ilikuwa na hitilafi pia kulikuwa na uzembe katika upimaji wa samples hizo

BBC


Sent using Jamii Forums mobile app
 
magari yaliyo mengi yanayoenda nchi za jirani yanaanzia dar kwa kuwa bandari ndo ipo hapo.
pia hata magari yanayoanzia mikoa tofauti na dar itawalazimu madereva waende kupata vipimo dar kisha waendelee na safari.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sidhani kama ndio sababu, unataka kusema na Kenya maabara iko Mombasa au South Africa maabara ya taifa iko Dubarn?
 
Hizi report za kupika huwa zinawaumbua vibaya saana watu;

Sababu ya kwanza..... ni kosa la nani? nani anasimamia utendaji wa maabara kwa ujumla .... majibu ni Waziri...alitakiwa kutumbuliwa Waziri.

Sababu ya pili...Ubovu wa mashine...hizi mashine ni mpya na ni chache (mbili tu ) kwa akili ya kawaida Waziri hakuwa na taarifa kuhusu ubovu?
 
Reactions: SMU
Naomba kuuliza hivi hiyo Press conference ya Waziri inakuwaga haina nafasi ya kuuliza maswali? manake sitaki kuamini kuwa wwandishi walipewa nafasi wakauliza maswali ya kupewa?

Maswali yangu: Ndio Mashine mbovu je vipi kuhusu matokeo ya upimaji kwa sasa? au zoezi limesimama.?
 
Hapa sitoshangaa kuwa hata yule dada walie mtumbua alikuwa hana makosa.
 
Hivi kweli kabisa wewe ulitegemea ripoti ya maana? Wachana na wanasiasa kabisa.....muda wote wanafikiria votes tu.
 
Kwahiyo maabara ya Taifa imejengwa kwa dharura Dar es Salaam ili kukabiliana na Corona? Meaning that maabara nyingine ya Taifa itajengwa Dodoma baada ya Corona kuisha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…