Elections 2010 Ripoti ya waangalizi wa uchaguzi inaleta kichefuchefu...

'a' na 'b' ni kweli
hususani wasomi kwa 'a'
na 'b' chadema hawakufika vijijini hasa hasa mikoa ya kusini na zbr.

2015 mipango ianze sasa.
 
Kwanini tunapenda sana kuwashinikiza watu waandike au wajibu kile tunachikitaka sisi?? Tukuue ndiyo, usile leo sawa, sema ccm chama cha mafisadi sawa, nchi hii imeharibika sawa, chadema inataka kurithi a failed state sawa, Huo si ni umbumbu kupita maelezo kwa maana nyingine ni upumbavu kukubaliana kila jambo hata kama halina msingi.

Kama unataka kupinga matokeo ya kitafiti ya mwenzio nawe fanya utafiti wako kwa misingi inayofanana ili upate jibu linalopingana. Utafiti wa kisayansi siyo utafiti ya kisiasa ndugu. Sayansi ina base kenye facts siyo political truth na ndiyo maana methodology inayotumika inawekwa wazi ili kwa wale wanoupinga utafiti huo wapinge kisayansi ili kutoa mapungufu au uongo uliofanywa na taasisi au mtu fulani na hiyo inakubalika.

Kiutaratibu report ya waangalizi wa uchaguzi kama ambayo mimi nimeshawahifanya inapelekwa kwa wadau wote Tume ya Uchaguzi ya nchi husika, mkuu wa nchi, vyama vya siasa vilivyoshiriki uchaguzi, taasisi husika na vyombo vya habari maana siyo siri.

Tuache majungu ya kisiasa kama ni maswala ya kichama peleka kwenye blog ya chama na siyo JF kama mmiliki wa JF anashadadia hayo aandike chama flani JF iwe ya jamii ya chama hicho tu na siyo wote.
 
the truth ni kuwa wanajua JK ni bwana misifa, bora wampe taarifa ya uongo ili apumbazike, kwa sababu ikiwa uchaguzi ungekuwa huru na wa haki, isingewachukua miezi mitatu kuikamilisha kwa sababu kusingekuwa na dosari yo yote ya kuchakachua.
 
kunawatu wanajua kufikiri sijui kwanini nchi hii inaongozwa na VILAZA!
 
hakuna haja ya kujadili hili eti 1.ccm ni chama imara 2.TISS na NEC yao hawakuhusika na uchakajuaji wa matokeo 3.watu 12 ml walisema hawaendi kupiga kura sbb wanajua ccm itashinda......hawa jamaa uwa wanafanya kazi na kutoa ripoti zao kwa ku-base na matakwa ya walio watuma ambao ni nchi za magharibi i.e wakioona rais ni easy kumwendesha kama jk basi wanatoa +tive ripoti wakioona ni ngangari kama bagbo basi tegemea -ve riport ili aondoke----hawa jamaaa uuuuuuuuuuh!...puuuuuuuuuuuuuuuuuh!...the go to hell
 
Hamna lolote nyie chadema wanafiki tu. Mwenzenu lipumba aliyakubali mpeema matokeo nyie mnataka kuleta vurugu eeh tumewagundua.
 
Ripoti za ulaya hata mie si ziamini kwani huwa wana muangalizi mmoja kila mkoa sijuwi anaangalia nini? Afadhali redet walikuwa na waangalizi wengi takriban kila kituo.
 
Hata mi niliisikia kwa mbali. Eti kampeni zilitawaliwa na chama tawala..................wehu wakubwa!!!
 

Umetupa source ya heading ya thread yako. Naomba utuwekee source ya mistari iliyowekea rangi nyekundu.

Kuna mstari nimeweka rangi ya kijani. Hapo nataka nikupe angalizo kuwa watu kujaa ktk mikutano ya mgombea haina maana kuwa watampigia kura. Mwaka 1995, Mhe A. L Mrema alikuwa anajaza watu vibaya lakini watu hao hawakumchagua. Mimi binafsi nilihudhuria mikutano yote ya wagombea urais mwaka 2010, je ina maana siku ya kupiga kura niliwachagua wote?

Kuhudhuria si kuchagua. Tunakwenda kusikiliza sera za mgombea na muda mwingine tunakwenda kushangaa helkopta na comedy kama watakuwepo. Hata kusikiliza muziki maana uwezo wa kuingi ktk kumbi za starehe hatuna
 
Kweli kuna watu wanafiki dunia hii, Hao jamaa wangesema Dr. Slaa alishinda ila akapokwa ushindi, wangesema kura ziliibwa, wangesema uchaguzi haukua wa huru na haki ungekuta wanashangiliwa mno ila tu kwa kuwa iko kinyume na mtakwa yao basi ooh siwaamini watu weupe ohh sijui unafiki gani. Hiyo ndiyo siasa ya maji machafu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…