KERO RITA Ilemela inawabebesha gharama wanaohitaji vyeti kwa makosa yanayofanywa na ofisi

KERO RITA Ilemela inawabebesha gharama wanaohitaji vyeti kwa makosa yanayofanywa na ofisi

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Kuna kero ambayo inatuumiza wananchi wa kawaida wilaya ya ILEMELA MKOA WA MWANZA kwenye ofisi ya usajili hasa wa vyeti vya kuzaliwa, tunachukua form tunajaza details zote ziko sawa msajili akifika yeye wakati wa kuziingiza zile taatifa kwa ajili ya kutoa cheti anakosea sana vyeti vinakuwa na typing errors nyingi.

Ukirudisha cheti unaambiwa lipia gharama za marekebisho ambayo ni elfu 13,000 na bado anakwambia na pesa yangu kama ni elfu 10 au elfu 5 wakati huo huo kosa ni lake, kwanini anatufanyia hivyo wananchi?

Mbaya zaidi hataki zile details ulizojaza mwanzo zitafutwe anasema documents ziko nyingi hawezi hizo kazi ujaze upya forms za kuomba cheti cha kuzaliwa.

Inakatisha tamaa na ni unyanyasaji wa wazi cheti cha shilingi elfu nane (8,000) unajikuta unatumia zaidi ya elfu 50,000 ni kero ya wengi tunaomba msaada wa kupaza sauti kwa mamlaka husika tafadhali.

Wako katika ujenzi wa taifa
Wananchi wa ILEMELA
MWANZA
 
watu wa RITA ni wasumbufu sana Nchi nzima wahusika walione ili
 
hii migumi ingewekwa online mtu ajaze mwenywe, ofisini mtu apeleke tu form ya ku uthibitisho na anaehusika anaipitisha online form, kipi chashindikana?
 
hii migumi ingewekwa online mtu ajaze mwenywe, ofisini mtu apeleke tu form ya ku uthibitisho na anaehusika anaipitisha online form, kipi chashindikana?
Mbona ndo hivyooo yaaan utakuta kijana wa form six anajqziwa fomu daah
 
Back
Top Bottom