RIWAYA: Black star

Black Star 2: Nemesis 43







Wakati huwo tayari Indra alishakaribia kama mita kumi hivi kutoka alipo Asura. Mkuki wake ukiwa mkononi, akavuta pumzi nyingi na kuuwinua juu ila kabla hajafanya shambulizi akamuona Asura akitabasamu.



"Wewe umefanya nini mpaka utabasamu" aliuliza kwa mshangao.



"Katika mipango yangu kulikuwa na asilimia hamsini kuwa sitakushinda hivyo nikapanga kuondoka na wewe" alijibu na kubonyeza sehemu katika kiganja chake.



"Mshe..." hakumaliza Indra akageuka na kutaka kukimbia lakini akawa kashachelewa. Mlipuko mkubwa ukatokea, sayari nzima ikawa nyekundu. Moto mkali sana ukawaka, Asura alihakikisha anamuua Indra lakini kitu ambacho hakukitegemea ni pale alipofumbua macho na kujikuta bado mzima.



"Mshenzi sana wewe, ulidhani sikufikiria kama utafanya hivyo" aliongea Indra aliekuwa pembeni yake. Alikuwa ameungua karibia mwili mzima.



"Hahaha! Sikujua kama adui yangu angeniokoa" aliongea Asura na kutema funda kubwa la mate. Akajiweka vizuri na hapo ndioa akagundua kuwa mwili wake ulibakia ngozi na mofupa tu nyama yote ilungua. Akacheka tena kwa nguvu na kumuangalia Indra.



"Bahati mbaya sana ulichokuwa unakitaka hakipo tena" aliongea kwa kejeli.



"Wewe ndio nishani yangu ya vita, nitahakikisha hufi lakini pia hutakaa ulione jua tena katika maisha yako" aliongea Indra.



"Sitakaa nilione jua, una uhakika" aliuliza Asura.



"Asilimia mia moja" alijibu na baada yapo akatumia mkuki na kuchana anga, akamnyanyua Asura na kuondoka nae. Waktokra Mythril ambako ndipo alipokubaliana na wengine. Lakini akashangaa kukuta mabadiliko makubwa. Katika akili yake ndio vita ilichukuwa muda mrefu lakini usingekuwa nrefu kiasi cha kuwepo mabadiliko hayo.



Akajifunika vizuri na kumsogelea mtu aliekuwa anapita karibu yake, "samahani nilikuwa naulizia leo ni mwaka gani" akauliza jwa sauti ya chini. Alipotajiwa mwaka, alihisi kama ndoto karibia miaka mia saba imepita tokea alivyoondoka Mythril kwenda kupambana na Asura.



Hakutaka tena kukaa eneo hilo, akaelekea porini kidogo na kwa kutumia mkono wake akapasua hewa na kupita. Safari hii akatokea juu ya kilele cha mlima Sumeru. Alipotokea watu wanne wakafika na kupiga magoto mbele yake.



"Bwana wetu karibu nyumbani" wakaongea kwa pamoja, "kwasasa sitaki wengine wajue kama nimerudi, mpelekeni huyu mpuuzi katika kina kabisa cha mlima huu" aliongea na kuwarushia mfuko mkubwa. Mmoja wao akaudaka, kabla hawajaondoka Indra akawapa pingu maalum.



Yeye akaelekea ndani katika hekalu kubwa na kukaa kwenye kiti chake, alikuwa amechakaa vibaya sana. Karibu nusu ya uwezo wake wote umepotea. Wale watatu baada ya kumfunga Asura wakaridi juu kuungana na Indra.



**********



"Fahad" aliita Karakantha na kugeuka, "wewe ni mimi na mimi ni wewe" aliendelea. Maneno hayo yakamshangaza Fahad na kutaka kuongea jambo lakini Karakantha akaweka kidole mdomoni.



"Nilipodhani kila kitu kimepotea, nilikuja kushtuka baada ya kupata upepo wenye joto. Sehemu ya roho yangu ilifanikiwa kutoroka mwili ikiwa imebeba meridian zangu nane za dragon. Siku hiyo nilioshtuka ndio siku ambayo wewe ulikuwa unazaliwa. Mwanzo nilitaka niuchukue mwili wako, maana yake wewe usingekuwepo leo lakini baada ya kufikiria sana nikaona nikuzawadie tu meridian hizo. Niliamni kabisa ipo siku utakuwa mwana martial art mkubwa japo umezaliwa katika sayari ambayo ina kiwango kidogo cha Qi" alifafanua.



"Kwanini mimi?" Aliuliza Fahad.



"Hata mimi sikuwa nikiijua sababu, ni ile hali ya kuamini hisia zangu tu" alijibu Karakantha.



Fahad alipomuangalia vizuri akagundua kuwa mwili wake umeanza kuwa mweupe. Ni kama vile mtu aliekuwa anatoweka taratibu.



"Fahad leo ndio itakuwa ni siku ya mwisho mimi na wewe kuonana. Muda wangu umeisha, lakini utakapozinduka utakuwa na tunda jekundu mkononi mwako. Lile hilo tunda na utarithi uwezo wangu wote uliobakia. Pili tengeneza njia yako, usifuate njia yangu mimi. Zile silaha kumi na mbili zipo katika mikono ya watu tofauti, wachache tayari ushawapata, watafute waliobaki. Kisha ingua nao mkataba na uwape insignia yako. Jinsi ya kuwapa utajua baada ya kula tunda hilo" baada ya maneno hayo mwili wa Karakantha ukatoweka kabisa. "Usifuate njia ya kisasi" maneno yakawa ndio ya mwisho.



Fahad akazinduka na kuangalia mkononi kwake, alikuwa na tunda dogo jekundu. "Pumzika kwa amani mwalimu" aliongea huku chozi likimtoka katika jicho la kushoto.



Akafunguwa kinywa na kulitupia tunda hilo mdomoni, akajiweka vizuri na kuanza kuzungusha Qi katika mwili wake. Akafumba macho na kuingia katika usingizi mzito, wakati huwo mwili wake ulikuwa unapitia mabadiliko ya hali juu zaidi.



Anafumbua macho, "master" akasikia sauti ikitokea pembeni yake.



"Rindelif, kuna habari gani huko" aliuliza akisimama.



"Vikosi vya mfalme Lorei vimewasiki nje ya ngome yetu muda si mrefu na wametoa masaa matatu ujitokeze. Bila kufanya hivyi wamesema watavamia na kuua kila ndani ya ngome yako" aliongea akiwa kapiga goti.



"Hhhmf, ahsante kwa taarifa. Mimi natangulia wewe utakuja. Ikiwa utaweza kuendana na kasi yangu unaweza kuunga" aliongea akiwa anatoka nje ya pango hilo.



Juwa lilikuwa linakaribia utosini, na hiyo ilimaanisha kuwa mchana ulikuwa unakaribia. Fahad akavuta pumzia nyingi na taratibu akaanza kuelea.



Bon!



Kwa kasi kubwa sana akatoweka, kutokana na kasi hiyo alionekana kama anaechana kakatikati ya upepo. Rindelif akafuata nyuma lakini aliishia kuona michirizi kama ya moshi tu ikiashiria mtu amepita.



Nje ya ngome ya Zinga.



"Zimebakia dakika chache mfalme wangu, inaonekana Fahad amewasiliti na kukimbia" aliongeaa mmoja kati ya mawaziri waliokuwa hapo.



"Hahaha! Nani ana uwezo wa kusimama mbele yangu, mimi mfalme mwenye nguvu" alijitamba mfalme Lorei. Alikuwa na upumbavu uliopitiliza, aliamini kabisa hakukuwa na mtu mwengine mwenye uwezo zaidi yake katika sayari hiyo.



Wakati huwo huwo, kitu chenye kasi sana kikapita juu yao. "Nyoika" walisikia sauti tu na wakati huwo katika nyumba ya Fahad ile fimbo ya chuma ikachomoka ardhini na kupotelea angani kwa kasi kubwa sana.



Ilisafiri kuelekea upande ambao Fahad alikuwa anatokea, Fahad alipoiona akageuka na kutanguliza miguu. Akaikanyaga na kuzunguka nayo kwa kasi kabla ya kutuwa na kusababisha vumbi kubwa sana.



Alipoakanyaga ardhi tu, ile fimbo yake ikasimama na kuelea pembeni. Wakati huwo huwo watu saba wakafika wakitokea ndani ya ngome hiyo na kupiga magoti mbele yake.



"Karibu nyumbani meya" wakaongea kwa pamoja.



"Samahanini kwa kuwatia wasiwasi" alijibu na kuwafanyia ishara wasimame. Wote walipoinua macho na kumuangalia pasi na matarajio yao wakarudi chini na kuinamisha vichwa. Jasho likaanza kauwatoka, wakati huwo walihisi wamesimama mbele ya kiumbe kisicho cha kawaida.



Na sio kama Fahad alikuwa akifanya makusudi laa, hiyo ilikuwa inatoka pasi na yeye mwenyewe kutambua. Alipoona hivyo akavuta pumzi nyingi ndani na kuitoa taratibu, "simameni" aliongea na wote wakasimama.



"Acha nimalizane na hawa nzi kwanza, tutajadiki mambo mengine baadae" aliongea na kuanza kutembea. Kila hatua aliyopiga ilifuatiwa na mtikisiko mdogo. Nguvu ya mtikisiko huwo iliongezeka kadiri alivyokuwa anawakaribia maadui zake.





 
Black Star 2: Nemesis 44







"Natoa onyo kwa wote, kama hutaki kupoteza maisha yako leo. Salimu amri, sitakuua na utarudi nyumbani kwa familia yako" aliongea akisimama mita kadhaa kutoka vilipo vikosi vya mfalme Lorei. Aliongea kwa makusudi ili kila mtu asikie, ili wasije kusema hawakupewa nafasi ya kutetea maisha yao.



"Unasema hivyo kama nani" alifoka mmoja kati watu watatu waliokuwa mbele kabisa. Baada ya hao ndio alifuata mfalme mwenyewe.



"Sijaongea na nyinyi nzi hapa mbele, ujumbe wangu huu ni kwa wanajeshi ambao leo mumewaleta kuja kufa" alijibu na kukunja sura.



"Wanajeshi waangu sikieni amri yangu, yeyote atakaeniletea kichwa cha huyu mpuuzi nitamuozesha binti yangu na atakuwa meya wa ngome ya Zinga" aliongea mfalme kwa sauti kali sana.



Kama ilivyo asili ya watu, linapokuja suala la madaraka hupata uroho waa hali ya juu. Kauli hiyo ya mfalme ikawapandisha morali wanajeshi hao na kuanza kupiga makelele.



"Hhmf, hawa watu wana upuuzi ulioshindikana" alijisemea Fahad na kushusha pumzi ndefu, akafika Garaaji na kumnong'oneza jambo.



"Alaa! Kumbe ndio maana wana kiburi, kwa hiyo nikiwauwa wote hapa kisha nikaivamia ngome yao na kuwamaliza waliobaki nitakuwa sijafanya makosa" aliongea Fahad.



"Kabisa" Garaaji alijibu na kurudi walipo wengine.



"Nimeambiwa hapa kumbe nyinyi wote ni watoto wa familia za kitajiri na mnawachukuliwa watu wengine kama wanyama tu. Basi msijali ile huruma yangu haipo tena kwasababu nimeamuwa kuwauwa hapa wote. Hatorudi hata mmoja na hamtazikwa bali nitawachoma moto kupoza roho nyingi zilizoangamia mikononi mwenu"



Aliongea Fahad kuishika ile fimbo yake, akafanya kama anakumuta hivi. Ukatoka upepo mkali sana, mfalme na wale wazee watatu wakawahi kuwek ngao ya Qi kwasababu walijua shambulio hilo halikuwa kawaida.



Hakukusikika hata sauti, baada ya upepo huwo kukata. Badala yake vilisikika vishindo tu ya miili ikianguka huku ikitengana na vichwa vyao. Karubu nusu ya wanajeshi wote walipoteza maisha katika shambulio hilo.



"Inaonekana sijaweka nguvu ya kutosha, nilitaka niwamalize wote" aliongea Fahad na kutikisa mkono wake kama vile alikuwa ananyoosha viungo.



"Oi oi oi, umeona kilichotokea. Upepo tu umesambaraisha nusu. Huyu mtu si wa kawaida, si tuliambia hana madhara huyu kwamba tunakuja kama kubeba mzoga na kuondoka tu. Jamani mini sijaja kufa leo, ndio kwanza nimeoa wiki iliyoisha tu" aliongea mwanajesho mmoja akiteteka.



"Kaldiryus itika wito" aliongea Fahad na kuinua mkono juu, sekunde chache tu ukafika upinde mkubwa wa chuma. Ulipotuwa tu mkononi kwake akazunguka kwa kasi na kuachia shambulio jingine. Hakuna alietegemea hilo kwasababu hakuwa hata na mshale mkononi.



Lakini kitendo cha kuuachia tu ukatokea mshale wa upepo uliozungukwa na Qi. Mshale huwo ukasafiri kwa kasi ya umeme. "Nguruma" akanena, mlipuko mkubwa ukasikika na kusababisha vumbi jingi.



Vumbi lilipotoweka walikuwa wamebakia watu wanne tu. Mfalme na wale wazee watatu, kikichofuata ilikuwa ni harufu kali sana ya damu.



"Haiwezekani" aliongea mmoja kati ya wale wazee.



"Haiwezekani nini, angalia nyuma yako kama kuna roho iliyopona" aliongea Fahad na upinde mdogo ukatokea ukielekea juu. Alikuwa akitabasamu kama kuwakejeli.



"Muueni, tukimuacha leo atatupa sana tabu mbele" akiongea mfalme. Wale wazee watatu wakapita mbele kwa kasi na kufanya mashambulizi yao makali zaidi. Vumbi likatibuka na lilipitawanyika hakukuwa hata na mchubuko katika mwili wa Fahad.



Aliwaangalia kisha akatikisa kichwa kuwasikitikia, akapiga hatua moja tu mbele. Wale wazee wakajikuta wakigandamizwa na nguvu iso onekana. "Pigeni magoti" ikatoka amri kinywani mwa Fahad. Pasi na wao kutaka wakadondokea magoti na vichwa vikagonga ardhini.



Fahad akawapita bila hata kuwagusa lakini nyuso zao ghafla zikapauka na miili yao kuwa ya baridi. Walipoteza maisha pasi na wao kutambuwa kama wamekufa.



"Umebakia peke yako" aliongea Fahad na kumuangalia mfalme Lorei aliekuwa amesimama kifua mbele. Bado aliamini kabisa alikuwa na uwezakano wa kushinda vita hiyo.



"Unadhani siwezi kukuuwa" aliongea mfalme Lorei.



"Ingekuwa miezi sita iliyopita labda ungefanikiwa hata kunigusa lakini kwasasa huna hata asilimia moja ya ushindi" alijibu Fahad na kucheka.



Mfalme huyo akataka kutoa upanga wake lakini akashangaa mwili wake ukikataa kutoa ushirikiano. Hapo ndio akahisi hali ya ubaridi kifuani kwake.



"Mi nkajua utakuwa na moyo tofauti na binadamu wengine lakini inaonekana huna tofauti" aliongea Fahad mkononi akiwa na donge kubwa la nyama lililokuwa linadunda.



Macho ya mfalme Lorei yakatuwa kifuani kwake na kukuta shimo kubwa upande wa kushoto. "Nisalimie Sakyubi huko unapokwenda" Aliongea Fahad na kuuminya moyo alokuwa nao mkononi.



Mfalme Lorei akaanguka chini na mwili wake ukatulia, hakuwa na uhai tena. Sekunde chache baadae wakafika wale saba.



"Kateni kichwa cha huyu mpuuzi, miili ilobaki chomeni moto. Kisha tutaelekea Lorei kwenda kunyofoa mizizi" aliongea na kugeuka na kuelekea katika ngome yake.



Alichokifanya hapo kiliacha mshangao mkubwa katika mioyo ya watu walioshuhudia tukio zima. Watu zaidi ya elfu kumi wamekufa ndani ya dakika zisizozidi kumi na tano. Vita ambayo walijipanga nayo kwa muda wa miaka mitatu imeisha ndani ya dakika kumi na tano.



"Nina uhakika alipo mfalme Lorei analaani tu saa hivi" aliongea Garaaji na kutoa upanga wake na kukata kichwa cha aliekuwa mfalme wa Lorei.



"Jamani ni mimi tu au kuna mwingine ambae ameshindwa kuona daraja halisi la meya" aliongea Rahee. Pembeni yake alikuwepo Oberoi, nae akatikisa kichwa kukubaliana na Rahee kuwa hakufanikiwa kuona daraja la Fahad.



"Hiyo ina maanisha kuwa amefika daraja la Nirvana, mtu yeyote aliekuwa chini ya daraja la milele hawezi kuona uwezo wa mtu aliefika daraha la Niravana na kwenda juu" aliongea Nephira.



"Hili ni dudu la aina gani" Fang Shi akajikuta akiropokwa na kuwafanya wengine wote wacheke. Baada ya hapo wakazikusanya maiti pamoja na viungo vilivyosambaratika na kuvichoma moto.



"Meya anaelekea safari ya kuwa katika daraja la wanaojiita miungu" aliongea Rondelif, akabadilika kuwa moshi na kutoweka.



"Haki ya nani, mtu wa ajabu atazungukwa tu viumbe vya ajabu" aliongea Garaaji na kugeuza macho. Ni kweli kabisa, kati yao hakukuwa hata na mmoja angethubutu kusema kuwa mtu wa kawaida. Walikuwa ni kikosi cha watu wasio wa kwaida kabisa.



Ndani ya ofisi ya meya.



"Hongera meya kwa kufika daraja la Nirvana" waliongea kwa pamoja na kuonesha heshima ya hali ya juu.



"Hahaha! Inueni vichwa vyenu, ipo siku na nyinyi mtafika. Nina imani kabisa juu ya hilo" aliongea na kukaa kwenye kiti kisha akawapa ishara wakae, nao wakafanya hivyo.



"Ingieni mkataba wa damu na mimi" aliongea bila kupepesa macho. Wote wakashtuka na kumuangalia kwa macho yalioyokaribia kutoka kwenye mapango yake. Wote walifahamu kuwa mkataba wa damu ulitumika kati ya binadamu na wanyama lakini si kati ya binadamu na binadamu.

 
Black Star 2: Nemesis 45







"Mimi niko tayari" Oberoi ndie aliekuwa wa kwanza kukubali bila kuuliza swali lolote. Wengine wote wakamuangalia kwa macho yalioyojaa mshangao.



"Mkataba huu hautwakuwa kama ule wa mnyama wa kiroho na bwana wake bali utakuwa mkataba huria ambao hautawazuia kufanya mtakalo. Kwa kuingia mkataba na mimi ninyi ndio mtafaidika zaidi, nahitaji watu wenye nguvu sana. Safari inapoelekea itakuwa ngumu zaidi na sio kama nitakuwepo kila siku kuwasaidia".



"Kuingia mkataba na mimi kutawawezesha karika uwezo wengu. Qi niliokuwa nayo itawafikia na nyinyi na itawapa faida kubwa sana katika safari yenu ya martial art. Mkataba huu utakatika endapo tu mimi nitapoteza maisha, na haitakuwa kama kwa wanyama kwamba nikifa mimi na nyinyi mtakufa, hapana bali mtakuwa huru na kuendelea na mambo yenu kama kawaida" alieleza kwa kina kuwatoa wasiwasi.



Baada ya maelezo hayo wote wakashusha pumzi kisha wakainamisha vichwa kuashiria kukubali. Baada ya hapo, Fahad akatikisa mkoni katika pete aliyovaa mkono wake wa kulia zikatoka karatasi saba. Akamkabidhi kila mmoja karatasi moja, "kata kidole weka sahihi ya damu" aliongea.



Wote wakafanya hivyo kisha wakazirudisha mezani, Fahad nae akakata sehemu katika kidole chake na kuweka sahihi yake katika kila karatasi. Baada ya kitendo hicho tu, karatasi zile zote zikawaka moto.



Ghafla wote saba wakaanza kuhisi joto kali sana katika miili yao. "Kaeni kitako na muanze kuzungusha Qi zenu, fanyeni kwa utaratibu bila pupa" aliongea na kusimama kisha akalegeukoa dirisha na kuangalia nje. Alionekana kama aliekuwa akiwaza jambo muhimu sana katika kichwa chake.



Kadri walivyozidi kuzungusha Qi zao, ndivyo walivyohisi mabadiliko katika miili yao. Baada kama nusu saa hivi, alama ikaanza kujichora nyuma yya viganja vyao. Ilikuwa ni nyota ya pembe sita.



"Hiyo ni insignia yangu, haitafutika katika viganja vyenu mpaka pale nitakapopoteza maisha. Kwa kuwa na alama hiyo, nitakuwa na jua afya zenu zinaendaje, hivyo itanipa mimi wakati wa kutoa msaada pale mmoja kati yenu atakapokuwa hatarini. Pia tutaweza kuwasiliana hata tukiwa umbali wa sayari moja na nyingine" alifafanua.



Baada ya saa nzima kukatika wote wakasimama, miiki yao ilionekana kujaa afya. "Tunashukuru kwa muongozo wako" waliongea kwa pamoja.



"Halafu na sisi tumekuandalia zawadi" aliongea Nephira na kufungua kabati kubwa lililokuwepo ndani ya ofisi hiyo. Ndani ya kabati hilo kulionekana sanduku kubwa la chumam. Rahee akalivuta na kuliweka chini.



Garaaji akalisogelea na kulifungua, ndani ya sanduku hilo kulikuwa na vipande vya suti maalumu. "Wakati ukiwa umejitenga kwa ajili ya mafunzo, tulijadili na kufikia tamati kuwa baada ya kumuua mfalme Lorei wewe ndio utakuwa mfalme. Hivyo tumekutengezea suti yako ambayo itakuwakilisha kimuonekano kama mfalme" aliongea Fang Shi na kuwageukia wengine. Akawapa ishara waondoke, wote wakaondoka isipokuwa Nephira peke yake.



*********



Robo saa baadae.



Mlango wa ofisi ukafunguliwa, akatangulia Nephira kisha akakaa pembeni. Nyuma yake akafuata mtu mkubwa ndani ya suti ya kung'aa.



"Sisi wote tunatoa heshima zetu kwa mfalme Fahad" Fang Shi na wenzake wakaongea kisha wakapigia magoti. Hawakuwa peke yao, kulikuwepo na kundi kubwa la watu. "Uishi maisha marefu ewe mtukufu mfalme, sisi wote tupo chini ya huruma yako. Hata ukituambie tuingie ndani ya shimo la moto mkali basi tutaingia bila kuuliza sababu" Sauti ya wengi ikasikika. Nephira nae akaungana na wengine na kupiga goti.



Fahad akawaangalia kisha akashusha pumzi, hakutaka kuwaangusha watu hao waliomuamini. Akainuka mkono juu na baada ya sekunde chache ile fimbo yake ya chuma ikafika kwa kasi na kutuwa mkononi kwake. Akaigonga chini mara tatu na mara ya nne akaigonga kwa nguvu.



"Kuanzia leo, ngome hii imebadilishwa jina. Itaitwa ngome ya Asura, katika ngome hii hakutakuwa na matabaka. Sheria zitafanya kazi kwa wote, hakutakuwa na mtumwa. Ukifanya kazi utalipwa, hakutakuwa na mtu ambae atakuwa juu ya sheria. Sheria zitaandikwa na kila mtu atakuwa na wajibu wa kufuata. Yeyote atakaekiuka ataadhubiwa na adhabu pia zitaainishwa kwenye sheria. Kila mtu katika ngome hii atakuwa na haki sawa" akiongea kwa nguvu.



Sauti yake ilipeleka mawimbi ya heshima kwa wengi, "kama mfalme wa ngome hii agizo langu la kwanza. Watumwa wote wapewe uhuru wao na walipwe kutokana na muda waliofanya kazi. Baada ya hapo ikiwa mtu atataka kuendelea kufanya kazi kwa fulani basi wataingia makubaliano na watajadili na malipo. Hakutakuwa na mtu atakae fanya kazi bure" aliongea.



Mayowe makubwa yakasikika kutoka katika umati mkubwa wa watu, japo kulikuwa na kundi kubwa la watu ambao agizo hilo liliwakera lakini hawakuwa na budi kukubali amri ya kwanza kutoka kwa mfalme. Ingekuwa ni uvunjaji wa heshima na utovu wa nidhamu.



Fahad akawangalia wale wajenerali wake na kuwapa ishara wamfuate. Wakaondoka katika ngome hiyo na kwa kasi ya ajabu wakaanza kuelekea ngome ya Lorei kwenda kufagia wanafamilia wa mfalme waliobakia.



Baada ya masaa matatu wakawasiki nje ya ngome ya Lorei, "nendeni mkamalize" aliongea Fahad na sita kati ya hao saba wakaondoka kwa kasi, Nephira akabakia na Fahad. Majenerali sita walifanya mauaji ya kinyama, hawakuacha hata mtoto mdogo aliekuwa na damu ya kifalme. Na baada ya nusu saa geti kubwa likafunguliwa, akatoka Garaaji na kufika mbele ya Fahad kisha akapiga goti.



"Tumekamilisha" aliongea.



Kwa mwendo wa taratibu Neohita akatangukia na Fahad akafuata nyuma. Ndania yaa ngome hiyo watu walikuwa wakishangaa ujio wa watu hao ambao wamesababisha vurugu katika ngome hiyo. Wakatembea mpaka sehemu ya makutano katika uwanja mkubwa.



Fahad akatembea mpaka katikati ya uwanja huwo, akasimama naa taratibu akaanza kupaa mpaka alipofika usawa wa kuonekana na watu wote.



"Mbele yenu ni mfalme wa ngome Asura, mwanzo iliokuwa ikiitwa Zinga. Furahini kwa maana masia wenu amewaletea uhuru" aliongea Fang Shi na kumuangalia Fahad aliekuwa akielea.



"Kuanzia leo ngome hii itakuwa chini ya utawala wangu, na mtu atakaeniwalikilisha atakuwa Garaaji. Hivyo namtawaza Garaaji kuwa Gavana wa ngome hii" aliongea.



Garaaji alivyosikia akashtuka, maana hakutegemea jambo hilo kabisa. Akaangukia magoti yake huku machozi yakimtoka. "Mimi Garaaji nina ahidi kuiongoza ngome hii kutokana na muongozo wako, ahsante kwa kuniamini" aliongea.



"Baada yaa hilo, watumwa wote waachiwe huru na walipwe. Wafungwa wote watasimama kotini kujibu mashtaka yao, ili na wao wapate hukumu na haki yao. Ikiwa mtu amesingiziwa au kufungwa bila hatia, kila aliehusika na kifungo hicho atamlipa na atakae kataa kufanya hivyo basi atatumikia kifungo mara mbili alichotumikia mtu huyo" aliongea Fahad.



"Mwisho kabisa, ghala la kifalme litafunguliwa na kila mtu atapokea kiwango kadhaa cha fedha kwa ajili ya kuanza maisha vizuri. Maelezo mengine nitampa Garaaji. Ni matumaini yangu kuwa hakuna atakae kiuka maagizo yangu kwa maana kufanya hivyo hakutakuwa na mwisho mzuri" alimalizia.








MWISHO WA KITABU CHA PILI..................................




ASANTENI NYOTE KWA KUSOMA HADI MWISHO.




NAOMBA MSAMAHA KWA KUCHELEWA KUIMALIZA KKWA MUDA MLIO HITAJI.




NAOMBA PIA KUWALAUM KWA KUGOMA KUNUNUA LABDA KAZI HII SIYO NZURI KWENU INGAWA MMEAMUA KUSOMA. WAKATI MWINGINE NITAJITAHIDI KUFANYA VIZURI.



MWISHO KWA HAPA.






KITABU CHA TATU NA NNE UTAKIPATA KWA TSH 10000/=


PIA NICHUKUE NAFASI NYINGINE KUWAKARIBISHA KWENYE UZINDUZI WA KITABU CHANGU KINGINE KIPYA ............




UKANDA WA GAZA


25/5/2024


MGENI RASMI NI WAZIRI WA.....................................................



HUU SI UTANI
 
KITABU CHA TATU
BLACK STAR 3





Black star 2: Nemesis 46







Baada ya hapo Fahad akamuachia maagizo mengine Garaaji na kuondoka na wengine akimuacha hapo. Ndani ya miaka miwili, Fahad akazipindua ngome nyingine kubwa nne. Moja akaikabidhi mikononi mwa Oberoi na nyingine mikononi mwa Rondelif. Mbili zilizobaki watawala wake walisalimu amri na kuapa kuwa chini yake hivyo akawaacha waongoze kwa niaba yake.



Ngome ya Asura.



"Muda niliyoaambia nitakaa hapa umekwisha na ndani ya muda huwo nimetimiza ahadi zangu zote" aliongea Fahad akiwa kakaa kwenye mbele ya majenerali wake.



"Hata kama bado tunahitaji muongozo wako zaidi lakini tunafahamu pia kuwa safari yako ni ya lazima" akiongea Fang Shi. Wote wakaangaliana na kuonesha simaniza katika nyuso zao.



"Hii ni safari yangu ya mafunzo, natakiwa nijifunze kadri inavyowezekana kabla ya miaka kumi na tano ya Dao haijaisha. Ila msijali, nikiwa narudi kuelekea Dao, nitapita hapa kuwachukuwa wote. Nimeamua kuwa katika sayari hii ndio yatakuwa makazi yangu rasmi. Hivyo nitarudi hapa na watu wengine pamoja na familia yangu pia. Nitahitaji msaada kuwasafirisha katika koridoo ya muda" aliongea Fahad.



"Tutakuwa tunasubiri ujio wako tena mtukufu mtawala" waliongea kwa pamoja na kuinamisha vichwa vyao.



"Nephira na Rahee, ninyi mtaondoka na mimi" aliongea na kuwaangalia wawili hao ambao walitikisa vichwa tu.



Baada ya kikao hicho, Fahad akawakabidhi mipango maalum kabla ya kuwaruhusu. Akabakia ofisini peke yake na kubadili nguo. Akatoka akiwa kavaa mavazi ya kawaida, wote kwa pamoja wakawasindikiza mpaka umbali mkubwa na ngome hiyo kisha wakaagana nae na kuondoka.



"Tunasubiri nini hapa" aliuliza Rahee.



"Utajua ndani ya dakika chache" alijibu na kutabasamu.



Ghafla upepo mkali sana ukaanza kuvuma, upepo ulikuwa na vugu vugu la joto kali sana. Sauti ya mbawa zikipasua anga ikasikika, kadri muda ulivyokwenda ndivyo sauti hiyo ilivyokaribia na kuwa kali.



Vum!



Akapita ndege mkubwa kwa kasi, Fahad akatabasamu na kuinua mikono yake juu kama dalili ya kuonesha furaha yake. Ndege mkubwa mweusi mwenye kipanga cha dhahabu katika kichwa chake akatuwa na kuinamisha kichwa.



"Fahad, ni muda mrefu hatujaonana" aliongea ndege huyo na kufungua mbawa zake kisha akainamisha kichwa.



"Inaonekana uwezi wako umeongezeka mara dufu, Vamilion" aliongea na kumgusa katika bawa lake la kushoto.



"Naona hata wewe umefika daraja la Nirvana" alijibu ndege huyo bila kuficha furaha yake, alihisi sasa anaweza kutumia uwezo wake wote akiwa na rafiki yake mpendwa.



"Nehpira, Rahee ni muda mrefu hatujaonana" aliwageuka wawili hao na kuwaangalia. Wote wakaangaliana, kumbukumbu zao hazikuwa na picha ya ndege huyo.



"Hahaha! Gorigo sasa amekiwa Vamilion" aliongea ndege huyo na kuinuwa kifua chake. Wawili hao wakaangaliana na kuonesha mshangao mkubwa. Fahad akaruka na kutuwa katika kichwa cha Vamilion kisha akawapa ishara wapande.



"Tunaelekea Vajra" aliongea Fahad na kukaa kitako, "tutachukuwa muda gani" aliuliza.



"Kuna milima katika bara la mashariki, katikati ya milima hiyo kuna njia ya kuelekea Vajra, kama kumbukumbu ziko vyema basi mlango huwo unafunguka mara mbili kwa mwaka na sasa hivi ni mara ya pili mwaka huu. Umebakisha masaa yasiyozidi matatu kufunga" alijibu.



"Kutoka hapa mpaka bara la Mashariki ni mwedo usiopungua miezi mitatu" aliongea Nephira.



"Hehehehe kwa wengine, kwa mtukufu Vamilion ni mwendo wa dakika chache tu" alijitamba Vamilion. Akafunguwa mbawa zake na kuzikumuta kwa nguvu. Hatua hiyo moja tu, akapaa kwa kasi mpaka katika mawingu na kutulia kidogo.



"Tafuteni sehemu za kushika" aliongea ndege huyo akiinua tema mbawa zake. Fahad akasimama na kurudisha miko yake nyuma. Hakuhangaika kushuka sehemu, uwezo ulikuwa unapingana kabisa na asili, haukuelekzeka kwa njia au sababu za kawaida.



Nephira na Rahee wakalala katika mgongo wake na kushika manyoya yake vizuri. Upepo mkali ukaanza kuvuma, mwili wa Vamilion ukaanza kung'ara kabla ya kuondoka kwa kasi kubwa sana. Fahad wala hakutikisika kutokana na kasi hiyo, alikuwa akifurahia kabisa.



Baada dakika tatu Vamilion akasimama mbele ya milima miwili mikubwa. Mwili wake ulikuwa ukitoa alama za radi na macho yake yalikuwa kama yanawaka moto moto. Katika mdomo wake kwa mbali ulionekana moshi ukitoka.



"Tushafika" aliongea taratibu akishuka, "usishuke, endelea na safari" Fahad alitoa amri. Vamilion akazunguka kwa kasi na kufyetuka, safari hii kadi yake ilikuwa mara tatu zaidi kuliko ile ya kwanza.



Akapita katika mlango huwo na kuendelea na kasi hiyo. Ndani ya mpasuko huwo wa muda, waliona watu wengine wakisafiri. Kila mtu alijaribu bahati yake kwasababu haikuwa kazi rahisi kuputa katika koridoo hizo za wakati. Ilihitaji mtu uwe na Qi ya kutosha na nguvu zisizo za kawaida ili kufika upande wa pili.



Kwa Fahad na Vamilion hilo halikuwa tatizo, wawili hao hawakuwa viumbe wa kawaida. Fahad akainamba na kumsika.



"Utaweza kunikamata" aliongea akitabasamu.



"Ukishuka mi nakuacha" aliongea Vamilion, aliamini kabisa Fahad hakuwa na uwezo mkubwa kuzidi yeye. Fahad akaruka na ghafla mgongoni kwa kujatokea mbawa kubwa za dhahabu. "Jaribu kuwa karibu" akaongea na kuondoka kwa kasi. Alionekana kama mstari tu, Vamilion kuona hivyo akatabasamu na mwili wake ukaanza kutikisika.



Mbawa zake pamoja na mkia zikabadilika rangi na kuwa za dhahabu. Viini vya macho yake vikawa vyekundu, akatoa mlio mkali sana kabla kuongeza kasi. Nae akaonekana kama mstari tu wa dhahabu. Sekunde chache akawasiki pembenu ya Fahad.



"Siyo mbaya lakini hapa mimi bado sijatumia hata theluthi moja ya uwezo wangu" aliongea Fahad akizunguka. Alikuwa ni kama anamdhihaki, "hahaha! Baba yako hapa natumia asilimia chache sana. Pia mimi nina hawa ndugu zako mgongoni. Nikienda zaidi ya hivi nina uhakika hawataishi kuona mwanga upande wa pili" aliongea.



"Mnamsikia, anadhani nyinyi mna uwezo mdogo sana" aliongea Fahad.



"Vamilion nenda utakavyo usijali kuhusu sisi" Rahee aliongea kisha mwili wake ukazungukwa na weigong na Nephira wake ukazungukwaa Qi.



Kwa mara nyingine tena, mwili wa Vamilion ukaanza kutetemeka. Katika kichwa chake likatokea taji jekundu la moto. Mbawa zake ambazo zilikuwa za dhahabu zikabadilika na kuwa nyeuso na kutoa moshi kabla ya kuwaka moto wenye rangi mbali.



"Moto wa azure" aliongea Fahad na kugeuka mbele, wakati huwo huwo huwo akahisa kitu kimempita bila kuacha sauti yeyote. Alikuwa ni Vamilion, kasi yake haikutoa sauti yeyote ile.



Fahad akajibonyeza sehemu katika moyo, Qi nyingi ikaanza kuzunguka katika mwili wake kisha akapotea. Kasi yake ilimfanya asihisi chochote, ni kama alikuwa akiteleza tu katika anga hiyo. Kwa mbali akaanza kuona moto na baada ya sekunde chache akafika pembeni ya Vamilion na kumkonyeza kisha akatoweka tena bila kuacha hata alama kama lipita katika njia hiyo.

 
Black star 2: Nemesis 47

Tariq Haji

0624065911

"Umechelewa" aliongea Fahad akiwa amesimama kwenye kingo za mlima mkubwa, mikono yakw ikiwa nyuma. Vamilion akatua pembeni yake, usoni alikuwa na ishara za sonono. Rahee na Nephira wakashuka kutika mgongo wa ndege huyo mkubwa na kusimama pembeni ya Fahad.

Upepo wa baridi ukawapitia kabla miale mekundu ya jua lichomozalo asubuhi kuwalaki. Fahad akavuta pumzi nyingi na kuitoa kisha akamuangalia Vamilion.

"Rafiki usiwe na huzunu sana, uwezo wako ndio kwanza umeingia katika daraja la Nirvana. Ukipata muda zaidi kuuzoea utaweza kwenda zaidi kuliko mimi" aliongea akimgusa katika bawa lake la kushoto.

Wanne hao ndio walikuwa wakwanza kuwasiki Vajra katika kundi lililoingia siku moja katika koridoo ya wakati. "Nguvu za asili zipo kwa wingi zaidi kuliko Sekai" aliongea Nephira, Fahad akamuangalia bibie kisha kwa kutumia jicho lake busara akaangilia mzunguko wake Qi.

"Hahaha! Tafuta sehemu ukae, nguvu zako zimefikia kiwango cha juu zaidi katika daraja lako la sasa, unatakiwa kuvuka" aliongea. Nephira akasogea pembeni na kukaa kitako, akakunja miguu na kufumba macho. Qi nyingi ikaanza kusafiri kutoka kwenye mazingira na kuingia kayika mwili wake.

Nephira akaiongoza Qi hiyo mpaka kitovuni kwake ambako dantian ndipo ilipokuwa imekaa. Kadiri muda ulivyokwenda ndivyo dantian yake ilivyozidi kujaa na kuanza kutengeza nyufa.

Zzzzzz!

Mlio kama wa waya za zenye kupitisha umeme mkali mkasikika kabla ya Nephira kufumbua macho. Mwanga mweupe ukatoka machoni na mdomoni kwake ukifuatiwa na mwanga ulioelekea juu na kutobia mawingu kama nguzo.

"Hongera malkia kwa kufika daraja la milele" aliongea Rahee akikunha ngumi ya kiganja kimoja na kukutanisha na kiganja kingine.

"Ahsante" alijibu na kutabasamu akisimama.

"Hongera" aliongea Fahad na kumuangalia, Nephira alipoyakutanisha macho yake na mwamba huwo akahisi mapigo ya moyo yakimuenda mbio.

Badum! Badum! Badum.

"Nyoika" akaita Fahad, ile fimbo yake ya chuma ikatokea. "Mimi na wewe hatuna mkataba, unaweza kuchagua bwana wako" akaendelea. Kwa kawaida mtu atadhani kwamba hiyo ilikuwa ni nafasi ya silaha hiyo kutafuta mmiliki wake. Lakini haikuwa hivyo, maneno hayo yaliyotoka mdomoni mwa Fahad yalimaanisha kuwa dimbo hiyo iingie mkataba na Nephira.

Ikapaa angaani kwa kasi, walioishuhudia kwa mbali walidhani ni kimondo. Kisha ikarudi chini kwa kasi mara mbili ya iliyoondoka nayo na kutuwa pembeni ya Nephira.

"Kuanzia leo ni yako hiyo" aliongea Fahad akimuangalia.

"Wewe utatumia nini" aliuliza.

"Nitatfuta silaha yenye kuhimili uwezo wako, hiyo haiwezi tena, itavunjika nikiendelea kuitumia" alijibu.

Nephira akatoa kisu kidogo na kukata kiganja chake, akaishika fimbo hiyo na kuingia "itika nyoika". Fimbo iliyokuwa nyeusi ikaanza kubadilika rangi na kuwa ya dhahabu, michoro ya ajabu ikaanza kujichora. Ilipokamilika ikatoa mwanga mkubwa sana na kutoweka.

"Hongera tena malkia" aliongea Rahee na kutoa heshima, Fahad akamuangalia na kuachia tabasamu laini. "Usijali ipo siku na wewe utapata silaha inayoendana na unachojifunza. Pia tukiwa huku, hakuna haja ya kuitana kwa majina ya vyeo vyetu" aliongea.

"Badi naomba nikuite kaka mkubwa na malkia nimuite dada mkubwa" aliongea Rahee, alishindwa kabisa kuwaita kwa majina yao.

"Sawa, bora hivyo" aliongea Fahad na kugeuka mbele kisha upandr ambao alikuwa Vamilion. "Rudi ndani" akaongea, "hahaha! Haiwezekani tena, kwa nilipofika sasa siwezi tena kuishi ndani ya mwili wako" alijibu kisha akapaa na kuzunguka anagani mara kadhaa kabla ya kurudi chini kwa kasi.

Taratibu mweli wake ukaanza kupungua ukubwa, akatua begani kwa Fahad akiwa katuka umbile la tai mweusi mwenye macho mekundu. "Hapa ndio yatakuwa makazi yangu" akaongea na kubetua kifua chake mbele.

"Unavyojisikia" alijibu Fahad na kugeuka upande ambao njia ilikuwa inashusha na kuanza kuondoka. Nephira akafuata upande wake wa kulia na Rahee upande wa kushoto. Baada ya saa taty wakafika katika kitako cha mkima huwo.

"Karibuni wageni kutika sayari nyingine" sauti ya kizee iliwakaribisha. Pembeni yake kulikuwa na gari la farasi.

"Ahsante" alijibu Fahad na kumgeukia Rahee, akatikisa kichwa na kusogea alipo mzee huyo.

"Tunataka taarifa kuhusu mji uliokuwa karibu na hapa" aliongea naa kutoa tael (pesa) moja ya dhahabu, mashavu ya yule mzee yakawa mekundu.

"Hehehe! Usijali umepata" aliongea akipeleka mkono wake mbele kupokea pesa hiyo.

"Mji wa karibu unaitwa Kunlun" akaanza kuongea, alitoa taarifa zote amazozijua kuhusu mji huwo. "Kama mnataka nitawapeleka" akaongezea. Rahee akamuangalia Fahad na baada ya muda akamgeukia tena yule mzee.

"Tutashukuru sana ukiwa utafanya hivyo" akaonge, yule mzee akafungua mlango na wote wakapanda na kukaa. Akaufunga kisha akapanda kwenye kiti cha mbele na kuwachapa farasi kiboko. Wakatoa sauti kisha wakaanza kuondoka.

"Tungeenda wenyewe ingetuchukuwa muda mchache sana" aliongea Nephira akikunja mdomo.

"Kwasababua wewe umezaliwa kwenye familia yenge uwezo huwezinjua mahangaiko wanayopitia watu ambao wapo katika haki duni" alijibu Vamilion akiwa ameketi kwenye mapaja ya mwanamke huyo.

"Mpaka umuone mtu asubuhi yote hii yuko kijiweni, basi tambua kuwa anatafuta chakula cha familia yake" aliongezea Fahad.

"Kumbuka hata uwe na nguvu kiasi gani, usipoteze asili yako. Sisi binadamu tunatakiwa kufikiria kuhusu wengine pia, unafika sehemu kuna mtu anauza chakula, hata kama sisi wana martial art hatuhitaji kula kwasababu tunapata kila kitu tunachokitaka kutoka nguvu asili. Nunua chakula hapo na ule, kwanza itakusaidia kukumbuka faida ya kuwa na ulimi na pili utatengeza tabasamu kwa muuzaji" aliendele.

"Faida ya watu kama sisi ni kuhakikisha ambao hawakujaalia kuwa na uwezo kama wetu wanaishi maisha bila shida".

"Kwanini umefunga safari hii" alishindwa kuzuia dukuduku lake Nephira, akaamua kuuliza.

"Matarajio ya wengi ni kutafuta nafasi ya kuwa na uwezo mkubwa, kwangu mimi sio hivyo japo kuwa na nguvu ni muhimu sana katika njia ya martial art. Mimi ninefunga safari hii kutafuta ukweli kwasababu ukweli ndio utakaomuweka mtu huru" alijibu Fahad.

Yule mzee muendesha farasi alikuwa akiyasikia mazungumzo hayo vyema kabida. Michirizi ya machozi ikajichora katika mashavu yake, "bado watu wenye utu wapo" alijisemea.

Baada ya safari ya saa nne, gari ya farasi ikasimama kisha yule mzee akagonga mlango. Rahee akaufungua na kushuka, "samahanini tutapumzika hapa kabla ya kuendelea na safari. Farasu wangu wote ni wazee, wanahitaji kupumzika" aliongea.

Rahee akazifikisha taarifa hizo kwa Fahad, wakashuka. Karibu na eneo hiko kulikuwa na mgahawa uliochakaa. Pembeni ya mgahawa huwo kuliko na mto mkubwa uliokuwa ukisafiri taratibu.

Wakati wanaelekea kwenye mgahawa, Fahad akasimama na kuwaangalia wale farasi wawili. Walikuwa weusi tii, weusi ambao si wa kawaida. Kwa kutumia jicho lake la tatu akawaangalia vizuri na kuthibitisha mashaka yake. "Hawa si farasi wa kawaida" alijisemea na kuungana na wengine.
 
Black star 2: Nemesis 48

Tariq Haji

0624065911

"Ulikuwa unaangalia nini" aliuliza Nephira baada ya Fahad kukaa. Kabla hajaongea, akafika mubudumu.

"Nipatie chai tu" aliongea Fahad na kuwaangalia wengine, kila mmoja akaagiza anachotaka. Wakati wanaendelea kula upepo wenye kasi ndogo ukawapitie. Kwa wote hapo upepo huwo ulikuwa wa kawaida lakini si kwa Fahad. Mara ya kwanza hakuupatikiza sana lakini ulipovuma kwa mara ya pili viini vyake vya macho vikajiminya.

"Samahani" aliinua mkono juu na kumuita mhudumu, mtu mmoja mzee kiasi akafika akiwa na mshaka usoni kwake.

"Mpendwa mteja hujavutiwa na chai yetu" aliongea kwa sauti ya kinyonge. Fahad akatabasamu kabla ya kujibu, "chai yenu ni nzuri sana hata hivyo sijakuita kwasababu ya hilo".

" Oh! Ni kitu gani kingine" akauliza kaa bashasha.

"Ni kuhusu huwo mto hapo mbele, nimegundua kwamba maji yake hayendi kasi lakini sijahisi alama zozote za maisha ndani yake" aliongea Fahad.

"Uko sahihi kabisa, ni hadithi ambayo inaeithishwa kutoka kizazi hadi kizazi. Inasemekana zamani sana eneo hili kulikuwa mji mkubwa wa kibiashara. Lakini siku moja inasemekena mbingu ilipasuka na kitu cha ajabu kikadondokea eneo hilo. Kuanzia hapo samaki na wadudu wengine wakaanza kulihama hili eneo. Na baada ya muda ardhi ikaanza kupoteza rutuba na mwishowe kabisa watu wakakimbia kutokana na majanga" alielezea.

"Anha! Sasa nimepaga jibu" akaongea na kuinuka, taratibu kwa hatua fupi akatembea mpaka kwenye kingo za mto na kusimama kwa muda. Pasi na matarajio ya wengi akapiga mbizi.

"Anafanya nini?" watu wengi wakagubikwa na sura ya swaali hilo isipokuwa Nephira na Rahee. Vamilion alikuwa amelala juu lile gari la farasi, akapigwa ukwenzi mdogo na kuendelea kulala.

Fahad akaogelea kwa kasi kuelekea chini, japo alipaona lakini alihisi kama hafiki. Baada ya dakika nzima akashangaa anaibuka sehemu. Kilikuwa ni kisiwa kidogo kilichomea vizuri kabisa. Akatoka kwenye na kuanza kutembea, ghafla akasimama na kutoa macho.

Mbele yake kulikuwa na kiumbe kikubwa sana, alikuwa ni mnyama ambae Fahad hajawahi hata kumuona. Akapwruzi katika kumbukumbu zake alizorithi kutoka mzee Karakantha lakini pia hakupata jibu.

Myama huyo baada ya kumuona Fahad nae akainua kichwa, wawili hao wakaangaliana. Hakuna hata mmoja aliejaeibu kufanya kitu. Kwa mara ya kwanza Fahad akahisi anapata uoga wa hali ya juu. Moyo wake haukuacha kwenda mbio, ama kweli ukijihisi una nguvu basi tambua yupo kiumbe ambae atakuwa amekuzidi tu.

Cha muhimu ni uhai.

Ndio sentensi iliyokuwa ikizunguka akilini mwa Fahad, alitambua kuwa kosa dogo tu hapo lingechukuwa uhai wake pasi na yeye kujuwa amekufanyaje.

Baada sekunde kadhaa mapigo yake yakarudi na kuwa tulivu. "Kama angetaka kuniua angeshafanya hivyo" akajisemea na kukaa kitako.

"Samahani kwa kuvamia mapumziko yako, jina langu ni Fahad" aliongea kwa sauti tulivu na yenye busara tele.

"Hatimae kuna kiumbe kimeitika wito wangu" alijibu mnyama huyo na kuinua kichwa kisha akamuangalia Fahad. "Umesikia kilio changu" aliongezea.

"Ndio, unaonekana upo kwenye maumivu sana".

" Sio mbaya sio mbaya, Fahad umesema ndio jina lako"

"Ndio, nikutambue kama nani"

"Myor ndio jina langu, uko tayari kusikiliza hadithi yangu"

"Ndio maana nimeitika" alijibu Fahad

"Mimi si mnyama wa sayari wala ulimwengu huu, najua wengu mnaamini baada ya Yuggdrasil hakuna limwengu nyingine. Hilo si kweli, anga la stari ni kubwa sana na lina sayari zaidi laki naa. Ninapo toka mimi hakuna mtu ambae amewahi fika. Ni viumbe tu wa asili nyingine ndio wanaishi".

" Kabila la myor ndio kabila kubwa zaidi na lilikuwa lenye nguvu, sisi tulikuwa ni kama miungu mpaka pale wengine kati yetu walipoamua kutusaliti. Ndani ya kabila, mdogo wangu aliamua kunigeuka na kushirikiana na wengine kunipindua. Vita kubwa sana ikazuka na kutokana na vita hiyo kabila letu zima likateketea isipokuwa mimi tu ambae nilifanikiwa kutoroka. Kwasababu nilikuwa na majeraha mengi sikuwaza sana nilifungua njia tu katika na kukimbia. Bahati mbaya nikaangukia hapa, kutokana na Qi kuwa kidogo sana hapa vidonda vyangu havikupona".

"Na huwo ni muda gani mpaka sasa" aliuliza Fahad.

"Nimepoteza hesabu za muda lakini ni zaidi ya laki sasa" alijibu.

"Nini sababu ya kuniita hapa"

"Ni ndogo sana, itachukuwa miaka mingi mpaka uhai kuacha mwili wangu. Ninachotaka kutoka kwako ni kunipa kifo cha haraka" alijibu Myor

"Kwanini umepoteza matumaini" aliuliza kwa mshangao.

"Kijana unatakiwa ujue uwezo wako ilie uendelee kuishi, nilipofika sasa hata kama nitaishi basi sitaweza kufanya chochote. Zaidi nitakaa hapa niendelee kusababisha madhara upande wa pili" aliongea. Usoni alikuwa na sonono, sio kama alitaka kufa lakini hakuwa na namna.

"Kijana kifo changu kitakuja na faidi kwako, katika mwili wangu kuna mionyo miwili. Punde tu baada ya kifo changu, mioyo yangu itabadilika na kuwa vito. Vito hivyo vitakuwa na asili yangu ndani yake, ukivipata mwagia damu yako na tutakuwa tumeingia mkataba wa milele. Utafanya nini vito vyangu ni juu yako japo ukitengeza silaha itakuwa vizuri zaidi" aliongea Myor.

"Funga macho, utahisi kama unachomwa na kitu" aliongea Fahad, jicho lake la kushoto likikuwa linatoka chozi jeusi.

"Black Star Orignal Technik: Void" alinena Fahad na kukutanisha viganja vyake, meridiani zote katika mwili wake zikafunguka pamoja na zile nane za ziada. Michoro meusi kajichora usoni kwake na katika ya nyusi mbele nyota ndogo ikatokea.

Alitaka kukifanya kifo chake kiwe cha mtelezo kadri inavyowezekana. Qi yake ikabadlika rangi na kuwa nyeusi ti.

Swuush!

Kichwa cha Myor kikadondoka chini, "ahsante Fahad" Ilikuwa kauli ya mwisho kabla ya macho kufunga. Vito viwili vikadondoka kutoka katika mwili wa Myor uliolala bila maisha.

Fahad akaviokota na kutoa kisu, akajikata kiganjani na kunyunyuzia damu yake. "Kuanzia leo utakuwa chini yangu na utaitika wito wangu, nitakutengeza katika silaha itakayonisindikiza katika maisha yangu yote mpaka mwisho. Na siku ikifika nitasafiri kukupeleka nyumbani kabla ya mimi kupumizika, amka! Myor"

Kivuli cha myor kikatoka kwenye vito hivyo na kunguruma kwa nguvu mpaka kusababisha tetemeko. Wakati huwo huwo nguvu za ajabu zikasafiri kutoka kwenye vito hivyo na kuingia mwili mwa Fahad. Bila kuchelewa akakaa kitako na kukunja miguu kabla ya kuanza kuizungusha Qi hiyo mwili mwake. Alihisi dantian yake ikitoa sauti na hatimae kupasuka kabla ya kujijenga upya.

Safari hii ilikuwa ni nyeusi ti, mwili wa Fahad ukatetemeka na kutoa mionzi ya rangi nyingi. Kutokana na maumivu makali akafumba macho na kung'ata meno.

Aaaagh!

Aligugumia, alipofungua macho alikuwa amesimama mbele ya njia mbili. "Chagua njia yako" alisikia mwangwi wa sauti kutoka kila kona ya eneo hilo. "Umefika daraja la Mythril, ni lazima uchague moja kati ya njia hizi mbili" aliisikia tena.
 
Heshima kwako mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…