Riwaya: I died to save my President

Riwaya: I died to save my President

HaMachiach

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2015
Posts
3,417
Reaction score
6,149
I died to save my president

Mtunzi Patrick Ck

Simu 0764294499

Season 1

Sehemu 1

Shughuli zote zilizopangwa kufanyika katika kikao cha bunge zilikamilika na kabla ya kusitisha shughuli za bunge kwa siku hiyo hadi siku inayofuata, spika wa bunge akamuita waziri anayeshughulika na bunge mheshimiwa William Kangoga ili aweze kutoa hoja ya kutengua kanuni.

“Mheshimiwa Spika, naomba kwa ruhusa yako sasa nitoe hoja kwamba bunge lako tukufu litengue kanuni ya bunge ili kuwaruhusu vijana wetu wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani yao ya kidato cha nne waweze kuingia bungeni hapo kesho. Mheshimiwa spika naomba kutoa hoja.”

Baada ya hoja ile kutolewa wabunge wote wakasimama na kuiunga mkono halafu spika akawahoji na wote wakakubaliana na hoja ile kwamba kanuni ya bunge itenguliwe na kuwaruhusu wanafunzi ishirini waliofanya vizuri katika mitihani yao ya kidato cha nne waweze kuingia bungeni ili waweze kupongezwa na bunge.

“Ahsanteni sana waheshimiwa wabunge kwa kukubali watoto wetu waje bungeni tuwapongeze na kuwatia moyo ili waweze kufanya vizuri zaidi huko mbele waendako,” akasema spika wa bunge halafu akasitisha shughuli za bunge hadi siku inayofuata saa tatu za asubuhi.
*********************
Ni saa tano za usiku sasa lakini bado Patricia hakuwa na usingizi. Yeye na mama yake walikuwa katika chumba kilichoko ghorofa ya nne ndani ya hoteli hii kubwa mjini Dodoma ijulikanayo kama Dodoma View Hotel. Ni moja kati ya hoteli yenye hadhi ya juu kabisa mjini Dodoma na ambayo wabunge wengi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hupenda kufikia.

“Patricia mbona hulali? Si unajua siku ya kesho itakuwa ndefu? Jitahidi ulale ili usije ukasinzia katika ukumbi wa Bunge,” akasema Bi Doroth Mwaukala, mama mzazi wa Patricia.

“Mama, nashindwa kabisa kupata usingizi siku ya leo. Usiku nauona mrefu sana,” akasema Patricia, binti aliyejaaliwa uzuri wa kipekee mno.

“Una wasi wasi?”

“Ndiyo mama, lakini si sana. Nawaza kuhusu kesho sijui itakuaje pale nitakaposhikana mkono na mheshimiwa waziri mkuu huku nikionekana katika televisheni nchi nzima. Mama, sikuwahi kuota siku kama ya kesho itakuja kunitokea katika maisha yangu. Bado siamini hadi hapo nitakaposhikana mkono na waziri mkuu ndipo nitaamini ni kweli. Mama, kesho ni siku yangu kubwa mno,” akasema Patricia.

Mama yake aliyekuwa akimtazama mwanae akatabasamu na kusema, “Usiwe na hofu Patricia. Hii si ndoto bali ni kitu cha kweli kinachokwenda kutokea hapo kesho. Kama ingekuwa ni ndoto tusingekuwa hapa Dodoma mida hii katika hoteli kubwa na nzuri kama hii. Patricia, unapaswa kujivunia mafanikio yako haya makubwa uliyoyapata. Mwanangu, umenitoa kimasomaso mimi mama yako kwani hakuna aliyemtegemea kama mwanafunzi aliyeshika namba moja nchini Tanzania atakuwa ni kutoka katika familia masikini kama ya kwetu. Umeidhihirishia nchi na dunia kwamba hata mtoto wa masikini anaweza akafanya mambo makubwa na ya kushangaza. Umelipandisha kileleni jina la familia yetu na kwa sasa sisi si watu wa kudharaulika tena kama ilivyokuwa hapo awali. Laiti baba yako angekuwa hai kushuhudia tukio hili, sipati picha angekuwa na furaha ya namna gani,” akasema Bi Doroth.

“Mama, sifa na shukurani zimwendee mwenyezi Mungu kwa neema na baraka zake nyingi kwangu lakini sifa na shukrani za pekee pia ni kwako wewe mama. Wewe ndiye kila kitu kwangu na ndiye uliyefanikisha haya yote yakawezekana. Umenipa ushirikiano mkubwa. Maongozi na maelekezo yako yameniweka katika nafasi hii nilipo sasa. Mama, unastahili sifa za kipekee kwa kunijali na kuwa nami na kunivumilia hata katika nyakati zile ngumu kabisa. Umejinyima mambo mengi ili mwanao niweze kusoma na haya ndiyo matunda yake,” akasema Patricia halafu akainuka na kuelekea dirishani, akalifungua na kuutazama mji wa Dodoma ulivyokuwa usiku hii.

“Huu ni mwanzo wa safari yangu ndefu ya maisha. Nina ndoto nyingi sana za kutimiza maishani na ndoto ya kwanza ni kuiondoa familia yangu katika umasikini huu mkubwa tulionao. Namuonea huruma mama yangu namna anavyohangaika kunisomesha. Lazima nikiri kwamba si kazi rahisi kwake lakini amejitahidi kwa kila namna na kuhakikisha kwamba hakuna siku nimekosa shule. Huyu ni mama anayestahili sifa za pekee kabisa.” Akawaza Patricia halafu akalifunga dirisha na kurejea kitandani.

“Patricia, jitahidi ulale. Muda umekwenda sana. Kesho tunatakiwa tuamke asubuhi na mapema,” akasema Bi Doroth.

“Mhh! Mama, sijui kama nitaweza kupata usingizi. Sijazoea kulala sehemu laini kama hii,” akasema Patricia na wote wakacheka.

“Patricia, unatakiwa uanze kuzoea vitu kama hivi. Huu ni mwanzo wako wa safari ndefu ya maisha yako. Siku moja vitu kama hivi utaviona vya kawaida. Jitahidi ulale,” akasema mama yake halafu akamfunika shuka vizuri akaenda kuzima taa wakalala.

*********************
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Patricia kuingia katika viwanja vya bunge. Aliustaajabia uzuri wa eneo hili. Hakukaukiwa na tabasamu. Siku hii alikuwa amependeza mno. Alivaa gauni lenye rangi nyeupe chini na juu likiwa na rangi nyeusi. Miguuni alivaa viatu virefu vilivyoendana na gauni alilovaa. Mavazi haya ya gharama alizawadiwa na Juliana mwanamitindo maarufu hapa nchini ambaye alifurahishwa mno na matokeo ya Patricia.

Wanafunzi bora ishirini walipokewa na katibu wa bunge halafu wakakabidhiwa kwa wafanyakazi wa bunge ambao walianza kuwatembeza sehemu mbalimbali za bunge. Patricia alionekana kuwa na furaha pengine kuliko wengine wote kwa sababu hakujua kama siku moja angeweza kufika mahala pale. Kati ya wanafunzi ishirini waliofanya vizuri mtihani wa kidato cha nne wengi walionekana kutoka katika familia bora zenye kujiweza kifedha. Ni Patricia pekee ambaye alitoka katika familia iliyo masikini zaidi lakini pamoja na umasikini wa familia yake iliyokuwa ikiishi katika chumba kimoja tu cha kupangisha, aliweza kuwaongoza wanafunzi wote nchini waliofanya mtihani wa kidato cha nne na kushika nafasi ya kwanza.

Kwa siku ya leo ingekuwa vigumu kuamini kwamba Patricia anatoka katika familia duni kwa namna alivyokuwa amependeza kwa mavazi aliyopewa na mwanamitindo Juliana. Wakati amekaa na wenzake wakisubiri kuingia katika ukumbi wa bunge, mara akatokea mama yake na kumuita pembeni. “Mama kuna nini mbona umefurahi namna hiyo?” Patricia aliuliza. “Patricia, huwezi amini. Juliana amekuja.” “Juliana?!” Patricia akastuka. “Ndiyo.” “Amekuja kufanya nini?” “Amekuja kukusapoti katika siku yako kubwa.” “Kweli mama?!” akauliza Patricia huku akiruka ruka kwa furaha. “Ndiyo Patricia. Anasema kwamba hakutaka kukutaarifu mapema kwamba atakuja. Alitaka akushangaze.” “Mama yuko wapi dada Juliana? Nipeleke nikaonane naye,” akasema Patricia na kwa haraka wakatembea hadi katika maegesho ya magari ambako Juliana alikuwa garini na rafiki yake aishiye mjini Dodoma. Mara tu Patricia alipotokea, Juliana akatoka garini na kumkumbatia.

“Wow! Dada Juliana sikujua kama utakuja Dodoma,” akasema Patricia. Juliana akatabasamu na kusema, “Sikutaka kukutaarifu mapema kama nitakuja Dodoma. I wanted to surprise you. Siwezi kukosa katika siku yako kubwa na muhimu kama hii ya leo. Patricia, najua una wasiwasi sana na nimeona katika orodha ya watoto ambao utaambatana nao leo bungeni, wote ni kutoka katika familia zenye uwezo mkubwa. Usijali, you have a huge support,” akasema Juliana na kumshika mkono Patricia wakaingia garini, akafungua mkebe mkubwa wa poda na kuanza kumremba, halafu akavua heleni zake nzuri za dhahabu na kumvisha. Akamuangalia na kutabasamu. “Now you look like a princess. Go now. Tutaonana baadaye,” akasema Juliana. Patricia akakimbia kwenda kuungana na wenzake. Uso wake ulikuwa na tabasamu zito. Baada ya Patricia kuondoka, Juliana akaagana na Bi Doroth kwa ahadi ya kuonana jioni ya siku hiyo katika sherehe ya kuwapongeza kina Patricia.

“Juliana, nakushukuru sana kwa msaada wako mkubwa. Umeweza kunifuta aibu kubwa siku ya leo. Bila wewe sijui Patricia angeonekanaje leo. Lakini kwa sababu yako leo Patricia ameng’aa na kupendeza kuliko wenzake wote,” akasema Bi Doroth. “Mama, hupaswi kunishukuru. Patricia ni kama mdogo wangu. Mimi ni mmoja wa watu walioguswa sana na matokeo yake mazuri. Ninathamini sana elimu hasa kwa mtoto wa kike na ndiyo maana nimeamua kwa moyo wangu kujitolea kumsaidia Patricia ili aweze kutimiza malengo yake. Bado ana safari ndefu sana na ili afikie malengo yake anahitaji sana sapoti yetu sisi sote,” akasema Juliana halafu akaagana na Bi Doroth na kuondoka kwa ahadi ya kukutana jioni.
***************
Kipindi cha maswali na majibu kilimalizika, Spika wa bunge akasoma baadhi ya matangazo ikiwa ni pamoja na kuwatambulisha wageni waliofika hapo bungeni kwa mafunzo halafu akamuita katibu ili aweze kusema ni kitu gani kilichokuwa kinaendelea. Katibu akasimama na kulitaarifu bunge kwamba ni wakati wa kuwaruhusu wanafunzi waliofanya vizuri waingie bungeni wakabidhiwe vyeti na waziri mkuu. Spika wa bunge akasimama na kusema, “Waheshimiwa wabunge, jana tulitengua kanuni ya bunge ili kuwaruhusu watu ambao si wabunge kuingia ndani ya ukumbi wetu huu. Wageni tuliowaalika ni wanafunzi ishirini bora katika mtihani wa kidato cha nne. Naombeni wakati vijana wetu wakiingia humu ukumbini, muwashangilie kwa makofi kwani wamefanya kazi kubwa sana,” akasema Spika na kumuamuru askari wa bunge awaongoze wanafunzi kungia ukumbini. Lango kuu likafunguliwa na wanafunzi wakaingia wakiwa katika mistari miwili, mmoja wa wanaume na mwingine wa wanawake. Makofi mengi, vigeregere pamoja na meza kugongwa vikasikika. Kilikuwa kipindi cha furaha sana kwa wabunge kuwashuhudia wanafunzi wale ishirini bora. Spika wa bunge akaomba utulivu halafu akamkaribisha waziri mkuu ili aweze kusema machache kabla ya kuwakabidhi vyeti. Waziri mkuu wa Tanzania mheshimiwa Thobias Kangeba kengaiza akasogea mbele na kusema:

“Mheshimiwa Spika, naomba nikushukuru sana kwa kunipa nafasi hii niweze kusema machache kuhusiana na tukio hili. Napenda nikushukuru wewe na bunge lako kwa kukubali kutengua kanuni ili wanafunzi hawa waweze kukaribishwa bungeni na kupongezwa. Binafsi ninafuraha kubwa sana kuwaona wanafunzi hawa ingawa ningefurahi zaidi kama kungekuwa na uwiano sawa baina ya wavulana na wasichana kwa sababu naona kati ya wanafunzi bora ishirini wasichana ni nane tu na kumi na mbili ni wavulana. Kuna haja ya kuendelea kuwekeza zaidi katika elimu ya mtoto wa kike ili kuwe na uwiano sawa wa ufaulu. Pamoja na hayo, kwa niaba ya serikali napenda kutoa pongezi zangu nyingi kwenu wanafunzi kwa ufaulu huu mzuri. Haikuwa kazi rahisi. Yalikuwa ni mapambano na leo hii mmeibuka vinara. Nawapongeza pia walimu na wazazi wenu kwa ushirikiano wao wa kuwasaidia kuwafikisha hapa mlipofika.”

“Mheshimiwa Spika, mfumo wetu wa elimu bado unakabiliwa na changamoto nyingi kama vile uhaba wa walimu, vitabu, vifaa vya kufundishia na kujifunzia, lakini serikali imekuwa ikijitahidi kutatua changamoto hizi na leo hii tunashuhudia mwanafunzi wa kwanza Tanzania ametoka katika shule ambazo zimejizolea umaarufu kama shule za kata ambazo zimekuwa na changamoto nyingi.” Makofi mengi yakapigwa halafu waziri mkuu akaendelea:

“Mheshimiwa Spika, ninaomba niseme kwamba hata kama tukifanikiwa kutatua changamoto zote zinazoikabili sekta ya elimu hapa nchini lakini bila juhudi binafsi za wanafunzi wenyewe kamwe hakutakuwa na ufaulu mzuri. Kuna shule zenye walimu wa kutosha na vifaa vya kufundishia na kujifunzia lakini hazikufanya vizuri. Kwa hiyo basi naomba niwaase wanafunzi waongeze kasi ya kujisomea. Mwalimu ana nafasi yake lakini mwanafunzi pia ana nafasi yake. Ni vyema kila mmoja akaitumia vyema nafasi yake.”

“Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie kwa kutoa pongezi zangu nyingi kwa niaba ya serikali na kuwatakia kila la heri wanafunzi hawa katika safari yao ndefu. Someni kwa bidii na taifa linawasubiri mje kulitumikia. Hongereni sana,” akamalizia nasaha zake mheshimiwa waziri mkuu, wabunge wakamshangilia kwa kugonga meza halafu Spika wa bunge akasimama:

“Tunakushukuru sana mheshimiwa waziri mkuu kwa nasaha zako. Natumai wanafunzi wote wamekusikia na watayafanyia kazi yale uliyowaasa. Waheshimiwa wabunge, kinachofuata sasa ni mheshimiwa waziri mkuu kuwakabidhi vyeti vijana wote ishirini,” akasema Spika na zoezi la kutoa vyeti likaanza. Wa kwanza kuitwa kwenda kupokea cheti alikuwa Patrcia. Ukumbi wote wa bunge ukalipuka kwa makofi na kushangilia wakimpongeza msichana huyu kwa kushika namba moja. Zoezi lilipomalizika baadhi ya wabunge walipata nafasi ya kusema machache na kuwaasa wanafunzi kusoma kwa bidii. Kila aliyesimama hakuacha kumpongeza na kumtolea mfano.
 
Here's the text in sentence case:

"I died to save my president

Mtunzi Patrick Ck

Simu 0764294499

Sehemu 2

Patrcia. Kila mbunge alikunwa vilivyo na uwezo wa kipekee aliouonyesha binti huyu. Hatimaye shughuli zote zilizopangwa kufanyika katika kikao cha asubuhi zikamalizika na spika akasitisha shughuli za bunge hilo hadi saa kumi na moja za jioni.

Nje ya ukumbi wa bunge, kila mbunge alitaka kumpa mkono na kumpongea Patricia. Waandishi wa habari hawakubaki nyuma katika kumuhoji Patricia na wenzake kuhusu siri ya ushindi wao. Baada ya zoezi lile kukamilika, Patricia na mama yake wakaingia katika gari na kurudishwa hotelini ambako walipata chakula cha mchana kisha wakaenda chumbani kwao kupumzika na kujiandaa kwa ajili ya sherehe za pongezi zitakazofanyika jioni.

“Nimepokea simu nyingi toka kwa majirani zetu wote pale mtaani wakisema kwamba wamekuona katika televisheni. Dah! Sikutegemea kama lingekuwa ni tukio kubwa namna hii,” akasema Bi Doroth mama yake Patricia.

“Mama, siku ya leo ni siku yangu ya furaha sana. Nashindwa niielezaje furaha niliyo nayo. Leo nimeshikaka mkono kwa mara ya kwanza na waziri mkuu. Ninaona ni kama muujiza. Nahisi ni kama ndoto,” akasema Patricia akiwa amekishika cheti alichopewa na waziri mkuu. Mama yake akatabasamu na kusema, “Haya, pumzika Patricia. Bado kuna shughuli nyingine leo jioni,” akasema Bi Doroth.
*******************
"Saa kumi na mbili za jioni mrembo Juliana akawasili katika hoteli waliyofikia Patrcia na mama yake Wow! Patricia my dear…!!!" akasema Juliana kwa furaha na kumkumbatia Patricia. "Karibu sana dada Juliana," akasema Patricia. "Ahsante sana Patrcia. Congratulations. It was your first time to enter that building and you showed a great confidence. Nilikuwa nakuangalia kupitia Luninga. Everybody is talking about you. Congratulations again," akasema Juliana. "Ahsante sana dada Juliana. Jumba lile ndiyo maana likaitwa tukufu. Linatisha kwa ndani kama ni mara yako ya kwanza kuingia," akasema Patricia.

"Unavaa nini jioni ya leo?" akauliza Juliana. Patricia akamuonyesha nguo ambayo alipanga kuivaa jioni hiyo. "Hapana, usivae hiyo. You have to look like a queen. All eyes must be on you tonight," akasema Juliana na kufungua begi alilokuja nalo akatoa gauni refu jeusi lenye kumeremeta. "Utavaa hili," akasema halafu akatoa vifaa vya urembo na kuviwekazani akaanza kumremba Patricia. Baada ya kumaliza kumremba, akamuangalia na kutabasamu. "Patricia, you are blessed with the natural beauty. You deserve a Miss World crown," akasema Juliana na wote wakacheka.

Baada ya kumaliza kumremba Patricia, Juliana akaanza kumremba na Bi Doroth. "Ahsante sana Juliana kwa kujia kwako. Bila wewe sijui tungeonekana vipi," akasema Bi Doroth. "Usihofu mama. Nisingeweza kukosa tukio kubwa kama hili kwa ajili ya mdogo wangu," akasema Juliana.

"Saa moja na nusu za jioni tayari walikuwa wamejiandaa, wakaingia garini na kuelekea mahali inakofanyikia sherehe ya kuwapongeza akina Patricia. Endapo ungebahatika kumshuhudia Patricia jioni ya leo, ungedhani ni mwanamitindo maarufu sana hapa nchini kwa namna alivyokuwa amependeza."

Waliwasili ukumbini wakapokelewa na kuelekezwa sehemu za kukaa. Patricia akawaacha mama yake na Juliana kwa ajili ya kwenda kukaa katika sehemu waliyokuwa wameandaliwa, kwani kulitengwa sehemu maalum ya wanafunzi kukaa.

"Patricia, don’t be nervous. Always put a smile on your face," akamnong’oneza Juliana wakati akienda kuungana na wenzake katika sehemu waliyoandaliwa. Kama alivyokuwa ametazamia Juliana, Patrica alikuwa anameremeta na kila mtu alimtupia jicho.

Bado waheshimiwa wabunge na wageni mbalimbali waliendelea kuwasili. Aliyekuwa akisubiriwa ni mgeni rasmi ambaye ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika sherehe hii, alikuwepo pia mke wa Rais, Bi Bernadetha Jumbo, ambaye ni mwanamke anayepambana sana kuhusu elimu ya mtoto wa kike.

"Hi," Patricia akasalimiwa na kijana mmoja mweupe mtanashati aliyevaa suti nzuri nyeusi iliyo mkaa vyema. Kijana yule alikuwa ni mmoja kati ya wanafunzi waliofanya vizuri. Patricia akageuza shingo na kumuangalia kijana yule. Wote wawili wakatabasamu na kisha Patricia akasema, "Hi."

Kijana yule aliyekuwa na sura nzuri na vishimo mashavuni anapotabasamu akamnyooshea mkono Patricia na kusema, "Hongera sana." Patricia akatabasamu na kusema, "Hongera nawe. Sisi sote tunapaswa kukupa hongera kwani ndiye uliyetuongoza," akasema yule kijana na kumfanya Patricia azidi kutabasamu.

"Sote tumeshinda. Sote tuko katika kundi moja la ishirini bora," akasema Patricia, halafu kikapita kimya kifupi yule kijana akasema, "By the way, I’m Elvis."

"I’m Patricia," akajibu Patricia.

"Huna haja ya kujitambulisha, Patricia. Hakuna mtu asiye kufahamu kwa sasa hapa nchini. Wewe ni mmoja wa watu maarufu sana hapa nchini," akasema Elvis na kumfanya Patricia atabasamu. Kabla hajasema kitu, mwanamama mmoja ambaye ni mbunge akamsogelea na kusema, "Patricia, nilikutafuta mchana pale bungeni sikukuona. Kuna jambo ambalo nilitaka nikufahamishe. Ni kwamba umechaguliwa kutoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzako wote."

"Mimi…?!" Patricia akauliza kwa mshangao.

"Ndiyo, wewe."

"Mheshimiwa, sidhani kama nitaweza kuongea mbele ya umati huu mkubwa wa viongozi. Tafadhali naomba utafute mtu mwingine afanye hivyo, mimi sitaweza."

"Hapana, Patricia, utaweza tu. Wewe ndiye uliyeshika namba moja kati ya wenzako wote, kwa hiyo unapaswa kuwaongoza wenzako pia katika kutoa shukrani." Patricia akafikiri kidogo na kusema, "Nitaenda kusema kitu gani?"

"Akauliza Patricia kwa wasi wasi."

"Say anything. Ili mradi liwe ni neno la shukrani. You can do it Patricia. Show all these people that you deserve to be number one," akasema yule mbunge na mara Elvis aliyekuwa kimya akifuatilia maongezi kati ya Patricia na yule mbunge akaingilia kati na kusema, "Madam usihofu, nitamsindikiza mimi ili kumpa sapoti na kumfanya asiogope," akasema Elvis.

"Good. Hilo ni jambo zuri. Patricia atakapoitwa utamshika mkono na kumuongoza mpaka pale mbele," akasema mbunge na kumgeukia Patricia. "Start preparing yourself. Itumie vyema nafasi hii," akasema yule mbunge na kuondoka. Patricia alionekana kuingiwa na woga mwingi.

"Usiogope Patricia. You can do it," akasema Elvis.

"Sijawahi kuongea mbele ya hadhira kubwa kama hii, tena kukiwa na viongozi wa juu wa serikali," akasema Patricia.

"Patricia, kama umeweza kuwazidi akili wanafunzi wote wa Tanzania na ukashika namba moja, huwezi kushindwa kuongea neno pale mbele. Just say anything you want to say."

"C’mon Elvis, ule ulikuwa ni mtihani na hatufanyi kwa kuongea. I don’t know what I have to say," Elvis akamtazama Patricia usoni, akatabasamu na kusema, "Unataka nikuandikie kitu cha kwenda kuongea pale mbele?"

"No! Don’t do that," akasema Patricia na kuinuka akaelekea katika meza walikokuwa wamekaa mama yake pamoja na Juliana. Akamuita Juliana pembeni.

"Patricia, what's wrong? Naona sura yako imebadilika. Unaogopa nini?"

"Dada Juliana, kuna kitu nimeambiwa muda huu ambacho kimenistua kidogo."

"Kitu gani Patricia?"

"Nimeambiwa kwamba mimi ndiye nitakayetoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzangu. Nimestukizwa na sijafanya maandalizi yoyote. Sielewi nitasema nini pale mbele ya viongozi hawa wakubwa wa kiserikali," akasema Patricia.

"Kwa nini hawakukutaarifu toka mapema ukae ujiandae?"

"Hata mimi sielewi ni kwa nini wamefanya hivi. This is unfair. Wangenieleza toka mapema ili nijiandae," akalalamika Patricia. Juliana akatabasamu, akamshika bega na kusema, "Relax my dear. Relax. Put back your smile. Usikwazike na hilo. Wamekuchagua kwa sababu wanajua una uwezo mkubwa. Kwa hiyo ukiitwa pale mbele nenda kawaonyeshe kwamba unaweza na unastahili kuwa namba moja Tanzania. Waonyeshe kwamba hukubahatisha kushika nafasi hiyo. Jambo lingine, jihadhari na matumizi ya lugha. Usichanganye lugha. Ongea Kiswahili fasaha na kilichonyooka. I believe in you Patricia. You can do it. Go and make your mom proud, make us all proud my dear," akasema Juliana na kumfanya Patricia atabasamu.

"Dada Juliana, nitaenda kusema nini pale mbele? I’m a bit scared," akauliza Patricia.

"Say anything you want to say. Ongea neno lolote la shukrani unalolijua. This is your time. Waandishi wa habari wako hapa na wote watayaelekeza macho yao kwako. Wamekupa nafasi hiyo makusudi ili kukupima. Kwa hiyo wadhihirishie kwamba unastahili," akasema Juliana, na mara ikasikika sauti ya muongoza shughuli akiwataka watu wote walio nje ya ukumbi kuingia ndani, kwani muda wowote sherehe zinarajia kuanza.

"Watu waliokuwa nje wakaingia ukumbini na sherehe zikaanza. Ilikuwa ni sherehe nzuri iliyoambatana na hotuba za viongozi mbalimbali, akiwemo Waziri Mkuu na mke wa Rais. Baada ya hotuba za viongozi, kikafuata kipindi cha utoaji wa tuzo na zawadi kwa wanafunzi wote na shule zilizofanya vizuri zikatolewa."

Baada ya zoezi lile kukamilika, muongoza shughuli akawafahamisha watu kwamba ni wakati wa chakula. Baada ya chakula, Patricia akaitwa mbele ili aweze kutoa neno la shukrani kwa niaba ya wenzake. Ukumbi wote ukalipuka kwa shangwe baada ya Patricia kuinuka na kuanza kuelekea mbele ya ukumbi, akiwa ameongozana na kijana mtanashati sana, Elvis. Uso wake haukukaukiwa tabasamu. Akafika mbele na kukabidhwa kipaza sauti. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kukishika na kukitumia. Mikono ilikuwa inamtetemeka na midomo kumcheza kiasi kwamba alishindwa aanze vipi. Watu wote wakakaa kimya tayari kumsikiliza.

Mara maneno ya Juliana yakamjia kichwani. “Wamekuchagua kwa sababu wanajua una uwezo mkubwa. Kwa hiyo ukiitwa pale mbele nenda kawaonyeshe kwamba unaweza na unastahili kuwa namba moja Tanzania. Waonyeshe kwamba hukubahatisha kushika nafasi hiyo. I have to do it..I can do it” akasema moyoni na kwa ujasiri akakishika vizuri kipaza sauti, akakohoa kidogo kurekebisha koo na kusema, “Mheshimiwa Waziri Mkuu, mpendwa mama yetu mke wa Rais, waheshimiwa mawaziri, wabunge na viongozi wengine wa serikali, walimu, wazazi, wanafunzi wenzangu, wageni waalikwa mabibi na mabwana, ninapenda kumshukuru sana Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia sote kuwepo hapa usiku huu.”

Maneno haya ya utangulizi yakazidi kumpa ujasiri. Akaendelea, “Waheshimiwa viongozi, wageni waalikwa mabibi na mabwana, nimesimama mbele yenu kwa unyenyekevu mkubwa ili kutoa neno la shukrani kwa niaba ya wanafunzi wenzangu wote tulioko hapa usiku huu.” Akatulia kidogo halafu akaendelea, “Baba yangu alifariki nikiwa darasa la tano. Alifariki kwa ajali ya gari. Kifo chake kiliacha pengo kubwa sana kwangu na kwa familia yangu. Baba yangu hakuwa tajiri, kwa hiyo alipofariki hakutuachia mali yoyote, hali iliyomlazimu mama yangu ashike nafasi zote mbili, kama baba na kama mama. Mama yangu Bi Doroth, ambaye niko naye hapa usiku huu, hakuwa na kazi ya maana zaidi ya kufua nguo katika majumba ya Wahindi. Pamoja na kazi hiyo yenye ujira mdogo, lakini bado alielekeza nguvu zake zote katika kuhakikisha kwamba hata hicho kidogo alichokuwa akikipata katika kazi zake za ufuaji, anakitumia katika kuniendeleza kielimu. Aliamini kwamba elimu pekee ndiyo itakuwa mkombozi wangu.”

Patricia akanyamaza na kuitazama hadhira ile iliyokuwa kimya ikimsikiliza, halafu akaendelea, “Nilichaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari katika moja ya shule zile zenye umaarufu kama shule za kata. Ni shule yenye changamoto nyingi; hatukuwa na walimu wa kutosha, vifaa vya kutosha vya kujifunzia n.k. Pamoja na hali hiyo, bado mama yangu aliendelea kuniunga mkono katika kila hatua niliyopiga. Alinunulia vitabu na kunilipia masomo ya ziada. Kuna nyakati ilimlazimu kukaa nami hadi usiku katika sehemu niliyokuwa nikijisomea, aidha na wenzangu au masomo ya ziada, ili kuhakikisha kwamba ninarudi nyumbani nikiwa salama. Alikuwa mkali sana kila pale ambapo sikufanya vizuri shuleni, jambo ambalo lilinifanya niongeze bidii sana katika masomo na hatimaye leo hii nimesimama mbele yenu, enyi waheshimiwa sana, nikiwa mwanafunzi niliyeshika namba moja katika mtihani wa Kidato cha Nne nchini Tanzania.”

Makofi mengi na vigeregere vikapigwa. Bi Doroth, mama yake Patricia, alishindwa kujizuia kutokwa na machozi. Patricia akaendelea
 
Kulubule the tale teller Shukrani sana!!

Nasubiri nasubiri viwii vya kulalia
 
I DIED TO SAVE MY PRESDANT

Mtunzi Patrick Ck

Simu 0764294499

Sehemu 3

Najua mtajiuliza ni kwa nini
nimeyasema haya
yote.Nimeyasema haya yote
kwanza kutoa shukrani zangu za
kipekee kwa mama yangu kipenzi
,walimu wangu na walezi wangu
walionisaidia mimi binafsi kufika
hapa nilipofika.Ni wengi
wamenisaidia na sintaweza
kuwataja wote kwa majina lakini
kwa ujumla wao ninasema
ahsanteni sana” makofi mengi
yakapigwa
“ Pili nimeyasema haya yote ili
kuonyesha wazi kwamba
mafanikio ya mtoto yanachangiwa
na mambo mengi lakini kubwa ni
ushiriki wa mzazi.Pamoja na
umaskini wake mama yangu
ameshirikiana nami katika kila
hatua niliyopiga.Pale
nilipoanguika alikuwa mtu wa
kwanza kunipa moyo nikainuka
nikasonga mbele.Mama huyu ni
mfano wa kuigwa na wazazi
wote.Kushindwa kwa wanafunzi
wengi kunachangiwa kwa kiasi
kikubwa na ushirikiano mdogo wa
wazazi .Sisi wanafunzi ishirini
tulioko hapa tulioko hapa usiku
huu tumepata mafanikio haya
kwa juhudi za wazazi
wetu.Ahsanteni sana wazazi wote
mlioko hapa kwa juhudi zenu na
ushirikiano mnaowapa watoto
wenu.Kwa wale wazazi na walezi
ambao hawako karibu na watoto
wao,ni wakati wenu wa
kubadilika.Watoto wenu
wanawahitaji sana.Kwa niaba ya
wenzangu wote tunawashukuru
nyote kwa mapokezi
mazuri,pongezi mlizotupa na
zawadi nzuri mlizotuzawadia.Tumejifunza
mengi toka kwenu na tutasoma
kwa bidii sana kwani tumetambua
nchi yetu inatuhitaji
sana.Tunawatakia nyote afya
njema na mafanikio katika
kufanikisha majukumu mliyonayo
kwa taifa.Ahsanteni na Mungu
awabariki.” Patricia akamaliza na
kumkabidhi muongoza shughuli
kipaza sauti.Watu wote
walikuwawamesimama wakipiga
makofi.Wote walikunwa na
maneno yale na kuduwazwa kwa
uwezo mkubwa aliokuwa nao
Patricia.Patriciai akaongozwa
akaenda kupeana mkono na waziri
mkuu ,kisha mke wa rais na
viogozi wengine wa meza kuu
halafu akageuka na kuanza
kupiga hatua kurejea kitini lakini
muongoza shughuli akamzuia Ndugu wageni waalikuwa
,mabibi na mabwana,nadhani
nyote mmeshangazwa na uwezo
mkubwa alio nao binti yetu
Patricia.Ameongea maneno mazito
sana na nina imani kila mmoja
wetu hapa ameguswa .Miongoni
mwa watu walioguswa ni mama
Bernadetha Jumbe mke wa rais
wetu ambaye anataka kusema
neno.Karibu sana mama”akasema
muongoza shughuli na makofi
mengi yakapiga.Bi Bernadetha
Jumbo mke wa rais wa jamhuri ya
muungano wa Tanzania
akasimama na kuelekea mbele
akapewa kipaza sauti.
“ Waheshimiwa wageni
waalikwa mabibi na
mabwana,nimesimama mbele
yenu tena kutokana na kuguswa
na maneno mazito aliyoyasema binti yetu Patricia.Ni maneno
yenye ukweli na ametukumbusha
wajibu wetu sisi kama wazazi,
ambao wengi wetu
tumeusahau.Napenda kuchukua
nafasi hii kumpongeza kwa namna
ya pekee kabisa Patricia kwa
ufaulu wake mzuri.Ameonyesha
njia na kuwa mfano wa kuigwa na
wengine hasa watoto wa
kike.Ninampongeza kwa namna ya
pekee pia kwa sababu amepitia
changamoto nyingi sana katika
maisha yake hadi hapa
alipofika,changamoto ambazo
zingepelekea yeye ashawishike
kuingia katika mambo yasiyofaa
na kumuharibia kabisa muelekeo
mzima wa maisha yake lakini yeye
hakuanguka na alielekeza akili
yake katika kitu kimoja tu
,kusoma.Watoto wengi wa kike hushawishika kuingia katika
mambo yasiyofaa kutokana na
changamoto mbali mbali
wanazokutana nazo katika maisha
yao ya kila siku na wakati
mwingine ni tamaa tu ya kutaka
kuishi maisha yasiyolingana na
uwezo wao .
“Binafsi nimeguswa sana na
historia ya Patricia na kuanzia
sasa ninatangaza kwamba
nitagharamia mimi gharama zote
za masomo yake hadi
atakaposema imetosha.”
Makofi mengi na vigere gere
vikapigwa halafu akaendelea
“Mama yake Patricia ni mama
wa mfano.Ametufundisha namna
bora ya kulea watoto wetu.Pamoja
na changamoto kubwa ya kipato
inayomkabili ,ameweza kufahamu
umuhimu wa elimu kwa mtoto wake na akaelekeza nguvu zake
zote katika kuhakikisha kwamba
mwanae anasoma.Hongera sana
mama Patricia na ninakuomba
kokote ulipo sogea hapa mbele.
Tafadhali”
Mama yake Patricia
akasimama na kuanza kusogea
mbele huku akishangiliwa kwa
nguvu.Akakumbatiana na mke wa
rais kwa furaha
“ Hongera sana mama
Patricia.Juhudi zako
zimeonekana.Wazazi wote natumai
wataiga mfano wako na kuwekeza
kila walichonacho katika elimu ya
watoto wao.” Akasema Bi
Bernadetha huku akimpa mkono
wa pongezi mama Patricia halafu
akaendelea
“ waheshimiwa wageni
waalikwa mabibi na mabwana,mimi pia ni mama na
ninaufahamu ugumu uliopo katika
ulezi wa familia na hasa ukiwa
peke yako.Kwa maana hiyo
ninamuunga mkono mwanamke
mwenzangu kwa kumpatia mtaji
wa biashara wa shilingi milioni
tano ili aachane na kazi ya ufuaji
anayoifanya na afungue biashara
ambayo itamuwezesha kujikimu
yeye na familia yake.” Bi
Bernadetha akashangiliwa kwa
nguvu sana na kelele zilipopungua
akaendelea
“ Najua wengi wenu hapa
mmeguswa kama nilivyoguwa
mimi kwa hiyo kama nawe
unajisikia kumsaidia chochote
mama Patricia unakaribishwa
kufanya hivyo.Pita hapa mbele
umpongeze mama huyu ambaye
ninaweza kumuita ni jasiri” Kauli ile ya mama Bernadetha
ilikuwa ni kama imewasha moto
kwa waheshimiwa wabunge kwani
ndani ya dakika chache Patricia
na mama yake walikuwa wanaoga
pesa.Elvis na Juliana walikuwa na
kazi ya kukusanya fedha
walizotunzwa Patricia na mama
yake.
Baada ya zoezi lile kumalizika
mama Patrcia akapewa kipaza
sauti ili aweze kutoa neno la
shukrani kwa niaba ya wazazi
wote
“ Sina maneno mengi ya
kusema ila ninaomba nimshukuru
sana mama Bernadetha Jumbo
kwa moyo wake wa huruma na
kwa msaada wake mkubwa
kwangu.Kwa kweli changamoto ni
nyingi sana ukiwa kama mzazi
mmoja na kubeba majukumu yote ya ulezi peke yako lakini
namshukuru Mungu nimeweza
kuvuka vikwazo vyote na
mwanangu ameweza kusoma japo
kwa shida.Naomba nikiri kwenu
kwamba haikuwa kazi rahisi lakini
kwa kuwa ninaamini kwamba
elimu ndiyo urithi pekee
ninaoweza kumpatia mwanangu
basi nilijifunga mkanda
kuhakikisha kwamba mwanangu
anasoma.Kuna nyakati ilinilazimu
kusoma pamoja naye japokuwa
nilikuwa nafunua tu vitabu na
kutazama picha bila kuelewa
chochote”
Watu wote ukumbini
wakaangua kicheko
“ Nawasihi wazazi wenzangu
wote mlioko hapa na wale walioko
majumbani,tujenge urafiki na
watoto wetu na tuwe nao karibu katika kuwapa msaada
wanaouhitaji kila mara.Tuwasaidie
hawa watoto hasa wa kike ambao
wanakabiliwa na vishawishi vingi
sana.Mwisho napenda
kuwashukuru nyote kwa
michango yenu wote.Mungu
awabariki sana” akasema mama
Patricia na kwa mara nyingine
tena akashikana mkono na mke
wa rais halafu akarejea kukaa
mahala pake akifuatana na
Juliana aliyekuwa amebeba pochi
lililojaa fedha.
Zoezi lililofuata lilikuwa ni
burudani toka katika kikundi cha
sanaa za ngoma za asili.
“ Hongera sana Patricia
ulifanya vizuri..Usiku wa leo
umedhihirisha kwamba unastahili
kuwa namba moja..” akasema
Elvis wakati burudani ya ngoma ikiendelea.Patricia akatabasamu
na kusema
“ Ahsante sana
Elvis.Ulinisaidia sana kuniondolea
uoga” akasema Patricia.
“ Usijali Patricia .Ni jambo la
kawaida kuwa na uoga
unaposimama mbele ya hadhira
kubwa kama hii.Pamoja na uoga
wote uliokuwa nao lakini umeweza
kuongea maneno mazito
yaliyomgusa kila mmoja na hata
mimi niliguswa
pia.Umenikumbusha baba yangu
alikuwa ni rafiki yangu
mkubwa.Ilikuwa ni ndoto yake
siku moja nifike mbali sana
kielimu.”akasema Elvis
“ Alikuwa ?! ..Patricia
akashangaa Ndiyo.Baba yangu alifariki
mwaka juzi.Mimi na wewe sote
tumebakiwa na mzazi mmoja tu”
“ Dah ! pole sana Elvis”
“ Ahsante.Pole nawe” akasema
Elvis halafu kimya kikapita
“ Patricia unaishi wapi kwa
sasa? Akauliza Elvis
“ Naishi Kimara Baruti Dar es
salaam.Wewe unatokea wapi?
“ Mimi natokea Arusha
.Ninaishi Njiro.Karibu sana
Arusha uje utembee siku
moja.Karibu uje utembelee mbuga
za wanyama na vivutio mbali
mbali vya kitalii” akasema Elvis na
kumfanya Patricia atabasamu
“Nitakuja kutembea siku
moja.Natamani sana kufika
Arusha”
“ Ukija nitakuwa mwenyeji
wako” akasema Elvis Ahsante ila naomba nikupe
tahadhari mapema kwamba
sintakuwa na hela ya kukulipa
kama muongozaji watalii”
Elvis akacheka sana na kusema
“ Sintakutoza fedha nyingi
kwa kuwa wewe ni mtalii wa
ndani.Tuna nyumba Dar es
salaam Mbezi,na mimi siku moja
nitakuja Dar na wewe utakuwa
mwenyeji wangu”
“ Usijali kuhusu
hilo.Nimezaliwa na kukulia Dar
kwa hiyo ninalifahamu vyema jiji”
akasema Patricia.
Baada ya burudani ya ngoma
za asili kumalizika mheshimiwa
waziri mkuu akafungua muziki na
watu wote wakajumuika ukumbini
kulisakata rhumba.
“ wakati wa muziki sasa.Can
we dance? Akauliza Elvis.Patricia alionekana kuogopa na kuona
aibu.Wanafunzi wenzao walikuwa
wanainuka na kujumuika na
wabunge katika kuusakata muziki
“Ninaogopa sijawahi kucheza
hata mara moja.” Akasema
Patricia
Wakati Elvis akimuomba
Patricia waende wakacheze muziki
mara akatokea mama yake akiwa
ameongozana na ndugu wengine
watano.
“ Elvis sherehe imemalizika.Ni
wakati wa kuodnoka
sasa.Tunatakiwa tupumzike kwani
kesho tuna safari ndefu ya kurejea
Arusha.Sitaki kuendesha gari
nikiwa nimechoka. Akasema
mama Elvis
“ Mama kabla ya yote kutana
na Patricia.Yeye ndiye
aliyetuongoza wote na kushika namba moja.Ni rafiki yangu wa
kwanza kukutanana naye ambaye
nitakuwa naye pale J.Y.Makamba
school of science.” Elvis
akamtambulisha Patricia kwa
mama yake
“Patricia huyu ni mama yangu
anaitwa Mrs Tarimo na hawa
wengine ni ndugu zangu
walionisindikiza kwa ajili ya
sherehe hii”
Patricia akainuka na kwa
adabu akamsalimu mama Elvis.
“ Shikamoo mama”
“ Marahaba Patricia.Nafurahi
kukutana nawe.Hongera sana kwa
kufanya vizuri”
“ Ahsante sana mama.Hata
mimi nafurahi kukutana
nawe.Hongera pia kwa Elvis kwani
naye amefanya vizuri sana” Amejitahidi ameshika
namba nane.Nilitegemea labda
angekuwepo katika nafasi tatu
bora.Kwa kuwa mtakuwa wote
shule moja naomba umkazanie
sana mwenzio aongeze juhudi na
kidato cha sita nyote muwe katika
nafasi tatu za juu” akasema mama
Elvis.
Usihofu mama.Kidato cha sita
Patricia hatanishinda
tena.Nitamshusha toka namba
moja” akasema Elvis na wote
wakacheka
“ Patricia unaishi wapi?
“ Mimi natokea Dar es
salaam”
“ Ouh vizuri sana.Sisi
tunaishi Arusha japokuwa hata
Dare s salaam tuna nyumba
pia.Karibu sana Arusha
ututembelee siku moja” Ahsante sana mama.Tayari
Elvis ameshanialika nije Arusha
siku moja na nitakuja pale
nipatapo nafasi”
“Ouh kumbe
ameshakukaribisha.Huyu naye
huwa hachelewi.Haya ukipata
nafasi tafadhali njoo ututembelee”
“ Ahsante sana mama
nitakuja siku moja”
“ Haya Patricia sisi
tunaondoka,tunatakiwa
tukapumzike kesho asubuhi tuna
safari ya kurejea
Arusha.Nakutakia safari njema ya
kurejea Dar es salaam”
“ Nashukuru sana
mama.Nami nawatakia safari
njema ya kurejea Arusha”
akasema Patricia.
“ Mama tangulieni katika gari
nitakuja baada ya muda mfupi.Nataka kuagana na Patricia
“ akasema Elvis na mama yake
huku akitabasamu akaondoka
kuelekea garini
“ Mama yako mcheshi sana”
akasema Patricia
“ Usimuone akiongea kwa
upole namna ile.Ni mkali sana
akiwa nyumbani.Tuachane na
hayo,Patricia nashukuru sana
kukutana nawe .Kwa kuwa sote
tunakwenda kuendela na masomo
katika shule moja,nina imani
tutazidi kuwa marafiki sana.”
“ Hata mimi nafurahi sana
kukutana nawe Elvis.” Akasema
Patricia
“Patricia najua hatutaonana
tena hadi tutakapokutana
shuleni.Unaweza ukanipa namba
yako ya simu ili mara moja moja niwe nikikupigia simu na
kukujulia hali”
Patricia akatabasamu na
kusema
“ Sina simu Elvis”
“ Huna simu?!....Elvis
akashangaa
“ Ndiyo sina simu” akajibu
Patricia.
“ C’mon Patricia ina maana
hufanyi mawasiliano?
“Nikitaka kuwasiliana na mtu
hutumia simu ya mama”
“Ok..! Ok ! ..Nipe basi namba
ya simu ya mama”
“ Hapana Elvis.Nipe wewe
namba zako na nitakupigia simu
mimi nikipata nafasi.”
Elvis akaandika namba zake
za simu na kumpatia Patricia
halafu wakaagana na
kuondoka.Watu bado waliendelea kujimwaga ukumbini wakilisakata
rhumba.Patricia akamfuata mama
yake aliyekuwa amesimama na
kundi la wabunge wanawake
wakimpongeza
Sherehe zilipomalizika
Patricia na mama yake
wakarejeshwa hotelini
“Dah ! ilikuwa ni siku ndefu
sana” akasema mama Patricia.
“ Ilikuwa siku ndefu lakini
nzuri.Mama nimefurahi sana
leo.Hii ni siku kubwa katika
maisha yangu” akasema Patricia
“ Hata mimi nimefurahi
sana.Unajua pale ulipoitwa uende
mbele kuongea neno la shukrani
nilistuka sana kwani nilijua
hujajiandaa kitu cha kuongea
lakini Juliana alinitoa wasi wasi
na kuniambia nisihofu.Ulipoanza
kuongea kijasho kilikuwa
kinanitoka lakini mwishowe
nilijikuta nikitoa machozi.Patricia Mungu amekujalia akili ya kipekee
kabisa.Ahsante sana kwa maneno
yale mazito ambayo yalichoma
mioyo ya kila mmoja pale
ukumbini.Ni kwa maneno yale
mazito tumefanikiwa kupata kiasi
hiki cha fedha.Bado siamini
macho yangu.” Akasema mama
Patricia na kulifungua pochi lake
kubwa na kumwaga pesa
kitandani.
“ Wow ! ..Patricia
akatabasamu
“ Patricia tunapaswa
kumshukuru sana Mungu kwa
muujiza huu mkubwa.Jana
tulikuwa hatuna hata fedha ya
kununua sukari lakini leo hii tuna
fedha hizi nyingi.Ouh Mungu
ahsante sana kwa jambo hili
kubwa” akasema mama Patricia
na kuanza kuzihesabu fedha
zile..Jumla zilikuwa ni shilingi
million mbili laki saba na sabini.Bi
Doroth hakuamini macho yake.Machozi ya furaha
yakamtoka.Akakumbatiana na
mwanae
“ Basi usilie mama.Ni wakati
wetu wa kufurahi na kumshukuru
Mungu kwani maisha yetu
yanaanza kuonyesha nuru.Pesa
hizi na zile alizokuahidi mama
Bernadetha zinatosha sana
kuanzisha mradi wowote ambao
utatuwezesha kujikimu na
kututoa katika lindi hili la
umasikini mkubwa” akasema
Patricia
“ Patricia mwanangu lazima
nilie kwa sababu nikikumbuka
taabu nilizozipata katika
kukusomesha.Mungu pekee ndiye
anayejua.Ninawashukuru wote
waliotuchangia fedha hizi ambazo
ni nyingi na zinatosha kabisa
kuanzisha bashara.Tunatakiwa
tukae na tubuni biashara ya
kufanya.Mimi nina wazo
moja.Siku ya jumatano
 
I DIED TO SAVE MY PRESDANT

Mtunzi Patrick Ck

Simu 0764294499

Sehemu 4


nitakapokwenda kuonana na
Mama Bernadetha katika taasisi
yake kama
alivyonitaka,nitamuomba anisaidie
nipate walau shamba au kiwanja
ili niweze kuanzsha mradi wa
ufugaji kuku.Unaonaje kuhusu
wazo hili?
“ Hilo ni wazo zuri sana mama
lakini nina imani utakapoonana
naye na kumweleza hali yako ,yeye
mwenyewe anaweza akatafuta njia
bora zaidi ya kukusaidia” akasema
Patricia huku akiuvua mkufu wa
dhahabu na mara akamkumbuka
Juliana
“ Dada Juliana amefanya
kazi kubwa sana na amenifanya
nipendeze na kusifiwa na kila mtu
leo ” akasema
“ Ni kweli Patricia.Tunapaswa
kumshukuru mno Juliana kwa
wema wake kwetu.Amesafiri toka
Dar es salaam hadi huku Dodoma
kuja kuungana nasi.Ana moyo wa huruma sana Yule binti.” Akasema
mama Patricia halafu akanyamaza
kana kwamba kuna kitu
anakikumbuka,akauliza
“ Patricia Yule kijana
aliyekusindikiza pale mbele
ulipokwenda kutoa shukrani
,mnafahamiana?
Swali lile likamstua kidogo
Patricia
“ Unasema Elvis?
“ Simfahamu kwa jina
.Umesema anaitwa Elvis?
“ Ndiyo mama anaitwa
Elvis.Nimefahamiana naye pale
pale katika sherehe.Yeye ameshika
namba nane na anatokea
Arusha.Kitu ingine ni kwamba
wote tumechaguliwa kuendelea na
kidato cha tano katika shule
moja.Kuna tatizo lolote mama?
“ Hapana hakuna tatizo
lakini kama unavyofahamu
kwamba sitaki ulewe sifa na
kubadilika.Safari yako ndiyokwanza imeanza.Masuala ya
vijana mimi sitaki kuyasikia.Kama
ni urafiki uwe ni wa kusaidiana
katika masomo tu na si
vingnevyo.Nitakuwa mkali sana
katika hilo na ninakuomba
usinione mbaya.Nataka ufahamu
kwamba utakapokwenda huko
shuleni utakuwa peke
yako.Hautakuwa na mimi
tena.Kwa hiyo zingatia yale yote
ambayo nimekuwa nikikuelekeza
japokuwa una uwezo wa kufanya
maamuzi yako mwenyewe kwa
sababu wewe ni binti mkubwa
sasa na unafahamu jema na
bayaa.Unazifahamu ndoto zako
kwa hiyo pambana ili kuzitimiza.”
Akasema mama Patricia.Patricia
akatabasamu na kumsogelea
mama yake.
“ Mama usiwe na hofu na
mimi hata kidogo.Ninajitambua
mimi ni nani na malengo yangu ni
nini kwa hiyo nakuomba usiwe na wasi wasi hata
kidogo.Sintakuangusha mama
yangu.Naomba uniamini” Patricia
akasisitiza
“ Nakuamini Patricia lakini
lazima nikukumbushe mara kwa
mara kwamba kwa sasa wewe ni
binti mkubwa na unazidi kuwa
mrembo.Urembo wako ni kama ua
lenye harufu nzuri ambalo huvutia
nyuki wengi kulifuata.Urembo
wako ukichanganya na jina
ambalo umelipata hivi sasa ni
vichocheo tosha kabisa
kuwafanya wanaume wengi ,vijana
kwa wazee kuanza kukuzengea na
katika umri huu mwili nao
hukumbana na vichocheo na
vishawishi vingi.Wasichana wengi
huanguka vishawishini katika
kipindi hiki. Patricia
mwanangu,umeweza kujilinda kwa
miaka minne na nina imani
utaweza pia kwa hiyo miaka miwili
na mingine mingi utakayokuwa masomoni.Kamwe usikubali
kuanguka vishawishini.Mapenzi
yapo na utaondoka
utayaacha.Tengeneza kwanza
maisha yako na mambo mengine
yatafuata baadae.Naomba
usiyasahau maneno haya ambayo
ni kwa faida yako wewe
mwenyewe” akasema Bi Doroth
“ Mama siwezi kuyasahau.Siku
zote maneno yako yamekuwa ni
dira na ngao
yangu.Nakuhakikishia mama
kwamba siwezi kuanguka na
nitamuweka Mungu mbele siku
zote.Usichoke kuniombea”
“ Mimi nitakuombea bila
kuchoka lakini hata wewe pia
unatakiwa usimame imara katika
maombi”
Ulikuwa ni usiku mrefu sana
kwa Bi Bernadetha na binti
yake.Waliongea mambo mengi
sana kuhusiana na maisha
yao.Walikumbushana mambomengi kuhusu waliyoyapitia katika
maishayao na ilipotimu saa tisa za
usiku wakalala.
**********************
Siku sita zimekwisha pita toka
Patricia arejee toke
Dodoma.Maisha yao yalianza
kuwa na mabadiliko.Tayari Bi
Doroth amekwisha onana na mke
wa rais na akampatia kiasi cha
fedha alichomuahidi.Mke wa rais
pia alikwenda mbali zaidi na
kuahidi kumpatia kiwanja ili
aweze kujenga nyumba walau
nyumba ndogo ya kushi yeye na
mwanae Patricia pamoja na
kufanya kazi ya ufugaji kama
alivyokuwa amepanga.Mwanga
ulianza kuonekana katika maisha
yao
Ni siku ya Ijumaa saa nne
asubuhi mrembo Juliana
akawasili nyumbani kwa akina Patricia.Akashuka toka ndani ya
gari lake aina ya Mercedece Benz
jeusi na kuwasalimu akina mama
waliokuwa kibarazani wakiendelea
na shughuli za usafi halafu
akanyoosha hadi katika chumba
cha akina Patricia akagonga na
mama Patricia ndiye aliyefungua
mlango
“ Ouh ! Juliana ! Karibu sana”
akasema Bi Doroth
“ Ahsante sana
mama.Shikamoo” akajibu Juliana
“ Marahaba Juliana.karibu
sana.Karibu ndani” akasema
mama Patricia huku akiweka vitu
vizuri ili Juliana aweze kupita
“ Karibu sana Juliana.Habari za
toka majuzi?
Habari nzuri mama .Habari za
hapa?
“ habari za hapa nzuri.Sijui
huko kwenu”
“ Kwetu kwema mama.Vipi
Patricia hajambo? Hajambo ,nimetuma hapo
dukani atarejea muda si mrefu”
“ Mama leo ndiyo ile siku
niliyokuwa nimeamuandalia
Patricia ile sherehe ndogo ya
kumpongeza nyumbani
kwetu.Watakuwepo marafiki
wachache tutakaojumuika
pamoja” akasema Juliana
“ Juliana ahsante sana lakinu
utanisamehe kwani sintaweza
kuhudhuria.Hivi unavyoniona
nina miadi ya kuonana na mama
Imelda Kulangwa ambaye
ameelekezwa na mke wa rais
aende akanionyeshe kiwanja
alichoninunulia.Utakwenda na
Patricia”
Patricia akatabasamu na
kusema
“ Ouh hizo taarifa njema sana
mama.Kama umepata kiwanja
tutasaidiana masuala ya
ujenzi.Nina rafiki yangu mmoja
ana duka la vifaa vya ujenzi tutamtumia huyo kupata vifaa vya
ujenzi”
“ ahsante sana Juliana” akajibu
Bi Doroth na mara mlango
ukafunguliwa Patricia akaingia
“ wow ! Dada Juliana” akasema
kwa furaha na kumkumbatia
Juliana
“ Karibu sana dada Juliana”
akasema Patricia
“ Ahsante sana Patricia” akajibu
Juliana halafu akamfahamisha
Patricia kwamba amekuja
kumchukua ili aende akashinde
nyumbani kwao ambako
kuliandaliwa sherehe ndogo ya
kumpongeza.Patricia alijiandaa
haraka haraka halafu akapanda
katika gari la Juliana
wakaondoka.Breki ya kwanza
ilikuwa Sabina beauty saloon
ambako Patricia alirembwa
“ Wow ! Patricia you are so
beautifu.You are amazing”
akasema Juliana baada ya Patricia kumaliza kurembwa.Toka hapo
walielekea katika maduka ya nguo
na urembo ambako Juliana
alimnunulia Patricia vitu mbali
mbali halafu wakaelekea
nyumbani kwa akina Juliana
Geti kubwa jeusi lilifunguliwa
wakaingia katika jumba kubwa
lenye rangi nyeupe.Patricia
akatabasamu kwa uzuri wa jumba
lile.
“ Patricia hapa ndipo
ninapoishi.Kwa sasa ninaishi
mimi, mdogo wangu Godson
pamoja na binamu zetu
wawli.Baba mama na mdogo wetu
wa mwisho wanaishi nchini Afrika
kusini ambako baba nafanya kazi
katika shirika moja la kimataifa.”
Akasema Juliana kabla ya
kushuka garini
“ Nafurahi kupafahamu
nyumbani kwenu dada Juliana.Ni
nyumba nzuri sana nimeipenda”
akasema PatriciaLaiti mama angeweza
kukubali ningekuchukua tukaishi
wote hapa kwetu lakini mama
katu hawezi kukuachia” akasema
Juliana huku akicheka halafu
wakashuka na kwa kupitia mlango
wa nyuma wakaingia ndani na
moja kwa moja wakaelekea
chumbani kwa Juliana.Patricia
akapatwa na mshangao baada ya
kuingia katika chumba kile
kikubwa na kizuri.
“ Patricia hiki ni chumba
changu cha kulala.Nimekuleta
huku moja kwa moja ili mtu
yeyote asikuone kabla ya sherehe
kuanza.” Akasema Juliana huku
akitabasamu
“ Dada Juliana una chumba
kizuri mno.Sijawahi kuingia katika
chumba kikubwa na kizuri kama
hiki katika maisha yangu”
“ Usijali Patricia.Hivi ni vitu vya
kawaida tu na utakapovizoea
utaviona ni vya kawaida .Kwa sasa usiwaze kuhusu maisha kama
haya.Una kazi ngumu ya kusoma”
akasema Juliana halafu
akafungua kabati kubwa la nguo
na kuanza kumchagulia Patricia
nguo nzuri itakayompendeza kwa
jioni ya siku ile.Alimchagulia suti
nzuri nyeupe na kumpa aijaribu
Patricia hakuna nguo
utakayoiweka mwili mwako
isikupendeze.Kama isingekuwa
bado ni mwanafunzi
ningekushauri uingie katika
ulimwengu wa mitindo.Una umbo
la kiuanamitindo na nina hakika
ungeweza kufika mbali sana lakini
usiwaze mambo kama haya kwa
sasa.Elekeza akili yako katika
masomo” akasema Juliana halafu
akamuacha Patricia mle chumbani
akaenda kuungana na rafikize
katika kuandaa sherehe ile ndogo
ya kumpongeza Patricia.Bado
maandalizi yalikuwa
yanaendelea.Wengine walikuwa jikoni wakiendelea kupika na
wengine walikuwa bustanini
wakipamba sehemu
itakapofanyikia sherehe
“ Wakati pilika pilika zikiendelea
huko nje, Patricia yeye alikuwa
chumbani kwa Juliana akiendelea
kutazama filamu.Wakati
akiendelea kuifurahia filamu ile
nzuri mara mlango ukafunguliwa
taratibu.Patricia alidhani ni
Juliana ndiye aliyeufungua
mlango ule lakini ghafla akapatwa
na mshangao alipoelekeza macho
yake mlangoni.Kijana mmoja
mweupe mwenye sura nzuri na
aliyefanana sana na Juliana
alikuwa amesimama
akitabasamu.Walitazamana kwa
sekunde kadhaa Patricia
akaingiwa na woga.Kijana yule
akaanza kupiga hatua taratibu
kumuendea Patricia.
“ helo Patricia” akasema Yule
kijana huku akinyoosha mkono wake na kumsalimu Patricia
ambaye alipatwa na uoga
mkubwa.Alimtazama kijana Yule
mwenye sura nzuri aliyekuwa
akitabasamu naye akajilazimisha
kutabasamu na kunyoosha mkono
akasalimiana na Yule kijana
“ I’m Godson” akasema kijana
Yule halafu akakaa katika sofa
lililoelekeana na lile alilokaa
Patricia
“ Tafadhali usiogope Patricia
Juliana hawezi kuja sasa
hivi.Nimemsikia akiwaambia
wenzake kwamba uko huku
chumbani kwake amekuficha na
kwa kuwa nilikuwa na hamu ya
kukuona nikaona ninyate ili nije
nikusalimie.Nimefurahi sana
kukuona na kukufahamu”
akasema Godson
“ dada Juliana aliniambia ana
mdogo wake anaitwa Godson ndiye
wewe? Akauliza Patricia.
“Ndiye mimi” akajibu Godson. Nimefurahi kukuona
Godson.Umefanana sana na
Juliana.Nilipokuona tu nilijua
lazima utakuwa ndugu yake”
akasema Patricia na kumfanya
Godson atabasamu.Kimya kifupi
kikapita .Patricia akaendelea
kumtupia jicho la wizi Godson
akimchunguza.Alikuwa ni kijana
mwenye sura nzuri sana na ya
kuvutia sana.Alikuwa na mwili
uliojengeka vyema.Fulana ile
aliyovaa iliyokatwa mikono
ilionyesha michoro aliyojichora
katika mabega yake.Kwa ujumla
alikuwa ni kijana mwenye kuvutia
mno ambaye kila binti angetamani
kuwa naye.Kwa mara ya kwanza
katika maisha yake Patricia
akajikuta akisisimka mwili
“ Patricia ! ..akaita Godson na
kumstua Patricia
“ Juliana ameniambia kwamba
umeshika namba moja katikamatokeo ya mtihani wa kidato cha
nne”
“ Ndiyo Godson” akajibu Patricia
“ Hongera sana
Patricia.Unastahili pongezi”
“ Ahsante sana
Godson.Namshukuru sana Mungu
kwa hilo”
“ By the way,umekwisha
pangiwa ni shule gani unakwenda
kuendelea na kidato cha tano?
“ Ndiyo.Nimechaguliwa
kuendelea na kidato cha tano na
sita katika shule ya J.Y.Makamba
school of science iliyoko Bumbuli
Tanga.Ni shule mpya kabisa na
nzuri.”
“Safi sana kama umechagua
mchepuo wa sayansi.Katika dunia
ya sasa sayansi ndiyo
inayoongoza.Hata mimi napenda
sana masomo ya sayansi
.Unafikiria kuwa nani huko
mbeleni? Napenda niwe daktari” akajibu
Patricia
“ That’s great.Mimi pia nilisoma
shule ya sayansi lakini nimejikita
zaidi katika teknolojia ya
kompyuta.”
“ Ouh safi sana.Hata mimi nina
hamu sana ya kujua kompyuta “
“ Katika shule uliyosoma
hakukuwa na somo la kompyuta?
“ Somo la kompyuta lilikuwepo
lakini hakukuwa na kompyuta
hata moja shuleni kwa hiyo
ilikuwa vigumu
kuelewa.Nafahamu kuna vitu
vinaitwa keyboard,monitor lakini
sijawahi kuvitumia
“ Uko tayari nikufundishe
kompyuta walau kwa siku hizi
chache kabla ya kwenda shuleni?
Nina hakika itakusaidia sana
katika masomo yako.”
“ Niko tayari Elvis.Natamani
sana kujua kompyuta” Basi usihofu kuhusu
hilo.Nitakufundisha katika kipindi
hiki kifupi kabla ya kuelekea
shuleni.” Akasema Godson na
mara mlango ukafunguliwa
akaingia Juliana.Alishikwa na
mshangapo mkubwa baada ya
kumkuta Godson mle chumbani
“ Godson !!!!!..akasema Juliana
“Nini kimekuleta chumbani
kwangu?Please get out of here
now” akafoka Juliana.
Huku akitabasamu Godson
akainuka na kumsogelea dada
yake.
“ Calm down big sister.Nilikuja
kumsalimu Patricia.Nimeshindwa
kuvumilia hadi jioni” akasema
Godson.
“ Ok go out now” akasema
Juliana na Godson akageuka na
kumtazama Patricia
“ Bye Patricia.See you later”
akasema Godson na kutoka mle
chumbani. sorry Patricia.Huyu mdogo
wangu ni mtundu
sana.Hajakwambia neno lolote la
kukukwaza?
“ Hapana dada
Juliana.Hajanitamkia neno lolote
baya.Alitaka kunisalimu tu na
tulikuwa tukiongea mambo ya
kawaida ya masomo.Godson ni
mcheshi sana” akasema Patricia
“ Sikutaka mtu yeyote akuone
kabla ya muda haujawadia.I
wanted to surprise them.Lakini
huyu Godson kajipenyeza mpaka
amekuja kukuona.” Akasema
Juliana na kumfanya Patricia
acheke kidogo
“ Dada Juliana ,Godson
ameniambia kwamba yuko tayari
kunifundisha kompyuta” akasema
Patricia na kumstua Juliana
“ Godson anataka kukufundisha
kompyuta?
“ Ndiyo dada JulianaAmesema atakufundishia wapi
na lini?
“ Bado hajasema ni lini na
wapi.Mbona umestuka hivyo dada
Juliana? Hana uwezo wa
kunifundisha? Akauliza Patricia
Juliana akavuta pumzi ndefu na
kusema
“ Godson amesoma kompyuta
na anaifahamu vyema .Ni hivi
majuzi tu amerejea toka nchini
Marekani alikokuwa akisomea
sayansi ya kompyuta.” Akasema
Juliana na kumtazama Patricia .
“ Are you sure you want to learn
computer? Akauliza Juliana.Huku
akitabasamu Patricia akajibu
“ Ndiyo dada Juliana”
“ Ok hakuna shida .Nitaongea
naye ili tuone namna
tutakavyoweza kufanya kuhusu
somo hilo lakini kabla ya yote
lazima mama akubali” Mama hatakuwa na shida
,mara zote huwa hana shida
linapokuja suala la masomo.”
“ Nitaongea naye jioni ya leo
nitakapokurudisha” akasema
Juliana
Ilikuwa ni siku nzuri sana na ya
kupendeza kwa Patricia na kwa
wote waliohudhuria sherehe ile
ndogo ya kumpongeza .Chakula
kitamu kiliandaliwa na vinywaji
vya kila aina vilikuwepo
Ilipotimu saa mbili za usiku
Juliana akamuomba Patricia
ajiandae ili aweze kumrejesha
kwao.Patricia akaagana na wote
waliohudhuria sherehe ile
,akawashukuru kwa kufika kwao
na kwa zawadi walizomzawadia
halafu akaingia garini yeye
Patricia na Godson ambaye
aliomba akapafahamu nyumbani
kwa akina Patricia
Waliwasili nyubani kwa akina
Patricia lakini mama yake bado alikuwa hajarejea.Juliana na
Godson hawakukaa sana
wakaondoka huku Juliana
akiahidi kuongea na mama yake
Patricia simuni kuhusu suala la
mafunzo ya kompyuta
“ Ilikuwa ni siku nzuri sana
kwangu kiasi kwamba ninaiona
kama imekuwa fupi mno.Sijui
nitamlipa nini dada Juliana kwa
wema wake huu
mkubwa.Ametokea kunipenda
sana na kunijali kama ndugu yake
wa damu.Ana roho nzuri sana ya
upendo na ndiyo aana
anafanikiwa.” Akawaza Patricia na
mara picha ya chumba kikubwa
cha Juliana ikamjia kichwani
akatabasamu
“ Nimekipenda sana chumba
cha Juliana.Kina kila kitu
ambacho mwanamke
anakihitaji.Natamani siku moja na
mimi niishi maisha kama yale ya
Juliana lakini yote haya yatawezekana tu kama nitaongeza
juhudi katika masomo.Familia
yangu ni masikini na haina uwezo
wa kunifanya niishi maisha kama
yale ya Juliana.Kitu pekee
kitakachonifanya niishi maisha
kama yale ni elimu..” akawaza
Patricia huku akiendelea
kufungua zawadi alizopewa picha
ya Godson ikamjia kichwani
“ What a handsome guy.Kusema
kweli sijawahi kuona kijana wenye
sura nzuri kama Godson.Uzuri
wake hata mimi umenigusa.Ana
sura nzuri,mwili laini na na hata
tabia yake inaonekana ni nzuri
japokuwa Juliana alisema
kwamba ni mtndu.Alikuwa
akiongea nami kwa lugha
laini.he’s so sweet” akawaza
Patricia huku akitabasamu na
kuendelea kuzifungua zawadi zake
 
Back
Top Bottom