Riwaya: Msako wa Hayawani

idawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2012
Posts
25,284
Reaction score
38,364
KAMBI YA NDALA.


MWANGAZA hafifu wa mapambambazuko
uliwafanya Luten Dennis Raymond Makete na wenzeke waonekane kama vivuli.Walikuwa katikati ya msitu wa Ndala wakienda mbio za mchakamchaka.
Wote walikua katika vazi kamili la kombati,bunduki mkononi ,mkoba mgongoni.


Rekuruti au 'Kuruta' wanaochukua mafunzo ya Uwanajeshi wa kawaida huamushwa mapema kuanza mazoezi.Lakini wanajeshi wanaojitayarisha kuchukua kozi ya ukomandoo huamushwa mapema zaidi -aghalabu hukesha na kufanya mazoezi usiku na mchana.
Na mazoezi yao huwa magumu kupindukia .Kwani lengo kuu ni kumkomaza mwanajeshi afikie kiwango cha hali ya juu kabisa ya ukakamavu na ujasiri ili awe tayari wakati wowowte ule kuhimili mazingira ya aina yoyote,hata mateso.Kwani iwapo atakuja shikwa na adui hapaswi kutoa siri.Anachopaswa kufanya ni moja wapo tu kati ya mambo matatu:Kuhimili mateso,kutoroka au kujiua.


Sehemu kubwa ya mazoezi yenyewe kwa kweli ni mateso matupu,Kwanza kabisa,mwanajeshi hutakiwa aishi maisha magumu kadri iwezekanzvyo.Kula kwa taabu,kunywa kwa taabu,kulala kwa taabu .Jua liwe lake ,mvua yake,baridi yake.Hakuna cha kukwepa .
Na juu ya hayo,kuna amri za ajabu ajabu ambazo lazima zitiiwe bila ya kusita .Kama vile kutembea au kukimbia msituni usiku wa manane .Kuchimba handaki katika muda mfupi usio wa kawaida .Pengine kwa kutumia zanz zisizo za kawaida,bakuli la mesi au hata vidole vitupu.Kupanda mti ambao pengine hata Nyani asingeweza kupanda.Kuvuka mto ambao mtu wa kawaida asingeweza kuuvuka ,tena na mzigo mgongoni na bunduki mkononi. Na kadhalika.
Baada ya mazoezi hayo ambayo huchukua takribani miezi mitatu,na ambayo hudhihirisha ukakamavu na ujasiriwa mutukabla ya kuchaguliwa kuanza kozi yenyewe ya ukomandoo,mwanajeshi hutakiwa adhihirishe pia kiwango cha hali ya juu cha werevu,busara,maarifa,ujanja utundu.
Kwa hiyo si ajabu kuona idadi ya makomandoo ni ndogo sana katika jeshi lolote lile duniani.Kwani hatimaye,idadi ya wanaofaulu kuteuliwa kuchukua kozi yenyewe huwa aghalabu haifikii asilimia hamsini.Na kati yao, wanaohotimu na kuwa makomandoo kamili huwa wachache zaidi..Mmoja au wawili-wakati mwingine zaidi ,kufia mafunzoni ni jambo la kawaida kabisa.Kwani mtihani wa mwisho ni wa kupambana kwa kutumia silaha za kweli kweli.


katika hali kama hiyo ,si ajabu pia kuona kuwa mwanajeshi huwa kwa kawaida halazimishwi kuchukua mafunzo ya ukomandoo.kila mmoja hujitolea yeye mwenyewe.
Na kawaida ,hakuana anaelazimishwa kumaliza kozi yote.Ye yote ,wakati wowote,anapoona imetosha huinua mokono juu na kurudia uanajeshi wa kawaida.
Na hakuna anayemcheka .Huwa kinyume chake.Hupongezwa na kila mmoja .Kwani yeye angalau ameweza kujaribu kuishi jehannam kwa siku chache,wiki chache au miezi michache.




*************
Dakika chache kabla ya saa nne kamili Dr.Raymund Makete aliliegesha gari lake aina ya Bentley kwenye uwanja wa kuegeshea magari nyuma ya Benki ya wakulima .Akateremka na kuelekea barabara ya Nkurumah ,uliko mlango wa mbele wa benki hiyo.
Dr.Makete alkua mtu mzima wa zaidi ya miaka sitini.Nywele zake zilikua nusu nyeupe nusu nyeusi.Lakini hata hivyo,hakuwa mkongwe aliekongoka .Akiwa na mwili wa wastani na wajihi mtulivu wa kiungwana .Alikuwa angali imara,nadhifu,alietembea kwa hatua madhubuti za uhakika.Si za pupa wala si za kinyonga .Suti yake ya kiafrika-ya mikono mifupi na kola pana -ilimkubali kikamilifu.
Aliumaliza uchochoro wa benki akaingia mtaa wa Nkurumah na kupinda kushoto.Hatua chache zaidi zikamfikisha kwenye mlango wa mbele wa Benki ya Wakulima.
Alipousukuma mlango huo ukamgonga mtu aliekuwa anataka kutoka ambaye macho yake yalikuwa kwenye karatasi alizozishika mkononi.


Alkua mrefu ,aliyenawili vizuri,wa umri wa kati ya miaka hamsini na tano,mwenye haraza kubwa lililotenganisha nywele kama matuta .Suti yake ya kunguru ilionyesha wazi kuwa ni ya thamani,Na yeye mwenyewe alionyesha wazi hakuwa na tatizo la ukwasi.
"Kumradhi,"Mzee Makete alisema haraka kama vile kosa la kumgonga mtu huyo lilikuwa lake peke yake.Mtu huyo alipoinua uso,macho yake na ya Mzee Makete yakafungamana.Macho yake yalikua makubwa kuliko kawaida,tena makali,ya dharau na jeuri.Ya mtu ayenata.Mtu anaeaminianaweza kupata chochote akitakacho au kufanya lolote apendalo.
Mzee Makete akaganda,macho yake mapole ameyafinya ,mdomo nusu wazi kwa mshangao na msituko .Kumbukumbu ya mambo ya kutisha ikamjia akilini.Akauliza kwa sauti kama si yake,"Wewe siye Kassim?"
"Nani?" Ingawa mtu huyo aliuliza kijeuri lakini uso ulikwishambadilika ghafla .Ulimwiva,na alikua akipumua kwa nguvu .Macho yake makubwa yaliingiwa na kila dalili ya hofu.Mshituko wake ulikua mkubwa zaidi kuliko wa Dr Makete.
Ingawa walitazamana kwa nukta moja au mbili tu,lakini ilikuwa kama muda mrefu zaidi ulipita kabla ya Dr.Maketekusema "Kassim Ha....."
 
Mwanzo wa riwaya waonesha mzuri .........tuongee nyingine'09.πŸ™‚
 
"Siye mimi."Mtu huyo alimkatiza,akijaribu kutoka haraka .Akaongeza,"Umekosea."


Mzee Makete akabaki mlangoni ameduwaa,amechanganyikiwa,akimtazama mtu aliemdhania kuwa ni Kassim akiondoka kwa hatua ndefu na za hima.Hatimaye,mtu huyo alipopinda kulia na kuingia uchochoro wa banki,akielekea kwenye egesho la magari,Makete alivuta pumzi ndefu na kuingia ndani.


Huku akipambana na mawazo yaliyomchafuka,alikwenda kwenye meza iliyotupu.Akaketi na kutoa kitabu cha hundi na kalamu.Lakini alipotaka kuandika hundi aliona kalamu inacheza,mkono ulikua unamtetemeka!


Hapana,alijiambia. Hawezi kuwa amekosea.Yule ndie Kassim.Asingeweza kuwa mtu mwingine.kama hakuwa yeye, kwa nini alisituka vile?


Sasa nifanye nini? Makete alijiulza.Kalamu ikiendelea kucheza mkononi.Wajibu wangu,alijijibu,ni kwenda kuripoti Polis.Lakini mbona imeshapita miaka mingi?Mingapi vile?Ishini na mnne?Au na mitano?Au na sita? Watanitia maanani? Si wanaamini kuwa Kassim Hashir ameshakufa zamani!


Au niache mambo kama yalivyo-yaliyopita yamepita? Mzee Makete aliendelea kujadiliana na nafsi yake.Nitapata usingizi kweli? Kwa vyovyote itanibidi nimweleze mama Denny. Kwa vyovyote sitaweza kumficha mke wangu jambo kama hil. Akiniona tu atajua nina kero moyoni.
Mzee Makete akajaribu kifikiria hali ya mkewe itakavyo kuwa asikiapo Kassim angali hai. Akajiuliza kama wangeweza kuendelea kuishi kwa raha na furaha kama wanavyoishi sasa.Mkewe lazima angekereka zaidi. Angefadhaika na kuhuzunika na kusononeka.Waliposikia Kassim amekufa walisali sala maalumu-sala ya kuuzika mzoga wa hayawani.
Na sasa....!
Alijaribu tena kuiandika hundi,akashindwa tena.Akarudisha kalamu na kitabu cha hundi mfukoni na kuinuka. Lazima arudi nyumbani na kushauriana na mkewe.Hili halikua jambo la kuamua yeye peke yake.
Akatoka na kuelekea kwenye egesho la magari.Alipokaribia kuumaliza uchochoro akasikia mvumo wa gali lijalo kwa kasi nyuma yake.Akageuka na kulitizama kwa mshangao.Uchochoro huo haukua wa kupita magari.
Gali hilo lilikua hatua chache tu nyuma yake.Lilikuwa Benz jipya jeupe,likiendeshwa na mtu ambaye Makete aliamini kuwa ndiye Kassim. Uso wake sasa ukiwa wa ulikuwa wa kihayawani,na ulionyesha waziwazi dhamira yake.
Dr.Makete akapigwa na butwaa,mwili mzima ukamfa ganzi.Kufumba na kufumbua,kabla ya kuweza lolote,gali hilo likamparamia na kumrusha hatua kadhaa.


***************



Siku ilikuwa ingali changa lakini jua lilikwishwa pamba moto. Kila mmoja alikuwa akivujwa jasho. Denny. akiongoza,aliinua mkono kuashiria kusimama. Akasema,"Tutapumzika kwa nusu saa"


Wote wakapumua kwa sauti. Wamekuwa mbioni tangu saa kumi na moja alfajiri. Denny akajiuliza kama anawaendesha wenzake kupita kiasi au kama hawakustahili kuwa makomandoo.Yeye,alikuwa na hakika angeweza kuendelea kwa masaa manne zaidi bila ya takilifu.


Ingawa alikua anakaribia kutimiza miaka ishirini na sita,pamoja na urefu na ukakamavu wake, Denny bado alionekana kama mwanafunzi wa sekondari.
Alikuwa na uso mtulivu wenye macho maangaavu.Yeyote asiyemjua asingeamini kuwa kijana huyo ni komandoo kamili.
Lakini hakuwa komandoo tu. Alikua mkufunzi wa kozi ya ukomandoo.Alipewa kazi hiyo mara tu baada ya yeye kufuzu miaka miwili nyuma.Nidhahiri alifuzu vizuri.
Ilibidi afuzu vizuri. Tangu utotoni darasani alikuwa mwerevu na ulingoni alikuwa na kipaji.Alikuwa mwanariadha na mshiriki wa michezo kadhaa,hasa masumbwi na kandanda.
Denny alijiunga na jeshi miaka mitano nyuma,mara tu baada ya kumaliza kidato cha sita.Baba yake alipendelea aendelee na masomo hadi awe mhandisi au daktari kama yeye lakini haikuwezekana.


Itaendelea.........!
 
Tupe story mkuuu naumwa mb'u tu na shemejiyo leo kanisusaπŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„πŸ™„
 
Yale yale ya akina kidi kudi na mapengo juniour, nawashauri muige mfano wa will gamba... otherwise ni busara kukaa kimya na hadithi yako kama huna uhakika wa kumaliza... au utangaze bei ya kitabu... au..
 
Hiki ni kati ya vitabu vichache sana maarufu vya enzi zetu ambavyo niliishia kuvisikia kwa majina tuu..
 
Ebwana eeeh kama unajua huwezi malizia story na kutupa kwa wakati usilete kiherehere cha kuanzisha uzi wa story
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…