Riwaya: Msako wa Hayawani

Mnoooo...watu tushaanza kua na arosto ya msako wa idawa...
 
Jaman kama mtu hanna uhakika wa wa kutuketea riwaya kwa mtiririko mpaka mwisho usilete kaa nayo tu maaana hii ni Kero sasa
 
SEHEMU YA ISHIRINI.


Zebra Inn ilikuwa uchochoroni, nyuma ya majengo mawili ya kale, ya kutunzia nyaraka za serikali. Pamoja na kuwepo bango getini lenye picha ya pundamilia, ungeweza kuupita mgahawa huo kama si harufu ya kukata pua ya vyakula mbalimbali.
Na ulikuwa mgahawa wa aina yake. Ulikuwa kama uwanja wa tenesi. Katikati palikuwa na meza chini ya miavuli, na pande tatu zilikuwa na vyumba vidogo vya mbao na milango ya pazia za shanga. Upande wa nne kulikuwa na kaunta kwa wapendao kuketi juu ya stuli. Na nyuma ya kaunta kulikuwa na jiko.


Mgahawa huo ulikuwa na sifa kubwa ya upishi wa kimataifa. Lakini bei za vyakula zilikuwa za kuchinja koo. Chiko aliingia humo akaenda moja kwa moja kijichumba Namba 8. Mlikuwa na meza ya wastani iliyozungukwa pande tatu na kitu kama siti ya nyuma ya gari la kifahari. Mara tu Chiko alipoketi, mhudumu aliyevaa suti nyeupe yenye picha ya pundamilia kwenye mfuko wa kifuani akaingia.

"Mheshimiwa." Alisema mhudumu huyo kwa adabu, "Hukioni hicho kibao kisemacho 'private' hapo mezani? Twende nikupeleke chumba kingine."
"Hapana. Ni Bwana Kembo aliyeniambia nije hapa. Yeye atafika sasa hivi."
"Ooh! Samahani sana."
"Hapana shaka." Alijibu Chiko kimkogo.
"Nipatie kifungua kinywa."
"Nikupatie menu?"
"Hapana, nipatie kifungua kinywa kamili." Mhudumu akasita. Akasema, Naamini unaijua bei yake."


Chiko akabetua midomo na kuuliza. "Unamashaka kuwa Bwana Kembo atashindwa kulipa?"
"Ooh, hapana. Hapana, bwana mkubwa. Samahani sana."
"Hapana shaka, usijali." Chiko akavua miwani yake ya jua na kuiweka mezani.
"My God!" Akawaza. "Kuitwa 'bwana mkubwa' na mhudumu wa Pundamilia! Pesa! Laiti angejua!"


Kembo akafika akaketi. "Tatizo gani linakusumbua? Simuni ulisikika kama kigoli aliyedondokewa na nyoka kitandani!"
"Nilikuwa sijapata shoti yangu ya asubuhi." Alikiri Chiko. "Vitu vyangu vipo Tupetupe ambako naogopa kwenda, polisi wazaweza kuwa wananiwinda."
Akiwasha sigara, Kembo akasema, "Chiko, huo wasi wasi wako ni wa kweli au...au."
"Au kitu gani Bwana Kembo?"
"Isiwe unataka kunitoa pesa za ziada. Kama ni pesa sema wazi tu."
"Bwana Kembo, ingawa watu hustihizai, lakini umeshawai kumwona mtu aliyekata tawi alilolikalia?"
"Sijawai. Na sitazamii kumwona."


"Isitoshe, kama ningekuwa mtu wa tamaa, ningemdai rafiki yako kifumba mdomo. Na usitazamie nitakuwa mpumbavu kama Kikoti."
"Alichokifanya rafiki yangu unakijua?"
"Sikijui kwa hakika, lakini nashuku anatafutwa na polisi kutokana na swala la yule Daktari aliyegogwa na gari jana asubuhi."
Kembo akainua mikono, ishara ya kumnyamazisha, kwani mhudumu aliingia.
"Shikamoo Bwana Kembo."
"Marahaba. Za asubuhi?"
"Shwari." Alijibu mhudumu, akiandaa vitu mezani. "Nikupate nini?"
"Kahawa tu kama kawaida. Bila ya sukari, bila ya maziwa."


Mhudumu alipoondoka Kembo akayarudisha macho yake kwa Chiko. "Naamini hutafanya kitu kama hicho."
"Kitu gani?" Chiko aliuliza akijikorogea chai.
"Kumdai rafiki yangu kifumba mdomo."
"Alaa, ningekuwa na hata chembe cha wazo hilo, ningekwambia niliyokueleza?"


Kembo akaafiki kwa kichwa. Akasema, "Subiri kahawa yangu iletwe kisha nieleze kila kitu."


*****************************************


"Twende Kituo Kikuu." Alisema Bessy akiingia garini, Denny akaliwasha. "Kuna nini Kituo Kikuu? Nilikuwa na mipango mingine."
"Kama ipi?"
"Kama kumtafuta mkora mmoja anaitwa Chiko." Denny aliligeuza gari na kulielekeza mjini.
"Chiko? Jina hilo si geni kwangu, lakini sura imenitoka. Kwani wa nini?"
"Ni rafiki yake Hoza."
"Unataka kumtafutia wapi?" Bessy aliuliza.
"Katika sehemu za kijinga kama vile Tupetupe."
"Unamjua alivyo?" Denny akatikisa kichwa. "Simjui."


"Basi twende Kituo Kikuu kwanza. Pengine tuna picha yake. Isitoshe," Bessy akaendelea, "Nataka kumhoji Butu."
"Ndiye nani huyo Butu?"
"Ni mwenzake Bob, askari wa barabarani aliyeuwawa jana usiku. Kifo chake kinanitatanisha na kunikereketa. Yeye na Butu walikuwa pamoja jana asubuhi, kwenye ajali ya babako walikuwa biti moja. Mara kwa mara walipangwa pamoja. Nadhani walikuwa marafiki. Nataka kufuatilia nyendo za Bob kwa jana. Pengine Butu anaweza kuwa anajua kitu kuhusu kifo cha rafiki yake. Nilipokwenda asubuhi, alikuwa hajawasili. Nikaacha maagizo afikapo anisubiri, asipewe biti."


"Inaelekea unashuka kifo cha huyo Bob kinahusia na mkasa wa babangu."
"Kuna kitu kinaniambia hivyo ubongoni mwangu." Alikri Bessy.
"Hisia ya sita?"
"Kitu kama hicho. Hebu niambie jambo moja. Mama alishawahi kukusimulia kisa kile,siyo?"
"Hata mara moja."
"Kumbe, kwa nini ukasema unazifahamu habari za mtoto wa Asha kabla ya mama kutusimulia?"


"My God! Bessy! Sikujua kama unaweza kuwa zumbukuku kiasi hicho!" Alisema Denny kwa ikirahi. Akalisimamisha gari pembeni ya na kuanza kufungua vifungo vya shati.
"Denny unataka kufanya nini?" Denny hakujibu. Akalifungua bega lake la kushoto. Bessy akatoa macho na kupiga yowe. "Nooooo!"
"Hilo jingine," Akasema Denny akivifunga vifungo, "Utaliona siku nyingine."
"Ooh! My God Denny, I'm sorry. Terribly! sorry!"


"Wanajeshi wenzangu hulitazama kovu hili kwa heshima kubwa, wakidhani nimelipata kishujaa."
"Lakini Denny, umelipata zaidi ya kishujaa. Mungu wangu,Denny umeanza kukwepa visu tangu ukiwa tumboni! Ndiyo maana huviogopi."
"Nani kakwambia uongo huo?" Denny aliuliza akiling'oa gari.


"Palikuwa na kimoja - tena cha kijahili, karibu na maiti ya Dikwe, huyo pusha aliyetafunwa na fisi. Kilikuwa na alama za vidole vyake."
"Kwa hiyo?"
Msichana Bessy akainua mabega. "Ni dhahiri kuwa yeyote yule aliyempeleka Uwanja wa Gofu , akamnyuka na kumtelekeza haogopi visu."


**********************************


"Sijui niazie wapi." Alisema Chiko. "Mambo yenyewe yananitatanisha hata mimi."
"Anza tangu mwanzo." Alishauri Kembo.
"Mwanzo wake unaujua. Ulimtuma Hoza akamlipue yule bwana aliyegogwa na gari, mgonjwa wa jengo D, chumba namba 13. Hakufanikiwa. Badala yake kalipuliwa yeye. Tena na msichana tu - Kachero Isnpekta Bessy. Kumbe yule mgonjwa analindwa na polisi masaa ishirini na nne."


Kembo akameza funda la kahawa yake chungu. Akasema, "Mpaka hapo sikioni cha kukipigia mayowe."
"Sio hilo tu. Pana mengine. Wakati sisi tuko kule darajani, polisi walikwenda Tupetupe. Bila sha Hoza alitembea na ufunguo wa chumba chake. Hata hivyo hawakuutumia, walimwamuru meneja afungue mlango. Kwanza walikuwa watatu, Bessy na makachero wawili wa kiume. Kisha akafika wa nne,kijana mdogo tu."
"Sasa wewe umeyajuaje yote hayo?"
"Bwana Kembo unadhani mimi naishi kijinga? Sehemu kubwa ya mapato yangu inaishia kwa washikaji zangu. Hapo Tupetupe watu kibao hufaidi fadhila zangu.


"Watumishi wa hoteli hiyo, mapusha, mashangingi na hata mashoga. Hata meneja wa hoteli hiyo hupokea fadhila zangu."
"I see!"
"Mimi na Fensy tuliporejea hapo hatelini jana usiku tulidakwa na washikaji kabla ya kuingia ndani. Walishanong'onezwa na meneja na watumishi wengine nini kinachoendelea. Mmojawapo akiwa Dikwe, jambo ambalo linanishangaza."
"Kwa nini?"
"Yeye alikubali kuchukuliwa na huyo askari wa nne na kupelekwa Uwanja wa Gofu."
"Labda hakujua kuwa askari."
"Inawezekana. Hata Chox ana mashaka kama jamaa ni askari. Aliwasili hapo Tupetupe na gari la aina ya kipekee. Linaitwa Bentley.


Lilly akataka kumdaka akaambiwa, 'Go screw yourself!' Dikwe akamtachi. Kijana huyo akasema anamtafuta Hoza,ambaye alidai ndie pusha wake wa kawaida. Kisha akaingia ndani na kwenda ghorofa ya nne, kwenye chumba cha Hoza. Chox akamfuta Dikwe akamuuliza, 'Vipi, yule kijana ni kastama wako?' Dikwe akajibu ni wa Hoza. "Sijapata kumwona ." Alisema Chox.
"Hakumwambia Hoza hayupo?"
Dikwe akasema alimwambia, lakini hata hivyo alikwenda juu kuhakikisha.


"Hukumwambia chumbani mwake kuna unaa?" Chox akamwuliza Dikwe.
"Dikwe akasemaje?"
"Akasema hafanyi kazi ya kanisa."
"Enhe, kisha?"
"Kijana huyo akaingia chumbani mwa Hoza, lakini hakukaa sana. Lakini habari zilishazagaa aliposhuka chini , Chox, ambaye hakuwa na chochote maungoni ili amcheki vizuri. Akamuuliza kama alihitaji huduma."
"Akamjibuje?"
"https://jamii.app/JFUserGuide off."
"Kuna chochote katika jibu hilo?"
"Ni vigumu teja kumjibu hivyo pusha. Wao ni watumwa wetu, kwa kawaida hutunyeyekea."
"Kisha ikawaje?"


"Kijana huyo akamwendea Dikwe. Wakaingia ndani ya gari lake. Chox akataka kwenda kumshitua Dikwe lakini hakuwahi. Udhaifu wa Dikwe ni kwamba alikuwa na tamaa sana. Na alikiamini sana kisu chake."
"Unasema alimpeleka wapi?"
"Uwanja wa Gofu."
"Kijana huyo ni kachero," Kembo aliuliza, "Kwa nini ampeleke Uwanja wa Gofu badala ya kumpeleka kituoni?"
"Ni wazi ili akamhoji. Na alitaka majibu ya haraka. Huwezi kupata majibu ya haraka kituoni."


Kembo akatikisa kichwa. "Sidhani kama polisi wanaweza kuchukua hatua kama hiyo. Hasa kwa kesi ya kugongwa na gari, na aliyegongwa hajafa."
"Kumbuka kuna kitendo cha Hoza kwenda hospitalini kummaliza."
"Nakumbuka. Lakini je, haupo uwezekano wa Dikwe kupelekwa huko Uwanja wa Gofu na mtu mwingine baada ya kuachana na huyo kijana?"
"Chox anasema haupo. Anasema kijana huyo ingawa ni mdogo kuliko mimi, si wa kawaida. Hasa macho yake."
"Yana nini?"
Chiko akabetua mabega. "Sijui."


Kembo alikiondoa kikombe mdomoni akailiza, "Sasa wasiwasi wako ni wa nini?"
"Dikwe anaweza kuwa kaimba."
"Kuna lolote la maana alilolijua?"
"Machache. Kama vile mimi na Hoza tulikuwa marafiki, na sote tuna vibweka. Alijua kwa sasa niko Tupetupe. Ndiyo maana nasita kwenda huko."
"Sikiza." Alisema Kembo. "Cha kufanya ni kupata uhakika kijana huyo ni nani. Kama ananunulika, anunuliwe. Kama hanunuliki,alipuliwe. Mimi na wewe hatujashindwa jambo hata siku moja.


*************************************


"Butu ameshafika?" Bessy alimuuliza sajini wa kwenye kaunta. "Ndiyo afande." Akajibu sajini huyo. "Yuko nyuma."
"Mwambie aje ofisini mwangu." Bessy akataka kuondoka, akakumbuka. "Na sajini, waulize watu wa kompyuta kama kuna faili la mkora aitwaye Chiko. Kama lipo waniletee."
"Sawa afande."


Bessy na Denny wakazipanda ngazi, huko juu wakaingia katika chumba cha wastani chenye meza mbili ndogo,viti vitatu na benchi moja. Ukutani palibandikwa ramani ya jiji na matangazo kadhaa.
Denny akaenda kuketi nyuma ya meza ya pili, ambayo haikuwa na chochote. Haikuwa hata na simu wala trei la majalada.
"Nikilazimishwa nishinde mchana kutwa katika chumba hiki," Akasema Denny, "Naweza nikajirusha dirishani."
Besy akatoa kicheko kidogo. "Unadhani mimi hujifungia mchana kutwa?"
Mezani pake palikuwa na simu na mafaili mawili matatu. Akalifungua la juu. Akasema. "Ooh, Ni ripoti za matukio ya jana usiku. Bob na huyo mwenzake waliouwawa kwenye saa sita za usiku. Walilipuliwa na bastola tofauti. Kwa hiyo wauaji walikuwa wawili. Kwa vyovyote si chini ya watu wawili."


"Ina maanisha chochote?"
"Sijui. Isipokuwa mauaji haya yanazidi kutatanisha." Bessy akasoma ukurasa mwingine. Akasema. "Na Dikwe alikufa karibu na alfajiri. Alivunjwa mfupa wa mkono wa kulia na wa mguu wa kushoto kabla ya kufa. Madaktari wanasema mifupa hiyo haikuvunjwa kwa meno ya fisi."
Dennya akataka kusema neno lakini mlango ukagongwa, na Kostebo mwenye jalada mkononi akaingia. Akasema. "Faili la Chiko afande."


Bessy akalipokea na kulifungua. Baada ya kulipitia haraka haraka, akamwambia Denny, "Ameshawahi kufungwa, lakini karibu miaka miwili iliyopita. Kifungo cha miezi sita, kwa kukutwa na bangi. Baada ya hapo amekuwa akikamata mara kwa mara na kuachiwa kwa ukosefu wa ushahidi wa kutosha."
"Picha je?"
"Ipo moja nzuri."

Denny aliinuka na kulichukua faili na kurudi mezani. Akajikuta anamtazama kijana mwenye sura ya kawaida kabisa. Akatikisa kichwa. "Nani angeweza kuamini anaweza kufanya kitendo kama kile?"
"Kitendo gani?"
"Cha kule Uwanja wa Gofu."
"Dennya sijaanza jana wala juzi kazi ya upolisi. Mtu aliyemvunjavunja Dikwe na kumtelekeza Uwanja wa Gofu si Chiko wala mtu mwingine yeyote zaidi yako."
"Bessy!"
Bessy akainua viganja. "Usiwe na wasi wasi! Sina hata chembe ya ushahidi."
"Ungekuwa nao?"
"Ooh! Usiniulize maswali yasiyojibika."


Wakakodolena macho kwa nukta mbili au tatu. Kisha Denny akasema, "Bessy, hatujaoana hali hii, ugomvi kila wakati, tutakapooana itakuwaje?"
"Yaelekea una uhakika kabisa na jambo hilo."
"Kabisa."
"Unataka tupinge?"
"Sawa, konzi kwa konzi."
"La wapi?"
"Mshindi ndiye mchaguzi."


Cc Joharia chiko18 gspace
 
Last edited by a moderator:

Mkuu endelea

idawa njoo mkuu tunakufa kwa hamu

Vp Mkuu mbona kimya leo? Tumia hata episode 1 mkuu

Muwe na subira kidogo ndugu zangu. Kitabu kimeliwa na panya upande mzima.

Kamata uyo panya...minya minya sana ateme iyo karatas asee...watu wanakaribia pasuka uku kwa hasira arif...

Kwa taarifa za kiintelijensia nilizopata kutoka chanzo cha kuaminika ni kwamba mkuu idawa anaandika soon atakuja hapa kutupa uhondo.

Nimeingia humu kwa mbwembwe nyiiiingi! Kumbe bado bila bila

na hivi nime-subscribe basi kila 'reply' inaniita nichungulie

Poleni kwa usumbufu wakuu, ni majukumu ya hapa na pale. Karibuni tuendelee.
 
Hahahahah butuuu mwoga sana

Hapana mkuu Bob ndiye kunguru ndo maana kamtuma mwenzake aende sehemu ngumu kama ile we polis kumkamata mwanajeshi wadhani mchezo halafu ana cheo cha luteni
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA



Baada ya kupiga honi na kufunguliwa geti la jumba Na.21, Mtaa wa kitosi, Buffalo Hill, Sam Kembo aliliendesha gari lake ndani. Hakuweza kujizuia kuangalia bustani, nusu akitazamia kumwona Kikoti akimwagia miwaridi.
Mtumishi mmoja alimlaki Kembo na kumwelekeza aliko tajiri yake. Kassim Hashir alikuwa nyuma, akiogelea bwawani.


"Good morning Mr. Kessy." Kembo akamsalim.
"Oh, morning Sam." Alijibu Kassim, "I hope it's good morning." Akayakata maji kwa michapo miwili mitatu ya nguvu na kutoka majini. Akaliokota taulo lililokuwa kwenye kiti na kuanza kujifuta, "Well, is everything ok?"
"Usiwe na wasiwasi, ni asubuhi njema."
"Keti." Wote wakaketi. "Kwa hiyo," Kassim akaendelea, "Si chochote?"
"Ammm, kwa upande tunaweza kusema hivyo."


Mtumishi akamletea Kassim glasi ya maziwa, bila ya sukari. Mtumishi alipoondoka, Kassim akauliza, "Una maana gani, Sam...kwa upande!"
"Nna maana Chiko hakuwa akilaghai. Tuna tatizo dogo. Lakini si la kutubabaisha."
"Tatizo gani?"
"Mawili, kwa kweli, si moja. Yule kijana tuliyemtuma akaifanye ile kazi ya hospitalini kaboronga, pengine halikuwa kosa lake. Dk.Makete analindwa masaa ishirini na nne, naye alikuwa halijui hilo. Akauwawa na askari mmoja wa kike maarufu sana hapa jijini, Kachero Inspekta Bessy."

Kahawa yake ikaletwa, akanyamaza akijijazia kikombe.
"Enhe?" Kassim akauliza akiuangalia mgongo wa mtumishi wake aliyekuwa akiondoka.
"Kwa njia moja ama nyingine,Bessy akagundua kijana huyo, Hoza, aliishi Tupetupe Hoteli. Mambo yakaharibika zaidi."
"Kivipi?"
"Hoza alikuwa pusha, na alikuwa rafiki wa Chiko. Kisha kijan mmoja ambaye tunamwita X kwa sababu mpaka sasa hatuna uhakika kama ni askari au ni nani, alimnasa pusha mmoja hapo Tupetupe na kumpeleka Uwanja wa Gofu. Tunashukuru alumhoji kifasishiti."


"Huyo pusha anaweza kuwa alilijua hilo?"
"No way. Hata Hoza hakuwa akilijua."
"Sasa pana nini tena zaidi?" Kassim aliuliza na kupeleka kuipeleka glasi ya maziwa kinywani.
"Tatizo ni kwamba Dikwe, huyo fal@ aliyepelekwa Uwanja wa Gofu, alifahamu kuwa Chiko na Fansy ni marafiki wa Hoza. Na Chiko na Fensy wanakufahamu. Jana usiku niliwaleta hapa."
"Ulifanya kosa kubwa kuwaleta."
"Hapana. Ilibidi wawe karibu, wewe mwenyewe unafahamu hivyo. Hatukujua nini Bob atasema. Hatukujua atasema pesa zikadondoshwe saa sita. Je,angesema zikadondoshwe dakika ile ile - ndipo tungeanza kuwatafuta Chiko na Fensy?"


"Oh! Hell!" Kassim aliyamalizia maziwa , akaiweka glasi tupu mezani na kuwasha moja ya sigara zake nene zenye harufu nzito. Akauliza, "Kama watabambwa, na kutikiswa kidogo, wanaweza wakaghani?"
"Chiko sina wasi wasi naye," Alijibu Kembo. "Alishatishwa mara kadhaa. Akiamua kuwa bubu, huwa bubu kweli kwel. Lakini Fensy," Kembo akatikisa kichwa, "Sina imani naye."


Kassim aliliondoa sigara lake mdomoni, akageuza kichwa na kumtazama Kembo usoni. Macho yakagongana na kung'ang'aniana.
Kembo akajikuta akiyaangalia macho yasiyo ya kawaida. Akasisimuka mwili mzima. Akayakumbuka maneno ya Chiko. 'Chox anasema huyo kijana siyo wa kawaida hasa macho yake.'


Kembo alidhani Chox alipayuka, lakini sasa aliamini kuna macho yasiyo ya kawaida. Tena macho ya bepari huyu yalizungumza kama yenye sauti.
"Kessy!" Ilikuwa ni mara ya kwanza Kembo kumwita hivyo tajiri huyo, "Kessy, hunitumi nikamtume Chiko kumuua rafiki yake!"
Kassim akalirudisha sigara lake mdomoni na kuyaangalia maji ya bwawa. "Huoni kuwa hiyo ndiyo njia fupi ya kulimaliza tatizo hili?"


***********************************


Kwa dakika mbili au tatu ofisi ilikuwa kimya kabisa, mrembo Kachero Inspekta Bessy akipekua mafaili. Kisha akainuka, akaenda dirishani na kuangalia nje. Bila kugeuka akaita kwa sauti ndogo, "Denny."
"Yes?"
"Denny - huoni kuwa ingekuwa busara zaidi kama ...kama ungetuachia sisi tuendelee na kazi hii?"
"Kwa nini?"
"Kwa sababu Kassim Hashir ni...ni..."
"Ni bull shit!" Denny alibweka. "Kassim Hashir ni bull shit. Hanihusu chochote mimi. Baba yangu ni Dk.Raymond Makete."
"Oh, niwie radhi." Kabla ya Denny kujibu,mlango ukagongwa. Bessy akageuka na kusema "Ingia."


Koplo Butu akaingia ndani kinyonge na kupiga saluti. Alikuwa katika sale yake ya usalama barabarani, ambayo siku hiyo ilionekane kumpwaya. Hata hivyo, V zake mbili za shaba zilimeta kwenye mkono wa shati lake.
"Karibu Butu," Bessy alimwambia. Akautazama uso wake uliopooza. Akasema, "Yaelekea umeshasikia."
"Ndiyo, afande. Nilikwenda hospitalini kuiangalia maiti." Alijibu Butu. Akamtazama Dennis. Macho yao yalipokutana wakakumbukana.
"Wewe siye..." Akaanza Denny, lakini Butu akamkatiza.
"Ndiyo,Luteni." Alisema Butu.
Bessy akauliza, "Vipi mnafahamiana?"


"Tulikutana jana katika mazingira ya ajabu ajabu." Alijibu Denny. Nilipokuwa nikiingia jijini kutoka Ndala, yeye na mwenzake wakiwa katika kigofu wakaniandama. Bila shaka ili wanikamate kwa kwenda kasi."
"Oh!" Bessy alishangaa. Akasema, "Huyo mwenzake bila shaka atakuwa ni Bob, sivyo Butu?"
"Ndiyo, afande."
"Keti."
Butu akaketi kwenye benchi, macho chini.
"Enhe," Bessy akamuuliza Denny,huku akirudi kuketi mezani pake, "Kisha ikawaje?"
"Waliniandama hadi hospitalini." Denny akaendelea.


"Bob akamsakizia Butu, yeye akabaki garini. Huyu bwana akanifuata.Lakini baada ya kunisimamisha, akabadili mawazo ghafla. Akaamua kudharau kila kitu. Alifanya jambo la busara sana. Sijui alikwenda kumwambia nini Sajini wake."
"Eti," Bessy akauliza, "Ulikwenda kumwambia nini Bob?" Butu akabaki kimya, akiendelea kutazama chini.
"Oh, niwie radhi." Bessy akasema haraka, "Sikunuia kustihizai. Alikuwa ni rafiki yako siyo?"
"Sana." Alijibu Butu, akikubali pia kwa kichwa.
"Inasikitisha sana kifo chake. Lakini ilikuwaje auwawe vile, mbona inatatanisha!"
Butu hakujibu.


"Ni dhahiri kauliwa na wakora," Bessy akaendelea. "Tena wakora hatari. Lakini kwa nini? Na kwa nini mahali pale? Au alikuwa na uhusiano na wakora - wamedhulumiana?"
Butu akatikisa kichwa akisema, "Hakuwa na uhusiano na mkora yeyote ."
"Kama angekuwa na uhusiano nao ungefahamu?"
"Naamini hivyo."
"Mlikuwa marafikia kiasi hicho?"
"Ndiyo. Alikuwa hanifichi jambo."
"Jana mliachana wakati gani?"
"Jioni," Alijibu Butu.


Denny akamuuliza, "Matembezi yalikuwa pamoja kila siku baada ya kazi?"
Butu akasita.
"Oh, nilisahau kukufahamisha," Alisema Bessy. "Huyu ndiye mwanae Dk.Makete. Yeye ni komandoo Luteni Dennis Makete. Tafadhali mjibu maswali anayokuuliza. Je, ulikuwa ukitembea na Bob kila siku jioni?"
"Ndiyo, afande."
"Wapi?"
"Kwanza kwa Shangazi Suzy,kisha Lulu Night Club."
"Kwa shangazi Suzy ndiyo wapi?" Denny aliuliza. "Ni baa au stoo au kilabu?"
"Hapana, ni nyumba ya kawaida, Mtaa wa Mshoneni. Huyo 'Shangazi' anauza bia na mapuya."


"Kwa hiyo mlitoka kwa shangazi Suzy mlikwenda Lulu."
"Ndiyo."
"Kisha?"
"Mara kwa mara tulirudi Polisi Laini kulala. Siku moja moja, hasa siku za Jumamosi, tulikwenda disko au dansini."
"Sasa tueleze mzunguko wenu wa jana," Alisema Denny, akaongeza, "Kikamilifu."
"Tulipomaliza zamu tulirudi Laini kuoga na kubadili nguo,kisha tukaenda kwa shangazi."
"Hukutaja kula.Au mlikuwa mkila kwa huyo shangazi?"


"Hapana, tulikwisha kula kantini. Sisi hula kantini. Mimi sijaoa, Bob kakimbiwa na msichana aliyekuwa akiishi nae. Tulijipikia kwa nadra sana."
"Sawa. Mkaenda kwa huyo shangazi?"
"Ndyo."
"Kwa gari la Bob?"
"Ndiyo."
"Ilikuwa saa ngapi?"
"Kwenye saa tisa. Saa tisa na robo au na dakika ishirini."


Denny akamtazama Bessy. Msichana huyo alikuwa akiandika kwa spidi ya ajabu. Denny akakisia alikuwa akiandika katika hati mkato. Akaridhia kimoyomoyo na kumuuliza Butu, "Hapo kwa shangazi Suzy palikuwa na watu wengi?"
"Uani walikuepo watu wakinywa mapuya, lakini sisi hukaa ndani, chumbani mwake shangazi."
"Hamkuwa na watu humo chumbani?"
"Hamkuwa na mtu mwingine zaidi ya Shangazi."
"Enhe, ikawaje?"
"Tukaagiza bia na kuanza kunywa."
"Kisha?"
"Muda mfupi baada ya saa kumi nikajisikia ovyo; nikaamua kuondoka."
"Una maana gani - 'ukajisikia ovyo?' Ulijisikia vibaya? Ulihisi kuumwa?" Denny akamuuliza.


"Si kuumwa hasa,"Akajibu Butu. "Nilihisi kupachoka mahali hapo, kama vile palinikifu."
"Ukaondoka peke yako?"
"Ndiyo. Bob alikuwa na makubaliano fulani na huyo shangazi, mara kadhaa nimeshawai kumwacha hapo. Hivyo halikuwa jambo la ajabu. Niliondoka na kumwacha hapo akiendelea kunywa."
"Wewe ukaenda wapi?"
"Mimi nikaenda Lulu, nikitazamia pengine Bob angekuja baadae kujiunga nami."
"Akaja?"
"Hapana, hakuja. Nilipomuaga hapo kwa shangazi Suzy ilikuwa ndiyo mara yangu ya mwisho kumuona akiwa hai."


"Wewe ulirudi Laini saa ngapi?"
"Kwenye saa tano."
"Ukaenda kwenye kota ya Bob?"
"Ndiyo."
"Alikuwepo?"
"Hapana, hakuwepo."
Ukafanya nini?"
"Nikaenda kulala."
"Hukuingiwa na wasiwasi?"
"La, sikuwa na wasi wasi. Kwanza ilikuwa bado mapema. Siku zingine tulirudi saa sita au saba. Hata saa nane za usiku. Na pilihalikuwa jambo geni kwa Bob kulala nje, wakati mwingine palepale kwa shangazi.


"Asubuhi je, ulikwenda kumtazama?"
"Ndiyo,"
"Ulipoona hayupo, bado tu hukuwa na wasiwasi?"
"Niliingiwa na wasiwasi kidogo, kuona angechelewa kuripoti kazini."
"Hukuwa na wasiwasi kwamba pengine kafikwa na jambo?"
"Hapana, wasi wasi huo sikuwa nao."

Bessy akaacha kuandika. Akashusha pumzi na kuuliza, "Huyo shangazi Suzy anakuhusu?"
Akajibu Butu haraka,"Hapana, kila mtu anamwita hivyo. Na nyumbani pake panaitwa kwa Shangazi Suzy."
"Yukoje?"
"Ni mama wa makamo, wa miaka kati ya thelathini na tano na arobain, na ana mwili."
"Umesema anauza nini na nini?"
"Ni bia na mapuya. Ni pombe ya kienyeji inayotengenezwa kwa ulezi na mahindi au mtama."
"Una hakika anauza vitu hivyo tu?"
"Sijakuelewa afande."
"Una hakika hauzi vitu vingine kama vile gongo,bangi, madawa ya kulevya?"
"Hapana afande, hauzi."
"Una hakika?" Bessy alisisitiza. "Ujue tutakwenda kuvamia na kumpekua, na baadaye kumhoji."
"Ah,nasikia anauza gongo siku moja moja."
"Na hivyo vingine? Unga? Bangi? Madawa ya kulevya?"


"Kama hivyo navyo anaviuza, basi anafanya hivyo kwa siri sana. Sina habari navyo."
Bessy akaandika haraka kisha akasema, "Sasa nataka ulijibu swali hili kwa makini sana. Kumbuka vizuri sana, kisha ndipo ujibu. Je, ulipomwaga Bob ulimwacha humo ndani akiwa peke yake au akiwa na watu wengine?"
Butu akataka kujibu,akasita.


"Kumbuka vizuri," Bessy alirudia. "Ni lazima utoe jibu sahihi. Jibu lako likitofautiana na huyo shangazi, na ikija kugundulika kuwa jibu lake ndilo sahihi, ndugu yangu hizo V zitakuwa si zako tena, kwani hutastahili kuitwa Koplo."
Butu akaanza kupumua kwa taabu, na vitone viwili au vitatu vya jasho vikimuota usoni. Hatimaye akasema kwa sauti ya kulazimisha, "Alikuwapo mtu mwingine,"
Ghafla Bessy akaketi mkunjuko,kama aliyeguswa sehemu nyeti.
"Ni nani mtu huyo?"
"Kikoti."Alinong'ona Butu.


Cc Joharia chiko18 gspace the-sniper skfull Master plan
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…