magnifico
JF-Expert Member
- Jan 14, 2013
- 11,075
- 24,634
MTEULE
UTANGULIZI
Mfalme Efroni alikuwa mtawala wa nchi ya Nahori. Mfalme huyu alimuoa binti wa mfugaji aliyeitwa Raheli na kujaaliwa kupata watoto kumi na wawili. Wote wa kike. Aliipenda sana familia yake. Mfalme huyu alikuwa mtawala mwenye huruma, hekima, busara na upendo. Uso wake ukitawaliwa na tabasamu wakati wote. Wakazi wote wa Nahori wakampenda.
Nahori ilipatikana ulimwengu wa mbali kabisa kutoka ule wa kibinadamu. Japo wakazi wake walifanana kila kitu na binadamu wa kawaida lakini wao walikuwa na kitu cha ziada. Kila mmoja alizaliwa akiwa na kipawa chake, wakiwa na uwezo na maarifa makubwa kupita wanadamu wa kawaida. Nahori ilizungukwa na milima mikubwa kwa midogo yenye ukijani wa kuvutia.
Na iliinasemekana pia ni katika ufalme huu kuna njia za siri za kuelekea ulimwengu mwingine. Njia hizi ziliitwa Njia za Mashimo ya giza. Hakuna aliyekuwa na uhakika wa jambo hili wala kuthibitisha habari hizi, sio vijana sio wazee. Nazo zikabaki kuwa hadithi za usiku wajukuu wakiwa wameuzunguka moto na babu akisimulia kwa utuo hadithi hizi kwa kadri atavyoona inavutia. Hakika ilipendeza.
Mashariki ya mbali mwa ufalme huu wa Nahori ilipatikana nchi ya Shekemu. Wamekuwa mahasibu wakubwa kwa miongo mingi sana. Na Inasadikika ni katika ufalme huu wa mbali kilipatikana kisima cha Shetani. Ukiyanywa maji ya kisima hiki utu hukutoka na nguvu za kishetani zinaishi ndani yako. Na hapo utajazwa tamaa ya kupata mali hata madaraka makubwa, huku ukitamani kubwaga damu pasi na sababu ya msingi. Nazo kama zilivyo habari za Njia za mashimo ya giza ndivyo hata habari hii ilivyokuwa. Hadithi njoo, utamu kolea.
Basi safari moja watu wa ufalme wa Shekemu huko inakosadikiwa kinapatikana kisima cha shetani walifanya uvamizi katika ardhi ya ufalme wa Nahori. Huu ulikuwa ni uvamizi wa pili kufanywa na watu wa Shekemu. Uvamizi wa kwanza waliufanya wakati Mfalme Efroni anarithi ufalme kutoka kwa baba yake. Na inasemekana lengo ilikuwa wapate kuteka kisima cha maji ya Maajabu.
Kisima hiki kilipatikana katika ufalme huu wa Nahori kikilindwa usiku na mchana na mashujaa waliofunzwa mafunzo ya kimapigano ya kivita ya hali ya juu kabisa pamoja na nguvu zao za asili. Hata sisimizi hakuthubutu kakatiza eneo lile. Maji haya hupewa mteule wa kiti cha ufalme tu, hii humpa uwezo na nguvu zaidi ya kiumbe chochote kile katika ulimwengu wao wote. Na ambaye sio mteule akijitia kiherehere kuthubutu kuyagusa maji yale huunguzwa vibaya mno hata akageuka majivu. Naam, kibali kilitoka kwa Wahenga wa Nahori.
Mara hii hapakuwa na budi kuupiga ufalme ule hata kwenye ardhi yao ya Shekemu. Mfalme Efroni aliongoza jeshi lake kwa kushirikiana na Jemedari wake mtiifu aliyeitwa Bethueli. Walishinda vita vile huku mashujaa wote wa ufalme ule wa Shekemu wakiuwawa sambamba na mfalme wao.
Na ndipo Jemedari Bethueli alijaribu kumshawishi mfalme kuhusu uwepo wa kisima cha shetani katika nchi ile. Lakini mfalme alikemea vikali kuhusu jambo lile na kumtaka asije akajaribu kuliongelea tena jambo hilo. Akatii amri.
Hapo Mfalme akaamuru tena hakuna kuua raia yoyote yule maana kisasi chao kilikuwa juu ya wale mashujaa na mfalme wao ambao wameuwawa tayari. Wakatii amri wote. Wakaianza safari kurudi Nahori.
********
Wiki kadhaa mbele Mfalme Efroni alipata taarifa kutoka kwa Jemedari Bethueli kuwa watu wa ufalme ule wa Shekemu wameuwawa wote kinyama. Hakuna kiumbe chenye uhai kimebaki hata miti yote imekauka kana kwamba eneo lile ni jangwa wakati ni masika. Mfalme akashtuka sana akasema, “kuna mmoja wa wale watu wa Shekemu katumia maji ya kisima cha shetani, hii ni hatari.”.
Jemedari alishtuka sana hata akauliza kwa kiwewe, “Sasa itakuaje? Vipi tukivamiwa?”, aliuliza mfululizo huku macho yakiwa yamemtoka pima. “Hatuwezi kuvamiwa, yoyote aliyokunywa maji yale anaijua nguvu yangu vyema kabisa, maji ya maajabu yapo ndani yangu.”, aliongea Mfalme Efroni kwa kujiamini kabisa hata ile hofu iliyokuwa machoni pa Jemedari Bethueli ikayeyuka huku akishusha pumzi za matumaini.
***************
Miaka mingi ikapita na mfalme Efroni umri ukazidi kumtupa mkono. Naye hakujiweza tena akawa mtu wa kulazwa kitandani siku nzima usiku hata mchana. Hata nguvu zake za maji ya maajabu hazikufua dafu mbele ya uzee ule.
Mkewe, Malkia Raheli alikuwa na ujauzito mkubwa kabisa lakini hakutaka mumewe ahudumiwe chochote kile na mtumishi. Aliyafanya yote kama mke pekee wa Mfalme Efroni huku akisaidiwa na mabinti zake kumi na wawili. Waliyafanya haya kwa mapenzi yote hata mfalme hakuwahi kujihisi upweke. Hakika walimpenda. Na katika siku zake za mwisho bado uso wake ulitawaliwa una tabasamu. Hakika tabasamu la mfalme, tabasamu la ufalme.
Jemedari Bethueli alitumika kufanya shughuli zote za kiuongozi wakati huu mfalme yupo kitandani. Alipokea maelekezo kutoka kwa mfalme na kuyatekeleza vyema kabisa hata pengo la mfalme lisiwepo tena mbele ya wakazi wa Nahori.
Mfalme Efroni alimuamini sana Bethueli, aliwachukua kuwalea tangu wakiwa watoto yeye na mdogo wake Rafaeli. Hii ni baada ya Baba na Mama yao kuuwawa baada ya uvamizi wa kwanza uliofanywa na jeshi la mashujaa wa Shekemu.
Jemedari Bethueli aliyatenda majukumu hayo kwa furaha na moyo wake wote akitambua fika yeye ni mrithi halali wa ufalme ule kwa kuwa mfalme hakubahatika kupata mtoto wa kiume. Kwa upande wa mdogo wake Rafaeli yeye hakutaka kujishughulisha na shughuli jeshi, alichagua kuwa tabibu, akirithi kazi ya marehemu mama yao. Mama yao alikuwa ni tabibu aliheshimika sana hata mfalme akampa hadhi ya tabibu mkuu wa Nahori akitibu mamia kwa maelfu ya watu. Kila homa ilisalimu amri mbele ya dawa zake. Mti gani wa dawa mama yule asiujue?.
Sheria za Nahori ziliamuru kama mfalme aliyekaa kwenye kiti cha ufalme atafariki na hakuna mtoto wa kiume wa kurithi kiti hicho basi ufalme ungehamia kwenye familia ya Jemedari mkuu wa wakati huo. Jemedari Bethueli alikuwa MTEULE ikitokea mfalme amefariki. Naye akazihesabu siku hizo kama mtoto mdogo anavyohesabu vidole vya mikono yake ili apate jawabu la hesabu ya kuongeza.
La, angalikkuwa makini, asingalipuuzia jambo lile linalokaribia kutokea. Ama kweli jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Ndiyo, walisema wahenga.
UTANGULIZI
Mfalme Efroni alikuwa mtawala wa nchi ya Nahori. Mfalme huyu alimuoa binti wa mfugaji aliyeitwa Raheli na kujaaliwa kupata watoto kumi na wawili. Wote wa kike. Aliipenda sana familia yake. Mfalme huyu alikuwa mtawala mwenye huruma, hekima, busara na upendo. Uso wake ukitawaliwa na tabasamu wakati wote. Wakazi wote wa Nahori wakampenda.
Nahori ilipatikana ulimwengu wa mbali kabisa kutoka ule wa kibinadamu. Japo wakazi wake walifanana kila kitu na binadamu wa kawaida lakini wao walikuwa na kitu cha ziada. Kila mmoja alizaliwa akiwa na kipawa chake, wakiwa na uwezo na maarifa makubwa kupita wanadamu wa kawaida. Nahori ilizungukwa na milima mikubwa kwa midogo yenye ukijani wa kuvutia.
Na iliinasemekana pia ni katika ufalme huu kuna njia za siri za kuelekea ulimwengu mwingine. Njia hizi ziliitwa Njia za Mashimo ya giza. Hakuna aliyekuwa na uhakika wa jambo hili wala kuthibitisha habari hizi, sio vijana sio wazee. Nazo zikabaki kuwa hadithi za usiku wajukuu wakiwa wameuzunguka moto na babu akisimulia kwa utuo hadithi hizi kwa kadri atavyoona inavutia. Hakika ilipendeza.
Mashariki ya mbali mwa ufalme huu wa Nahori ilipatikana nchi ya Shekemu. Wamekuwa mahasibu wakubwa kwa miongo mingi sana. Na Inasadikika ni katika ufalme huu wa mbali kilipatikana kisima cha Shetani. Ukiyanywa maji ya kisima hiki utu hukutoka na nguvu za kishetani zinaishi ndani yako. Na hapo utajazwa tamaa ya kupata mali hata madaraka makubwa, huku ukitamani kubwaga damu pasi na sababu ya msingi. Nazo kama zilivyo habari za Njia za mashimo ya giza ndivyo hata habari hii ilivyokuwa. Hadithi njoo, utamu kolea.
Basi safari moja watu wa ufalme wa Shekemu huko inakosadikiwa kinapatikana kisima cha shetani walifanya uvamizi katika ardhi ya ufalme wa Nahori. Huu ulikuwa ni uvamizi wa pili kufanywa na watu wa Shekemu. Uvamizi wa kwanza waliufanya wakati Mfalme Efroni anarithi ufalme kutoka kwa baba yake. Na inasemekana lengo ilikuwa wapate kuteka kisima cha maji ya Maajabu.
Kisima hiki kilipatikana katika ufalme huu wa Nahori kikilindwa usiku na mchana na mashujaa waliofunzwa mafunzo ya kimapigano ya kivita ya hali ya juu kabisa pamoja na nguvu zao za asili. Hata sisimizi hakuthubutu kakatiza eneo lile. Maji haya hupewa mteule wa kiti cha ufalme tu, hii humpa uwezo na nguvu zaidi ya kiumbe chochote kile katika ulimwengu wao wote. Na ambaye sio mteule akijitia kiherehere kuthubutu kuyagusa maji yale huunguzwa vibaya mno hata akageuka majivu. Naam, kibali kilitoka kwa Wahenga wa Nahori.
Mara hii hapakuwa na budi kuupiga ufalme ule hata kwenye ardhi yao ya Shekemu. Mfalme Efroni aliongoza jeshi lake kwa kushirikiana na Jemedari wake mtiifu aliyeitwa Bethueli. Walishinda vita vile huku mashujaa wote wa ufalme ule wa Shekemu wakiuwawa sambamba na mfalme wao.
Na ndipo Jemedari Bethueli alijaribu kumshawishi mfalme kuhusu uwepo wa kisima cha shetani katika nchi ile. Lakini mfalme alikemea vikali kuhusu jambo lile na kumtaka asije akajaribu kuliongelea tena jambo hilo. Akatii amri.
Hapo Mfalme akaamuru tena hakuna kuua raia yoyote yule maana kisasi chao kilikuwa juu ya wale mashujaa na mfalme wao ambao wameuwawa tayari. Wakatii amri wote. Wakaianza safari kurudi Nahori.
********
Wiki kadhaa mbele Mfalme Efroni alipata taarifa kutoka kwa Jemedari Bethueli kuwa watu wa ufalme ule wa Shekemu wameuwawa wote kinyama. Hakuna kiumbe chenye uhai kimebaki hata miti yote imekauka kana kwamba eneo lile ni jangwa wakati ni masika. Mfalme akashtuka sana akasema, “kuna mmoja wa wale watu wa Shekemu katumia maji ya kisima cha shetani, hii ni hatari.”.
Jemedari alishtuka sana hata akauliza kwa kiwewe, “Sasa itakuaje? Vipi tukivamiwa?”, aliuliza mfululizo huku macho yakiwa yamemtoka pima. “Hatuwezi kuvamiwa, yoyote aliyokunywa maji yale anaijua nguvu yangu vyema kabisa, maji ya maajabu yapo ndani yangu.”, aliongea Mfalme Efroni kwa kujiamini kabisa hata ile hofu iliyokuwa machoni pa Jemedari Bethueli ikayeyuka huku akishusha pumzi za matumaini.
***************
Miaka mingi ikapita na mfalme Efroni umri ukazidi kumtupa mkono. Naye hakujiweza tena akawa mtu wa kulazwa kitandani siku nzima usiku hata mchana. Hata nguvu zake za maji ya maajabu hazikufua dafu mbele ya uzee ule.
Mkewe, Malkia Raheli alikuwa na ujauzito mkubwa kabisa lakini hakutaka mumewe ahudumiwe chochote kile na mtumishi. Aliyafanya yote kama mke pekee wa Mfalme Efroni huku akisaidiwa na mabinti zake kumi na wawili. Waliyafanya haya kwa mapenzi yote hata mfalme hakuwahi kujihisi upweke. Hakika walimpenda. Na katika siku zake za mwisho bado uso wake ulitawaliwa una tabasamu. Hakika tabasamu la mfalme, tabasamu la ufalme.
Jemedari Bethueli alitumika kufanya shughuli zote za kiuongozi wakati huu mfalme yupo kitandani. Alipokea maelekezo kutoka kwa mfalme na kuyatekeleza vyema kabisa hata pengo la mfalme lisiwepo tena mbele ya wakazi wa Nahori.
Mfalme Efroni alimuamini sana Bethueli, aliwachukua kuwalea tangu wakiwa watoto yeye na mdogo wake Rafaeli. Hii ni baada ya Baba na Mama yao kuuwawa baada ya uvamizi wa kwanza uliofanywa na jeshi la mashujaa wa Shekemu.
Jemedari Bethueli aliyatenda majukumu hayo kwa furaha na moyo wake wote akitambua fika yeye ni mrithi halali wa ufalme ule kwa kuwa mfalme hakubahatika kupata mtoto wa kiume. Kwa upande wa mdogo wake Rafaeli yeye hakutaka kujishughulisha na shughuli jeshi, alichagua kuwa tabibu, akirithi kazi ya marehemu mama yao. Mama yao alikuwa ni tabibu aliheshimika sana hata mfalme akampa hadhi ya tabibu mkuu wa Nahori akitibu mamia kwa maelfu ya watu. Kila homa ilisalimu amri mbele ya dawa zake. Mti gani wa dawa mama yule asiujue?.
Sheria za Nahori ziliamuru kama mfalme aliyekaa kwenye kiti cha ufalme atafariki na hakuna mtoto wa kiume wa kurithi kiti hicho basi ufalme ungehamia kwenye familia ya Jemedari mkuu wa wakati huo. Jemedari Bethueli alikuwa MTEULE ikitokea mfalme amefariki. Naye akazihesabu siku hizo kama mtoto mdogo anavyohesabu vidole vya mikono yake ili apate jawabu la hesabu ya kuongeza.
La, angalikkuwa makini, asingalipuuzia jambo lile linalokaribia kutokea. Ama kweli jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Ndiyo, walisema wahenga.