Brodre
JF-Expert Member
- Aug 23, 2012
- 2,585
- 1,771
- Thread starter
-
- #381
165
Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)
Age ……………………………………………………18+
Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188
Website……………………………………………… www.storyzaeddytz.com
ILIPOISHIA
“Sasa kaka yule demu akija kuishi kwenye hili jumba nina imani lita mfaa sana. Jambo la kwanza nina mpiga mimba anizali mtoto kabla ya mke wangu ambaye kuna mambo nina hisi kwake”
“Mambo gani?”
“Nina hisia mbaya na mke wangu na nina hisi ana hitaji kutumia ndoa yetu kama daraja la kufanikishia mambo yake na familia yake”
“Mmmm mambo gani hayo kaka?”
“Bado sijayajua, ila kwa sasa nina jifanya ni mjinga kwake, ila nina mpeleleza taratibu endapo nikipata uhakika wa kile ninacho kihisi PUUUUUUU, nita muua”
Devi akastuka sana huku akimtazama Jery usoni mwake kwa maana endapo Jery ana sema jambo la kumuua mtu huwa ana dhamiria kufanya hivyo na sio mtu muoga wa kumuua mtu kwa maana ana roho mbaya na ngumu kumpita hata baba yake japo amepewa sura nzuri, yenye ucheshi na tabasamu la plastiki.
ENDELEA
“So una muua mke wako wa ndoa?”
Swali la Devi likamafanya Jery kumtazama kwa sekunde kadhaa.
“Una jua nikizungumza huwa nina maanisha. Sina ukoo naye wala undugu naye. Nilitengena naye kwa miaka kama kumi hivi, na mbaya alinidanganya kwamba ni bikra na majibu ya dokta yalivyo toka nika ambiwa ni kweli ana bikra. Hadi jana tulivyo fanya mapenzi nilimkuta ni bikra”
“So kama ume mkuta na usichana wake, ina kuwaje sasa una taka kumuua?”
“Ila ni bikra feki. Am the doctor tena professional doctor. Sikwenda Marekani kucheza nilisoma na nina ujua vizuir sana mwili wa binadamu, kuanzia ndani hadi nje. Nilimuonyesha fura ya nje ila ukweli, nina hitaji ni kufahamu ni kwa nini aliweka bikra ya bandia na ana mpango gani katika maisha yangu na baba yangu”
Devi alikabaki akiwa amejawa na mshangao pasipo kujua achangie nini kwenye hilo jambo kwa maana ni swala la kusghangaza sana.
“Sikia nahitaji nyumba ijazwe fenitures sasa hivi ni saa sita kanitafutie sofa za kisasa, vitanda vitatu vya kisasa. Naamini una jua nini napenda, tulipo kuwa tuna ishi Marekani ulikuwa una tambua jinsi gani ninavyo ipamba nyumba yangu”
“Ndio nina weza kusema ni mtu ambeye nina kujua vizuri kuliko mtu mwengine”
“Yaaa, ila jambo moja hili eneo litakuwa ni la siri sana. Mimi na wewe tu ndio tuta kuwa tuna jua. Credit card yangu hii kanitafutie hivyo vitu”
“Sawa mkuu”
Devi akaondoka na kumuacha Jery peke yake akiendelea kukagua mazingira ya jumba hilo. Hakika ni jumba lililo jengwa kisasa. Lina viwanja viwili vya michezo, kimoja ni kiwanja cha Tennes na kiwacha kingine ni cha Basketball. Sweeming pool lake ni kubwa kiasi cha kuweza kutosheleza watu hamsini wakaogelea kwa wakati mmoja. Kuna chumba maalumu cha mazoezi pamoja na chumba maalumu cha kutazamia filama kwa mfumo wa Sinema.
“Wooo huyu mzee alijenga”
Jery alishangaa huku ekihesabu viti vilivyomo katika chumba hicho. Akapata idadi ya viti ishirini, hivyo akiwa na marafiki zake kumi na tisa basi wana weza kutosha katika chumba hicho. Baada ya masaa mawili na nusu, Devi akafika nyumbani hapo huku akiwa ameongozana na gari mbili aina ya Scania zenye tela mbili zilizo jaa mizigo ya vitu vya ndani. Vitu hivyo vikashushwa na kuanza kupangwa ndani ya jumba hilo na wafanyakazi wa kampuni hiyo ambayo Devi alinunua viti hivyo vya ndani. Baada ya lisaa moja kila kitu kikawa kime wekwa sehemu yake. Hapakuwa na kitu kilicho kosekana hapo.
“So una kwenda kumuita yule demu hapa?”
Devi alizungumza huku akimkabidhi Jery kadi yake ya malipo(credit card).
“Hapana”
“Kwa nini?”
“Nahitaji kumpima akili yake kwanza ipo vipi si una jua sipendi kukurupuka. Nilimpatia ahadi ya kuonana naye ila sinto mpigia wala sinto muambia chochote. Turudi ikulu, na nikimaliza mazishi ya mama ndio nita kuja naye huku”
“Sawa na hizo document vipi una rudi nazo ikulu?”
“Ndio ila hato ziona”
“Sawa”
Jery na Devi wakarudi ikulu. Moja kwa moja Jery akaelekea ofisini kwa baba yake.
“Shikamoo hatuja onana baba leo?”
“Marahaba, yaa niliwahi kuamka mapema sana kuna majukumu nilipaswa kuya weka sawa”
“Okay kuna jambo moja nahitaji kukushirikisha kwa maana wewe ndio uliye baki kwenye maisha yangu.”
Jery alizungumza huku akiweka nyaraka hizo za ununuzi wa jumba hilo la kifahari juu ya meza ya baba yake.
“Ni nini hizo?”
“Nime nunua jumba moja la kifahari lipo Mbezi Louis”
Raisi Mtenzi akazichukua nyaraka hizo na kuanza kufunua moja baada ya nyingine. Katika nyakaraka hizo kuna picha za juma hilo.
“Waooo ni zuri. Ume kua sasa”
“Ni kweli baba, nami nahitaji kuw ana mji wangu kwa maana endapo muda wako ukiishia hapa ikulu, siwezi kwenda kuishi kwenye ile nyumba yako kule, ni lazima nikaishi kwangu”
“Yaa huo ndio uwanaume, kama umeweza kufikiria jambo kama hilo, ni kitu kivuzi sana”
“Ni kweli, ila sinto kwenda kuishi kwenye hii nyumba na mke wangu”
“Nini, una taka kwenda kuishi na nani!!?”
Raisi Mtenzi aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana usoni mwake.
“Nime jikuta nikianza kuwa na mashaka na mke wangu baba, toka nilivyo pata ile hasira, sina amani naye kabisa. Yaani nina fikiria kuwa na mwanamke mwengine kabisa”
“Ume changanyikiwa wewe?”
Raisi Mtenzi aliuliza kwa msisitizo kidogo.
“Sijachanganyikiwa baba ila nina zungumza kitu ambacho kipo moyoni mwangu. Kuna vitu nina endelea kumpeleleza mke wangu, endapo niki mkuta na huo ushahidi basi nita kuambia.”
“Vitu gani?”
“Kwa sasa siwezi kukuambia ila nitakapo kamilisha ushahidi wangu basi nita kueleza. Jambo la msingi nina kuomba sana usimuonyesha mkweo dalili yoyote ya kwamba nimesha anza kumtoa kwenye ufahamu wangu wa akili”
“Jery ngoja kwanza nikuambie kitu mwanangu”
Raisi Mtenzi alizungumza huku akinyanyuka na kukaa kwenye moja ya sofa na Jery akamfwata sehemu alipo kaa.
“Ndoa ina pande kuu mbili. Upande wa kwanza kabisa ni furaha ambayo ndani yake ina sababishwa na mambo mengi sana yatokanayo na amani munayo jaribu kuitengeneza. Upande wa pili ni majonzi, ambayo yana sababishwa na mchafuko wa amani ndani ya watu wawili. Mke wako kukukatalia kufanya tendo la ndoa haimaanishi kwamba yeye ni malaya, hapana ni mwana mke anaye kupenda sana. Aliweza kutazama hichi kipindi tunacho kipitia cha kumpumzisha mama yako, ndio maana liweza kumaptia heshima. Je ulivyo fanya naye jana hukumkuta na usichana wake”
Jery akatabasamu kidogo huku akimtazama baba yake.
“Nili mkuta nao”
Jery alijibu kwa kuadangana kwa maana ana tambua kwamba alimkuta mke wake na bikra ya bandia.
“Basi kama uli mkuta nao ni kwamba alijituza siku zote”
“Baba bikra ina weza kusababisha mwanaume au mwanamke aka mpenda mmoja wapo?”
“Ndio hususani ikitolewa katika ndoa.”
“Ila baba ni wanawake wangapi wana olewa pasipo kuwa na bikra na hao walio wavunja uta kuta nao wana familia zao”
“Ni hao, ila kwenye mfumo wangu wa maisha, niliweza kumtoa mama yako usichana wake, ndani ya ndoa yetu. Kitendo hicho kime tufanya tuishi kwa upande hadi alivyo tutoka duniani. Hivyo kwa changamoto ya juzi isije kukufanya uka uka muacha mtoto wa watu kisa ni hisia zako. Tume elewana”
“Ndio baba nime kuelewa, ila nina ufanya upelelezi wangu ukikamilika sawa nita kuambia. Ila nina kuomba sana uni tunzie hizo nyaraka, kwa maana nahitaji iwe siri juu ya ununuzi wa ile nyumba kule”
“Sawa nime kuelewa, ila hakikisha humu achi mtoto wa watu na ukifia wakati muafaka wa kumueleza juu ya hii nyumba ufanye hivyo”
“Sawa baba”
Jery alipo maliza kuzungumza na baba yake akanyanyuka na kutoka ndani hapo.
Julieth akafungua akaunti yake ya mtando wa Facebook. Akajifikiria kwa muda na kutafuta jina la Evans Shika. Wakatokea watu kadhaa, ila mtu aliye kuwa ana mtafuta, ni wa tatu kutoka kwenye hiyo listi ya watu alio waorodhesha hapo. Akaingia upande wa picha za Evans na kuanza kuzitazama moja baada ya nyingine.
‘Nakupenda sana Evans, natambua nime kuacha kwenye kipindi ambacho hukupaswa kuachwa na mimi n anime fanya hivi kwa ajili ya maisha ya familia yangu. Ila moyo wangu na hisia zangu zote zipo kwako. Nipo na mwanaume kimwili tu mpenzi wangu’
Julieth alijisemea kimoyo moyo huku machozi yakimlenga lenga. Kusema ukweli ni kwamba ana mpenda sana Evans kwa maana ndio mwanaume wake wa kwanza kumuingiza kwenye dira ya mapenzi. Isitoshendio mwanaume ambaye aliweza kumshirikisha vitu vyake vingi sana kuliko hata mume wake wa ndoa ambaye waliharakisha sana katika kuifunga ndoa hiyo.
‘Upo wapi mpenzi wangu. Tafadhali niambie upo wapi?’
Julieth aliendelea kulalama, gafla mlango wake ukafunguliwa, alipo iona sura ya Jery, moyo wake uka anza kumuenda kasi. Akafuta faili facebook kwenye laptop yake hiyo iliyopo mezani hapo.
“Hei baby”
Jery alizungumza huku uso wake ukiwa umejawa na furaha kubwa sana.
“Vipo honey”
Julieth alizungumza huku akijiweka vizuri uso wake.
“Safi”
Jery akambusu Julieth mdomoni mwake, kisha akaka kwenye kiti cha mbele ya meza hiyo ya Julieth na kaunza kuangaza angaza ndani ya ofisi hiyo.
“Ofisi ime kupendeza ehee?”
“Yaa nime ipenda kwa kweli mume wangu”
“Vipi macho yako mbona ni mekundu?”
“Mafua mpenzi wangu”
“Ooohoo pole sana mke wangu, yame kuanza muda gani?”
“Mchana huu”
“Pole sana mama watoto. Vipi lunch una hitaji kula nini?”
“Mmmm chochote”
“Basi kachukue kantini nahitaji tule hapa hapa ofisini kwako”
Julieth akajifiria kwa sekunde kadhaa kisha wakakubaliana na mume wake, aende kuchukua chakula hicho. Julieth akachukua simu yake, wakanyonyana denda kidogo na mume wake kisha akatoka ndani hapo na kuelekea kwenye kantine ya ikuku kuchukua chakula wanacho kipenda yeye na mume wake.
Jery kwa haraka akainyanyuka na kutoa kifaa kidogo alicho kabidhiwa na Devi ambacho kina uwezo wa kunasa mazungumzo yote yanayo weza kufanywa ndani ya ofisi hiyo. Akakinatisha kifaa hicho chini ya meza hiyo kubwa ya mke wake. Akia ana taka kurudi kwenye kiti chake, akaitazama laptop hiyo ya Julieth. Akafungua faili la Mozila. Moja kwa moja akaenda upande wa ‘History ili kuweza kujua ni kitu gani alicho kifanya kifungua magreth kwenye faili hilo. Moyo wake uka mstuka mara baada ya kuona maandishi yanayo someka EVANS SHIKA FACEBOOK na mbaya zaidi faili hilo lime funguliwa kama dakika sitazilizo pita. Jery akafilifungua faili hiyo na kukutana na picha ya Evans.
‘Ahaa huyu mshenzi bado ana mfikiria mjinga wake?’
Jery alijisemea kimoyo moyo huku hasira na chuki dhidi ya Julieth vikizidi kumtawala. Akalifunga faili hilo vizuri kisha akarudi kwenye kiti chake na kukaa. Hazikupita dakika tano, Julieth akarudi akiwa na vyakula hivyo.
“Karibu chakula mume wangu”
“Nashukuru, kuna jambo moja nahiyaji tuzungumze mke wangu”
Jery alizungumza huku akimtazama mke wake kwa tabasamu ambalo kwa haraka haraka ukimtazama una weza kuamini kwamba moyo wake ume jawa na furaha nyingi sana.
“Jambo gani baby”
“Nahitaji tutafute mtoto sasa”
Julieth akastuka kidogo huku akimtazama mume wake.
“Nahitaji tusimalize hata mwaka huu, ume umesha pata mimba”
“Jery mume wangu, ndoa yetu bado change una onaje kwanza uka nipa muda wa kuzoea maisha ya ndoa kisha ndio nika beba mimba”
“Kwani huwezi kuzoea maisha hayo pasipo kuwa na mtoto tumboni mwako?”
“Siwezi mume wangu”
Julieth alijibu kwa msisitizo pasipo kujua kwamba Jery kuuliza maswali ya namna hiyo ana maana yake ikiwa ni njia moja wapo ya kuendelea kumpeleleza mke wake ambaye hadi sasa hajui kama mume wake ana endelea kumpeleleza.
***
“Yule pale yule pale”
Samson alizungumza huku akimuonyesha Magreth mtoto huyo aitwaye Mathayo. Samson akachukua kamera na kuanza kumpiga picha mtoto hyo huku wakiwa katika gari maalumu walio pewa na raisi kwa ajili ya kazi hiyo na gari hilo halijasajiliwa kwa namba za ikulu. Mtoto huyo aliye toka kwenye geti la shule hiyo huku akiwa emevalia begi mgongoni mwake pamoja na sare za shule, akaingia kwenye gari moja ina ya Benz CLASS C.
“Ni nani yule?”
Magreth aliuliza huku akitazama gari hilo linavyo anza kuondoka getini mwa shule hiyo taratibu.
“Ile gari ina tumiwa na house boy”
“House boy ana tumia Benz?”
“Yaa ana kuja kumchukulia mtoto wa bosi, huwa halali hapa shule”
“Ahaa sawa”
Gari hili likapita pembeni yao kwa mwendo wa taratibu. Magreth akawasha gari hilo na kuligeuza gari hilo na kuanza kulifwatilia gari alilo panda Mathayo. Wakia katika barabara iliyo tulia na isiyo na nyumba zozote. Magreth akaongeza mwendo wa gari hilo na kulipita gari hiyo kisha akalizibia njia kwa mbele na kumsababisha kijana huyo wa kazi kufunga breki za gafla pasipo kujua ni nini kinacho endelea.
“Una fanya nini?”
Samson aliuliza huku mapigo ya moyo yakimuende kasi.
“Tulia”
Magreth alizungumza huku akichomoa bastola yaka. Akajifunga kitamba chake nusu uso, akavaa miwani nyeusi na kushuka kwenye gari. Akatembea kwa mendo wa haraka na kumuhimiza dereva kushuka kwenye gari. House boy huyo akashuka kwenye gari huku mikono yake akiwa emeinyoosha juu. Magreth akamuhimiza kulala chini na akatii amri. Magreth akafungua mlango wa nyuma na kumkuta kijana huyo akiwa ana tetemeka.
“Una…ju….a mam….amm…..a yan….g…u ni…..ni…..nani?”
Kijana huyo alijitahidi kujibaragazua mbele ya Magreth, ambaye hakutaka kumtazama sana, akampiga shingoni mwake kwa ubapa wa kiganja chake cha kulia na akazimia. Akamchomoa kwenye gari hili na kumuingiza kwenye gari walilo nalo na kuondoka eneo hilo huku wakiwa wamemuacha house boy huyo akiwa ameendelea kulala kifudi fudi.
“Ame kufa?”
“Ata kufaje ikiwa tuna haja naye”
“Sasa mbona ame tulia kimya?”
Samson aliuliza huku akiwa na wasiwasi.
“Samson kwani hujawahi kufanya hii kazi?”
“Hata siku moja, kwenye maisha yangu ninacho kijua ni computer tu”
“Basi tulizana, ume shirikiana na mimi katika hii kazi na uta fanya kile nitakacho kuambia. Sawa”
“Sawa”
Magreth akasimamisha gari kwenye nyumba yake ambayo ana itumia kwa ajili ya kazi zake za siri. Akafungua geti la nyumba hiyo iliyo jitenga pembezoni mwa bahari na eneo hilo halina mtu yoyote anaye ishi.
“Ingiza gari”
Samson akahamia kwenye siti ya pembeni na kuendesha gari hilo hadi eneo maegesho. Magreth akafunga geti huku akihakikisha hakuna anaye wafwatili.
“Hapa ni wapi?”
Samson aliuliza huku akishangaa mazingira ya majani mengi katika eneo hilo la nyumba hiyo.
“Hapa ni kwangu, mshushe huyo dogo”
Samson akambeba Mathayo na wakaingia ndani. Akamalaza mtoto huyo kwenye moja ya sofa lililo jaa vumi.
“Hii nyumbana haitumiki ehee?”
“Ndio. Samson fanya hivi nahitaji kumpigia simu yule mama.”
“Una hitaji kumuambia nini?”
“Nahitaji kumpa onyo la kuhakikisha kwamba nina mpima ana toa siri yote ya wapi alipo rafiki yangu”
“Nina wazo”
“Wazo gani?”
“Una onaje uka mrekodi video huyu kijana kisha ukaituma kwenye namba yake na utampatia maelezo ya kuhitaji kujua alipo Josephine”
“Wazo zuri”
Magreth kwa haraka akanyanyua kijana huyo na kumkalisha kwenye kiti, akamfunga miguu yake na mikono yake kwa nyuma. Akamziba mdomo kwa kumfunga kitambaa kisha akamfunga macho yake na kumwagika maji na kumfanya kijana huyo akazinduka. Akaanza kugugumia kwa woga, kwa maana hajui hapo alipo ni wapi. Samson akarekodi video ya sekunde thelathini, kisha akaindika maandishi mfupi yanayo someka, ili mwanao apone, tuna muhitaji Josephine la sivyo ata kufa ndani ya masaa kumi na mbili. Baada ya kufanya hivyo akaituma video hiyo kwenye namba ya mwana mama Sia Kamara na ubaya ni kwamba video hiyo hiyo hiyo iliingia pasipo kuonyesha namba ya Samson aliye ituma.
****************************************************************************************************************
**
ITAENDELEA
Haya sasa, Magreth ame fanikiwa kumteka mtoto wa SIA KAMARA, wame mtumia video hiyo je ata kuwa tayari kumtoa siri ya kwamba yeye ndio ame husika na kumteka Josephine ikiwa huo ndio mtego wao ambao hawana uhakika kama wata fanikiwa au wata feli? Usikose sehemu ya 166.
Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)
Age ……………………………………………………18+
Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188
Website……………………………………………… www.storyzaeddytz.com
ILIPOISHIA
“Sasa kaka yule demu akija kuishi kwenye hili jumba nina imani lita mfaa sana. Jambo la kwanza nina mpiga mimba anizali mtoto kabla ya mke wangu ambaye kuna mambo nina hisi kwake”
“Mambo gani?”
“Nina hisia mbaya na mke wangu na nina hisi ana hitaji kutumia ndoa yetu kama daraja la kufanikishia mambo yake na familia yake”
“Mmmm mambo gani hayo kaka?”
“Bado sijayajua, ila kwa sasa nina jifanya ni mjinga kwake, ila nina mpeleleza taratibu endapo nikipata uhakika wa kile ninacho kihisi PUUUUUUU, nita muua”
Devi akastuka sana huku akimtazama Jery usoni mwake kwa maana endapo Jery ana sema jambo la kumuua mtu huwa ana dhamiria kufanya hivyo na sio mtu muoga wa kumuua mtu kwa maana ana roho mbaya na ngumu kumpita hata baba yake japo amepewa sura nzuri, yenye ucheshi na tabasamu la plastiki.
ENDELEA
“So una muua mke wako wa ndoa?”
Swali la Devi likamafanya Jery kumtazama kwa sekunde kadhaa.
“Una jua nikizungumza huwa nina maanisha. Sina ukoo naye wala undugu naye. Nilitengena naye kwa miaka kama kumi hivi, na mbaya alinidanganya kwamba ni bikra na majibu ya dokta yalivyo toka nika ambiwa ni kweli ana bikra. Hadi jana tulivyo fanya mapenzi nilimkuta ni bikra”
“So kama ume mkuta na usichana wake, ina kuwaje sasa una taka kumuua?”
“Ila ni bikra feki. Am the doctor tena professional doctor. Sikwenda Marekani kucheza nilisoma na nina ujua vizuir sana mwili wa binadamu, kuanzia ndani hadi nje. Nilimuonyesha fura ya nje ila ukweli, nina hitaji ni kufahamu ni kwa nini aliweka bikra ya bandia na ana mpango gani katika maisha yangu na baba yangu”
Devi alikabaki akiwa amejawa na mshangao pasipo kujua achangie nini kwenye hilo jambo kwa maana ni swala la kusghangaza sana.
“Sikia nahitaji nyumba ijazwe fenitures sasa hivi ni saa sita kanitafutie sofa za kisasa, vitanda vitatu vya kisasa. Naamini una jua nini napenda, tulipo kuwa tuna ishi Marekani ulikuwa una tambua jinsi gani ninavyo ipamba nyumba yangu”
“Ndio nina weza kusema ni mtu ambeye nina kujua vizuri kuliko mtu mwengine”
“Yaaa, ila jambo moja hili eneo litakuwa ni la siri sana. Mimi na wewe tu ndio tuta kuwa tuna jua. Credit card yangu hii kanitafutie hivyo vitu”
“Sawa mkuu”
Devi akaondoka na kumuacha Jery peke yake akiendelea kukagua mazingira ya jumba hilo. Hakika ni jumba lililo jengwa kisasa. Lina viwanja viwili vya michezo, kimoja ni kiwanja cha Tennes na kiwacha kingine ni cha Basketball. Sweeming pool lake ni kubwa kiasi cha kuweza kutosheleza watu hamsini wakaogelea kwa wakati mmoja. Kuna chumba maalumu cha mazoezi pamoja na chumba maalumu cha kutazamia filama kwa mfumo wa Sinema.
“Wooo huyu mzee alijenga”
Jery alishangaa huku ekihesabu viti vilivyomo katika chumba hicho. Akapata idadi ya viti ishirini, hivyo akiwa na marafiki zake kumi na tisa basi wana weza kutosha katika chumba hicho. Baada ya masaa mawili na nusu, Devi akafika nyumbani hapo huku akiwa ameongozana na gari mbili aina ya Scania zenye tela mbili zilizo jaa mizigo ya vitu vya ndani. Vitu hivyo vikashushwa na kuanza kupangwa ndani ya jumba hilo na wafanyakazi wa kampuni hiyo ambayo Devi alinunua viti hivyo vya ndani. Baada ya lisaa moja kila kitu kikawa kime wekwa sehemu yake. Hapakuwa na kitu kilicho kosekana hapo.
“So una kwenda kumuita yule demu hapa?”
Devi alizungumza huku akimkabidhi Jery kadi yake ya malipo(credit card).
“Hapana”
“Kwa nini?”
“Nahitaji kumpima akili yake kwanza ipo vipi si una jua sipendi kukurupuka. Nilimpatia ahadi ya kuonana naye ila sinto mpigia wala sinto muambia chochote. Turudi ikulu, na nikimaliza mazishi ya mama ndio nita kuja naye huku”
“Sawa na hizo document vipi una rudi nazo ikulu?”
“Ndio ila hato ziona”
“Sawa”
Jery na Devi wakarudi ikulu. Moja kwa moja Jery akaelekea ofisini kwa baba yake.
“Shikamoo hatuja onana baba leo?”
“Marahaba, yaa niliwahi kuamka mapema sana kuna majukumu nilipaswa kuya weka sawa”
“Okay kuna jambo moja nahitaji kukushirikisha kwa maana wewe ndio uliye baki kwenye maisha yangu.”
Jery alizungumza huku akiweka nyaraka hizo za ununuzi wa jumba hilo la kifahari juu ya meza ya baba yake.
“Ni nini hizo?”
“Nime nunua jumba moja la kifahari lipo Mbezi Louis”
Raisi Mtenzi akazichukua nyaraka hizo na kuanza kufunua moja baada ya nyingine. Katika nyakaraka hizo kuna picha za juma hilo.
“Waooo ni zuri. Ume kua sasa”
“Ni kweli baba, nami nahitaji kuw ana mji wangu kwa maana endapo muda wako ukiishia hapa ikulu, siwezi kwenda kuishi kwenye ile nyumba yako kule, ni lazima nikaishi kwangu”
“Yaa huo ndio uwanaume, kama umeweza kufikiria jambo kama hilo, ni kitu kivuzi sana”
“Ni kweli, ila sinto kwenda kuishi kwenye hii nyumba na mke wangu”
“Nini, una taka kwenda kuishi na nani!!?”
Raisi Mtenzi aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana usoni mwake.
“Nime jikuta nikianza kuwa na mashaka na mke wangu baba, toka nilivyo pata ile hasira, sina amani naye kabisa. Yaani nina fikiria kuwa na mwanamke mwengine kabisa”
“Ume changanyikiwa wewe?”
Raisi Mtenzi aliuliza kwa msisitizo kidogo.
“Sijachanganyikiwa baba ila nina zungumza kitu ambacho kipo moyoni mwangu. Kuna vitu nina endelea kumpeleleza mke wangu, endapo niki mkuta na huo ushahidi basi nita kuambia.”
“Vitu gani?”
“Kwa sasa siwezi kukuambia ila nitakapo kamilisha ushahidi wangu basi nita kueleza. Jambo la msingi nina kuomba sana usimuonyesha mkweo dalili yoyote ya kwamba nimesha anza kumtoa kwenye ufahamu wangu wa akili”
“Jery ngoja kwanza nikuambie kitu mwanangu”
Raisi Mtenzi alizungumza huku akinyanyuka na kukaa kwenye moja ya sofa na Jery akamfwata sehemu alipo kaa.
“Ndoa ina pande kuu mbili. Upande wa kwanza kabisa ni furaha ambayo ndani yake ina sababishwa na mambo mengi sana yatokanayo na amani munayo jaribu kuitengeneza. Upande wa pili ni majonzi, ambayo yana sababishwa na mchafuko wa amani ndani ya watu wawili. Mke wako kukukatalia kufanya tendo la ndoa haimaanishi kwamba yeye ni malaya, hapana ni mwana mke anaye kupenda sana. Aliweza kutazama hichi kipindi tunacho kipitia cha kumpumzisha mama yako, ndio maana liweza kumaptia heshima. Je ulivyo fanya naye jana hukumkuta na usichana wake”
Jery akatabasamu kidogo huku akimtazama baba yake.
“Nili mkuta nao”
Jery alijibu kwa kuadangana kwa maana ana tambua kwamba alimkuta mke wake na bikra ya bandia.
“Basi kama uli mkuta nao ni kwamba alijituza siku zote”
“Baba bikra ina weza kusababisha mwanaume au mwanamke aka mpenda mmoja wapo?”
“Ndio hususani ikitolewa katika ndoa.”
“Ila baba ni wanawake wangapi wana olewa pasipo kuwa na bikra na hao walio wavunja uta kuta nao wana familia zao”
“Ni hao, ila kwenye mfumo wangu wa maisha, niliweza kumtoa mama yako usichana wake, ndani ya ndoa yetu. Kitendo hicho kime tufanya tuishi kwa upande hadi alivyo tutoka duniani. Hivyo kwa changamoto ya juzi isije kukufanya uka uka muacha mtoto wa watu kisa ni hisia zako. Tume elewana”
“Ndio baba nime kuelewa, ila nina ufanya upelelezi wangu ukikamilika sawa nita kuambia. Ila nina kuomba sana uni tunzie hizo nyaraka, kwa maana nahitaji iwe siri juu ya ununuzi wa ile nyumba kule”
“Sawa nime kuelewa, ila hakikisha humu achi mtoto wa watu na ukifia wakati muafaka wa kumueleza juu ya hii nyumba ufanye hivyo”
“Sawa baba”
Jery alipo maliza kuzungumza na baba yake akanyanyuka na kutoka ndani hapo.
Julieth akafungua akaunti yake ya mtando wa Facebook. Akajifikiria kwa muda na kutafuta jina la Evans Shika. Wakatokea watu kadhaa, ila mtu aliye kuwa ana mtafuta, ni wa tatu kutoka kwenye hiyo listi ya watu alio waorodhesha hapo. Akaingia upande wa picha za Evans na kuanza kuzitazama moja baada ya nyingine.
‘Nakupenda sana Evans, natambua nime kuacha kwenye kipindi ambacho hukupaswa kuachwa na mimi n anime fanya hivi kwa ajili ya maisha ya familia yangu. Ila moyo wangu na hisia zangu zote zipo kwako. Nipo na mwanaume kimwili tu mpenzi wangu’
Julieth alijisemea kimoyo moyo huku machozi yakimlenga lenga. Kusema ukweli ni kwamba ana mpenda sana Evans kwa maana ndio mwanaume wake wa kwanza kumuingiza kwenye dira ya mapenzi. Isitoshendio mwanaume ambaye aliweza kumshirikisha vitu vyake vingi sana kuliko hata mume wake wa ndoa ambaye waliharakisha sana katika kuifunga ndoa hiyo.
‘Upo wapi mpenzi wangu. Tafadhali niambie upo wapi?’
Julieth aliendelea kulalama, gafla mlango wake ukafunguliwa, alipo iona sura ya Jery, moyo wake uka anza kumuenda kasi. Akafuta faili facebook kwenye laptop yake hiyo iliyopo mezani hapo.
“Hei baby”
Jery alizungumza huku uso wake ukiwa umejawa na furaha kubwa sana.
“Vipo honey”
Julieth alizungumza huku akijiweka vizuri uso wake.
“Safi”
Jery akambusu Julieth mdomoni mwake, kisha akaka kwenye kiti cha mbele ya meza hiyo ya Julieth na kaunza kuangaza angaza ndani ya ofisi hiyo.
“Ofisi ime kupendeza ehee?”
“Yaa nime ipenda kwa kweli mume wangu”
“Vipi macho yako mbona ni mekundu?”
“Mafua mpenzi wangu”
“Ooohoo pole sana mke wangu, yame kuanza muda gani?”
“Mchana huu”
“Pole sana mama watoto. Vipi lunch una hitaji kula nini?”
“Mmmm chochote”
“Basi kachukue kantini nahitaji tule hapa hapa ofisini kwako”
Julieth akajifiria kwa sekunde kadhaa kisha wakakubaliana na mume wake, aende kuchukua chakula hicho. Julieth akachukua simu yake, wakanyonyana denda kidogo na mume wake kisha akatoka ndani hapo na kuelekea kwenye kantine ya ikuku kuchukua chakula wanacho kipenda yeye na mume wake.
Jery kwa haraka akainyanyuka na kutoa kifaa kidogo alicho kabidhiwa na Devi ambacho kina uwezo wa kunasa mazungumzo yote yanayo weza kufanywa ndani ya ofisi hiyo. Akakinatisha kifaa hicho chini ya meza hiyo kubwa ya mke wake. Akia ana taka kurudi kwenye kiti chake, akaitazama laptop hiyo ya Julieth. Akafungua faili la Mozila. Moja kwa moja akaenda upande wa ‘History ili kuweza kujua ni kitu gani alicho kifanya kifungua magreth kwenye faili hilo. Moyo wake uka mstuka mara baada ya kuona maandishi yanayo someka EVANS SHIKA FACEBOOK na mbaya zaidi faili hilo lime funguliwa kama dakika sitazilizo pita. Jery akafilifungua faili hiyo na kukutana na picha ya Evans.
‘Ahaa huyu mshenzi bado ana mfikiria mjinga wake?’
Jery alijisemea kimoyo moyo huku hasira na chuki dhidi ya Julieth vikizidi kumtawala. Akalifunga faili hilo vizuri kisha akarudi kwenye kiti chake na kukaa. Hazikupita dakika tano, Julieth akarudi akiwa na vyakula hivyo.
“Karibu chakula mume wangu”
“Nashukuru, kuna jambo moja nahiyaji tuzungumze mke wangu”
Jery alizungumza huku akimtazama mke wake kwa tabasamu ambalo kwa haraka haraka ukimtazama una weza kuamini kwamba moyo wake ume jawa na furaha nyingi sana.
“Jambo gani baby”
“Nahitaji tutafute mtoto sasa”
Julieth akastuka kidogo huku akimtazama mume wake.
“Nahitaji tusimalize hata mwaka huu, ume umesha pata mimba”
“Jery mume wangu, ndoa yetu bado change una onaje kwanza uka nipa muda wa kuzoea maisha ya ndoa kisha ndio nika beba mimba”
“Kwani huwezi kuzoea maisha hayo pasipo kuwa na mtoto tumboni mwako?”
“Siwezi mume wangu”
Julieth alijibu kwa msisitizo pasipo kujua kwamba Jery kuuliza maswali ya namna hiyo ana maana yake ikiwa ni njia moja wapo ya kuendelea kumpeleleza mke wake ambaye hadi sasa hajui kama mume wake ana endelea kumpeleleza.
***
“Yule pale yule pale”
Samson alizungumza huku akimuonyesha Magreth mtoto huyo aitwaye Mathayo. Samson akachukua kamera na kuanza kumpiga picha mtoto hyo huku wakiwa katika gari maalumu walio pewa na raisi kwa ajili ya kazi hiyo na gari hilo halijasajiliwa kwa namba za ikulu. Mtoto huyo aliye toka kwenye geti la shule hiyo huku akiwa emevalia begi mgongoni mwake pamoja na sare za shule, akaingia kwenye gari moja ina ya Benz CLASS C.
“Ni nani yule?”
Magreth aliuliza huku akitazama gari hilo linavyo anza kuondoka getini mwa shule hiyo taratibu.
“Ile gari ina tumiwa na house boy”
“House boy ana tumia Benz?”
“Yaa ana kuja kumchukulia mtoto wa bosi, huwa halali hapa shule”
“Ahaa sawa”
Gari hili likapita pembeni yao kwa mwendo wa taratibu. Magreth akawasha gari hilo na kuligeuza gari hilo na kuanza kulifwatilia gari alilo panda Mathayo. Wakia katika barabara iliyo tulia na isiyo na nyumba zozote. Magreth akaongeza mwendo wa gari hilo na kulipita gari hiyo kisha akalizibia njia kwa mbele na kumsababisha kijana huyo wa kazi kufunga breki za gafla pasipo kujua ni nini kinacho endelea.
“Una fanya nini?”
Samson aliuliza huku mapigo ya moyo yakimuende kasi.
“Tulia”
Magreth alizungumza huku akichomoa bastola yaka. Akajifunga kitamba chake nusu uso, akavaa miwani nyeusi na kushuka kwenye gari. Akatembea kwa mendo wa haraka na kumuhimiza dereva kushuka kwenye gari. House boy huyo akashuka kwenye gari huku mikono yake akiwa emeinyoosha juu. Magreth akamuhimiza kulala chini na akatii amri. Magreth akafungua mlango wa nyuma na kumkuta kijana huyo akiwa ana tetemeka.
“Una…ju….a mam….amm…..a yan….g…u ni…..ni…..nani?”
Kijana huyo alijitahidi kujibaragazua mbele ya Magreth, ambaye hakutaka kumtazama sana, akampiga shingoni mwake kwa ubapa wa kiganja chake cha kulia na akazimia. Akamchomoa kwenye gari hili na kumuingiza kwenye gari walilo nalo na kuondoka eneo hilo huku wakiwa wamemuacha house boy huyo akiwa ameendelea kulala kifudi fudi.
“Ame kufa?”
“Ata kufaje ikiwa tuna haja naye”
“Sasa mbona ame tulia kimya?”
Samson aliuliza huku akiwa na wasiwasi.
“Samson kwani hujawahi kufanya hii kazi?”
“Hata siku moja, kwenye maisha yangu ninacho kijua ni computer tu”
“Basi tulizana, ume shirikiana na mimi katika hii kazi na uta fanya kile nitakacho kuambia. Sawa”
“Sawa”
Magreth akasimamisha gari kwenye nyumba yake ambayo ana itumia kwa ajili ya kazi zake za siri. Akafungua geti la nyumba hiyo iliyo jitenga pembezoni mwa bahari na eneo hilo halina mtu yoyote anaye ishi.
“Ingiza gari”
Samson akahamia kwenye siti ya pembeni na kuendesha gari hilo hadi eneo maegesho. Magreth akafunga geti huku akihakikisha hakuna anaye wafwatili.
“Hapa ni wapi?”
Samson aliuliza huku akishangaa mazingira ya majani mengi katika eneo hilo la nyumba hiyo.
“Hapa ni kwangu, mshushe huyo dogo”
Samson akambeba Mathayo na wakaingia ndani. Akamalaza mtoto huyo kwenye moja ya sofa lililo jaa vumi.
“Hii nyumbana haitumiki ehee?”
“Ndio. Samson fanya hivi nahitaji kumpigia simu yule mama.”
“Una hitaji kumuambia nini?”
“Nahitaji kumpa onyo la kuhakikisha kwamba nina mpima ana toa siri yote ya wapi alipo rafiki yangu”
“Nina wazo”
“Wazo gani?”
“Una onaje uka mrekodi video huyu kijana kisha ukaituma kwenye namba yake na utampatia maelezo ya kuhitaji kujua alipo Josephine”
“Wazo zuri”
Magreth kwa haraka akanyanyua kijana huyo na kumkalisha kwenye kiti, akamfunga miguu yake na mikono yake kwa nyuma. Akamziba mdomo kwa kumfunga kitambaa kisha akamfunga macho yake na kumwagika maji na kumfanya kijana huyo akazinduka. Akaanza kugugumia kwa woga, kwa maana hajui hapo alipo ni wapi. Samson akarekodi video ya sekunde thelathini, kisha akaindika maandishi mfupi yanayo someka, ili mwanao apone, tuna muhitaji Josephine la sivyo ata kufa ndani ya masaa kumi na mbili. Baada ya kufanya hivyo akaituma video hiyo kwenye namba ya mwana mama Sia Kamara na ubaya ni kwamba video hiyo hiyo hiyo iliingia pasipo kuonyesha namba ya Samson aliye ituma.
****************************************************************************************************************
**
ITAENDELEA
Haya sasa, Magreth ame fanikiwa kumteka mtoto wa SIA KAMARA, wame mtumia video hiyo je ata kuwa tayari kumtoa siri ya kwamba yeye ndio ame husika na kumteka Josephine ikiwa huo ndio mtego wao ambao hawana uhakika kama wata fanikiwa au wata feli? Usikose sehemu ya 166.