X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,605
- 1,843
Mambo ya Ajabu Yaliyompata Allan Quatermain na Wenzake.
Leo nitadonoa kidogo Hadithi ya Allan Quatermain, Simulizi za Sir H. Rider Haggard kwenye moja ya simulizi zake zinazo elezea visa vya mwindaji Tembo hodari Bwana Allan Quatermain.
allan Quatermain (Makumazan or Macumazahn)... Na msaidizi wake Msolopagazi (Umslopogaas) na shoka lake Inkosi kazi (Inkosi-kaas)... Bwana Henry Curtis, na rafikie Siri Good, (Bwana Mzuri).
Kwenye riwaya hii ndipo pia lilipo patikana jina Gagula... Kibibi kilichokuwa kichawi (Kigagula).
Vitabu hivi ni miongoni mwa vitabu ambavyo vinaonyesha au kusimulia ujasiri na ushujaa wa hali ya juu sana... Soma pia riwaya ya Machimbo ya Mfalme Suleiman na nchi ya Wakukuana... Na vitabu vyake vingine ambavyo havikuwahi kutafsiriwa kwa kiswahili kama vile SHE, Ayesha, The Virgin of the Sun na Vingine vingi. Gonga HAPA kupata orodha ya vitabu vyake.
Wale waliowai kusoma Hadithi ya Allan Quatermain watamkumbuka sana Bwana Mslopagazi (Umslopogaas), na majigambo yake a.k.a Mikwara mizito aliyokuwa akiwatishia maadui zake...!
Basi tega sikio, nikumegee japo kidogo.