Robo ya vituo havina huduma nzuri ya simu, tume ya uchaguzi Kenya yasema

Robo ya vituo havina huduma nzuri ya simu, tume ya uchaguzi Kenya yasema

Donatila

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,772
Reaction score
22,598

_97207789_mediaitem97207788.jpg

Kituo cha taifa ya kutangaziwa matokeo ni ukumbi wa Bomas, jijini Nairobi.
Tume ya taifa ya uchaguzi nchini Kenya, IEBC, imetangaza kwamba robo ya vituo vyote vya kupigia kura nchini humo havina huduma nzuri ya mtandao wa simu wa 3G au ya 4G.

Tume hiyo imesema maafisa wasimamizi wa uchaguzi katika vituo hivyo watalazimika kusongea hadi maeneo yenye huduma nzuri ya mtandao ndipo waweze kupeperusha matokeo.

Uchaguzi mkuu nchini Kenya utafanyika Jumanne tarehe 8 Agosti.

Taarifa ya tume hiyo inasema kuna jumla ya vituo 11,155 ambavyo havina huduma nzuri ya mtandao ya 3G kati ya jumla ya vituo 40,883 kote nchini humo.

"Maafisa wasimamizi wa uchaguzi watatafuta pahala penye huduma nzuri ya mtandao au watumie simu za setilaiti kupeperusha matokeo," tume hiyo imeandika kwenye Twitter.

Vituo hivyo visivyo na huduma nzuri ya simu vinapatikana katika kaunti 45 kote nchini humo.

Ni kaunti za Nairobi na Mombasa pekee ambazo hazijakumbwa na tatizo hilo.

Takwimu kutoka kwa Mamlaka ya Mawasiliano Kenya zinaonesha maeneo mengi nje ya miji nchini humo hayana huduma ya 3G.

Ripoti kuhusu huduma ya simu na mtandao nchini Kenya ya mwaka jana inaonesha huduma ya 3G inapatikana katika asilimia 17 pekee ya ardhi ya Kenya. Hata hivyo, tofauti katika wingi wa watu maeneo mbalimbali, huduma hiyo huweza kufikia asilimia 78 ya wananchi nchini humo.

Ripoti hiyo iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Kenya inasema kufikia wakati huo, kaunti ya Isiolo ndiyo pekee ambayo haikuwa na eneo hata moja ambalo lina huduma ya 3G.

Katika maeneo mengi, huduma inayopatikana ni ya 2G.

Hayo yakijiri, afisa mkuu mtendaji wa IEBC Ezra Chiloba pia amefafanua kwamba karatasi za kupigia kura zitahitajika kuwa na muhuri wa tume hiyo kabla ya mpiga kura kupiga kura.

Amesema karatasi ambazo zitapatikana ndani ya masanduku ya kura zikiwa hazina muhuri hazitahesabiwa kama kura halali.

Marekebisho katika kanuni na sheria za uchaguzi yaliyofanywa mwaka huu yalikuwa yamefutilia mbali hitaji la kuwepo kwa muhuri katika karatasi za kura.

Hata hivyo, Bw Chiloba amesema tume hiyo imeamua kuwa karatasi za kura ni lazima zipigwe muhuri.


Chanzo: BBC
 

_97207789_mediaitem97207788.jpg

Kituo cha taifa ya kutangaziwa matokeo ni ukumbi wa Bomas, jijini Nairobi.
Tume ya taifa ya uchaguzi nchini Kenya, IEBC, imetangaza kwamba robo ya vituo vyote vya kupigia kura nchini humo havina huduma nzuri ya mtandao wa simu wa 3G au ya 4G.

Tume hiyo imesema maafisa wasimamizi wa uchaguzi katika vituo hivyo watalazimika kusongea hadi maeneo yenye huduma nzuri ya mtandao ndipo waweze kupeperusha matokeo.

Uchaguzi mkuu nchini Kenya utafanyika Jumanne tarehe 8 Agosti.

Taarifa ya tume hiyo inasema kuna jumla ya vituo 11,155 ambavyo havina huduma nzuri ya mtandao ya 3G kati ya jumla ya vituo 40,883 kote nchini humo.

"Maafisa wasimamizi wa uchaguzi watatafuta pahala penye huduma nzuri ya mtandao au watumie simu za setilaiti kupeperusha matokeo," tume hiyo imeandika kwenye Twitter.

Vituo hivyo visivyo na huduma nzuri ya simu vinapatikana katika kaunti 45 kote nchini humo.

Ni kaunti za Nairobi na Mombasa pekee ambazo hazijakumbwa na tatizo hilo.

Takwimu kutoka kwa Mamlaka ya Mawasiliano Kenya zinaonesha maeneo mengi nje ya miji nchini humo hayana huduma ya 3G.

Ripoti kuhusu huduma ya simu na mtandao nchini Kenya ya mwaka jana inaonesha huduma ya 3G inapatikana katika asilimia 17 pekee ya ardhi ya Kenya. Hata hivyo, tofauti katika wingi wa watu maeneo mbalimbali, huduma hiyo huweza kufikia asilimia 78 ya wananchi nchini humo.

Ripoti hiyo iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Kenya inasema kufikia wakati huo, kaunti ya Isiolo ndiyo pekee ambayo haikuwa na eneo hata moja ambalo lina huduma ya 3G.

Katika maeneo mengi, huduma inayopatikana ni ya 2G.

Hayo yakijiri, afisa mkuu mtendaji wa IEBC Ezra Chiloba pia amefafanua kwamba karatasi za kupigia kura zitahitajika kuwa na muhuri wa tume hiyo kabla ya mpiga kura kupiga kura.

Amesema karatasi ambazo zitapatikana ndani ya masanduku ya kura zikiwa hazina muhuri hazitahesabiwa kama kura halali.

Marekebisho katika kanuni na sheria za uchaguzi yaliyofanywa mwaka huu yalikuwa yamefutilia mbali hitaji la kuwepo kwa muhuri katika karatasi za kura.

Hata hivyo, Bw Chiloba amesema tume hiyo imeamua kuwa karatasi za kura ni lazima zipigwe muhuri.


Chanzo: BBC


JUSTIFICATION YA KUMUIBIA ODINGA
 
I think Odinga already knew this .....if it was an issue of importance he would have gone to court to rectify it.....IEBC is not The one with the problems this elections


Fake News
Intimidation of voters
Intimidation of opposition parties
General Lack of Decorum and Misuse of power is the real issue

IEBC will conduct a free and Fair Elections....just went to the countu tallying centre in Nakuru and IEBC is The most Secure Electoral body i have seen they have been bench marking everyone [emoji817]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom