Roho Mtakatifu na Mwamini

Roho Mtakatifu na Mwamini

ZVI ZAMIR

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2015
Posts
921
Reaction score
2,163
Shalom Shalom.

Habari ya jioni. Hongereni kwa Ibada na mapumziko ya wikendi. Leo naomba kwa uchache tushirikishane juu ya Roho Mtakatifu. Kama sehemu ya Utatu mtakatifu yaani Mungu Baba, Mwana na Roho mtakatifu.

Ikiwa wiki moja imetimia sasa tangu sherehe ya pentekoste. Kuna mambo ningependa tushirikishane kwa wale ambao teyari wameshamwamini Yesu Kristo(Wakati mwingine nitaongelea Roho mtakatifu na wale ambao bado hawaamini).

Kumekuwa na mafundisho mengi sana juu ya Roho mtakatifu ambayo kwa sehemu kubwa yameishia kwenye nadharia na sio vitendo halisi vya kuona udhiirishwaji wa kile ambacho kimekuwa kikifundishwa au kuhubiriwa. Kiuhalisia Roho Mtakatifu ndo kila kitu kwenye kanisa la leo katika kumuishi Yesu Kristo kwa uthabiti na uhakika pasipo yeye ukristo unakuwa mzigo mzito sana na mwishoe ni kujipata kwenye misingi ya sheria zaidi. Kama waamini tutajidhatiti kuwa chini ya maongozo yake (Mungu Roho mtakatifu) hakuna namna yale ambayo Bwana Yesu aliahidi kuwa tutayafanya zaidi yake yatashindikanika.

Yako Mengi ya kuyaongea juu ya Mungu Roho Mtakatifu juu ya utendaji wake, na mengi yanayo muhusi kwa namna ya kawaida ambayo kwa hakika kila ataweka nia kufanya majaribio ataona matokeo. Kumbuka ni kupitia nguvu na uweza wa Roho mtakatifu ndimo karama na vipawa vyote hufanya kazi na hata ile hali ya ushuhuda halisi wa mwamini kuthibitika.

Nafahamu hapa watu wengi tu wamekuwa encountered na Roho mtakatifu hivyo maswali yatakayo ulizwa nina hakika yajibiwa kwa kina .Karibuni kwa michango na Maswali..
 
Roho Mtakatifu ndio kipind chake sasa,kama kanisa tunatakiwa jua hlo kama mtoa maana ulivosema..bila yy Kwa sasa mamb hayaendi kabisa..

Ushuhuda,, before sijamjua nilikua nakula sana loss ktk biashara yangu ya mikopo na ilifika kipind nataka rudisha lesen na kufunga ofisi sabb watu wanakopa ndio ila ulipaji ni wa kusumbuana sana..

Baadae ya kufatilia maandiko nikapata neema ya kumjua uyu Roho Mtakatifu aiseeee mamb yamebadilika jumla,, before Mtu sijamwidhinishia mkopo naenda kumuuliza nimpe au nisimpe..ananipa majibu yupi apewe mkopo na yupi asipewe..since then sijawah sumbuliwa kurejeshewa na sijawah dhulumiwa tena..afu wateja kama wote..wapinzan wananifatilia wanazan nimepata mganga amenisaidia hawajui nachojua mm nipo nawazooom tuu na sitowaambia Siri!!!
 
Roho Mtakatifu ndio kipind chake sasa,kama kabisa tunatakiwa jua hlo kama mtoa maana ulivosema..bila yy Kwa sasa mamb hayaendi kabisa..

Ushuhuda,, before sijamjua nilikua nakula sana loss ktk biashara yangu ya mikopo na ilifika kipind nataka rudisha lesen na kufunga ofisi sabb watu wanakopa ndio ila ulipaji ni wa kusumbuana sana..

Baadae ya kufatilia maandiko nikapata neema ya kumjua uyu Roho Mtakatifu aiseeee mamb yamebadilika jumla,, before Mtu sijamwidhinishia mkopo naenda kumuuliza nimpe au nisimpe..ananipa majibu yupi apewe mkopo na yupi asipewe..since then sijawah sumbuliwa kurejeshewa na sijawah dhulumiwa tena..afu wateja kama wote..wapinzan wananifatilia wanazan nimepata mganga amenisaidia hawajui nachojua mm nipo nawazooom tuu na sitowaambia Siri!!!
Woah.Hallelujah. Hongera sana kwa mafunuo uliyopata juu ya Holy spirit huwezi baki vile vile hata kidogo kwenye maisha yako kiujumla pale unapo surrender kila jambo lako kwake..(Yohana 16:13)

Kwahakika iko siri kubwa sana katika kumfahamu kwa kina na hapa ndipo ilipo siri ya ukristo na hata namna njema ya hata kufanya ibada zetu mbeze za Mungu..
 
Unaweza kuwa huna ABC yoyote juu ya Roho mtakatifu au kuna maarifa yoyote ungependa kufahamu tafadhari naomba muulize nina uhakika yako mengi tutajifunza kutoka kwa wetu wengi walipata encounter na Holy Spirit.
 
Woah.Hallelujah. Hongera sana kwa mafunuo uliyopata juu ya Holy spirit huwezi baki vile vile hata kidogo kwenye maisha yako kiujumla pale unapo surrender kila jambo lako kwake..(Yohana 16:13)

Kwahakika iko siri kubwa sana katika kumfahamu kwa kina na hapa ndipo ilipo siri ya ukristo na hata namna njema ya hata kufanya ibada zetu mbeze za Mungu..
Aminaaaaa...
 
Nionyeshe Utatu Wa Mungu Kwenye Biblia,Mbona Kama Unatunga Vitu.
Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.

22 Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele;

Soma nilimo bold majibu yako yapo hapo.. Ukiafhana na Genesis1.. ambapo kwa kizungu ni Elohim ambayo ingekuwa imemaliza mchezo
 
Nionyeshe Utatu Wa Mungu Kwenye Biblia,Mbona Kama Unatunga Vitu.
Hiki watu wengi hawajakijua. Hakuna miungu mitatu kwenye Biblia ila kuna Mungu mmoja anayejifunza katika nafsi 3 kwa kulingana anataka fanya nini (Mission gani). Aliposema Baba inamaanisha Elohim alipojifunua kama (Muumbaji) aliposema Mwana ina maana Yeheshua (Mkombozi) au Neno katika uumbaji na alipojifunua kama Roho Mtakatifu(Hapa akimaanisha ukamilishaji wa misioni husika) kwenye uumbaji na ukombozi.
Mathayo 28:18-20 aliposema Mtawabatiza kwa Jina la Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu akimaanisha Mungu kujifunua katika nafsi tatu kwa kulingana na misioni. Hii ni sawa na Maji. Maji yakiwa kwenye Liquid state ni Maji. Yakiwa kwenye Gas state ni Mvuke na solid state ni Barafu ila yote ni Maji mkuu.
 
Nionyeshe Utatu Wa Mungu Kwenye Biblia,Mbona Kama Unatunga Vitu.
Kabla ya kukujibu naomba kukuuliza hivi huwa unapenda kujisomea biblia kibinafsi kwa lengo la kujifunza au kwa lengo la mashindano au hausomi mwenyewe umekalilishwa.?
 
1 Yohana 5:7-8
[7]Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
[8]Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.
Ndo Matatizo Ya dini Ya Paulo,

Matendo ya Mitume 7:55
Lakini yeye akijaa Roho Mtakatifu, akakaza macho yake, akitazama mbinguni, akauona utukufu wa Mungu, na Yesu akisimama upande wa mkono wa kuume wa Mungu.

Yesu(Neno) Kasimama Upande Wa Kuume(Kulia)Wa Mungu na Sio Mungu Kasimama upande Wa kulia Wa mungu.
Jaribu Kuelewa Maandiko Hapo Yesu(Neno)hausishwi Na Umungu,Amesimama Upande wa Kulia wa Yule Anayeitwa Mungu

Kutoka 20:3
Usiwe na miungu mingine ila mimi.

Marko 12:29
Yesu akamjibu, Ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

1 Timotheo 2:5
[Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;

Naomba Andiko linalosema yesu Ni Mungu au Yesu Mumwabudu Au Yesu anasema yy Ni Miongoni mwa Miungu
 
Hiki watu wengi hawajakijua. Hakuna miungu mitatu kwenye Biblia ila kuna Mungu mmoja anayejifunza katika nafsi 3 kwa kulingana anataka fanya nini (Mission gani). Aliposema Baba inamaanisha Elohim alipojifunua kama (Muumbaji) aliposema Mwana ina maana Yeheshua (Mkombozi) au Neno katika uumbaji na alipojifunua kama Roho Mtakatifu(Hapa akimaanisha ukamilishaji wa misioni husika) kwenye uumbaji na ukombozi.
Mathayo 28:18-20 aliposema Mtawabatiza kwa Jina la Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu akimaanisha Mungu kujifunua katika nafsi tatu kwa kulingana na misioni. Hii ni sawa na Maji. Maji yakiwa kwenye Liquid state ni Maji. Yakiwa kwenye Gas state ni Mvuke na solid state ni Barafu ila yote ni Maji mkuu.
Mungu Ni Mmoja Hawezi Exist Kama Kama Roho Mtakatifu pia kama Binadamu

Hosea 11:9
Sitatumia ukali wa hasira yangu, sitarudi kumwangamiza Efraimu; kwa maana mimi ni Mungu, si mwanadamu mimi; mimi ndiye aliye Mtakatifu katikati yenu; wala sitaingia ndani ya mji.

Mungu Anasema yeye Ni Mungu na si Mwanadamu,Mungu kautakaa Ubinadamu Baada Ya hapo aje Tena Kama binadamu wakati Kashajitapa Kwa watu Kama yeye Ni Mungu.Mungu Wa Aina gani Huyu mimi Mwenyewe Ningemdharau Mungu Wa Namna hii Kwa sababu Kajitofautisha na sisi Alafu baadae Kaja Kama sisi Tena.

Pia Kwenye Nafsi tatu Mmmh Ngoja tuone Maandiko.

Amosi 6:8
Bwana MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema BWANA, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na wote waliomo ndani yake.

Mungu ameapa Kwa nafsi yake Na Si Nafsi Zake, Hizo Tatu Unazosema.
Mungu ana Nafsi Moja Na Kaapa Kwa nafsi Yake Moja.
 
Kabla ya kukujibu naomba kukuuliza hivi huwa unapenda kujisomea biblia kibinafsi kwa lengo la kujifunza au kwa lengo la mashindano au hausomi mwenyewe umekalilishwa.?
Nijibu Swali Langu Kwanza Hilo suala La Mimi Kusoma Biblia kwa Mashindano au Kukalilishwa Ni Very Personal Najua Kwa Nini Nasoma Biblia.

Mimi Sijarithi tu Dini Kwa Wazazi Nimeisoma Nikapima Uzani Nikaiona Haki
 
Wengi wetu katika mapokeo ya dini na dhehebu tulifundishwa kuhusu Mungu wa nafsi tatu bila kumjua kiundani.

Lakini kiuhalisia aliyeumba ni mmoja tu na sio nafsi tatu.
 
Nijibu Swali Langu Kwanza Hilo suala La Mimi Kusoma Biblia kwa Mashindano au Kukalilishwa Ni Very Personal Najua Kwa Nini Nasoma Biblia.

Mimi Sijarithi tu Dini Kwa Wazazi Nimeisoma Nikapima Uzani Nikaiona Haki
Umeingia sehem ambayo huielewi ILa unajifanya kuielewa. Sasa maandiko yanasema mpumbavu aachwe na upumbavu wake
 
Wengi wetu katika mapokeo ya dini na dhehebu tulifundishwa kuhusu Mungu wa nafsi tatu bila kumjua kiundani.

Lakini kiuhalisia aliyeumba ni mmoja tu na sio nafsi tatu.
Mimi Mwenyewe Sielewi mara Mungu Yupo Kwenye Utatu Ana Nafsi Tatu,Mara Yesu Ndo Mungu Mwenyewe Mara Yesu Yeye Ni Mtoto wa Mungu Mama yake Mariam Yaani Taflan
 
Back
Top Bottom