Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 20,137
- 26,189
Siku zote katika maisha ili ufanikiwe inapaswa uwe na moyo mkunjufu ,moyo uliojaa shukurani bila kusahau kufanya kazi kwa bidii na kuwaheshimu wale wote wanaokusaidia ili uweze kutimiza ndoto zako.
Msanii Richard Mavoko ni miongoni mwa wasanii waliojaa chuki, husda na roho ya kwa nini.
Miaka michache iliyopita Mavoko alikuwa kwenye bifu zito na msanii grade one wa kimataifa Diamond Platnumz na kila kukicha alikuwa akimrushia vijembe na kumponda Diamond kwamba hajui kuimba ila anabebwa tu media .
Lakini siku zote Mungu si athumani baada ya miaka miwili kupita 2016 mwanzoni zilianza kama tetesi kwamba Mavoko ni msanii wa WCB bado tu kukamilisha mambo machache ili arasimishwe kwenye lebo hiyo, Mavoko kwa kuona aibu mwanzoni alipinga vikali jambo hilo lakini mwisho wa siku akaja kutia saini kweupe pee .
Ila Mavoko kwa kifupi aliamua kujiunga WCB ili tu aweze kujua mbinu anazotumia Mondi kutoboa kimataifa ili akishazipata hizo mbinu atoke katika hiyo lebo na aanzishe na yeye lebo yake.
Baada ya kuona lengo lake linakaribia kutimia akaamua kutafuta visababu visivyo vya msingi ili avunje mkataba na kutoa visingizio visivyo vya msingi ili mradi alipwe fidia ambayo ingemsaidia katika kuanzisha lebo yake ya Billionears Kids.
Lakini siku zote kwenye haki ,uongo hujitenga licha ya kubuni vijisababu na kwenda kushitaki Basata, Mavoko aliumbuka peupee na mwisho wa siku yeye ndiye aliyeonekana ana matatizo ndiyo maana hata siku zile baada ya kikao alionekana ni mtu mwenye stress nyingi na hasira za kijinga kwa sababu lengo lake lilibuma na akaishia kuumbuka peupe na mbaya zaidi amepoteza idadi kubwa ya mashabiki na ngoma zake wamezisusia ikiwemo ngoma mpya aliyoitoa hivi karibuni.
Mavoko hasira zake ameamua kuzituliza kwa kuwa unfollow watu wote ambao wameegemea zaidi upande wa Mondi ,mfano Ricardo Momo alikuwa ni swahiba sana wa Mavoko ila baada ya Mavoko kuleta chokochoko na Mondi Momo amekuwa akirusha utani wa hapa na pale ambao ulikuwa unamlenga Mavoko jambo ambalo lilimkera Mavoko na kuamua kum unfollow.
Mtu mwengine ambaye Mavoko amem unfollow ni Rommy Jones licha ya kuwa naye alikuwa swahiba wake mkubwa.
Wengine ni hawa , Rayvann,Salam Sk,Babu Tale, Mkubwa Fella na Diamond mwenyewe.
Msanii Richard Mavoko ni miongoni mwa wasanii waliojaa chuki, husda na roho ya kwa nini.
Miaka michache iliyopita Mavoko alikuwa kwenye bifu zito na msanii grade one wa kimataifa Diamond Platnumz na kila kukicha alikuwa akimrushia vijembe na kumponda Diamond kwamba hajui kuimba ila anabebwa tu media .
Lakini siku zote Mungu si athumani baada ya miaka miwili kupita 2016 mwanzoni zilianza kama tetesi kwamba Mavoko ni msanii wa WCB bado tu kukamilisha mambo machache ili arasimishwe kwenye lebo hiyo, Mavoko kwa kuona aibu mwanzoni alipinga vikali jambo hilo lakini mwisho wa siku akaja kutia saini kweupe pee .
Ila Mavoko kwa kifupi aliamua kujiunga WCB ili tu aweze kujua mbinu anazotumia Mondi kutoboa kimataifa ili akishazipata hizo mbinu atoke katika hiyo lebo na aanzishe na yeye lebo yake.
Baada ya kuona lengo lake linakaribia kutimia akaamua kutafuta visababu visivyo vya msingi ili avunje mkataba na kutoa visingizio visivyo vya msingi ili mradi alipwe fidia ambayo ingemsaidia katika kuanzisha lebo yake ya Billionears Kids.
Lakini siku zote kwenye haki ,uongo hujitenga licha ya kubuni vijisababu na kwenda kushitaki Basata, Mavoko aliumbuka peupee na mwisho wa siku yeye ndiye aliyeonekana ana matatizo ndiyo maana hata siku zile baada ya kikao alionekana ni mtu mwenye stress nyingi na hasira za kijinga kwa sababu lengo lake lilibuma na akaishia kuumbuka peupe na mbaya zaidi amepoteza idadi kubwa ya mashabiki na ngoma zake wamezisusia ikiwemo ngoma mpya aliyoitoa hivi karibuni.
Mavoko hasira zake ameamua kuzituliza kwa kuwa unfollow watu wote ambao wameegemea zaidi upande wa Mondi ,mfano Ricardo Momo alikuwa ni swahiba sana wa Mavoko ila baada ya Mavoko kuleta chokochoko na Mondi Momo amekuwa akirusha utani wa hapa na pale ambao ulikuwa unamlenga Mavoko jambo ambalo lilimkera Mavoko na kuamua kum unfollow.
Mtu mwengine ambaye Mavoko amem unfollow ni Rommy Jones licha ya kuwa naye alikuwa swahiba wake mkubwa.
Wengine ni hawa , Rayvann,Salam Sk,Babu Tale, Mkubwa Fella na Diamond mwenyewe.