RONALDINHO atangaza kutundika daluga, ninakushukuru kwa niaba ya Dunia

Kurzweil

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
6,621
Reaction score
8,411
Nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil na vilabu vya PSG, Barcelona na AC Milan, Ronaldo de Assis Moreira Maarufu kama Ronadinho Gaucho amestaafu soka.

Licha ya Ronadinho kutocheza soka la kiushindani lakini toka mwaka 2015 amekua akicheza michezo ya mabonanza

Kaka na wakala wa mchezaji huyo Roberto de Assis Moreira amethibitisha kuwa umefika mwisho kwa fundi huyo wa kibrazil kucheza soka.

Ronaldinho alianzia soka lake katika klabu ya Gremio ya nchini kwao kabla ya kujiunga na Paris St-Germain mwaka 2001 na baadae kujiunga na Barcelona alikong'ara sana.

Katika msimu wa 2010 -2011 alijiunga na Ac Milan ya Italia kabla ya kurudi kwao na kujiunga na Flamengo mwaka 2011. Kisha alichezea vilabu vya Atletico Mineiro, na Queretaro ya nchini Mexico na kurudi tena kwao Brazil katika klabu ya Fluminense.

Tujikumbushe kidogo aliyokuwa wanafanya uwanjani Ronaldinho

<<More>>
 
Arsenal tulikoma mbele yake, ila Chelsea walikoma zaidi.

Akiwa anatabasamu huku anakata viuno aliachia shuti lililotinga moja kwa moja wavuni. Hata kipa hakuruka kuonyesha ushahidi.

Hiyo ilikua Barcelona na Chelsea.

Zidane akavalishwa kanzu ya kwanza, akavuliwa, akapigwa tobo halafu jamaa akachanja mbuga.

Mwisho wa mchezo Zidane akawa anaongea na jamaa huku wanacheka.

Akiwa anadhihirisha ile free spirit aliyonayo, akaenda kwenye press conference huku anakunywa Pepsi wakati ana mkataba na Coca.

Mkataba na Coca ukasitishwa.

Jamaa ni moto
 
Hiyo game ya Chelsea unayosema Chelsea walikoma zaidi kama huna kumbukumbu vizuri ni kwamba Barcelona walijapwa 4-2 na kuondolewa kwenye michuano ya Uefa
 
weka Yale maneno ya @Gangchomba ili watu wamkumbuke huyu nabii na mtume wa kwanza na wa mwisho katika soka.
Deo gracious Gaucho
Overrated tu huyo lakini si lolote kwa messiah cuccittini
 
Reactions: PNC
Best attacking middfielder

Best flank player

Playmaker

Assistor

Ball dancer

Ball controller


Huyu ni fundi haswa hakika Legacy yake itazidi kukumbukwa vizazi na vizazi... Kina Ramos hawataweza kumsahau huyu jamaa kwa harrasy aliyokuwa akiwafanyia...

Gracies per tot Ronaldo de Assis Moreira...

La sonrisa de la futbal
 
Huo ni mtazamo wako,ila dunia nzima inatambua bado hajaonekana gold player like Morreira
Huyo hana chochote zaidi ya kujipiga vyenga ndyo maana record zake binafsi za barca na Brazil zimefunikwa na neymar Jr
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…