Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,621
- 8,411
Nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil na vilabu vya PSG, Barcelona na AC Milan, Ronaldo de Assis Moreira Maarufu kama Ronadinho Gaucho amestaafu soka.
Licha ya Ronadinho kutocheza soka la kiushindani lakini toka mwaka 2015 amekua akicheza michezo ya mabonanza
Kaka na wakala wa mchezaji huyo Roberto de Assis Moreira amethibitisha kuwa umefika mwisho kwa fundi huyo wa kibrazil kucheza soka.
Ronaldinho alianzia soka lake katika klabu ya Gremio ya nchini kwao kabla ya kujiunga na Paris St-Germain mwaka 2001 na baadae kujiunga na Barcelona alikong'ara sana.
Katika msimu wa 2010 -2011 alijiunga na Ac Milan ya Italia kabla ya kurudi kwao na kujiunga na Flamengo mwaka 2011. Kisha alichezea vilabu vya Atletico Mineiro, na Queretaro ya nchini Mexico na kurudi tena kwao Brazil katika klabu ya Fluminense.
Tujikumbushe kidogo aliyokuwa wanafanya uwanjani Ronaldinho
<<More>>
Licha ya Ronadinho kutocheza soka la kiushindani lakini toka mwaka 2015 amekua akicheza michezo ya mabonanza
Kaka na wakala wa mchezaji huyo Roberto de Assis Moreira amethibitisha kuwa umefika mwisho kwa fundi huyo wa kibrazil kucheza soka.
Ronaldinho alianzia soka lake katika klabu ya Gremio ya nchini kwao kabla ya kujiunga na Paris St-Germain mwaka 2001 na baadae kujiunga na Barcelona alikong'ara sana.
Katika msimu wa 2010 -2011 alijiunga na Ac Milan ya Italia kabla ya kurudi kwao na kujiunga na Flamengo mwaka 2011. Kisha alichezea vilabu vya Atletico Mineiro, na Queretaro ya nchini Mexico na kurudi tena kwao Brazil katika klabu ya Fluminense.
Tujikumbushe kidogo aliyokuwa wanafanya uwanjani Ronaldinho
<<More>>
Football Events7910:______Makala NO-83:______Jan 2018:_______{1/2}
GOODBYE RONALDINHO,MWANAMAGEUZI WA SOKA
Ni wiki ambayo wapenzi wengi wa soka duniani wamebaki midomo wazi na huzuni kubwa baada ya kusikia taarifa za mkali wa kweli Ronaldinho Gaucho,37,38 march, kutangaza kustaafu soka rasmi. Nikiwa kama mwana familia wa soka na miongoni mwa watu waliomshuhudia Ronaldinho katika ubora wake basi sina budi nikuletee uchambuzi kidogo wa gwiji huyu wa soka kutoka Brazil ambae alikuwa yuko zaidi katika kuburudisha watazamaji.Hakucheza mpira kwa kutafuta tuzo ya mchezaji bora wa dunia kama wakina Neymar kwa sasa.
Ukweli ni kwamba mwanasoka huyu bora wa dunia mwaka 2004 na 2005 hakucheza kwa muda mrefu akiwa katika kiwango bora kulinganisha na wenye mpira wao kwa sasa Cristiano Ronaldo na Lionel Messi. Pia hakutwaa mataji mengi kama walivyo hao watu wawili {Messi & Ronaldo} lakini kwa miaka yake ya 2003-2007 aliyokuwa katika kiwango chake bora ilitosha kabisa kuacha kumbukumbu kubwa kwa wapenzi wa soka waliomshuhudia. Kutokana na hili inasadikika kuwa Ronaldinho ndie mchezaji bora mwenye ufundi mwingi wa mpira kuliko yeyote yule.
Ronaldinho ni miongoni mwa wachezaji wachache kabisa walio fanikiwa kutwaa taji la kombe la dunia, Champions League pamoja na tuzo ya mchezaji bora wa dunia. Ni miongoni mwa wachezaji wachache pia ambao wanakubalika na kila shabiki wa soka. Mashabiki wa Real Madrid walidhihirisha hili pale Santiago Bernabeu (Nov 19,2005) ambapo pamoja na timu yao kufungwa 3-0 dhidi ya Barca ya Gaucho, mashabiki wa Madrid walisimama na kumpigia makofi akiwa anatoka uwanjani baada ya kupiga mpira mwingi na kuwa kaweka kambani goli 2 kati ya 3.Ni siku pia ambayo beki wa kulia wa Real ,Salgado, hatomsahau Gaucho.
Baada ya fainali za kombe la dunia mwaka 2002 kule Korea na Japan ambapo Brazil alikuwa bingwa kwa kumdungua Ujerumani 2-0, huo ndio ulikuwa mwanzo wa Ronaldinho kuanza kuonekana rasmi. Free kick yake dhidi ya golikipa wa England {David Seamen} mita 40 inabaki kuwa moja ya pigo huru la kukumbukwa katika fainali hizo. Baada ya mwaka mmoja wa fainali hizo kupita hapo ndipo Gaucho mapinduzi yake ya soka yalianza rasmi, aliachana na PSG na kujiunga na FC Barcelona mwaka 2003.
Usajili wake hasa wa kutoka PSG kuelekea FC Barcelona ndio ulikuwa chanzo cha hayo yote. Ukweli ni kwamba nyakati zile Barca hawakuwa na mpango wa kumsajili Ronaldinho, David Beckham ndie aliyekuwa haswa akitakiwa na Barca. Joan Laporta aliyekuwa akigombea nafasi ya juu kabisa ya uongozi{Rais}wa FC Barcelona alikwisha ahidi kuwa punde atakapo chaguliwa tu basi nyota wa Man U wakati huo David Beckham angetua Camp Nou. Lakini mwisho wa siku mambo hayakuwa hiyvo, Beckham alichepuka Real Madrid ambayo nayo ilikuwa inaanza sera zake za Galactico.
Kitendo cha David Beckham kujiunga na Madrid, Man U nao waliingia sokoni kumtafuta mbadala wake. Ronaldinho ndilo jina la kwanza lililopendekezwa na tayari kila kitu kilikuwa kama kiko tayari kuwa Gaucho anakwenda zake United lakini mwisho wa siku mambo yakageuka. Barca nao baada ya kuona tageti yao {Beckham} imeenda upande wa pili wa shilingi basi wakatafuta mpango B. Mpango wenyewe ulidondoka kwa Ronaldinho ambapo mpaka harakati hizo zote zinakuja ilikuwa ikiaminika kabisa kuwa Gaucho anakwenda Old Trafford.
Urafiki wa karibu wa makamu wa rais wa FC Barcelona bwana Sandro Rosell pamoja na Ronaldinho ambao ulikuja baada ya kaka yake Gaucho kuwa na urafiki na Rosell ulichangia sana uhamisho huo. Ni kipindi ambacho Barca walikuwa hawajatwaa taji la La Liga tangu mwaka 1999 chini ya mzee Louis Van Gaal. Hivyo viongozi hao wa Catalunya walipigana kuhakikisha kuwa wanapata jina kubwa ambalo linakuja kuhamasisha timu na kutengeza kipindi kipya cha kihistoria cha timu yao.
Kiasi cha €30m kilimg’oa Ronaldinho kutoka PSG na kujiunga na FC Barcelona rasmi mwaka 2003. Usajili huu ulikuwa ni bora sana kwa timu ya FC Barcelona pengine kuliko wa Beckham aliyekwenda upande wa pili wa shilingi ambae ndie alikuwa chaguo lao la kwanza. Man U walibaki midomo wazi baada ya wao nao kuona tageti yao {Ronaldinho} kutua Camp Nou, walibidi sasa watafute mbadala mwingine wa Beckham. Jina la kijana mdogo wa kireno Cristiano Ronaldo lilikuja na kufanya kijana huyo kuja OT na kukabidhiwa jezi namba 7.
Usajili wa Ronaldinho ulikuwa ni wa mbolea sana na hapo ndipo historia mpya ya soka Barca na duniani ikaanza kujengwa. Uwezo wake mkubwa wakuufanya mpira atakacho na kutii ndio alama kubwa ya Gaucho. Mwaka mmoja baada ya kuwa Camp Nou, Ronaldinho alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia. Ni wakati ambao tuzo hii ilikuwa ni uwezo kwanza wa mchezaji na sio kufunga magoli mengi hata kama mpira wako ni wa kawaida kukufanya utwae tuzo hiyo kubwa kabisa kwa mchezaji wa soka.
Uwezo mkubwa wa Ronaldinho uliifanya Barca kurudi ulaya hasa pia baada ya kuwa wamemuongeza Samuel Eto’o kutoka Madrid pamoja na Edgar Davids. Msimu wa 2005/06 utabaki kuwa msimu bora kabisa wa Ronaldinho kwani alikuwa mstari wa mbele kuiwezesha Barca kutwaa ubingwa wa ulaya kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1992,aliweza pia kuweka kambani goli 26 wakati huo ikiwa ndiyo rekodi yake bora kwa msimu.
Ujio wa Pep Guardiola katika kikosi cha FC Barcelona kama kocha mkuu msimu wa 2008/09 ulikuwa ndio chanzo cha Gaucho kuoneshwa njia ya kutokea. Pep aliweka hadharani majina matatu makubwa yakuondoka klabuni hapo, jina la Ronaldinho lilikuwa miongoni mwao mengine ni Deco pamoja na Samuel Eto’o. Kitendo hicho kiliwashangaza mashabiki wa soka kwani ni wakati ambao Ronaldinho alikuwa na miaka 28 tu.
Watu hawakumuelewa Guardiola nikiwa miongoni mwao,lakini Pep alikuwa akitengeneza kipindi kipya cha timu chini ya bwana mdogo wakati huo Lionel Messi. Ilibidi Ronaldinho aondoke Barca ili Messi aendelee kukua katika mazingira bora kwani tayari Ronaldinho alikuwa ni mtu wa starehe sana na kijana Messi alikuwa anamwona Gaucho kama ndie mwalimu wake wa soka. July 2008 Ronaldinho alitimkia zake AC Milan na kuweka kambani goli 10 katika mechi 32 ndani ya msimu wake wa kwanza San Siro.
Baada ya Gaucho kuwa tayari ameondoka Barca{2008} miaka minne mfululizo iliyofuata Lionel Messi alishinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia. Unaweza kuona ni namna gani mageuzi ya Dinho yalivyo fanya kazi. Ikumbukwe tu kuwa hata goli la kwanza la Messi pale Barca lilitengenezwa na Ronaldinho. “Remember the name, Lionel Messi at the age of seventeen score his first goal for Barcelona” yakiwa ni maneno ya mtangazi ya mechi hiyo baada ya Messi kufunga goli hilo.
Unaona kwa miaka hii 10 yani 2008,09,10,11,12,13,14,15,16 na 17 tuzo ya mchezaji bora wa dunia imekwenda kwa watu wawili tu yani Lionel Messi na Cristiano Ronaldo. Wote hao wawili uwepo wao hapo ulipo jina la Ronaldinho liko nyuma yao. Kama Ronaldinho kweli angeenda Man U basi ni vigumu kujua kama CR7 angetua OT nakufanya yale aliyofanya. Pia uwepo wa Ronaldinho katika klabu ya FC Barcelona unaweza kusema kuwa kwa namna moja ama nyingine kumemuweka Messi hapo alipo hii leo ikiwa ni pamoja na jitihada zao binafsi.
Hakika Ronaldinho ambae jina lake ni Ronaldo de Assis Moreira, aliitwa Ronaldinho ikimaanisha Ronaldo mdogo kwani kipindi anachipukia tayari kulikuwa na jina kubwa la Ronaldo De Lima, atabaki kama alama ya mchezaji mwenye uwezo mkubwa wa kuuchezea mpira na kuufanya atakavyo na ukatii. Tuzo ya mchezaji bora wa dunia ilimtafuta Gaucho na sio Gaucho aliitafuta tuzo hiyo kama wachezaji wa sasa.
View attachment 680580
.
. .
.
Makala kama hizi pia unaweza kuziona katika page ya facebook Football Events7910 .
Mawasiliano:+255 657 00 58 77 or +255 763 619 770 or +255 625 76 13 88
Email: ernestmazengo@gmail.com
Prepared By
Mr Mazengo {Football Pundit /Analyst}
Please share na washikaji…Thanks