Room 1 watu 8! Hapa MUST mmechemka

Room 1 watu 8! Hapa MUST mmechemka

Ford89

Senior Member
Joined
Jul 31, 2011
Posts
128
Reaction score
15
mbeya university of science and technology...nilikuwa nasoma join instruction yao hawa jamaa...nilipofika kwenye mambo ya hostel nikachoka....eti chumba watu 8. jaman ...,kama watoto wa secondary....kumbe ni watu wanaosomea shahada....
 
Me enyewe nmeshangaa sana baada ya kuisoma ile fom aisee !! Wa2 8 duuuuuuh
 
mbeya university of science and technology...nilikuwa nasoma join instruction yao hawa jamaa...nilipofika kwenye mambo ya hostel nikachoka....eti chumba watu 8. jaman ...,kama watoto wa secondary....kumbe ni watu wanaosomea shahada....

unashangaa nini!
 
unashangaa nini!

Unajua nin mkuu...wengi wetu huwa tunaongea mambo kutokana experience,mi nimetoka diploma dit...mwaka wa 3 tulikuwa tunakaa room watu 2 tu....na watu wa shahada wao kuanzia mwaka wa kwanza mpaka wa mwisho wanakaa room watu wa2 tu....kwa hyo nikiona sehemu kuna tofaut lazima nishangae...tena afadhali ingekuwa tofauti ndogo kama vile watu 3 au wa4..lkn kutoka wa2 mpaka 8...hapo nikishangaa si ajabu...
 
mbeya university of science and technology...nilikuwa nasoma join instruction yao hawa jamaa...nilipofika kwenye mambo ya hostel nikachoka....eti chumba watu 8. jaman ...,kama watoto wa secondary....kumbe ni watu wanaosomea shahada....
kapange kijana mbona vyumba vipo vingi huko nje
 
itakuwa inategemea na ukubwa wa chumba..isitoshe waenda kusoma si kulala.. urefu wa kamba
 
Kweli umezoea raha...ukitaka kujua adha,kero na maudhi ya accomodation waulize wanafunzi wa udsm
 
Nenda kasome dogo acha lawama na kusikitika ukubwa wa chumba unaujua??!!
Faclities unazijua zilizopo!!!
Fika ukaone kama kuna kitanda, meza na kabati basi weka kambi piga shule!!!!!

Mkizoeana humo mbona hata kunyoa mtaweza tu!!!
 
Hahaha wenzenu wanalilia chance za kusoma, nyie mnawaza room. Sasa wasomi mnalala saa ngapi? Mlalamike hamna maabara. Ukishamaliza na kishahada chako unatupwa tandahimba huko, sirikali yenu haina nyumba waligawana wazee zote. Utapangisha nyumba ya udongo na kumbembeleza baba mwenye nyumba asikutimue hadi miezi 4 iishe uanze kupata mshahara manake hazina wanaingiza mshahara taratiiibu
 
Kweli umezoea raha...ukitaka kujua adha,kero na maudhi ya accomodation waulize wanafunzi wa udsm

Niliwahi kukuta jamaa kalala kitandani kwangu mchana akaamka nikamuuliza babu vipi tena, akaniambia kaka we una kitanda mi kupumzika kupumzika mchana tu una maindi basi nipe kiwe changu mi nikubebe semista nzima!!! Alikuwa ni mshikaji wa mate wao wakisoma UCLAS

Nikacheka sana ila kwa masikitiko basi jamaa akiwa kachoka anakuja na shuka lake pale anapumzika usiku anasoma tu yule msela...baadae akaomba kuweka na begi chini ya kitanda tukawa tunaishi mtu tano rum moja block C pale ye akawa analala kitanda ambacho hakina mtu wote tukiwepo analala ma mshikaji wake!!!!

Leo imebaki stori kama hivi. Dogo akasome maisha ya chuo mapito tu!!!
 
Wewe dogo shukuru tu Mungu kwamba umepata chumba,kuna wenzio mlimani pale ukipata tu mtu anaekubali kukubeba unashangilia kama umeokota tanzanite,tena hapo cost za chumba zote unalipia wewe na jamaa siku akiwa anataka "kumenya chenza" na mpenzi wake basi unapigwa exile hiyo utajuwa mwenyewe utakapokwenda kukaa muda wote huo,tena exile bila taarifa.
Kuna dogo mmoja alikuwa anaishi STORE ya wafanya usafi pale hall 2 main campus.hii store ilikuwa next to toilets,ikifika usiku anachukua shuka analala juu ya meza(kulikuwa na kimeza kidogo ambacho watu wa usafi huweka vitu vyao vya usafi). Aliishi maisha haya kwa miaka miwili yaani 2nd year na 3rd year.now imebaki kuwa stori tu, dogo aliondoka na GPA ya 4 saaaaafi!
Nakushauri ukitaka starehe panga chumba nje ya chuo ila jiandae na kupigwa nondo..haha mambo ya mbeya hayo nondo nje nje
 
Niliwahi kukuta jamaa kalala kitandani kwangu mchana akaamka nikamuuliza babu vipi tena, akaniambia kaka we una kitanda mi kupumzika kupumzika mchana tu una maindi basi nipe kiwe changu mi nikubebe semista nzima!!! Alikuwa ni mshikaji wa mate wao wakisoma UCLAS

Nikacheka sana ila kwa masikitiko basi jamaa akiwa kachoka anakuja na shuka lake pale anapumzika usiku anasoma tu yule msela...baadae akaomba kuweka na begi chini ya kitanda tukawa tunaishi mtu tano rum moja block C pale ye akawa analala kitanda ambacho hakina mtu wote tukiwepo analala ma mshikaji wake!!!!

Leo imebaki stori kama hivi. Dogo akasome maisha ya chuo mapito tu!!!

Mlikuwa mnakaa watano? Aisee mwaka gani huo? Mi wakati nasoma kukaa nane ilikuwa ni kawaida sana....ndo chumba kinakuwa kimekamilika
 
Mlikuwa mnakaa watano? Aisee mwaka gani huo? Mi wakati nasoma kukaa nane ilikuwa ni kawaida sana....ndo chumba kinakuwa kimekamilika

Aaaanh nyie watu wa crisis eeenh 2004 -2006 ndio mlikoma saaaana!!!!
 
Back
Top Bottom