Rostam aanza kutikiswa

Hivi kuna haja ya kuendelea kumjadili huyu...........status yake wote tunaifahamu.............hashikiki kwa sasa....kumtoa huyu si rahisi lakini siku zake zinahesabika.......miaka mitano ijayo ikiisha chochote kinaweza kutokea huyu RA mwisho wake naona utakuwa mbaya sana kwa jinsi anavyoichezea nchi hii.
 
kila mtu ana haki ya kugombea iwapo tu atakuwa ametimiza masharti yaliyowekwa
 
Nimethibitishiwa na mtu wa umoja wa vijana kwamba yuko asilimia 100 kwamba Rostam hatagombea ubunge mwaka kesho.

Kama hii habari sio ukweli basi niumbueni mwakani. Kinachofanyika sasa ni RA kutafuta mtu wa kumrithi; ndio siasa za TZ hizo, wenye nchi kurithiana kazi utafikiri nchi yao wenyewe.

Tunapoteza muda bure kujadili hii thread maana Rostam sio mgombea mwakani.
 

BADO NAENDELEA KUSEMA CCM INAOKOLEKA KWA SASA huu ndio mwanzo na bado cha msingi ni fikra na mapinduzi ndani ya mioyo yetu.

Rostam ni binadamu kama wengine na anaweza kushindwa vile vile sababu yeye si Mungu.

Hongera Mtambalike kwa kuimarisha mapambano dhidi ya vita hii tuliyopo.
 
Haya ni makati ya siasa Mbovu za karne ya ujima..!! Baada ya Miaka 5 kuanzia sasa ,Hakuna mtanzania atakaye ruhusu ujinga wa serikali ya JK.
 

Tunakubaliana nawe kiasi fulani lakini ukweli wana Igunga kwa asilimia 100 wanafahamu kuwa Peter Kafumu ndie chaguo la RA ili baadaye amtumie kufanikisha malengo yake na RA atatumia nguvu yake yote kumnadi jamaa yule
 
Nadhani swala hapa sio RA kutikiswa bali ni wakati muafaka wa kufanya mabadiliko ili kupata mawazo mapya, kupata fikra mpya na kupata maono mapya yenye manufaa na faida kwa watanzania katika majimbo mengi ya ubunge. Hii nchi (pamoja na jimbo la Igunga) ni mali ya watanzania woote na kila mwenye sifa za kuchaguliwa anahaki ya kuchaguliwa. HAKUNA JIMBO LA UCHAGUZI LILILO MALI YA MTU FULANI.
 
ingekua igunga ni pemba hapo sawa maana wapemba uwape nini lakini ccm no bora wampe mbwa kura kuliko ccm bado watz tuna tatizo njaa zetu hatuiwezi akipewa fulana moja tu anasahau yote yatakayo pata ya miaka 5 ni viziwi vipofu mabubu
 
Rostam atashinda tu hilo halina ubishani ,kwanza huyu jamaa anajuwa kula na vipofu pili rangi yake ni kivutio kwa vipofu hao.amekuwa akiwajengea mambo mazuri na wengi wanafurahishwa na kazi yake Mungu amsaidie ashinde kipindi kijacho ili kuendeleza majukumu ya chama aliyopewa.
 
MMhm..
Labda wale wenye tamaa ya fedha... na hili ni la mtu binafsi zaidi na sio la kichama?
Maalim Seif kung'ang'ania uprez kwa miaka 15 sasa ana maana gani?

Hivi kibunago umemuona mtu mmoja tu ? hebu angalia hivi vizee katika bunge kuna wakati asatahafiru kusema ni kinya kuna wakati unahisi unataka kutapika ukiwangalia bado wamo tu mauti yatawakuta wakiwa ndani ya jumba la kuhubiri ubaya.lakini hawataki kupumzika na kucheza na vijukuu au kutupia hiyo pencheni yao mtu anamika 70 -85 anasubiri nini palipobki ni mauti tu hapo.
 


Duh !! babylon

Ndio umetuambia nini hapo labda uandike tena lol

Hivi kweli wewe ni mtanzania na unaeishi bongo? Na hata kama huishi bongo basi tueleze unajua anayo yafanya mshikaji wako RA ? ama unaishi planet nyingine. kama huishi bongo basi waonee huruma ndugu zako waliopo bongo maana ukiambiwa mikataba ambayo uncle wako ameifanya ungelia kuanzia leo mpaka x-mass

haya hebu tumwagie Data za ushabiki wako kwa fisadi
 

Huyu jamaa anatekeleza magizo ya wakubwa wa nchi sasa kumuhukumu peke yake ni kumuonea.kama ilivyo mkapa kuwa awachiwe na kupumzika kama alivyosema Rais Jk basi na jamaa achiwe afanye majukumu yake kwa wananchi waliomchaguwa ambao wengi wao wanamfurahia kwa msada wake anawapa.
 

Huyu ni njaa tu, angekuwa anataka kumuondoa rostam agombee kupitia CHADEMA
 

Mtambalike ninayemfahamu hawezi kuhongwa ni mtu mwenye msimamo.
 
Huyu Mtambalike ni mmoja kati ya wale watanzania wasanii na ambaye ametayarishwa na Rostam huyo huyo kuanza kupiga kelele. Wewe mtu mwenye nia thabiti na unayejua uwezo wako katika siasa na unataka kuingia kwenye siasa huwezi kuanza kwenda kuomba ruhusa kwa kiongozi aliyepo madarakani ili ugombee. Anasema alimwambia mwaka 2000 akasema amsubiri mpaka 2005 na yeye akakubali. Alikubali kivipi?? alipewa nini ili akubali?? alikuwa amejitayarisha kwa mwaka 2000? je 2005? je na mwaka kesho akiambiwa asubiri 2015?? huyu ni msanii wa ajabu na tumepoteza muda wetu kumjadili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…