Rostam atingisha mkutano wa hadhara igunga

RA ajibu hoja kuhusu KAGODA na RICHMOND, asitumie hela zetu alizoiba kutugawa,wale wananchi wa Igunga maskini anawalaghai kwa hizo hela ,aitishe maandamano Dar ,au aende mwembe yanga kama alivyofanya Dr Slaa ndo nitajua kweli ye mwanaume,Anamuonya Mengi yeye kama nani?Hao wabunge waliozunguka mkoa wa Tabora na Mengi ni akina nani,ninachojua Mengi hajazunguka Tabora,alialikwa na Mbunge wa viti maaluma mh Aziza kwenye hafla ya NGO hapo Tabora mjini,je huko ndo kuzunguka?
Je Mengi angekuwa anaonekana katika shughuli kama hizo na wabunge wa upinzani huyo RA angesema nini?asitake kuwawanyamazisha wapiganaji ,Mengi kaza buti,Vita bado ni ngumu lakini nawahakikishia wapiganaji wote kuwa bado kitambo kidogo tutashinda vita hii.Nani angejua kuwa leo hii makamba haruhusiwi kuwa front katika majukwaa ya kampeni ya C.C.M? walimwondoa mbeya na sasa wamemuondoa busanda .wanaingiza wapiganaji wa Ufisadi mmoja baada ya mwingine,walianda na kuwaita kina mwakyembe mbeya na leo tunamuona Kilango huko busanda.
 
aidha alitoa tahadhari kwa wabunge wa mkoa wa tabora wanaopenda kuongozana na Mengi kwenye ziara zake za mkoa wa tabora na kuwa kamwe hawatvumiliwa tena jambo ambalo lilishangiliwa kwa nguvu kubwa
Pamoja na kutuwakilishia vizuri taarifa ya paymaster wako,,,,, yeye kama mbunge anawapiga mkwara mzito wabunge wa Tabora kwa lengo gani? Anamaanisha nini? Yuko juu yao? Yeye ni zaidi ya mbunge? Hebu mwulize vizuri mkuu kisha tupashe.
 
No! si kwamba RA anawazuia wabunge wa mkoa wa Tabora kutembea na Mengi bali kuna wabunge ambao wanadai kuwa wanapambana na ufisadi wakimuweka RA kwenye list ambao pia ni wapambe wa karibu wa Mengi katika mkutano huo wa jana yaani Mh Aziza ambaye kwenye mikutano mingi ya Mengi hachezi mbali lakini cha ajabu hata kwenye mkutano wa RA jana Mh Aziza aliungana na wananchi wote kumpokea RA na mara kadhaa Mh Aziza alisikika akimwambia RA Sema Babaaaaa! sasa sijui Mengi akiona picha hizo atamuelewa vipi Mpambe wake Aziza. kwa wale wanaodhani ni ishu ya kutengenezwa nilikuwa pale kati kati ya Mkutano isipokuwa sikutegemea kama ishu hii ingekuwa mapema hivi JF naanza kumuogopa na kumheshimu taratibu Fisadi Mtoto i guess ningekuwa wa kwanza kutundika post hii JF kwa kuwa naishi hatua chache kutoka kwa Mh RA! Fisadi Mtoto anayebisha hili mwambie aniulize zaidi ni kwamba waliokuwepo si watu wa jimbo la Mh RA tu hata wenyeviti wa CCM wa mikoa mitatu walikuwepo, mawaziri watatu, viongozi wote wa CCM wa mkoa , viongozi wote wa vijana wa Mkoa
 
Last edited:
A bit confused...
"Rostam atingisha mkutano wa hadhara igunga" halafu mkutano wenyewe umefanyika Nzega??? Hii haijatulia...
 
Huo ndo ukweli halisi japo mpambe wa Mengi Mh aziza wa Tabora alikuwepo na alikuwa akishangilia mkutano huo bila kujali kuwa atagombana na wenzie wanaopiga vita ufisadi
 
Ndanda usidanganye watu alikwambia Makamba kaondolewa Busanda nani? una ushahidi gani, makamba yupo huko Busanda na kwa taarifa yako ana maandalizi pia ya jimbo la Biharamulo kama una mtu yeyote wa chato muulize akwambie makamba anafanya nini kwenye majimbo ya Busanda na Biharamuro
 
Kwa wanaojua ramani ya Tanzania Nzega haiko jimboni Igunga. Nzega ni wilaya inayojitegemea na wanaoujua Mkoa wa Tabora uwanja wa kumbukumbu ya Samora upo wilayani/jimboni Nzega. Confusion dhahiri kama hii leaves a lot to be desired!! Niko mbioni kupata ukweli wa hayo mengine kutoka huko unyamwezini.
 
Ni upuuzi kumshangilia fisadi,wananchi mbumbumbu ndio waliwao,leo Tabora -nzeaga road halafu mnapoteza mda kushangilia wabunge wasionahuruma kwa wapiga kura,loo,inasikitisha.
 
- Waache wafu wazikane wenyewe huko Igunga na kiongozi wao, maana kama hizi habari ni za kweli basi sikio la kufa hilo!

William.

Alisema Kapt. Komba:
“Wabunge mmefanya makosa makubwa sana kumlazimisha mpendwa wetu Lowasa ajiuzulu eti kisa kashfa ya Richmond! 2010 wapigakura hawatatuuliza hiyo Richmond wala umeme bali tumetekeleza ilani ya CCM kwa kiasi gani?”
Anaonekana kuwa sahihi katika baadhi ya majimbo ya nchi yetu na ukimuuliza leo atakupa mifano halisi. Atakukumbusha mapokezi ya Lowasa jimboni baada ya kujiuzuru, atakupa ukatafakari Chenge alipokwenda Shinyanga na kasha uatakufungia ukurasa na hii iliyoingia hivi punde ya RA toka Ngega. Si ajabu ziko nyingine kali kuliko zaja.
 
PM,

Wajinga ndio waliwao, hata wewe ukiweza si unachukua huku na huku na kisha kuendelea na msimamo wako.

Watu sio wajinga kiasi hicho, mtu hajawahi kusaidia hata siku moja sehemu husika, ghafla kuna uchaguzi karibuni, wanaona baiskeli na pikipiki zinaanza kumwagwa.

Hata mimi ningejiuliza kulikoni?

Muhimu ni wananchi wachukue hiyo misaada whether ni ya RA au Mengi na waendelee na mambo yao na siku ikifika wampatie kura mtu aanayewafaa zaidi.
 


Kwa nini usifikiri kuwa RA ndiye anayeshindwa ujanja na Mengi na kuwa huyo Aziza yupo na RA kama shushushu wa Mengi..??
 
Pamoja na kutuwakilishia vizuri taarifa ya paymaster wako,,,,, yeye kama mbunge anawapiga mkwara mzito wabunge wa Tabora kwa lengo gani? Anamaanisha nini? Yuko juu yao? Yeye ni zaidi ya mbunge? Hebu mwulize vizuri mkuu kisha tupashe.
Yes yuko juu yao kwa mamna nyingi labda nikupe chache,kwanza yeye ndioaliwafadhili kampeni zao kuanzia uchaguzi wa mwaka 1995 kwa fedha zake binafsi na wakati huo ukumbuke hata huo ufisadi haukuwepo...pili yeye ni mjumbe wa kamati ya siasa ya mkoa ambayo wabunge wako chini yake kichama,yeye ni mjumbe wa nec na kamati kuu ya ccm anayo mamlaka ya kuonya na kuelekeza.
 

Mie nawashangaa watu hapa jamvini hamjui mnabishana na nani
KWA TAARIFA YENU MNAYEBISHANA NAE NI HUYU HUYO PAPA
Kwa macho yangu nimeoina kwenye laptop yake anawajibia hoja zenu JF busy kucheki updates

HALO HALO IDUMU JF HAWALALI KUCHUNGULIA DEVELOPING ISSUE
 
- Waache wafu wazikane wenyewe huko Igunga na kiongozi wao, maana kama hizi habari ni za kweli basi sikio la kufa hilo!

William.

Wakazi wa Igunga wanapenda PIPI, nadhani ndiyo maana ni miongoni mwa wilaya zilizo nyuma kimaendeleo. Waliofika Tabora na kwenye wilaya zake wanaijua INAVYOTIA HURUMA utadhani imelaaniwa ila leo nimegundua ni kwa ajili ya HIZO PIPI.
 
Kupigana vita ya ufisadi kwa ku-face mtu mmoja mmoja, haina tofauti sana na mashindano ya muziki wa taarabu, especially enzi zile za vikundi hivi viwili.

Muungano Cultural Troup Vs Tanzania One Theatre.

Akitunga mmoja wimbo huu, baada ya wiki unajibiwa na mwenzake! Mimi naona kama imekuwa mipasho vile... haya. Wiki endi Njema.
 
Wakazi wa Igunga wanapenda PIPI, nadhani ndiyo maana ni miongoni mwa wilaya zilizo nyuma kimaendeleo. Waliofika Tabora na kwenye wilaya zake wanaijua INAVYOTIA HURUMA utadhani imelaaniwa ila leo nimegundua ni kwa ajili ya HIZO PIPI.
eeeh bwana eeeh... hadith hii kakusimulia nani?
 
Wakazi wa Igunga wanapenda PIPI, nadhani ndiyo maana ni miongoni mwa wilaya zilizo nyuma kimaendeleo. Waliofika Tabora na kwenye wilaya zake wanaijua INAVYOTIA HURUMA utadhani imelaaniwa ila leo nimegundua ni kwa ajili ya HIZO PIPI.


Hili la kugawa pipi limenikuna na kunikumbusha kampuni ya Caspian walipomaliza project ya kujenga bwawa pale Geita Gold Mine RA alitayarisha asante kwa wafanyakazi wote, amini usiamini mwanaume yule aligawa pipi machungwa mbili mbili kwa kila mfanyakazi, anayebisha afuatilie kwa wafanyakazi waliokuwepo, jamaa nuksi kwelikweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…