Kosa kubwa ni kwamba Chadema hawana Makamanda au tuseme wamefurahi kuongeza wabunge na sasa wanakwenda likizo kulala mpaka 2015, ukweli Chadema kama itachukulia umuhimu wa kuanza kujipanga hivi sasa na kuwa na makada wao mikoani, Wilayani na vijijini haki ya mungu 2015 wanamvua nguo CCM mchana kweupeeeee kwani waTz walivyochoka na usanii hawatachagua tena usanii wa hawa jamaaa, wengi waliochagua Chadema hawakuwa wanachama wa Chadema bali walifuata Nondo zilizokuwa zinamwagwa na Dr wa ukweli, Dr wa Phd, Dr wa kung'oa ufisadi, Dr wa walala hoi waleee kama mtawakumbuka 70% waliotajwa na JK kwamba ni fuata upepo na kweli wamemhakikishia kuwa upepo ukielekea mashariki na wao hukohuko hawaangaliii makunyanzi ya mtu, kofia, fulana, wala khanga zao, nilifurahi sana pale Mwanza vijana walivyokuwa wanaweka shinikizo la kutangazwa mshindi kwani pia kulikuwa na baadhi ya askari waliokuwa wakitoa signal za chadema lakini kwa kificho ili mabosi wao wasione madole mawili alama ya ushindi ndipo nikajua kuwa CCM wamekwishney na 2015 wasifikiri askari watazuia vijana wa chadema kwani na hao askari nao choka mbaya, wamepigika kama mimi na wewe, kila la kheri Chadema wangu