Rostam MUST Resign; CCM Must Act

We are on the same trail biggy
 

MMK kwanza nakushukuru kwa makala yako yenye maswali tisa kwa Rostam Aziz kuhusu Dowans iliyoandikwa kwenye gazeti la Tanzania Daima la leo. Lakini pia nimepata fursa ya kupitia makala ya Ezekiel Kamwaga yenye yenye kichwa cha habari " Anayedai Mabilioni Dowans ni Rostam" iliyoandikwa kwenye Mwanahalisi ya leo.

Kitu kimoja kinachoshabihiana ninachokiona kwenye hizi makala mbili ni kuwa Rostam Aziz hakufanya haya yote anayotuhumiwa peke yake. Kimsingi zoezi la kuhamisha mkataba liliratibiwa na kusimamiwa kwa karibu sana na viongozi wa ngazi za juu serikalini ambao inaonekana walikuwa wakishirikiana kwa karibu sana na bwana Rostam. Viongozi wote hawa walikuwa ni wabunge kwa maana ya wawakilishi wa wananchi waliopigiwa kura kwenda kulinda raslimali za taifa letu.

Nachelea kuamini kuwa mambo yote haya ya Dowans yangefanikiwa kama Rostam Aziz asingepata msaada mkubwa kutoka wizara ya nishati na madini (ikiongozwa na Bw. Karamagi wakati huo) ambayo kimsingi iliishinikiza Tanesco kuhamisha mkataba kati yake na Richmond kwenda Dowans. Rostam Aziz peke yake asingeweza kufanya hili kwani tayari uongozi wa Tanesco walishakataa kuhamisha mkataba huo.

Sipingani kimsingi na mawazo yako kuwa ni vyema Rostam akaachia ngazi kwenye uongozi wa taifa hili. Hii inatokana na ukweli kwamba hata kanuni za mgongano wa kimaslahi (conflict of interest) zinamtaka mtu kuweka wazi maslahi yake anapofanya biashara inayogonganisha maslahi yake binafsi na yale ya mwajiri wake. Mwajiri wa Rostam hapa (kama mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano) ni dola (state) ya Jamhuri ya Muungano kwa ujumla wake. Napoongelea dola hapa namaanisha nguzo zote tatu za dola yaani mahakama, bunge na serikali kuu.

Hoja yangu ya msingi ni kuwa Rostam Aziz siyo tatizo la msingi linalotukabili bali ni dalili tu za tatizo kubwa tunalokabiliana nalo kama taifa. Tuna mfumo wa kisiasa ambao umewezesha watu wajanja kama Rostam Aziz na wengine wengi ama kupenya wao wenyewe au kupenyeza vibaraka wao kwenye uongozi wa chama na serikali. Ni hawa vibaraka ambao kimsingi ndiyo wanaotuibia mali asili zetu bila huruma. Hata ukimuondoa Rostam leo kwa mfumo uliopo watazaliwa kina Rostam mia moja. Na tayari tunao wengi, na wengine ni ndugu na marafiki zetu, isipokuwa tu ni kuwa hawavumi kwa sasa.

Tukilifanya tatizo la Dowans kuwa ni la Rostam dhidi ya wananchi tutafanya kosa moja kubwa nalo ni kuikosa picha ya tatizo lote kwa upana wake. Rostam anaweza kabisa kuachia ngazi kama unavyoshauri lakini kama bado kuna watu serikalini na kwenye chama waliofika hapo walipo kwa ufadhili wake na kwa makubaliano waliyofikia (Memorandum of Understanding) ataendelea kufanya yale anayoyafanya sasa kwa uhuru zaidi kwani sasa hatakuwa kwenye mwangaza (spotlight) wa vyombo vya habari kama ilivyo sasa.

Sisi wenye asili ya ufugaji tunaamini kuwa ni rahisi zaidi kumwangusha ng'ombe ukimkamata kwenye mapembe yake kuliko ukimkamata mguu wake. Lakini hili haiondoi ukweli kuwa kumkamata ng'ombe kwenye mapembe yake ni hatari zaidi kuliko kumkamata mguu kwani kuna hatari ya kujeruhiwa na hizo pembe. Kudeal na Rostam ni sawa na kuwekeza kwenye miguu ya ng'ombe badala ya mapembe. Tatizo letu lipo juu kabisa kwenye mapembe. Nadhani kila mtu anafahamu mapembe hapa yana maana gani katika suala la Dowans.

Majirani zetu ambao ni wavuvi wanaamini kuwa samaki siku zote huwa anaoza kutoka kwenye kichwa chake. Hii ndiyo sababu kina mama hukimbilia kukagua mapezi ya samaki (fish gills) kujiridhisha kuwa samaki bado hajaoza. Hapa kwetu kichwa cha samaki hakiwezi kuwa Rostam Aziz. Inabidi tukague mapezi ya kichwa cha huyu samaki wetu (dola) kuona kama bado hiki kichwa kio sawa.

Tunapoendelea kuongelea suala la Dowans kana kwamba ni tatizo la Rostam Aziz peke yake tunawapoteza wananchi na kuwafanya waelekeze hasira zao kwa mtu ambaye anawakilisha dalili tu za tatizo na siyo kiini hasa cha tatizo lenyewe. Lazima sasa tuwekeze kwenye kuumbua kiini hasa cha tatizo linalotukabili.
 

Kaka,
Hii imekaa ki-ukweli kabisa. Kama Rostam akikumbwa na masahaba yoyote kama yeye au akamatwe, au ajiuzulu CCM, chama hiki kitakufa flat, au msambaratiko utakaotokea hakuna anayeweza kuutabiri. Ni mkubwa mno!

CCM haipo bila Rostam, na serikali yenyewe haina lolote bila Rostam kudecide kwa JK yes lifanyike jambo au au no lisifanyike...na je assume Rostam ametoweka ghafla! Hata Rais atakimbia...! Ulishaona nchi yoyote Rais anakubali 'kulowa mvua' (mascandal) kama JK, wakati 'mwavuli amemfunika mwingine' Rostam? La hasha, anajua kama sio Rostam, hata yeye JK hatakuwepo! Finish...
 
Sio RA tu wa kuresign, kuna Mbowe, Chege etc.

Kila mchafu hafai kuwa kiongozi, tunahitaji viongozi wasafi, wasio na madoa. Hawa ndio wana mamlaka ya kimaadili kusafisha ufisadi.

No double standards.
 
Sidhani kama ni busara kwa RA kujiuzulu, maana hawezi kujiuzulu katika nyadhifa za kisiasa au nyadhifa za ufisadi, maana hizo nyadhifa kwake zina ndoa nzuri tu. It's a high time that he gets ASSASSINATED and his monies + mali get confiscated.
 
kwa ccm hii ...hajiuzuru na chama hakitachukua hatua yoyote........tanzanians we need to act...n force them to step down...hawawezi kutafuna nchi namna hii na post za umma bado wamekalia.....
 
Mere Resignation is not enough...., the gentleman should be accountable na afilisiwe... ili at least turudhishe pesa zetu ambazo allegedly ameziiba... Kuresign peke yake haitasaidia ataendelea kutanua... kwahiyo afukuzwe, afilisiwe na ashitakiwe
 
I don't agree with you MM. I think it should be very straight forward to say 'JK MUST RESIGN' because he is the one letting RA play around and manipulating Tanzania's economy HOWEVER he want. How a president can see the same name appearing in every dirty saga and still doing NOTHING about him!!

In another view RA anatumiwa na viongozi wa juu kwa maslahi yao binafsi kwa sababu yeye anajua kuendesha dili chafu. Kwa mfano the question was who will be involved in making sure the top figures get those 94b of Dowans? It's hard for any, but RA came out and took the BURDEN using his skills to formulate the way out while top figures only ensures his safety by bleaching some laws and regulations like PPA etc.

Resignation of RA won't be of much help because he is already in touch with every part of the governing, judicial and legislative systems. Kumbuka JK kamruhusu amuweke Makinda pale bungeni, akamuweka Jaji mkuu, mwanasheria mkuu na serikalini JK mwenyewe kashikika.

NO OTHER WAY but JK must resign automatically will go down with RA
 

... could it be that RA is actually CCM leadereship? That although RA might be seen as an individual, his actions are actions of the entire collective leadership of CCM. In that case, not only should RA quit, CCM ought to quit as well and present themselves for custody pending prosecution.
 
Mwanakijiji is spot on Rostam! Rostam is not only a liability to the President and the ruling party CCM but an embarrassment to all of us in the sense that as a nation we have allowed just one conman masquerading as a businessman cum politician take us for a ride. However, having said that, I wonder where Mwanakijiji got the the guts to even consider that UVCCM can have the temerity to call Rostam Aziz to order!

I am saying this because not long ago we saw how the very UVCCM benefited from the " donation" by one Soni Tomaiya, the suspected beneficiary of the Radar lootocracy and one of the kingpins of the UFISADI mentioned by Mengi last year. That "donation" was supposedly given to help UVCCM to organize its elections.

To that effect UVCCM had no moral authority to talk about grand corruption let alone calling anyone to order!! This shows how UVCCM has sunk to that level! It is a big shame.
 
Rostam kwa kweli ametuudhi naafiki kabisa.

Lakini kwa upande mwingine......kama amekosea kweli kwa nini wakulu wake wasimwadabishe?? Why?

Kwa nini shinikizo litoke kwetu (umma aka "nguvu ya Mungu") eti kumshinikiza a "nobody" (in political hierarchy terms) like Rostam? Why??

Seriously, it goes without even saying kuwa "umma" uko more powerful than that...and therefore it'll be going too low for the "umma" to take it out on a "nobody" (not the emphasis "nobody") like Rostam.

Kwa nini tusiwe kama wenzetu wa pale Misri ambao pamoja na Mubarak katika kipindi cha karibuni ku-attempt kuwapooza kwa kufanya hili au ile lakini watu bado wanaendelea kulilia kichwa chake? Why not us??

Hatuoni kuwa kwa kumshambulia sana na kum-target Rostam hatulengi kwenye bull?

Hili suala la Dowans linahitaji nothing but one big mass uprising (Egypt-like).....uprising ambayo target yake ni kulilia kichwa cha "Mubarak" wetu ambaye katika mazingira ya kawaida ana uwezo hata wa kunyoosha kidole tu and Rostam will be reduced into nothingness! Sadly...huyu "Mubarak" wetu yuko kimyaa!

Kweli tuendelee kutegemea kudra za Mwenyezi Mungu? Mpaka lini?

Anyways.....
 



I could not say it better than you guys....CCM must go, JK must go, then these Rostalism cancer will automatically cured!!! I repeat Rostam is nothing in this country, you will only support my words after we learn how to be nationalist and good citizens, we can only know this when we KNOW OUR POSITION IS HIGHER THAN THE WORLD ROSTAM!!! talking Rostam in this kind of governments is lowering ourself.... we are begging him to step down... what a joke!!! it means we are coward and full of words... because the problem is not Rostam and Dowans is a system that accomodating Rostam, FYI we have so many dubious deals worth more than 94billions these deals are being done not by Rostam!!! let Rostam be swept while we are overhauling the whole system.
 


Nyie wanasisiemu, hayo maelezo yenu katika maandishi mekundu ndio yanafanya jamaa azidi kutafuna nchi huku chama kikiwa kimya! Mjasiriamali yeyote lazima chukue risk ili aendelee. Likewise, ili chama kiwe katika msitari, lazima baadhi ya wanachama wenzenu wajitolee muhanga kushinikiza Rostam avuliwe uanachama ili kunusuru maslahi ya nchi na chama pia. Maelezo yenu ya woga na kukata tamaa hapo juu hayawafikishi popote katika chama. Hakuna kazi rahisi!
 

So what is your suggestion, aendelee kufanya anayoyafanya? Wewe unaona nchi hii inakalika kwa sasa?
 

Siamini kwamba Rostam ndio anayefinance election za CCM. Wewe ndio unayefinance hizo elections kwa kodi yako. Wananchi wakiamua asiendelee kutumia kodi yao kufinance ushindi wa CCM hilo linawezekana.

Wanahitaji kujua na kuelekezwa wafanye nini basi. Get this knowledge son!
 

Hakuna mtu anayeitwa untouchable in this revolutionary error!
 

Kwa hiyo unasemaje, kwa sababu watu wanahusika serikalini basi Rostam aachwe tu. We must start somewhere, wote wapo kwenye target list. Wezi wote including wewe cos maandishi yako yanaonyesha ni mshirika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…