Unanena nini wewe kiumbe
Ukiangalia ukiritimba wa TAWALA NA WENYE MAMLAKA TU utakuwa bado unaongea kihisia sana.....Ukiritimba umezidi. Uko kila mahali.
Katiba ukiritimba. Kukusanyika ukiritimba. Kuona ukiritimba. Kufikiri ukiritimba. Tusipoangalia hata kupumua na kufa itakuwa pia ukiritimba.
Wewe huoni hivyo?
Mkuu Brazaj.....
Inaonekana umechukizwa sana na wanaoipinga ROYAL TOUR...na wanaompinga mh.Rais SSH kwa kuamua kulipambania taifa katika nyanja ya UTALII...hasa hayo malengo kuntu ya UTALII WA KITAMADUNI......
My take:
KUJIFUNZA NI SAFARI NDEFU MNO
#SiempreJMT
Nimekupata vyema mkuu wangu....Ninachukizwa na mazuio.
Juzi kati, tulikuwa na zuio la la aina yake Kwamba kuona mapicha huru kutokea royal tour ni marufuku ila tu yale yaliyo haririwa na wale mabingwa wa kufahamu tunapaswa kuona, kusikia, kukusanyika, kufikiria, nk, vipi.
Yote ikiwa ni kwa hisani yao.
Wewe waona kuna afya kwenye kunyimana uhuru hivyo?
My take resembles yours:
KUJIFUNZA NI SAFARI NDEFU MNO
Ukiangalia ukiritimba wa TAWALA NA WENYE MAMLAKA TU utakuwa bado unaongea kihisia sana.....
Umesema uko kila mahali....basi tuanze kufundishana VYEMA NGAZI YA FAMILIA....VIJIJI....MITAANI NA SHULENI....hii itakuja kuzibadilisha "mindset zetu".....
Ila kutaka tu ukiritimba uondoke "POLITICALLY" basi tutakuwa tunazitia nafsi zetu hamanikoni na msambweni tu.......
My take:
HAKUNA JAMBO GUMU KAMA KUBADILISHA TABIA/HULKA ZA WENGINE
#SiempreJMT
🤣🤣Kwanini wanufaika na status quo mnapenda kutuchagulia pa kuanzia?
Tangu lini mtuhumiwa au mkosaji akajichagulia jaji, adhabu, au hatua za kumchukulia ili kumtia adabu?
Jitihada kubwa inayowekwa kumnasua huyu mamlaka kwenye ndoano ni kwa maslahi ya nani?
My take:
Yote kabisa yanafanyika kuhakikisha nafasi ya kusimamisha uchumi wa watu fulani kwanza haitatiziki hata kama ikibidi:
View attachment 1934128
Nimekupata vyema mkuu wangu....
Ila.......
Kuhusu "wao" kuzizuia picha za ROYAL TOUR mbona ni jambo la kawaida tu.....
Hao wanataka walimalize "zoezi" la hiyo "shooting" halafu ndio RASMI tuone kila kilichojiri.....
#SiempreJMT
🤣🤣
Mkuu Brazaj.....
Hakuna TAWALA inayosimamishwa na binadamu "viumbe dhaifu" ikakosa MAPUNGUFU.....
Na ndio maana baba wa taifa El Comandante JKN(Siempre) akatuachia kakitabu "TUJISAHIHISHE".....
My take:
Waswahili husema nyumba mbili njozi mbili
#SiempreJMT
Sawa mkuu....Haki, uhuru, usawa na demokrasia vitatunasua.
Vikundi vya watu wachache haviwezi kuachwa kuhodhi madaraka na kuikamata nchi mateka.
Kunako demokrasia hakuwezi kuharibika jambo.
Sawa mkuu....
Ila kusema tu "demokrasia hufanana/lazima ifanane" kote duniani ndipo hapo PENYE VITA/BALAA NA SINTOFAHAMU....dunia haijawahi kuikubali TAFSIRI moja tu ya demokrasia....
Mathalani ni majuzi tu tuliyaona ya mh.TRUMP akiilalamikia mifumo ya "demokrasia inayoonekana bora kabisa duniani"......
#SiempreJMT
AiseeUkiritimba umezidi. Uko kila mahali.
Katiba ukiritimba. Kukusanyika ukiritimba. Kuona ukiritimba. Kufikiri ukiritimba. Tusipoangalia hata kupumua na kufa itakuwa pia ukiritimba.
Wewe huoni hivyo?
Kwa sababu Trump alikuwa na fikra za kimagufuri,mseveni na kagame ilimfanya akumbane na Demokrasia halali ya USA.Sawa mkuu....
Ila kusema tu "demokrasia hufanana/lazima ifanane" kote duniani ndipo hapo PENYE VITA/BALAA NA SINTOFAHAMU....dunia haijawahi kuikubali TAFSIRI moja tu ya demokrasia....
Mathalani ni majuzi tu tuliyaona ya mh.TRUMP akiilalamikia mifumo ya "demokrasia inayoonekana bora kabisa duniani"......
#SiempreJMT
Safi sana mkuu,ujumbe umefika na umepokelewa vema,"Mwenye macho haambiwi tazama"Demokrasia kama asemavyo beberu ni:
"a system of government by the whole population or all the eligible members of a state, typically through elected representatives."
Demokrasia huanzia kwenye uchaguzi wa wakilishi ambao ni shuruti kuwa huru, haki na wa kuaminika.
Mengine ya kudai demokrasia ni tegemezi ya mahali na mahali (ikiwamo mifano butu ya kina Trump), hizo ni janja janza za mabaradhuli tu za kujaribu kuukimbia ukweli.
Museveni, Kagame, Nkurunziza, Mugabe, Magufuli, na wa namna hiyo ni mifano mizuri ya waminya demokrasia na kuja na janja janja kama zako.
Hawana tofauti na wapinga chanjo za Corona walio busy kutafuta ziliko exceptions zozote hata kama ni za kijinga ili kuhalalisha pumba zao.
Safi sana mkuu,ujumbe umefika na umepokelewa vema,"Mwenye macho haambiwi tazama"
Kwa sababu Trump alikuwa na fikra za kimagufuri,mseveni na kagame ilimfanya akumbane na Demokrasia halali ya USA.
Tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...