Rudisheni kiboko katika shule za primary na secondary kurudisha ili kurudisha Heshima

Rudisheni kiboko katika shule za primary na secondary kurudisha ili kurudisha Heshima

Mwanafikra huru

Senior Member
Joined
Jan 17, 2013
Posts
141
Reaction score
18
Sisi tulio pigwa kiboko leo tunajua umuhimi wa kiboko
leo wanafunzi mashureni kwa utovu wa nidhamu ni hali tata na ni zaidi ya walimu sababu kubwa mwalimu hawezi kumgusa mtoto
hawa watoto walio chora haya mazombi na Messi na matusi watafutwe wapigwe kiboko hadharani kwa sababu wanajulikana kama walikuwa wanaaandika number zao kwenye karatasi na wawekwe hadharani kinyume chake kila mwaka hawa watoto wataongezeka hiyo ni hatua ya kwanza na nyingne zichukuliwe na serikali kuzui haya mambo ni aibu

ni mawazo huru
 
Haisaidii kitu
, Inasaidia sana. Jamani mimi nilisoma shule ya Temeke. Kulikuwa na mwalimu anaitwa mwalimu Kisaka, siku ya zamu yake shule nzima ni kimya haina kelele watu ni kujisomea kwa kwenda mbele. Na shule yetu ilikua inaongoza kwenye michezo karibu yote hata kwaya na Ngoma za kienyeji. Darasani ndo usisema. Kulikua na mwalimu wa histori jina lake nimelisahau. Akikusanya madaftari usiporudishiwa ujuwe siku hiyo utafinywa au kupigwa na rula kwenye vidole hadi kesho kinaeleweka. Na matunda tunayaona kwa kweli mimi binafsi nawashukuru sana wale walimu.

Ila siku hizi mwalimu akimchapa mtoto. Mzazi anakuja pigana na mwalimu mbele ya wanafunzi wengine halafu ukute mzazi ndio ana nguvu. Hiyo picha inakuaje. Ukimkuta ana vijisenti, utakuta anampeleka mzazi polisi.

Mfano. Kuna shule nilimpeleka mwangu ya mission - huko Tanga tukakuta mzazi kwa kuwa ameambiwa mtoto wake ana wastani wa chini ya ule unaotakiwa na shule ile, aje waone jinsi gani washirikiane aweze kupanda kiwango. Yule mzazi alimtishaje yule mwalimu akamuambia nitaifunga hiyo shule na kweli alirudi Dar akaenda kushitaki Wizara ya Elimu kilichotokea hapo waliitwa wale walimu njooni mripoti wizarani haraka sana, bila kukosa siku fulani. Bila ya kujua ratiba yao ya shule ikoje. Kwenda kule wakaambwia wastani huo mnaoutaka mmeutoa wapi wakati wastani wa serikali ni 35. Bahati wale wenye shule walikua na msimamo wakawaambia sisi tunataka tutoe elimu bora kama mnataka tutoe bora elimu tuko tayari kufunga shule tugeuze kanisa.

Basi tulivyoletewa hiyo taarifa siku ya wazazi kwa kweli tulihudhunika - na watu kwa pamoja tukawasapoti wale walimu kama yeye mtoto wake ni mjinga asituletee ujinga wake hapa shuleni. Hebu aifunge hiyo shule tuone. Kwa kweli watu wakalifanyia kazi jambo lile na bado hiyo shule iko kwenye kumi bora.

Sasa ninachosema hapa, nidhamu kwa shule ni muhimi katika matokeo ya mtoto kitu ambacho watu wengi tumekisahau au hatutaki kukiangalia. Na nidhamu inatakiwa ianze kwa mzazi hadi kwa mtoto. Na utaona matokeo yake. Mbona hizi shule za seminary zinafanya vizuri. Kwa sababu wao wanazingatia nidhamu. Na wanafuatilia hadi hata wewe mzazi wakati mwingine unaona ni kero. Lakini ukiangalia kwa jicho la tatu unajitahidi tu ili mtoto awe na msingi mzuri.
 
Shule hazina vitabu, mwalimu mmoja madarasa kibao na bado mshahara zengwe, kwenye practical mnasoma theory tu, curriculum za kichina n.k n.k hata wakichapwa viboko kama punda tatizo halijatatuliwa bado.....
 
Shule hazina vitabu, mwalimu mmoja madarasa kibao na bado mshahara zengwe, kwenye practical mnasoma theory tu, curriculum za kichina n.k n.k hata wakichapwa viboko kama punda tatizo halijatatuliwa bado.....
Wale wanaofaulu kwenye hiyo hiyo shule wao wanapata wapi vitabu? au wanafundishwa na mwalimu tofauti na hao wengine. Kwani kuna hizo hizo shule waliofaulu wapo na waliofeli pia. Hapa nidhamu tu ndio suluhisho. Mengine yanafuata. Walimu wa watu wanajitahidi pamoja na vitabu vichache. Kama mzazi huchangii kununua vitabu anavyooandikiwa mtoto unategemea nini. Wazazi haohao wakiitwa kwenye mikutano ya shule waje wazungumze na walimu utaona shule ina watoto 300 lakini wanakuja wazazi wa watoto 20. Hiyo pia ni nidhamu.
 
Sisi tulio pigwa kiboko leo tunajua umuhimi wa kiboko
leo wanafunzi mashureni kwa utovu wa nidhamu ni hali tata na ni zaidi ya walimu sababu kubwa mwalimu hawezi kumgusa mtoto
hawa watoto walio chora haya mazombi na Messi na matusi watafutwe wapigwe kiboko hadharani kwa sababu wanajulikana kama walikuwa wanaaandika number zao kwenye karatasi na wawekwe hadharani kinyume chake kila mwaka hawa watoto wataongezeka hiyo ni hatua ya kwanza na nyingne zichukuliwe na serikali kuzui haya mambo ni aibu

ni mawazo huru
Si uchukue wa kwako uchape unavyotaka, na uende shuleni ukawape ruhusa walimu wachape wanavyotaka? lakini mimi wa kwangu hachapi mtu, siku mtu akithubutu patakuwa hapatoshi hapo shuleni!

 
Wale wanaofaulu kwenye hiyo hiyo shule wao wanapata wapi vitabu? au wanafundishwa na mwalimu tofauti na hao wengine. Kwani kuna hizo hizo shule waliofaulu wapo na waliofeli pia. Hapa nidhamu tu ndio suluhisho. Mengine yanafuata. Walimu wa watu wanajitahidi pamoja na vitabu vichache. Kama mzazi huchangii kununua vitabu anavyooandikiwa mtoto unategemea nini. Wazazi haohao wakiitwa kwenye mikutano ya shule waje wazungumze na walimu utaona shule ina watoto 300 lakini wanakuja wazazi wa watoto 20. Hiyo pia ni nidhamu.

unaniambia wamefeli kwasababu hawana nidhamu????
 
Si uchukue wa kwako uchape unavyotaka, na uende shuleni ukawape ruhusa walimu wachape wanavyotaka? lakini mimi wa kwangu hachapi mtu, siku mtu akithubutu patakuwa hapatoshi hapo shuleni!

Ndio kati ya watakaochora Zombi. Halafu unalalama
 
Ngugu zanguni,hivi ukimpa mwalimu ruhusa ya kuchapa viboko huku ana-frustration za maisha huyu mtoto unmtakia mema?Je hataadhibiwa kwa hasira sababu mwalimu anahasira na serikali?Kama walimu wangekuwa hawana mgomo baridi basi adhabu hii ingeweza kusaidia,lakini kwa mwendo huu wa mgomo baridi duh ,hata sikubali haitasiaidia bali itafanya watoto waipende hata hiyo shule.

Tuanze na serikali iwalipe vizuri walimu na kuongea nao kukubaliana katika kutokubaliana.Serikali iboreshe mazingira ya kufundishia na iongeze elimu za walimu.

Serilaki iache kutumia walimu wa vodafasta ,i-train walimu wa kutosha na nchi yeti inahitaji walimu bora na si bora walimu.

Serikali itafanye kama zamani mwanafunzi mwenye talent ya kufundisha apewe kipaumbele kwenye nafasi za ualimu(Courses) siyo wa train wanafunzi walikosa maeneo mengine na kufanya ualimu kichaka cha wajinga.
 
Back
Top Bottom