Rufaa ya kina Sabaya yashindwa kuendelea leo Februari 20, 2023

Rufaa ya kina Sabaya yashindwa kuendelea leo Februari 20, 2023

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), kupinga hukumu iliyomwachia huru aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi, imeshindwa kuendelea baada ya mawakili wa wajibu rufaa kuomba kufanya mapitio Mahakama ya Rufani.

Leo Jumatatu Februari 20, 2023 Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilipanga kuendelea kusikiliza rufaa hiyo, ambapo DPP aliwakilishwa na Mawakili wa Serikali waandamizi Felix Kwetukia, Timotheo Mmari na Hebel Kihaka.

Wajibu rufaa waliwakilishwa na mawakili Mosses Mahuna, Fauzia Mustapha, Fridolin Bwemelo na Sylvster Kahunduka.

Mbali na Sabaya wajibu rufaa wengine ni Enock Mnkeni, John Aweyo, Sylvester Nyegu, Jackson Macha na Nathan Msuya.

Mbele ya Jaji Salma Maghimbia anayesikiliza rufaa hiyo, Wakili Kwetukia aliieleza mahakama kuwa, Februari 3, 2023 walipokea maombi ya kufanya mapitio yaliyoandaliwa Januari 27, 2023 inayoomba Mahakama ya Rufani ifanye mapitio ya mwenendo wa rufaa hiyo na uamuzi mdogo uliotolewa Desemba 14, 2022.

"Kwa msingi huo kwa kuwa kuna maombi ya mapitio ni rai yetu rufaa hii isubiri kwa muda ikisibiri uamuzi wa maombi ya upande wa wajibu rufaa ualiyopelekwa katika mahakama ya rufani," ameeleza Kwetukia.

Jaji Maghimbi amesema kutokana na maombi hayo katika mahakama ya juu, shauri hilo la rufaa litasubiri hadi uamuzi wa mahakama ya Rufani yatakapotolewa.

Leo mbali na Sabaya mjibu rufaa mwingine aliyekuwepo mahakamani hapo ni Mnkeni, huku wajibu rufaa wawili ambao ni Aweyo na Nyegu wakiwa hawapo mahakamani hapo, ila mawakili wanaowawakilisha wakiwepo, ambao pia waliieleza mahakama kuwa hawana taarifa za Msuya na Macha.

Desemba 14, 2022 Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilitupilia mbali pingamizi lililokuwa limewasilishwa mahakamani hapo na mawakili wa Sabaya.

Miongoni mwa hoja ambazo mahakama imetolea uamuzi ni pamoja na kutupilia mbali hoja ya rufaa kukatwa nje ya muda pamoja na ufafanuzi kuhusu mrufani wa tatu, Watson Mwahomanhe ambaye awali upande wa wajibu rufaa uliibua hoja ya kutokuonekana mahakamani.

Uamuzi huo mdogo ulitolewa na Jaji Maghimbi ambapo Wakili Mahuna anayemwakilisha mjibu rufaa wa kwanza (Sabaya), aliwaasilisha hoja mbili za pingamizi za kutaka rufaa hiyo itupiliwe mbali.

Kuhusu hoja ya wakili Mahuna ya rufaa hiyo kuwasilishwa nje ya muda, Jaji Maghimbi amesema rufaa hiyo imewasilishwa ndani ya wakati na kuwa kwa mujibu wa sheria siku 45 za kukata zinaanza kuhesabiwa pale ambapo nakala za mwenendo wa kesi na uamuzi unakuwa umetolewa.

Amesema anakubaliana na hoja ya wakili wa serikali mwandamizi Patrick Mwita ambaye jana akijibu hoja za pingamizi hilo la awali aliileza mahakama kuwa siku 45 za kukata rufaa zinaanza kuhesabiwa baada ya kukabidhiwa nakala ya mwenendo wa kesi na hukumu.

Kuhusu hoja ya pili iliyotolewa na Mahuna akidai kuwa notisi ya nia ya kukata rufaa inatofautiana na maombi ya rufaa, Jaji amesema anakubaliana na hoja ya wakili wa serikali mwandamizi Patrick Mwita kuwa baada ya kupata mwenendo wa shauri na hukumu ndipo unaweza kuamua nani umkatie rufaa.

Chanzo: Mwananchi
 
Inabidi mawakili watuelezee huu utaratibu wa mahakama zetu za Tanzania misingi ya hii rufaa ya serikali kwenye hii kesi.

Kwa sababu kwa uelewa wangu mdogo wa jurisprudence (mimi sio mwanasheria) anyway huku kijijini kwetu na sehemu nyingi duniani hukumu ya mahakama ya ‘not guilty’ kwenye kesi za jinai uwezi kuikatia rufaa.

Na uwezi fungua criminal case tena illyosikilizwa ndani ya nchi moja kwa shitaka hilo hilo wanaita ‘double jeopardy’.

Unachoweza fanya kama ukuridhika na maamuzi ya kesi ya jinai ni kufungua civil case kudai fidia, lakini uwezi tena fungua kesi ya jinai wala kupinga hukumu ya ‘not guilty’.

Unaweza appeal against a guilty decision only; ndio utamaduni duniani. Kwetu huwa sielewi kabisa misingi ya hizi appeal za not guilty verdicts, ni sheria inaruhusu au ni utamaduni wa kutoka sehemu gani.
 
Mama yupo nyuma dhidi ya hii kesi ya Sabaya na sio ajbu naye anaingizwa pesa kwenye hizi project za kesi..,alafu hichi kikundi cha wahuni kilichopo serikali inatengezea kesi kwasababu ili wajilipe pesa..kwa hiyo hii niproject ya akina xweka na wengine.
Namshangaa sana huyu mama hana uwezo wa kuona huu uchafu..
 
Inabidi mawakili watuelezee huu utaratibu wa mahakama zetu za Tanzania misingi ya hii rufaa ya serikali kwenye hii kesi.

Kwa sababu kwa uelewa wangu mdogo wa jurisprudence (mimi sio mwanasheria) anyway huku kijijini kwetu na sehemu nyingi duniani hukumu ya mahakama ya ‘not guilty’ kwenye kesi za jinai uwezi kuikatia rufaa.

Na uwezi fungua criminal case tena illyosikilizwa ndani ya nchi moja kwa shitaka hilo hilo wanaita ‘double jeopardy’.

Unachoweza fanya kama ukuridhika na maamuzi ya kesi ya jinai ni kufungua civil case kudai fidia, lakini uwezi tena fungua kesi ya jinai wala kupinga hukumu ya ‘not guilty’.

Unaweza appeal against a guilty decision only; ndio utamaduni duniani. Kwetu huwa sielewi kabisa misingi ya hizi za not guilty, ni sheria inaruhusu au ni utamaduni wa kutoka sehemu gani.
Umesema hujui sheria sasa mbona unabwabwaja tuu? Rufaa ni haki kwa pande zote hivyo tulia
 
Umesema hujui sheria sasa mbona unabwabwaja tuu? Rufaa ni haki kwa pande zote hivyo tulia

Walau ungeelezea basi unatumia legal doctorine ipi au sheria ipi; sio kuja na maelezo ya jumla tu.


Anyway majibu nishayapata kwenye section 378 ya sheria husika apparently mtu pekee anaeweza kukata rufaa kwenye ‘not guilty’ verdict za jinai kwa Tanzania ni DPP pekee (sio kila mtu) na ata yeye akifanya hivyo kesi inabidi isikilizwe mahakama za juu.

Na kwenye kufanya hivyo lazima aonyeshe makosa ya mahakama za chini na kuna vigezo vigumu vya kupeleka ushahidi mpya.

Mimi simtetei Sabaya kama ana hatia apewe adhabu ata mimi kuna mambo yake nilikuwa naona ovyo kwa kuangalia video clips tu.

Halikadhalika taasisi za haki zinatakiwa kuonekana zinaendeshwa huru ‘leo kwangu, kesho kwako’ sasa tusifurahie kuona mahakama ikiwa ina najisiwa na mtu kama DPP kisa mamlaka yake ya kisheria.

Umeshatumia mamlaka yako ku appeal, onyesha basi mapungufu ya maamuzi ya mahakama ya chini yaliyomwachia Sabaya au peleka huo ushahidi mpya kesi isikilizwe hukumu itolewe.

Lakini uwezi kumuweka mtu huru jela kwa miezi zaidi ya sita bila ya kuwa umekamilisha ushahidi wa vigezo vya kufanya appeal.Sasa on what grounds did you make the appeal in the first place kama ushahidi aujakamilika na mahakama gani inatoa tarehe za kusikiliza kesi bila ya kujiridhisha mwendesha mashtaka ana ushahidi uliokamilika.

Heck ata appeal yenyewe imepelekwa mahakamani baada ya kupita siku zinazokubalika baada ya hukumu na wameruhusiwa.

Hiyo katiba mpya inabidi iliangalie na hili swala kumbe na DPP nae ni mungu mtu huko kwenye sheria. Haya mamlaka hawa watu huwa wanapewa with good intentions (kwa kesi zinazoendeshwa ovyo kama ilivyokuwa kwa ‘Akasha’ mtuhumiwa wa madawa ya kulevya zilizotaka kuzimwa kihuni) lakini mwishowe watu hawa uanza kuyatumia hayo madaraka yao vibaya.
 
'Wanaomlipa' sabaya wao watalipwa na nani? Au malipo yanaishia kwa sabaya? Wekeni akiba ya maneno
Watalipwa na wataokuepo wakati huo, NB kumtegemea mwanadam ni dhambi na laana!! Maana mwanadam ni kama ua huchanua nakusinyaa, akisinyaa basi unakosa pa kuegemea. Ni vzr tuishi vzr na watu maan hatuijui kesho yetu!!
 
Wale wapambe zake na kundi la jiwe ndiyo hao hao wanamtetea ila sabaaya alitumia nguvu kubwa ya madaraka ila mwisho iliingis nyumba mbaya angetuuliza hata wale ndege wanaotoboa miti hata migumu akifika baadhi ya miti huruka kama nyaa hatoboi yeye sabaaya alijua kote Yuko na nguvu kumbe imekula kwake Bora abaki jela akiachiwa huru ataugua maradhi yakumtesa ni vizuri aendelee huko huko
Hata wanaomtetea jiwe nawashangaa sana
 
Back
Top Bottom