Ruhusa za kwenda nje ya nchi kwa wafanyakazi wa serikali

Ruhusa za kwenda nje ya nchi kwa wafanyakazi wa serikali

Kanyafu Nkanwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2010
Posts
850
Reaction score
103
Kwa hakika kitendo cha Serikali kuamua ku-centralise mambo ya kuomba ruhusa kwenda nje ya nchi kinatuvuruga sana sana. Suala la kwamba kila mfanyakazi wa serikali ni lazima apewe ruhusa na IKULU kama akitaka kwenda nje ya nchi ni kitendo kisichokubalika kabisa na usumbufu uliopitiliza. Sasa imekuwa kawaida kwa wafanyakazi kutoka mikoani kuomba ruhusa kwa immediate bosses wao ili wapeleke hizo barua Wizarani. Mimi ninachoshindwa kuelewa ni:

1. Hivi hii serikali haikupata nafasi ya kutambua kuwa kuna baadhi ya wafanyakazi wao kusafiri kwenda nje ya nchi ni sehemu ya kazi zao? Mtu kama huyu itabidi awe anashinda Dar es Salaam kupeleka barua za ruhusa?!
2. Serikali haioni kuwa matumizi ya fedha ya umma yataongezeka sana kwa kitendo cha watu kulipa perdiems kwenda Dar es Salaam kufuatilia hizo barua?
3. Hivi serikali haikuona kuwa itakuwa ni upotezaji mkubwa wa muda kwa watu kupanda safari za kufuatilia barua zao badala ya kufanya kazi za kawaida za serikali?

Mh. Balozi Idd hii strategy uliokuja nayo ili kudhibiti matumizi mabaya ya safari za nje inaweza kuwa kinyume na hayo matarajio. Ikibidi kama ni lazima basi ziwekwe centres mikoani ili watu waweze kuzitumia hizo badala ya usumbufu uliopo sasa hivi kwa kweli.
 
Enzi za mwalimu ilikuwa hivyo. hata ofisa ukiwa likizo na unasafari binafsi ni lazima upate kibali cha ikulu
 
Kwa hakika kitendo cha Serikali kuamua ku-centralise mambo ya kuomba ruhusa kwenda nje ya nchi kinatuvuruga sana sana. Suala la kwamba kila mfanyakazi wa serikali ni lazima apewe ruhusa na IKULU kama akitaka kwenda nje ya nchi ni kitendo kisichokubalika kabisa na usumbufu uliopitiliza. Sasa imekuwa kawaida kwa wafanyakazi kutoka mikoani kuomba ruhusa kwa immediate bosses wao ili wapeleke hizo barua Wizarani. Mimi ninachoshindwa kuelewa ni:

1. Hivi hii serikali haikupata nafasi ya kutambua kuwa kuna baadhi ya wafanyakazi wao kusafiri kwenda nje ya nchi ni sehemu ya kazi zao? Mtu kama huyu itabidi awe anashinda Dar es Salaam kupeleka barua za ruhusa?!
2. Serikali haioni kuwa matumizi ya fedha ya umma yataongezeka sana kwa kitendo cha watu kulipa perdiems kwenda Dar es Salaam kufuatilia hizo barua?
3. Hivi serikali haikuona kuwa itakuwa ni upotezaji mkubwa wa muda kwa watu kupanda safari za kufuatilia barua zao badala ya kufanya kazi za kawaida za serikali?

Mh. Balozi Idd hii strategy uliokuja nayo ili kudhibiti matumizi mabaya ya safari za nje inaweza kuwa kinyume na hayo matarajio. Ikibidi kama ni lazima basi ziwekwe centres mikoani ili watu waweze kuzitumia hizo badala ya usumbufu uliopo sasa hivi kwa kweli.

Pamoja mkuu... Mi nikihoji watu wanawaza kwa kutumia akili gani, wengine wanasema ooh, nakosa adabu kwa kuhoji akili za watu. Lakini ukweli ni kwamba, ni punguani peke yake anayeweza kuamua 'kudhibiti' safari za wafanyakazi za nje kwa kuwataka waombe kibali ikulu...
 
Watumishi wa moshi vijijini,vunjo na rombo wao hufanya shopping na shughuli zao taveta kila jumamosi hicho kibali ndio wanakisikia!
 
Kwa hakika kitendo cha Serikali kuamua ku-centralise mambo ya kuomba ruhusa kwenda nje ya nchi kinatuvuruga sana sana. Suala la kwamba kila mfanyakazi wa serikali ni lazima apewe ruhusa na IKULU kama akitaka kwenda nje ya nchi ni kitendo kisichokubalika kabisa na usumbufu uliopitiliza. Sasa imekuwa kawaida kwa wafanyakazi kutoka mikoani kuomba ruhusa kwa immediate bosses wao ili wapeleke hizo barua Wizarani. Mimi ninachoshindwa kuelewa ni:

1. Hivi hii serikali haikupata nafasi ya kutambua kuwa kuna baadhi ya wafanyakazi wao kusafiri kwenda nje ya nchi ni sehemu ya kazi zao? Mtu kama huyu itabidi awe anashinda Dar es Salaam kupeleka barua za ruhusa?!
2. Serikali haioni kuwa matumizi ya fedha ya umma yataongezeka sana kwa kitendo cha watu kulipa perdiems kwenda Dar es Salaam kufuatilia hizo barua?
3. Hivi serikali haikuona kuwa itakuwa ni upotezaji mkubwa wa muda kwa watu kupanda safari za kufuatilia barua zao badala ya kufanya kazi za kawaida za serikali?

Mh. Balozi Idd hii strategy uliokuja nayo ili kudhibiti matumizi mabaya ya safari za nje inaweza kuwa kinyume na hayo matarajio. Ikibidi kama ni lazima basi ziwekwe centres mikoani ili watu waweze kuzitumia hizo badala ya usumbufu uliopo sasa hivi kwa kweli.

Hiyo imepitwa na wakati sana! Nahisi Kambarage aliiweka hiyo ili kuwatisha watu na kuwa-monitor movements zao sababu alikuwa yuko so insecure
 
Tatizo linakuwa kubwa kwa watu wanaotoka mikoani,maana sio rahisi ukawasilisha barua yako na kupata majibu/ruhusa ya barua yako siku hiyohiyo.Lazima utapewa tarehe ya kwenda kuangalia majibu ya barua yako na sio mara moja.Hapo sasa watu wanapopoteza muda na pesa pia.
 
Nimefuatilia sana hili. Kumbe easy tu. Taarifa niliyonayo ni kwamba kwanza wafanyakazi wa wizara wanaohusika na hiyo section ya kupokea barua wako down sana. Sababu ni kwamba barua ni nyingi mno na wanashindwa ku-handle. Lakini kumbe pia, unachotakiwa ni kupeleka barua, hakikisha mhuri wa kuonyesha kuwa imepokewa unapigwa. Baada ya hapo katoe fotokopi na original waachie. Tunza fotocopi. Unaweza kupanda ndege na kuondoka baada ya hapo. Bongo tambarare kabisa
 
Enzi za mwalimu ilikuwa hivyo. hata ofisa ukiwa likizo na unasafari binafsi ni lazima upate kibali cha ikulu

Tatizo Tanzania tunafanya mambo kama robot, hasa yakiwa hayana mshiko kwa viongozi. Enzi za Nyerere ilikuwa muhimu kufanya hivi kwa ajili ya mambo ya usalama, ukizingatia kwamba Tanzania ilikuwa kitovu cha ukombozi kusini mwa Afrika. Kumbuka hata kuhamishia makao makuu Dodoma sababu mojawapo ilikuwa ni usalama. Sasa kama viongozi wa leo hawaoni umuhimu wa kubalili kanuni kama hizo ni wazi kwamba wana-ukihiyo fulani.

Ajabu ni kwamba wamekuwa wepesi wa kubadilisha sera za Azimio la Arusha kwa kisingizio cha kwenda na wakati! Kama tunaenda na wakati, kwa nini mambo kama kanuni za watumishi wa serikali kwenda nje hayajabadilishwa?
 
Kwa hakika kitendo cha Serikali kuamua ku-centralise mambo ya kuomba ruhusa kwenda nje ya nchi kinatuvuruga sana sana. Suala la kwamba kila mfanyakazi wa serikali ni lazima apewe ruhusa na IKULU kama akitaka kwenda nje ya nchi ni kitendo kisichokubalika kabisa na usumbufu uliopitiliza. Sasa imekuwa kawaida kwa wafanyakazi kutoka mikoani kuomba ruhusa kwa immediate bosses wao ili wapeleke hizo barua Wizarani. Mimi ninachoshindwa kuelewa ni:

1. Hivi hii serikali haikupata nafasi ya kutambua kuwa kuna baadhi ya wafanyakazi wao kusafiri kwenda nje ya nchi ni sehemu ya kazi zao? Mtu kama huyu itabidi awe anashinda Dar es Salaam kupeleka barua za ruhusa?!
2. Serikali haioni kuwa matumizi ya fedha ya umma yataongezeka sana kwa kitendo cha watu kulipa perdiems kwenda Dar es Salaam kufuatilia hizo barua?
3. Hivi serikali haikuona kuwa itakuwa ni upotezaji mkubwa wa muda kwa watu kupanda safari za kufuatilia barua zao badala ya kufanya kazi za kawaida za serikali?

Mh. Balozi Idd hii strategy uliokuja nayo ili kudhibiti matumizi mabaya ya safari za nje inaweza kuwa kinyume na hayo matarajio. Ikibidi kama ni lazima basi ziwekwe centres mikoani ili watu waweze kuzitumia hizo badala ya usumbufu uliopo sasa hivi kwa kweli.

Hii ni ngumu sana kutekelezeka pamoja na kuwa na nia njema hasara zake ni kubwa kuliko faida ni kama kuuza ng'ombe kumaliza kesi ya paka wako!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom