Rupia: Hazina ya Mjerumani

Sio zote.baadhi zilitengenezwa kwa kufanyiwa makafara ya damu na kuwekwa uchawi mzito.
Inamaana huo uchawi katika hizo rupia uliwekwa kiwandani wakati wa kutengenezwa au wakati zinafukiwa? Na kuna mtu humu a melee za kuwa wajerumani walikatazwa kutoka na vitu zaidi ya nguo zao sasa huo muda wa kufukia hizo Mali kwenye mitaro ya zege waliupata wapi iwapo waliondolewa Chini ya ulinzi mkali na kama kweli wote walifanikiwa kufikia na kufanya hayo mnayoita makafara, inamaana wajerumani wote ni wachawi?
 
Bashite kweli wewe.?
 
Uzi wa 2012 uliokuwa na lengo la kujuzwa ukweli... mwaka 2017 umevamiwa na matapeli..
 
Ndugu hivi vitu vipo "live" ila utapeli umeashika hatamu, ndugu mercury ipo halisi ila kwa hakika kuifikisha mahala ukapata pesa si jambo dogo niseme ni majaaliwa ukipewa na muumba hilo lawezekana, lakini amini mercury ipo na watu wanayo kwenye hifadhi zao.
 
yani umenifanya nianze kuchimba kila mahali kutafuta mali za kale hapa naelekea j.k nyerere airpot kuna uwezekano wa kuwa na hazina fulani si kwa security hii
nimekua nikifuatiria tokea mwanzoni nimeona watu wengi wanataka kujua tatizo wanaoleta mada inawezakana pingine wamesimuliwa tu ndiomana wamepata chakuanzia ila ukweli mimi nimmoja wapo muhanga wa haya mambo nazungumzia pesa za kizamani pamoja na mercury historyndefu kidogo kwani nilijikuta napoteza mda mwingi juu ya haya mambo mwisho nikajikuta naanza kujifunza uchawi kwaupande wa mercury ilibaki kidogo sana niingie mimkononi mwa usalama wataifa pasipo kujua kama nipo mtegoni labda kidogo nielezee mercury imegawanyika ktk langi tofauti ila langi pendwa ni mbili yani nyeupe na nyekundu pia kuna makundi mawili yani ya asili namaanisha ya kwenye mwamba na yakutengeneza kazi kuu ya mercury ni kuosha malanyingi hutumiwa kwenye machimbo ya dhahabu kuoshea dhahabu ila yakutengeneza hapa ndipo kwenye utata ulipo nianzia baada ya tafuta tafuta na kujifanya mjuuaji wa hivi vitu ndipo nilikutana na kaka mmoja akaniambia ana viboxi 20 vya unga wa mercury ikumbukwe unga huu ndio hutengeneza mercury ambayo yakutengeza na pia unga huu wa mercury hutumika kuoshea mizinga ya jeshi nazani kidogo mnaanza kunipata na ikisha tengenezwa mercury tofauti yake hua ni ndogo sana kuijua na yamwamba paka ufahamishwe nivipimo gani hua vinatofauti kama ni umeme sawa sijui maji sawa sijui tambaa sawa kwawanao jua watakua wamenielewa sasa huyu kaka akaniambia tutafute soko ikumbukwe hizo chupa hakunionyesha ila kwamaneno nilimuamini nakwavile nilikuwa nataka pesa ndipo nilipo ingia mzigoni kutafuta tajiri mama yangu ngoja kwanza humu kuna usalama wa taifa .
 
Hiyo mercury nyekundu ulishawahi kuiona?

Unaweza kuweka hapa picha yake
 
Ikawaje
 
Nawewe unataka kubembelezwa.

Hawapo humu we endelea bana.
 
Eti umnaenda kutafuta Mali huna Hata silaha n a makombora.!!!unaenda Ukiwa Na. Kisu Chako mkononi Na. Kipensi sana utavaa buti Ya tope.sasa Hayo mambo Ya Kuona nyoka sio issue.kwani Hawafi Kwa kombora
 
Nilichojifunza Ktk hii threads.
1.Wanerumani wameacha Mali nyingi sana Hapa Tanzania
2.mali Hizo zipo Ktk majabali.mawe Mkubwa.misitu.mapangoni .makanisani.majengo Ya zaman.kuna Eneo Dodoma njia Ya shinyanga kuna mlima mkubwa kiasi ,Chini ya huo mlima pamejengwa kijumba limeshakuwa gofu wameweka bango lina Alama yao.hivi km freemasonic sign
3.watanzania wengi waoga sana Na. Hawana ujasiri.unaambiwa Hapa kuna Mali Chini Lkn naogopa Hata kujaribu kufukua.km utakufa so basi?Lkn ukifanikiwa Pia ni faida kwako.
4.hayo mavitu yaliyopo chini ya ardhi sio mali wala nini.km ni mali je serikali yetu haijui Hizi Mali?mtu una jeshi polisi.na silaha za kivita unashindwaje kuzivamia Hizo Mali zilizopo Chini na kuzibeba.na Kwa uongozi Wetu huu kweli tunashimdaje?
5.Kama kweli makanisa yameshikilia Hayo Mali Chini napata Picha Sasa kuwa tunadanganywa Kwa mgongo Wa kanisai .kumbe watu wana yao
6.Kwenye makaburi mengi utakuta yammewekewa misalaba maeneo mbalimbali.lkn kumbe kuna Mali imefukiwa badala Ya mtu.lkn mengine yanalindwa.
7.Wazungu wachoyo sana km.kweli huku kuna Mali nyingi wamefukia kwanni haawasemi Na. Kishirikina Na. Serikali yetu hii Na. Kuziingoa Mali Na. Kuziigawana?
 
Moja kwa moja utawaza kuhusu rupia(rupee ya mjerumani) na pesa nyingine za kale na yale yanayosemwa kuzihusu hasa kwenye habari nzima za kichawi
Watu wamezinguka na kuzinguliwa hasa watu wametapeliwa na wengine kufa wakitafuta hivi vitu vinavyotajwa kuwa na thamani kubwa

Ukweli huu hapa na si pesa tu bali na vitu vingine vya kale
1. Aina ya malighafi iliyotumika
Wakati huo vilitengenezwa vitu imara sana kutokana na upatikanaji wa malighafi ya kutosha ...vitu kama vyombo vya bati na chuma urembo kama bangili mikufu pete nk leo hii ukivipata na kuviyeyusha kila kimoja unaweza kutengeneza kumi kupitia hicho kimoja

2. Uhifadhi
Wajerumani kwa hapa kwetu walikuta malighafi vito na madini ya kutosha sana! Kutokana na uhifadhi hafifu wakati huo vingi ya hivi vitu viliwekwa tu majumbani mwao wakiviandaa kuvidafirisha kwao
Vita ya pili ya 1939-45 iliwachanganya mno na walipoelekea kushindwa waliamua kuficha mali yote kwenye mashimo makubwa mashambani misituni kwenye mahandaki na milimani kusikofikika kwa urahisi kisha wakawaua watu karibia wote walioshiriki na wanaojua yale maficho wakasepa
Huku kote mali hizo zilihifadhiwa kwenye vyumba imara vilivyojengwa kwa zege gumu hasa ili iwe ngumu kuchimbua ama kuvunja na kama ni mapangoni yalikuwa mapango ya mbali hasa milimani na misituni

3. Dhana ya majoka na viumbe wa ajabu
Huko kwenye hayo maficho kuna baadhi ya watu walisalimika hivyo wakasimulia vizazi vilivyofuata
Kizazi cha kusaka utajiri wa haraka kikaona fursa na kuamua kuchangamkia dili. ..Wajerumani hawakuweka ulinzi wowote wa majoka! Hao ni viumbe tu walijitwalia makazi huko ambako ndio maisha yao yaliko
Watu walioenda bila tahadhari waliumwa na hayo madubwana na kupoteza maisha! Waliosalimika walitimua mbio na kuunda stories za kufikirika

4. Dhana ya uchawi na majini
Kwa wale waliosaka kwenye mahandaki na mashimo marefu yenye vyumba vilivyojengwa kwa zege , baada ya kufanikiwa kuvunja hayo mazege na kutaka kuingia ndani nao walikutana na mauzauza ya kila aina
Unajua ni kwa nini? Sehemu yoyote yenye mfumo wa nyumba ama chumba isiyokaliwa na binadamu roho zinazotangatanga na mapepo hufanya makazi yao kumbuka ile mada ya kutakasa makazi! Hivyo ukiingia huko lazima ukutane na vitu vya ajabu...Mjerumani hahusiki kabisa!

5. Uamuzi wa kufanya kafara ama tambiko kabla ya kuchimba ama kuingia pangoni
Wengi walitafuta waganga wa kienyeji kwenye hili na hawakufanikiwa. ..waliofanikiwa walifanikiwa kwa ujanja tuu....ukienda kwenye pango misituni ukachinja mnyama ukapiga manyanga automatically mkiondoka ile nyama italiwa na kuna wakati manyanga huleta kelele na kufukuza mnyama yoyote aliyeko pangoni...ndio maana baada ya kafara hamuingii siku hiyo hiyo bali kesho yake nk
Wale wa kwenye mashimo NA mahandaki ni ibada tu ya kuziomba roho ziondoke ama kuzifukuza kwa kutumia mitishamba na harufu wasizozipenda....mkikutana na roho korofi mtachezea kichapo mpaka muache kila kitu na kutimua mbio kali sana

6. Ukweli hasa ni UPI?
Baada ya vita ya pili kukoma na baadae Uhuru wajerumani walishindwa kurudi kwa ubabe hivyo wakatumia njia za kijanja kurudi
Unajua waliondoka na ramani zote kule mali zilikofichwa hivyo walirudi kuzichukua kwa njia ya kununua yale maeneo na kuyaendeleza kwa kujenga shule vyuo hospital nk ama miradi ya barabara ufugaji na kilimo
Kwa njia hii walichukua vyao kiulaini mno

7. Thamani na umaarufu wake ni UPI!?
Vitu vya kale kwa wenzetu vina thamani kubwa sana....wenzetu wana utaratibu wa kuweka vituo vya antiques na kuchaji watalii pesa ndefu kuviangalia . kila kimoja kinakuwa kimeandikiwa historia yake. Kwa hiyo wakija huku kuvitafuta wengi huenda kuviuza kwenye hayo maduka kwa bei kali mno

8. Nguvu ya utajiri
Biashara imevamiwa , vitu vya kale haviwezi kukupa utajiri wa miujiza ..havina huo uwezo bali kuna baadhi kutokana na malighafi iliyotumika kuvitengeneza vina mvuto kwenye ulimwengu wa giza kama mabangili ya shaba

9. Usumbufu
Kuna watu wanawachezea wenzao shere na kuwasumbua bila sababu.. Miaka hiyo pesa ilitengenezwa kwa mpango maalum(nadhani hata sasa) na zilitengenezwa kwa miaka... Kuna miaka pesa hazikutengenezwa. Sasa mtu anakupa dili na kukuahidi kukupa pesa ndefu ukimletea rupee ya mwaka fulani

10. Hitimisho
Kuna baadhi ya sehemu kulikofichwa hizo mali wafichaji walinuizia ama kufanya mambo ya giza ili atakayejaribu kuchukua ama apate madhara au asizione kabisa...lakini kwa sehemu kubwa ni habari zilizotiwa chumvi nyingi


JUMAPILI NJEMA
Jr[emoji779] [emoji781]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…