Nani anareactive site za Germany hidden treasury and antique left . Yàani site ambayo ukiweka tu juu chupa ya coca inapasuka au dasani inabadili rangi baada ya dk 10 . Tuwasiliane kwa namba 0785059995. Au mwenye pasi au stove
Mkuu huyu LENHNER hata mimi huwa nashindwa jiuliza maana LENHNER Sr alijenga pale Mbalizi karibia na mto kaja LENHNER jr kajenga Ifisi na kumiliki hadi lile bonde lote na sasa ukiwa unaenda Tunduma mbele kule baada ya kutoka kijiji cha Songwe nako kajenga shule karibia na mto Songwe.Mkuu kutokana na uzoefu wangu ktk sekta mbalimbali nianze na hv,kama utakuwa mfuatiliaji mzuri wa mambo ya FREEMANSORY au ILLUMINATI na alama zao kishetani utagundua kuwa alama zao nyingi hupenda kuziweka kwenye fedha iwe ya coin au noti mfano mzuri ni USD ambayo ina bundi,fuvu,nyota,piramidi,satanic eye,nk alama zote hizo zinalengo moja kuu nalo ni mazindiko! Na kama ujuavyo mazindiko yote ni moja ya ibada za kishetani ambazo hujumuisha majini,mapepo,mizimu,roho chafu pamoja na kafara hasa kafara ya damu ya binadamu!
Na ukifuatilia kwa umakini utagundua hao ma-FREEMANSONS & ILLUMINATI wana origin ya sehem moja nayo ni UJERUMANI ktk jimbo moja linaitwa BAVARIA!
Sasa swala la kujiuliza ni hili ikiwa dunia ya sasa ya sayansi na technology mambo ya mashetani na makafara yapo ktk ela kubwa kama USD na tena kwa kiasi kikubwa SEMBUSE ENZI ZILE ZA GERMANY EMPIRE?.sasa ndio nakuja kwenye Rupia,nikweli ile coin ya rupia inamaajabu flan ambayo yakichanganywa na mazindiko na kafara zingine huwa inaleta kile mtu anakuwa anatake either pesa,cheo au utajiri hii inatokana kuwa ela ya rupia ilipata zindiko la damu ya binadamu wkt wa utengenezaji inasadikiwa madin yaliyotumika kuitengeneza yalikuwa yakichanganywa na damu za binadam thats y wajeruman wkt wanaondoka walizificha hzi ela sehem mbalimbali za tanzania hasa ktk maboma,makanisa(moravian),mito,visima na mashimo marefu.
sehem nyingi hupatikana mkoa wa mbeya,iringa na swanga! Na wajeruman waliweka alama kibao hasa katika magome ya miti mikubwa na mawe na huwa wanakuja kuchukua hizo rupia + madini mengine waliyoyaifadhi baadhi ya sehem zilikofichwa madini haya kwa mkoa wa mby ni hizi hapa,
1.Wilaya ya chunya-makongorosi-kijiji cha ujerumani(hapo panamgodi wa dhahabu wa zaman wa mjerumani ni DEEP GOLD MINE)kunamashimo makubwa ma4 nimakubwa sana!, 2.Sehem zote zilizojengwa hospitali za mission za moravian hasa na mjerumani flan ambaye kwa sasa ni marehemu ila watoto wake wanaendeleza game anaitwa LENHNER(LENA) hospitali ya mbalizi,IFISI SONGWE NA MATEMA BEACH!
Duh,this is so deep..got me scared!Labda kwa kuongezea zaidi kuna baadhi ya mambo najaribu ku connect dots kuanzia utawala wa mkapa hadi sasa nakumbuka mwishoni mwa utawala wake 2005 aliitwa akafanye ziara ujerumani,kilicho shtua mataifa mengi ni namna alivyopokelewa mkapa! Ilikuwa hv ndege ya mkapa wkt imeingia anga la ujerumani zilirushwa ndege za kivita 4 kwenda kumlaki mawinguni ! Zikaizunguka hyo ndege kila moja na upande wake then akapata mapokezi ya kutisha kuanzia airport had ikulu ya ujerumani ambako alikutana na raisi wa ujerumani kwa mazungumzo behind door,inasadikiwa moja ya mambo ambayo wajeruman waliyapa kipaumbele ni hizo mali zao walizoziacha inasadikiwa kuwa BWM alikubali hasa ukizingatia mchonga alikuwa katangulia mbele ya haki so hakukuwa na kipingamizi tena! Immediate wiki moja baada ya BWM kurejea marekani kupitia balozi wao dar wakatuma ujumbe mzito mkapa endapo akiwaruhusu wajerumani kurudi kuchukua mizigo yao tanzania tunge suffer kuanzia kunyimwa misaada hadi kuwa ukanda wa vita kama congo so mipango yote ya wajerumani ikaishia hapo! Ninavyowajua wajerumani sidhan kama ndo waligive up kirahisi hivyo hasa baada ya kushtukiwa na CIA so nadhan (sina uhakika sana najaribu ku connect dots) wamekuja na technic nyingine ya kukifadhili chama fulani cha upinzani ambacho viongozi wake wengi wa juu mbali na kuwa wamesoma huko pia wamekuwa wanakwenda huko mara kwa mara kuhudhuria makongamano mbali mbali!,na kumekuwa na tuhuma hasa kutoka chama tawala kuwa kunachama kinafadhiliwa na mataifa flani ya nje huko,Lakini ni mapema sana kuhisi hicho chama ila "TIME WILL TELL" kama wameshaandaliwa kuwa ma-puppet au ni misaada tu thats y marekani wakaenda kuweka CIA base na ubalozi mdogo kule mbalizi mbeya wakijifanya wanapaita UTENGULE COURT HOTEL kwa lengo la kumonitor pilikapilika za wajerumani!
KWANINI MBEYA? Na sio mikoa mingine haya mambo yanatokea na kufanyika nitaendelea kudadavua next time
Hawa wametimua kutoka shimoni,sijui wameona nini?dah!Kiukweli mm bado sina uhakika kama yapo kwasababu BINAFSI sijafuatilia kiundani na sikutilia maanani kwa kuwa kuna mengine kama hayakuniingia akilini(niliona ni mepesi sana), ILA ninachofahamu hadi sasa kuna eneo nilienda kulingana na maelezo niliyopewa nikakuta kuna dalili za hiyo kitu.
ILIKUWAJE:
Nilivoulizia zile alama ktk mawe kule mwanza(mawe mengi yana alama za michoro km chokaa, mfano alama ya jiwe ambalo maji yalikua yakitiririka kupitia hapo kisha yakakauka)..... Maelezo nlopewa yaliendana na hicho mshana jr alichosema, ila jamaa alikua na ushahidi zaidi, kwa kuwa alinifundisha maana ya alama zote kuanzia hiyo michoro ya chokaa, aina ya miti, mchanga.... na alinipitisha ktk maeneo yote yaliyo karibu ili kuona mifano halisi.
Kwa ufukunyunyu wangu siku moja nikaenda mbali sana huko nyegezi af unapanda huko ndani ndani. Nikachagua moja ya alama na kuanza kufatilia kadri alivyonieleza..... nikakuta kuna mahali kuna jiwe(ama zege hivi) kama limeegeshwa...... nilipologonga.... ulitoka mlio mithili kuna uwazi kwa chini....sikufatilia zaidi ya hapo kwa kuwa nilijawa hofu........ ila ipo siku nitakwenda na team tukafanye mambo.
Maeneo yenye hizi mambo mengine unakuta ni kambi za jeshi, na kwa maelezo ya jamaa waliofanikiwa kupata hazina hii ni wajeda wakubwa tu(haiwekwi wazi) ingawa wao walitumia njia rahisi ya kununua maji(au mafuta) toka kwa familia za kijerumani zinazojua maswala haya(hii ni kwa mujibu wa maelezo ya jamaa).
Masharti ya kuingia maeneo haya.
1. Usisex wala kujielekeza sana na mawazo ya sex kwa muda usiopungua miezi6(maana yake uwe masafi(pure), kuna uwezekano ukiwa bikra unafanikiwa zaidi) pia usiwe na mawazo ya chuki, hasira.
2. Ukiwa eneo hili hamtakiwi kula kula(kama ni kula mkalie mbali huko)
3. Usiende kwa mganga kwa nia ya kudhuru(wapo waganga wanaoelewa hilo na wanajua namna ya kuwashauri)
4. Mnapoenda, msiwe na mawazo ya kidhuluma(yani km ni mgawo, uwe sawa sawa kama mlivokubaliana)
5. Uwe jasiri, vile vitu unapokutana navyo ni vitisho tu, havidhuru, mtu anadhurika kwa woga wake na panic, na pia utakapoogopa na kupiga kelele ndo mauza uza yanapozidi.
6.Msiwe waropokaji, hapa jamaa alisema utakaposema sema habar hizo kwa wasiohusika(kwamba mna mzigo) utakua unapotea potea....
7. Haitakiwi kelele, msiongee ongee, mnatakiwa kuweka akili yote katika jambo mnalofanya(ikiwezekana mjifunze kuwasiliana kwa ishara kabla hamjaingia)
Kikubwa hapa ni kuwa waangalifu kwa mazingira yanayokuzunguka, kuchunga hali ya hatari ili usidhurike na vitu halisi mfano nyoka, wanyama, wadudu na mawe kuporomoka.
Kuna uwezekano ndani ya Ifisi kuna mali nyingi unaweza jiuliza Hotel, Hospital, maonesho ya wanyama vyote vinapatikana ndani ya eneo moja na vipo tangu huyo Lehner kaja mwanae na hivisasa yupo mjukuu naye akiondoka atakuja kitukuu lisemwalo lipo.Mkuu huyu LENHNER hata mimi huwa nashindwa jiuliza maana LENHNER Sr alijenga pale Mbalizi karibia na mto kaja LENHNER jr kajenga Ifisi na kumiliki hadi lile bonde lote na sasa ukiwa unaenda Tunduma mbele kule baada ya kutoka kijiji cha Songwe nako kajenga shule karibia na mto Songwe.
Pia nimewahi sikia ana hotel ukifuata lile korongo la Ifisi hospital ila kwa chini zaidi..why kila kitu karibia na makorongo,ziwa au mito?
mmmh siyo matango pori kweli?Maeneo ya mvomero kwenye safu za milima ya Unguu kuna Mzee wangu aliungana na wasaka rupia walipanda kuelekea kileleni kwa muda wa siku 4 walishangaa kumkuta mjeruman kapiga suti na yupo bize kwenye kaofisi kazuri ka vioo huko karibu na kilele!, kuna mganga walikuwa nae akapiga manyanga bila mafanikio wakaamua kupiga jiwe mlangoni walishtukia yule mjerumani yupo miongon mwao! Walitimua mbio walikutana nyumban yule mganga aliuacha mkoba wake hakuufata tena. Kuna wengine walikuta pango lenye mlango finyu wakaona masanduku lakini kwa juu kuna bunduki ikielekea mlangoni halafu kuna nyaya zimeingia kwenye trigger lakini chanzo cha zile nyaya hakionekani na kuna mjeda ndugu yangu aliefika hapo aliàmua kurusha jiwe mlangon anasema bunduki ilitema risasi hadi jiwe lililokuwa kwa mbele liliçhakaa na akagundua kuna mkanda wa risasi usioisha kibaya zaidi ile bunduki inacheza pande zote za mlango! Alikwenda karibu Mara 7 bunduki bado active.
😵Abunuwasi
Mkuu walichimba kwa siku ngap?mimi nimesoma iyunga technical sec.school pale mbeya,hii habari za kutafuta rupia ni kweli kabisa nakumbuka mwaka 1996-1999 kuna jamaa walikuja kuchimba shimo kukwa na refu tu kule kwenye bweni la ruthuli wakutafuta hizo rupia,sasa sijui kulikuwa na mkono wa serikali sijui kwakuwa jamaa wakuja wamejandaa na walikuwa na dhana za kazi za uhakika