Rushwa huleta upofu sawa kwa wote

Rushwa huleta upofu sawa kwa wote

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Tunaoishi sasa tunaamini tuna akili kubwa na maarifa mengi kuliko walioishi kale, jambo ambalo siyo kweli.

Naamini watu wa kale walikuwa na akili kuliko tunaoishi leo. Kwenye maarifa, kwa sababu maarifa huwa ni mwendelezo kutoka aliyetangulia alipoishia, hivyo yalipofika leo ni mbele zaidi kuliko hapo kale.

Watu wa zamani walikuwa na akili zaidi kuliko wa sasa kwa sababu waliiona kesho kabla haijafika.

Kule kwenye biblia, mtu mwenye hekima kubwa kuliko wanadamu wote, mfalme Sulemani, anasema RUSHWA HUPOFUSHA.

Mkiwa vipofu mnafanana katika kutoona. Yawezekana kabla ya kupofuka, mmoja alikuwa anaona wastani, mwingine anaona kidogo,mwingine alikuwa anaona sana, mwingine alikuwa anaona kwa kusaidiwa na miwani. Kwa hiyo kabla ya kupofuka mnatofautiana sana katika uwezo wa kuona. Lakini mkipofuka, wote mnafanana, wote mnakosa uwezo wa kuona.

Kwenye hoja ya bandari, ukimsikiliza Musukuma, Mbarawa, Nape, Kibajaji, Japipo, mwansheria wa wizara, kama hujaambiwa backgrounds zao, huwezi kujua kama miongoni mwao kuna wa darasa la saba, profesa, wa degree moja au wa darasa la nne. Wote wamefanana. Utofauti wao wa kuona umesawazishwa.

Nadhani kitu kimojawapo kinachojali sana usawa, rushwa ni miongoni maana inawafanya mfanane bila ya kujali utofauti wa hali zenu za zamani.
 
Watanzania twapenda ona maendeleo mazuri ila hatuwazi kuwekeza tangu kwenye msingi

Mfano leo nasikia kuwa wachezaji wenye uraia pacha ambao wanatakiwa wabaki na uraia wa TZ tu kisha waingizwe kwenye kikosi cha timu ya Tanzania (Timu ya Taifa) kitakachoingia kambini kujiandaa na mchezo ujao wa kimataifa

Inamaana wakishamaliza michezo hiyo wanarejea kuwa na pasport mbili za uraia pacha ama?
 
Rushwa inapofusha kweli, kwasababu unapoona watu na akili zao timamu wanatetea mkataba mbovu kama ule wa bandari, ujue zile sio fikra zao, ni kile walichopewa ndio kimewatia upofu wasione madhara ya wanachokitetea.
 
Rushwa inapofusha kweli, kwasababu unapoona watu na akili zao timamu wanatetea mkataba mbovu kama ule wa bandari, ujue zile sio fikra zao, ni kile walichopewa ndio kimewatia upofu wasione madhara ya wanachokitetea.
Rushwa ni janga la taifa. Udumavu wo wote wa maendeleo Tanzania na Afrika unatokana na RUSHWA. Kiongozi ye yote anayesimama imara kwenye suala la rushwa atapendwa na watu wake. Atachukiwa na viongozi wenzake, ndio maana viongozi kwa hofu ya kuishi wanajiona wakae kwa jinsi hiyo hiyo ya kutopinga rushwa kwa nguvu nyingi.
 
Rushwa inatakiwa ianze kufundishwa toka chekechekea maana ndiyo adui no 1 wa maendeleo ya watanzania
 
Tunaoishi sasa tunaamini tuna akili kubwa na maarifa mengi kuliko walioishi kale, jambo ambalo siyo kweli.

Naamini watu wa kale walikuwa na akili kuliko tunaoishi leo. Kwenye maarifa, kwa sababu maarifa huwa ni mwendelezo kutoka aliyetangulia alipoishia, hivyo yalipofika leo ni mbele zaidi kuliko hapo kale.

Watu wa zamani walikuwa na akili zaidi kuliko wa sasa kwa sababu waliiona kesho kabla haijafika.

Kule kwenye biblia, mtu mwenye hekima kubwa kuliko wanadamu wote, mfalme Sulemani, anasema RUSHWA HUPOFUSHA.

Mkiwa vipofu mnafanana katika kutoona. Yawezekana kabla ya kupofuka, mmoja alikuwa anaona wastani, mwingine anaona kidogo,mwingine alikuwa anaona sana, mwingine alikuwa anaona kwa kusaidiwa na miwani. Kwa hiyo kabla ya kupofuka mnatofautiana sana katika uwezo wa kuona. Lakini mkipofuka, wote mnafanana, wote mnakosa uwezo wa kuona.

Kwenye hoja ya bandari, ukimsikiliza Musukuma, Mbarawa, Nape, Kibajaji, Japipo, mwansheria wa wizara, kama hujaambiwa backgrounds zao, huwezi kujua kama miongoni mwao kuna wa darasa la saba, profesa, wa degree moja au wa darasa la nne. Wote wamefanana. Utofauti wao wa kuona umesawazishwa.

Nadhani kitu kimojawapo kinachojali sana usawa, rushwa ni miongoni maana inawafanya mfanane bila ya kujali utofauti wa hali zenu za zamani.
Na sasa rushwa imerasimishwa kwenye jamii yetu. Sehemu kubwa ya upambe na uchawa ni matunda ya rushwa. Hivi sasa, inaelekea kuna fedha nyingi sana zinatumika kununua watu wenye sauti, ushawishi na vyombo vya habari ili kusemea, kusifia wanasiasa na kutukuza wanasiasa na watawala. Hii yote ni rushwa. Viongozi, hasa wenye dhamana ya madaraka ya umma wanaotekleza wajibu wao hawahitaji kusemewa, kupambwa, kusifiwa wala kutukuzwa. Kuendekeza mambo haya ni kuendekeza rushwa katika jamii.
 
Ni sawasawa na wabunge wanavyolipwa mishahara na miposho posho isiyoeleweka na serikali na kuishia kupitisha hadi mikataba ya kimchongo, hiyo ni rushwa. Ndo maana nilishasema wabunge wachangiwe posho na wananchi wao kule majimboni na siyo kulipwa na serikali ili wawe na nguvu ya kuithibiti serikali.​
 
Ni sawasawa na wabunge wanavyolipwa mishahara na miposho posho isiyoeleweka na serikali na kuishia kupitisha hadi mikataba ya kimchongo, hiyo ni rushwa. Ndo maana nilishasema wabunge wachangiwe posho na wananchi wao kule majimboni na siyo kulipwa na serikali ili wawe na nguvu ya kuithibiti serikali.​
Na kwa kweli tukifaka bunge liwe la watu wazalendo qebye dhamira ya kweli ya kuwasaidia wananchi, lazima tubadilishe mambo mengi kuhusiana na bunge na wabunge.

Kwa sasa bunge limekuwa kama kakikundi fukani ka wahuni waliotafuta njia rahisi kupatia rushwa.
 
Back
Top Bottom