Sir robby
JF-Expert Member
- Jun 22, 2022
- 2,396
- 4,080
CCM imejikita kwa kutumia makada wake kina Kibajaji, Msukuma, Kigwangala na Kihongosi kumsema na kumtukana balozi Bashiru badala ya kuzijibu hoja zake kwa umakini.
Wakati huo huo CCM ipo kwenye uchaguzi wa viongozi wake nchi nzima uchaguzi uliotawaliwa na utoaji wa rushwa wa kutisha kwa wanaotaka kuchaguliwa kwa wapiga kura.
Kwa mujibu wa katiba ya CCM inamtaka kila mwanachama aahidi kuwa
"Rushwa ni adui wa haki sitatoa wala kupokea rushwa"
Lakini ahadi hiyo haitekelezwi kwa vitendo na CCM ipo kimya.
Nilitarajia kwa kuwa CCM ndio chama tawala kingeonyesha mfano kwa vitendo kukitumia chombo cha Serikali TAKUKURU kuwakabidhi wanachama wake waliojihusisha na utoaji na upokeaji wa rushwa kwa chombo hicho ili wafikishwe mahakamani lakini CCM inaishia kufuta chaguzi.
Kwa mtazamo wangu suala la rushwa tena ktk chaguzi ni hatari sana kuliko malumbano ya CCM na Bashiru.
Wakati huo huo CCM ipo kwenye uchaguzi wa viongozi wake nchi nzima uchaguzi uliotawaliwa na utoaji wa rushwa wa kutisha kwa wanaotaka kuchaguliwa kwa wapiga kura.
Kwa mujibu wa katiba ya CCM inamtaka kila mwanachama aahidi kuwa
"Rushwa ni adui wa haki sitatoa wala kupokea rushwa"
Lakini ahadi hiyo haitekelezwi kwa vitendo na CCM ipo kimya.
Nilitarajia kwa kuwa CCM ndio chama tawala kingeonyesha mfano kwa vitendo kukitumia chombo cha Serikali TAKUKURU kuwakabidhi wanachama wake waliojihusisha na utoaji na upokeaji wa rushwa kwa chombo hicho ili wafikishwe mahakamani lakini CCM inaishia kufuta chaguzi.
Kwa mtazamo wangu suala la rushwa tena ktk chaguzi ni hatari sana kuliko malumbano ya CCM na Bashiru.